July 2025

MJI WA SERIKALI, DODOMA –

Serikali ya Tanzania imepongezwa kwa mafanikio yake katika kuimarisha mifumo ya tahadhari na ufuatiliaji wa majanga kupitia Kituo cha Dharura cha Taifa (Situation Room) kilichopo Mtumba, Dodoma.

Pongezi hizo zimetolewa na wataalamu kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso waliopo nchini kwa mafunzo ya siku tatu ya kubadilishana uzoefu, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Menejimenti ya Maafa, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amesema kituo hicho kimeongeza uwezo wa taifa kutoa tahadhari mapema kwa wananchi na kuratibu mashirika mbalimbali kukabili majanga.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Kituo hicho, Bi. Jane Kikunya, amesema wageni hao wameonesha nia ya kuiga mfumo huo katika nchi zao kutokana na mafanikio waliyojionea.

Aidha, wageni hao wameeleza kufurahishwa na jinsi taarifa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kuwasilishwa kwa wananchi kwa haraka na kwa usahihi.










 NAMWANDISHI MAALUM

Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. James Kilabuko amehimiza ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na majanga ya kibinadamu yanayochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa, kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kuimarisha vituo vya ufuatiliaji wa majanga na tahadhari ya mapema (Situation Room).

Akizungumza leo wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalum ya kubadilishana uzoefu, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na UNDRR na Kituo cha Sayansi cha Afrika Magharibi kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (WASCAL), Dkt. Kilabuko alisema mafunzo hayo ni sehemu ya kuimarisha uwezo wa kanda katika kukabili matukio ya majanga. Mafunzo hayo yalihusisha ujumbe kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso.

Dkt. Kilabuko alieleza kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa majanga, kupitia vituo vyenye uwezo wa kukusanya taarifa mbalimbali, zikiwemo za hali ya hewa, maji, kijamii na kiuchumi, jambo linalosaidia kukabili majanga kama vile ukame na mafuriko.

 “Tunauzoefu mkubwa wa kiutendaji ambao unasaidia kuhakikisha vituo vyetu vinafanya kazi kwa ufanisi kwa kuratibu taasisi mbalimbali kukabiliana na majanga,” alisema Dkt. Kilabuko.






Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.