November 2016

Mchungaji mmoja huko nchini Afrika Kusini, Lethebo Rabalago anatumiwa dawa ya mbu ya kupuliza kama njia ya uponyaji kwa waumini wake wanaokwenda kanisani kwake kwa ajili ya maombi ya matatizo mbalimbali ya kiroho.Image result for lethebo rabalago
 
Mchungaji anaamini kwamba dawa hiyo ya mbu ya kupuliza inaweza kumponya mwanadamu na kumwezesha mtu kupata upako wa bwana baada ya kuombewa na kupuliziwa kama sehemu ya ufunuo wa kutoka kwenye dimbwi la dhambi na mikosi.
 
Lethebo Rabalago, kutoka kwenye kanisa la Mount Zion General Assembly (MZGA) katika mji wa Limpopo, alituma picha kwenye mitandao ya kijamii kama vile Facebook na kuonyesha akitumia dawa hiyo kali ya kuua mbu kama nyenzo yake ya uponyaji.
 
Siku chache zilizopita kwenye mitandao ya kijamii kulijaa taarifa za mchungaji huyo anayetumia dawa hiyo ya mbu kama njia ya uponyaji kwa waumini wake hapo kanisani, baada ya kutuma picha hizo mijadala ilikuwa ikiendelea kwenye mitandao sehemu kubwa ya Afrika kuhus aina hiyo ya maombezi.
 
Mmoja wa waumini aliyepitia huduma alinukuliwa akisema kwamba “Nilikuja hapa na maumivu sehemu ya nyuma na tumbo, lakini sasa baaada ya maombezi ya mchungaji nimepata uponyaji wa kutosha na pua yangu iliumia tangu wiki iliyopita na baada ya mchungaji kuniombea na kunipuliza dawa nimepata nafuu kubwa,” alinukuliwa akisema.

SPIKA Mstaafu, Anna Makinda ameiomba serikali na mamlaka husika kuanza mchakato wa kusukuma mabadiliko ya sheria ya ndoa ili kupanua wigo wa haki za wanawake na watoto nchini.
 
Image result for ndoa
 
Akizungumza katika kongamano la wanawake lilioandaliwa na Mfuko wa msaada wa kisheria nchini (LSF) jana jijini Dar es Salaam, Makinda alisema kwamba sheria ya ndoa ya mwaka 1971 imepitwa na wakati na inahitaji marekebisho makubwa ili kutoa haki kwa wanawake nchini.
 
“Hii sheria ya ndoa inawatenga sana wanawake nchini katika swala la mirathi na kuacha watoto wengi wakiteseka ni wakati muafaka sasa kwa wanaharakati kusaidia na wabunge ili kuleta marekebisho hayo kwa manufaa ya nchini nzima,” alisema Makinda ambaye ni spika mstaafu.
 
Alisema kwamba marekebisho hayo makubwa au kuandikwa upya kwa sheria ya ndoa itakuwa hatua moja kubwa katika kulinda haki za wanawake za kumiliki mali, kama vile mashamba na kadhalika.
 
Alisisitiza kwamba swala la mirathi ni tatizo kubwa sana nchini ambapo wanawake wengi wamepoteza mali zao walizochuma na wenzi wao wakati wa ndoa.
 
“Nikiwa mbunge, waziri na baadaye spika tulipambana vikali katika kubadilisha sheria ya ardhi ili kuwapa watu wa hali ya chini kupata nafasi ya kumiliki ardhi, sasa na hii sheria ya ndoa inapaswa kushughulikiwa kwa haraka ili kuweza kutoa matokeo chanya kwa jamii,” aliongeza.
 
Alifafanua kwamba marekebisho hayo ya sheria ya ndoa yatasaidia kunusuru maelfu ya wanawake ambao wanateseka kutokana na kila aina ya unyanyasaji wa kijinsia na vipigo ambavyo vinaongezeka kila kona ya nchini.
 
Aliomba mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kushirikiana na serikali katika majadiliano hasa katika mambo ya mirathi na ndoa ili kuhakikisha upatikanaji wa marekebisho hayo yanapatikana haraka.
 
“ni muhimu pia maswala haya ya haki za wanawake na watoto kufundishwa katika shule za msingi na sekondari ili kupeleka elimu hiyo ya uraia kwa wanafunzi nchini nzima, ila ni muhimu kushirikiana na serikali ili kufanikisha hayo,” aliongeza 
 
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu, Mfuko wa Msaada wa Kisheria (LSF), Bw, Kees Groenendijk alisema kwamba mfuko lengo lake kuu ni kuongeza haki na usawa kwa wanawake nchini kupitia uwezeshaji wa fedha na mafunzo.
 
“Kutokana na mustadha huo, mfuko uliamua kwamba mfuko kusaidia mashirika yasiyo kuwa ya kiserikali yanayotoa msaada wa kisheria kwa jamii hasa wanawake ambao wapo katika wilay zote za Tanzania Bara,” alisisitiza.
 
Alisema tangu mfuko huo uanze zaidi ya wanawake 2,000 walifikiwa kwa msaada wa kisheria ambao ni asilimia 60% ya wanawake nchini nzima.
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) Bi, Tike Mwambipile alisema kwamba serikali ni lazima kuanzisha kitengo maalum cha kushughulikia matatizo ya ndoa na mirathi katika mifumo ya utoaji haki nchini.

Scholarship-Poitions.com 

 
Swedish Institute Study Scholarships for Developing Countries, 2017-2018
Ministry for Foreign Affairs of Sweden and administered by the Swedish Institute (SI)
Application Deadline: January 16, 2017
Apply Now


University of Adelaide Undergraduate Scholarship Program (AIUS) in Australia, 2017
The University of Adelaide, Australia
Application Deadline: January 20, 2017
Apply Now

Master of Health Leadership International Scholarships in New Zealand, 2017

University of Auckland, New Zealand
Application Deadline: December 8, 2016
Apply Now


NUS Graduate School Scholarship (NGSS) for International Students in Singapore, 2017
National University of Singapore, Singapore
Application Deadline: January 15, 2017
Apply Now


L’Oréal USA For Women In Science Fellowship Program, 2017
L’Oréal Foudation
Application Deadline: February 3, 2017
Apply Now

Fee-waiver Scholarships for International Students at University of Bristol in UK, 2017
University of Bristol, United Kingdom
Application Deadline: May 2, 2017
Apply Now


Fully-funded Scholarships at International Fashion Academy in France, 2017
International Fashion Academy, France
Application Deadline: May 31, 2017
Apply Now


Institute for Transport Studies Master Scholarships for International Students at University of Leeds in UK, 2017
University of Leeds, United Kingdom
Application Deadline: June 22, 2017
Apply Now


20 College of Social Sciences Scholarships at University of Glasgow in UK, 2017-2018
University of Glasgow, United Kingdom
Application Deadline: February 3, 2017
Apply Now


Free Online Course on Financial Market Analysis
International Monetary Fund (IMF)
Course Starts on January 25, 2017
Apply Now

Free Online Course on International Project Management
Rochester Institute of Technology
Course Starts on August 28, 2017
Apply Now


Information and Communications Technology (ICT) Excellence Scholarships in Australia, 2017
University of Queensland, Australia
Application Deadline: January 23, 2017
Apply Now


University of Brighton Fully-funded International Research Scholarships in UK, 2017
University of Brighton, United Kingdom
Application Deadline: June 30, 2017
Apply Now

Search for Common Ground Africa Program Spring Internship in USA, 2017

Search for Common Ground (SFCG)
Application Deadline Contact Employer
Apply Now


KSP Excellence Scholarships for International Students in France, 2017-2018
Kuwait Program at Sciences Po and Kuwait Foundation for the Advancement of Sciences (KFAS)
Application Deadline: December 11, 2016
Apply Now

UN Knowledge Management Internship at RET International in Geneva, Switzerland, 2017

RET International
Application Deadline December 16th 2016
Apply Now


Africa Organisation for Standardization 4th Continental Essay Competition, 2017-2018
Africa Organisation for Standardization
Application Deadline: 30th January 2017
Apply Now

ICTP Visiting Fellowships for Mathematicians from Developing Countries in Italy, 2017

The Abdus Salam International Centre for Theoretical Physics (ICTP)
Application Deadline: January 7, 2017
Apply Now

London School of Economics and Political Science LLM Scholarship for Female Africans in UK, 2017

London School of Economics and Political Science, United Kingdom
Application Deadline: April 26, 2017
Apply Now


2017 CBS Ph.D. Scholarship in Political Science and Public Management, Denmark
Copenhagen Business School, Denmark
Application Deadline: December 31 2016
Apply Now


10 Undergraduate Scholarships for International Students at University of Brighton in UK, 2017
University of Brighton, United Kingdom
Application Deadline: July 31, 2017
Apply Now


PhD Positions in Artificial Intelligence, Virtual Reality, and Multimodal Signal Processing at Southern Illinois University, USA
Southern Illinois University, USA
Application Deadline: Contact Employer
Apply Now

Fulbright Foreign Student Program for Bangladeshi Students in USA, 2017-2018

United States Government
Application Deadline: April 28, 2017
Apply Now

Molly Bartlett Endowed Scholarships at American University in Egypt, 2017
American University in Cairo, Egypt
Application Deadline: December 20, 2016
Apply Now

Science & Engineering Merit Extension Undergraduate Scholarship at Curtin University in Australia, 2017
Curtin University, Australia
Application Deadline: December 31, 2017
Apply Now

University of Birmingham Cadbury Research Fellowship Scheme in UK, 2017
University of Birmingham, United Kingdom
Application Deadline: December 9, 2016
Apply Now

The Asian Development Bank Essay Competition for Graduate and Postgraduate Students in Uzbekistan, 2017
The Asian Development Bank
Application Deadline: December 5, 2016
Apply Now

University of Copenhagen PhD Scholarships at the Faculty of Law in Denmark, 2017
University of Copenhagen, Denmark
Application Deadline: January 17, 2017
Apply Now

Graduate Scholarships for Thai Students at Webster University in Thailand, 2017
Webster University, Thailand
Application Deadline: December 16, 2016
Apply Now

ICN2 PhD Student Fellowship in Advanced Surface Electromechanics, Spain
Application Deadline:
Apply Now

PhD Research Fellowship in Analytical Chemistry at University of Oslo in Norway, 2017
University of Oslo, Norway
Application Deadline: December 5, 2016
Apply Now

Vice Chancellor’s PhD Studentships in Psychology at Roehampton University in UK, 2017
Roehampton University, United Kingdom
Application Deadline: December 2, 2016
Apply Now

ANU-Study Canberra Indonesia Scholarships in Australia, 2017
Australian National University, Australia
Application Deadline: January 15, 2017
Apply Now

PhD Position in Marine Biogeochemistry at Heriot-Watt University in UK, 2017
Heriot-Watt University in UK
Application Deadline: January 31, 2017
Apply Now

Higher Education Scholarships for Palestinians (HESPAL) in UK, 2017
HESPAL is funded by participating UK Higher Education Institutes (UK HEIs); a range of private sponsors (details provided on request); the Department for Business Innovation & Skills (BIS); Foreign & Commonwealth Office (FCO) and the Arab Fund in Kuwait and managed and administered by British Council Palestine.
Application Deadline: January 23, 2017
Apply Now


Applications Open for University of Edinburgh MBA Scholarships in UK, 2017-2018
University of Edinburgh, United Kingdom
Application Deadline: March 2017
Apply Now

Decision Making Online Course by University of Lausanne
University of Lausanne
Course Starts on December 12, 2016
Apply Now

Lund University Free Online Writing Courses
Lund University
Course Starts on December 12, 2016
Apply Now

Cleveland Foundation Summer Internship Program in USA, 2017
Cleveland Foundation, United States of America
Application Deadline January 23rd, 2017
Apply Now

Facebook Supply Chain Internship in USA, 2017
Facebook
Application Deadline Contact Employer
Apply Now

UMOJA wa Nchi za Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wameweka nguvu ya pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Ruaha kwenye semina iliyoelezea malengo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani ambapo kati ya hao, vijana 50 wamepata semina ya mwongozo wa kuwa mabalozi wa malengo hayo (Global Goals Champions). Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania. 


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa misaada ya maendeleo UNDAP II 2016-2021 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akifafanua jambo juu ya ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Mpango wa misaada ya Maendeleo 2016-2021 (UNDAP II) kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa
Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa, Martin Noel akiwa ameongozana Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano chuoni hapo sambamba Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendesha semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia.

Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akielezea fursa za ufadhili wa masomo nje ya nchi katika tovuti ya Umoja wa Ulaya Tanzania wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia iliyofadhiliwa na EU.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akiwapiga msasa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia kwenye semina hiyo iliyofadhiliwa na EU.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akiwa amejumuika na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia ambapo semina hiyo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) nchini.
Pichani juu na chini ni vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha walioshiriki semina maalum ya kuwa mabalozi wa malengo ya dunia (Global Goals Champions) iliyoandaliwa na UN na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) akimkabidhi cheti Rais wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa Athman Waziri aliyehitimu kuwa balozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champion).
Picha juu na chini Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendelea na zoezi la kutunuku vyeti kwa mabalozi wa malengo ya dunia kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champions) baada ya kuhitimisha semina maalum iliyoshirikisha vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Martin Noel baada ya kuhitimisha semina ya malengo ya dunia mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Afisa Habari wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU), Muazarau Matola
Baadhi ya Global Goals Champions katika picha ya kumbukumbu na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akibadilishana mawazo na wahitimu wa semina malengo ya dunia (Global Goals Champions) mara baada ya kuhitimisha semina hiyo iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Ruaha mjini Iringa ambapo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).

Customer Satisfaction is More Important Than Ever During the Festive Season
dhl.jpg
During the festive season, a company’s top priority is to make sure that its platforms are effectively managed and prepared to deal with an increased influx of customers
CAPE TOWN, South Africa, November 29, 2016/ -- The end of year festive season is almost upon us and for many businesses, especially those in the retail sector, this means the start of the peak activity period. In order to realize revenue targets, as well as offer a shopping experience that attracts a loyal following, it is imperative that retailers, both traditional and online, are properly geared for the expected upsurge in sales that is synonymous with the ‘silly season’.

This is according to Hennie Heymans, CEO of DHL Express Sub-Saharan Africa (www.dpDHL.com), who points to the findings in a 2016 study by McKinsey & Company, which indicates that shoppers in the African market are developing and demanding more creative, engaging and integrated shopping experiences from brands. “Multi-channel access points and reliable digital platforms are increasing in importance as consumers continue to look for products that are value for money. Companies must give consumers solid reasons to choose their product or store over alternatives,” he says.

Shoppers based in Africa shop across a number of channels and respondents claimed to have shifted a considerable amount of their spending toward modern retailers and away from the small independent retailers.

During the festive season, a company’s top priority is to make sure that its platforms are effectively managed and prepared to deal with an increased influx of customers. This period is also a highly competitive time for retailers and Heymans comments that supply chain management strategies are critical.

“Retailers need to ensure their supply chain is agile enough to handle the volume spike. To maximize profitability, retailers need quick, smart and cost-effective methods to fulfill orders timeously and accurately across multiple sales channels. Additionally, effective reverse logistics processes are also essential for managing returns to ensure a smooth, hassle-free customer experience. As e-tailers often extend or introduce free shipping offers over the festive season – it’s important for businesses to understand their shipping costs and processes to mitigate any potential shortfalls. Repeat deliveries stemming from incorrect products or address changes can result in additional shipping costs. Customers should also be reminded of potential duties, taxes and additional costs when importing from a site overseas. Ultimately, it’s all about managing expectations and satisfying the customers’ needs.”

Heymans adds that when problems do arise, it is important for businesses to be ready to resolve them effectively. “Customers with queries or complaints should be able to access various escalation channels easily. Access to senior managers should be clearly defined so that customers do not have the added frustration of trying to track down someone who can’t assist them. At DHL Express, we introduced a best-in-class feature on our website which allows customers access to the whole Senior Management team, through our ‘Straight To The Top (STTT)’ initiative. All STTT queries are logged and reported at a country and regional level; these are effective in helping highlight broader issues and we use root-cause analysis to identify solutions,” Heymans says.

Customer experience is what makes or breaks a business. “We’ve been in Africa for over 38 years, and our team of experienced employees, also known as Certified International Specialists, works hard to keep the customer at the center of everything we do. We have a saying at DHL in Africa, where we ‘take it personally’. The only way you can delight a customer is if you take the time to personally understand what they need, and do everything in your power to deliver it,” concludes Heymans.

Statistics: McKinsey & Company http://APO.af/b80kVG; http://APO.af/z4Oqut.
Distributed by APO on behalf of Deutsche Post DHL.
Media Contact: 
Megan Collinicos
Head of Marketing, Sub-Saharan Africa, DHL Express
Tel: +27 21 409 3613
Mobile: +27 76 411 8570
Megan.Collinicos@DHL.com

About DHL:
DHL – The logistics company for the world

DHL (www.dpDHL.com) is the leading global brand in the logistics industry. Our DHL family of divisions offer an unrivalled portfolio of logistics services ranging from national and international parcel delivery, e-commerce shipping and fulfillment solutions, international express, road, air and ocean transport to industrial supply chain management. With about 340,000 employees in more than 220 countries and territories worldwide, DHL connects people and businesses securely and reliably, enabling global trade flows. With specialized solutions for growth markets and industries including technology, life sciences and healthcare, energy, automotive and retail, a proven commitment to corporate responsibility and an unrivalled presence in developing markets, DHL is decisively positioned as “The logistics company for the world”.

DHL is part of Deutsche Post DHL Group. The Group generated revenues of more than 59 billion euros in 2015.

For more information: www.dpDHL.com.
Stock images available: www.dpDHL.com/en/media_relations/media_library.html.
SOURCE
Deutsche Post DHL

UMOJA wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wamejiunga pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania . Aidha kwa pamoja wamezuru miradi iliyofadhiliwa na EU. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Mkwawa kwenye semina iliyoelezea malengo hayo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani. Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania. 
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (kushoto) akisalimiana na mmoja wa wahadhiri wa chuo hicho alipowasili katika ofisi za Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akiwa ameambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez.(Picha zote na Zainul Mzige wa Moblog)

Semina katika vyuo hivyo ni sehemu ya mpango madhubuti wa Umoja wa mataifa uliozinduliwa Arusha Mei mwaka huu na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wenye lengo la kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia. Ujumbe huo wa EU na UN pia ulipata nafasi ya kutembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na EU ukiwamo wa Boma la Kijerumani ambalo lilikarabatiwa kwa ruzuku ya EU kupitia 'fahari yetu – Southern Highlands Culture Solutions'. Boma hilo ni moja ya majengo ya zamani katika mji wa Iringa na lilijengwa na Wajerumani mwaka 1900 kama hospitali ya kijeshi. Baada ya vita ya Kwanza ya Dunia, jengo hilo lilibadilishwa matumizi na watawala wapya, Uingereza, na kulifanya kuwa jengo la utawala. EU imesema inaona fahari kuwa mmoja wa wawekezaji wakubwa katika sekta ya sanaa na urithi wa kitamaduni nchini Tanzania, ikifadhili miradi 10 iliyo chini ya programu ya 10 ya EDF ya kusaidia masuala ya kitamaduni. 

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akiwa kwenye mazungumzo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (upande wa kushoto katikati) pamoja na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Hoyce Temu (kushoto) alipotembelewa ofisini kwake na ugeni huo. Kulia ni Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever pamoja na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, Henry Mditi.

Masuala yanayohusu urithi wa kitamaduni ni muhimu katika kuchagiza ukuaji wa uchumi, ajira na huku ikifuma mahusiano ya kijamii, na kutoa fursa ya kuboresha utalii endelevu mkoani Iringa huku ikileta faida kwa wakazi wa eneo hilo. Bw. Rodriguez, akizungumza katika kampeni hiyo alisema kwamba ajenda 2030 ambayo ni ajenda ya maendeleo endelevu inahitaji ushiriki wa kila mmoja.Aliwapongeza wanachuo hao na wanazuoni kwa kujikita kutambua malengo hayo ya dunia. Aidha aligusia umuhimu wa vijana kushiriki katika masuala ya maendeleo kutokana na ukweli kuwa, kwa taifa kama la Tanzania vijana ni asilimia 60 ya wananchi wote waliopo.Alisema kwamba vijana wanajukumu kubwa la kushiriki katika maendeleo hayo kwa lengo la kuipeleka nchi katika hatua nyingine ya maendeleo. 

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwa ameongozana na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, Henry Mditi kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano Chuo Kikuu cha Iringa.

Hata hivyo alisema kwamba ni wajibu wa kila mtu hasa vijana, kuhakikisha kwamba malengo hayo ya dunia yanafanikiwa . Alisema Umoja wa Mataifa kwa kusaidiwa na wadau wake muhimu kama Umoja wa Ulaya, utaendelea kusaidia Watanzania kuwajibika katika shughuli mbalimbali za maendeleo katika kuunga mkono malengo hayo ya dunia. Mmoja wa washiriki alipongeza Umoja na wa Mataifa kwa kuwafikia vijana wa vyuoni na kuwapa semina hiyo. “Ninajisikia mtu mwenye bahati kupata nafasi ya kujifunza maendeleo endelevu kutoka kwa Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini. Nikiwa kama kijana, naona faraja kuona kwamba viongozi wetu wanafuata maelekezo yaliyofafanuliwa kwenye malengo 17 ya maendeleo endelevu; naamini kama tukijitahidi kuyafikia ifikapo 2030, basi Tanzania na duniani kwa ujumla itakuwa eneo jema la kuishi. Na kwa kuwa sasa natambua kuhusu malengo hayo ya dunia, ninaweza kutoa mchango wangu kusaidia kuyafikia -najisikia kuwezeshwa sana.” amesema Mary, mmoja wa washiriki. 

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akisoma taarifa fupi ya Chuo Kikuu cha Iringa mbele ya ujumbe kutoka Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya wakati semina kuhusu malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akizungumza kwenye semina ya malengo ya dunia kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa ambapo aliwaasa wakawe mabalozi wazuri wa malengo hayo kwenye jamii zao na wanafunzi wenzao wa vyuo vingine.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akitoa salamu za Umoja wa Ulaya kwa niaba ya Balozi wa Umoja huo, Bw. Roeland Van De Geer wakati wa semina Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa wanachuo wa Iringa iliyowezeshwa na EU.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwapiga msasa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa kuhusu Malengo ya Dunia katika semina iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
Mwanafunzi wa mwaka wa tatu anayechukua Shahada ya Sayansi katika Uchumi na Fedha wa Chuo Kikuu cha Iringa, Sarafina Sayi akiuliza swali kwa mkufunzi wa malengo ya dunia Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (hayupo pichani) wakati wa semina hiyo.
Mwanafunzi wa Shahada ya Sayansi katika Uchumi na Fedha wa Chuo Kikuu cha Iringa, Geoffrey Kadori akiuliza swali kwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela wakati wa semina ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa wanafunzi wa Chuo hicho.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akijibu swali wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwenye semina kuhusu malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.

Pichani juu na chini ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa kutoka vitivo tofauti chuoni hapo waliohudhuria semina ya malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla makabrasha na majarida yenye ripoti na taarifa mbalimbali za Umoja wa Mataifa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ripoti na makabrasha mbalimbali ya Umoja wa Mataifa mara baada ya kuhitimisha semina kuhusu SGDs kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa tatu kulia) katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya pamoja na Balozi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs Champion), Sabinus Paul (kushoto) nje ya ukumbi kulikofanyika semina kuhusu SDGs kwa wanachuo wa Iringa.
Picha ya pamoja na sehemu ya washiriki wa semina hiyo huku wakiwa na mabango ya SDGs.
Muonekano wa nje wa jengo la Makumbusho ya Mkoa na Kituo cha Utamaduni -Iringa Boma ambalo limejengwa kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).
Kibao cha Makumbusho ya Mkoa wa Iringa kinachoratibiwa na Mradi wa Fahari yetu kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Iringa
Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever akielezea dhumuni la mradi Fahari Yetu unaolenga kuendeleza utamaduni nyanda za juu kusini kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (mwenye suti) ambao ndio wafadhili wa jengo hilo la Makumbusho ya Mkoa wa Iringa. Wengine katika picha ni wahadhiri na maprofesa kutoka Chuo Kikuu cha Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akisaini kitabu cha wangeni ndani ya Makumbusho ya mkoa wa Iringa.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa.
Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever akitoa maelezo picha mbalimbali zinazoelezea historia ya mkoa wa Iringa wakati wa utawala wa Chifu Mkwawa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro walipotembelea makumbusho ya mkoa wa Iringa
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akisoma historia mbalimbali za enzi za utawala wa kichifu ndani ya Makumbusho ya Mkoa wa Iringa.
Mwongoza wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Jacob Shenyagwa (mwenye miwani) akitoa maelezo ya picha mbalimbali kwa ugeni huo wa UN na EU uliotembelea makumbusho hiyo iliyojengwa chini ya ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).
Mwongoza wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Deonis Mgumba akitoa maelezo ya vifaa mbalimbali vilivyokuwa vikitumika enzi za utawala wa kichifu kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, Henry Mditi (katikati) walipotembelea makumbusho hayo mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro wakitwanga mahindi kienyeji katika moja ya kinu kilichokuwa kinatumika enzi hizo za utawala wa kichifu kilichopo katika makumbusho hayo.
Mwongoza wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Matatizo Kastamu akitoa maelezo ya picha mbalimbali zenye kumbukumbu za utawala wa kichifu na historia ya mji wa Iringa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (kushoto), Mtalaam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu na Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever wakipitia vipeperushi vyenye maelezo ya kina ya Mradi wa Fahari Yetu unaoendesha Makumbusho na Kituo cha Utamaduni mkoa wa Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro katika picha ya pamoja kwenye sanamu maalum za mavazi ya kipindi cha utawala wa Chifu Mkwawa walipotembelea Makumbusho ya mkoa wa Iringa.

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.