Articles by "Habari"

Showing posts with label Habari. Show all posts

Na Mwandishi Wetu
WAKAZI wa Temeke wamehamasika na kuamua kuunda vikundi vya usafi wa mazingira, ‘Usafi Clubs’, ikiwa ni moja ya matunda ya mradi wa kuwawezesha wakazi wa mijini, ‘Urban Legal Empowerment’ unaolenga kusaidia jamii ya watanzania kupata haki zao za kuishi katika mazingira salama na safi, haki za kiuchumi na za kijamii.  
Kupitia mradi huu, unaotekelezwa na shirika la LEAT kwa ufadhili wa LSF, wakazi wa Temeke pamoja na kata zake, viongozi wa serikali za mitaa na jamii kwa ujumla wamehamashishwa kutunza mazingira katika maeneo wanayoishi au kufanyia shughuli zao za kila siku.
“Kama sehemu ya utekelezaji wa mradi huu, LEAT tumetoa elimu kwa wananchi, viongozi wa kata, madiwani, na wanafunzi, kuhusu sheria za mazingira, kanuni, na namna gani elimu hii itakavyowezesha wananchi kutunza na kuboresha mazingira yao,” amesema Bi. Glory Kilawe, Mratibu wa mradi kutoka LEAT.
Baada ya kupata elimu, wakazi wa Temeke wameunda vikundi vya mazingira, maarufu kama “Usafi Clubs”—ambavyo vinatumika kama vyombo vya kuhamasisha usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali wilayani Temeke.
Tunawashukuru LEAT kutupatia elimu hii nzuri ya mazingira, kujua sheria na taratibu mbalimbali zinazohusu mazingira,” anasema mmoja wa wakazi wa Temeke, Hassan Juma, katika kikao maalum cha kutathmini utekelezaji wa mradi wa LEAT wilayani humo.
Hemed Pazi, Mwenyekiti wa Kituo cha Wasaidizi wa Kisheria-Temeke (Temeke Paralegal Centre), anasema wamefanikiwa kuunda vikundi (Usafi Clubs) vinne—viwili viko kata ya Mbagala and 2 kata ya Mianzini–kama sehemu ya utekelezaji wa mradi huo.
“Kinachotufurahisha zaidi ni kwamba hata viongozi wa serikali za mitaa ni sehemu ya vikundi ni wajumbe wa Usafi Clubs. Hii inatia moyo, kwa sababu uwepo wa viongozi hawa unafanya vikundi hivi viaminike kwa jamii, na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake,” kwa mujibu wa Pazi.
Diwani wa Kata ya Mianzini, Abdallah Kipende amesema elimu inayotolewa na Usafi Clubs mitaani imebadilisha tabia na mitazamo ya wakazi wengi kuhusu maswala ya mazingira, hata kuwawezesha kununua vyombo na mapipa  ya taka kwa ajili ya majumbani na mitaani, kuacha kabisa tabia ya kutupa taka ovyo, kama walivyozoea siku za nyuma.
“Sasa hivi, jamii  ya Temeke iko makini sana katika maswala ya mazingira; kila mtu sasa anajua usafi wa mazingira maana yake nini. Kama kuna mtu (leo hii) anataka kujenga kiwanda au kuleta uwekezaji wowote Temeke, lazima ajiandae kujibu maswali magumu ya wananchi kama vile mbinu gani atakazotumia kutunza na kulinda mazingira,” alisema  Kipende.
Mbali na kuwezesha uundaji wa vikundi vya mazingira, LEAT imesaidia kutatua migororo ya mazingira 19, kuelimisha wanafunzi zaidi ya 600, kusambaza machapisho mbalimbali yanayohusu mazingira kwa jamii, kuandaa midahalo na vipindi maalum vya television na radio –kujadili maswala ya mazingira—kama sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Urban Legal Empowerment katika wilaya ya Temeke.
Mradi huu umebuniwa na kufadhiliwa na shirika la Legal Services Facility (LSF) na lengo kuu la mradi huu ni kuwezesha watanzania waishio mijini, hasa wasiojiweza kifedha, katika maswala mbalimbali ya kisheria, kijamii na kiuchumi.
Legal Services Facility (LSF) imeyawezesha mashirika sita yasiyokuwa ya kiserikali kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Urban Legal Empowerment katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam

Temeke residents have set up several environmental groups, dubbed “Usafi Clubs” as part of a urban legal empowerment project, which gears at sensitizing and empowering local communities to clean up their environment, among other things.
Urban legal empowerment project is a brainchild of the Legal Services Facility (LSF)—a basket funding mechanism, which provide grants to legal aid organizations involved in the implementation of paralegal and related projects across the country. More than 50 legal aid organizations have already benefited from LSF funding since its inception in 2011.
Among other things, urban legal empowerment intends to empower urban dwellers and enable them to access their social and economic rights—including access to safe water, education, health services, clean environment, and other social and economic rights.
Lawyers Environmental Action Team (LEAT)—is one of six legal aid organizations which received LSF funding for the implementation of urban legal empowerment project in different parts of Dar es Salaam. Basically, LEAT focused on environmental-related issues—educating/training local communities, paralegals, paralegal units, local executives on the importance of cleaning up their environment, exposing them to environmental and hygienic laws, rules and regulations and other related matters in Temeke District.
The knowledge acquired from LEAT trainings, encouraged Temeke residents to establish their own environmental groups, popularly known as “Usafi Clubs” –an instrument which is used to sensitize and mobilize people, local authorities and leaders, investors to clean their environment—from the streets up to the district levels.
“We thank LSF on one hand, and LEAT on the other…we thank LSF because it supported LEAT to give us such good education on environment, laws and regulations. Thanks to the two of them,” said one Temeke resident, Hassan Juma, at a special session organized by LEAT to review implementation of a one-year pilot project.
“It’s because of their support, now we have Usafi Clubs in place…everybody is eager to join to these clubs,” added Juma as recalls successes registered in the implementation of the project.
Hemed Pazi, Chairman of Temeke Paralegal Centre, said four Usafi Clubs have been formed –2 clubs in Mbagala Ward and 2 in Mianzini Ward –in the context of project implementation, which also involved paralegals.
Interesting part of the story is that local government executives are “part and parcel of these clubs…they are members of the clubs” according to Pazi, noting that “involvement of local leaders increased public trust and confidence on the clubs, thus making them more effective.”
Mianzini Ward Councilor, Abdallah Kipende said door-to-door environmental knowledge spread by Usafi Clubs has significantly changed altitudes and behaviour of Temeke residents, enabling them to set up dust-bins and tanks across the streets, stopped littering the environment, as they used to do in the past.
“In fact, the entire Temeke community is now sensitive about environmental issues; many people are aware of their environmental rights. Today, if somebody wants to put up industries or any large-scale investment in the district should get prepared for tough questions from communities on strategies they would employ to protect the environment,” says Kipende.
Besides establishment of Usafi Clubs, according to Ms. Glory Kilawe, LEAT official-in-charge of the project, said 19 environmental cases were resolved, over 600 students received environmental education, several educative materials distributed to communities, special television and radio programmes were aired, public dialogues organized on the subject—as part of urban legal empowerment pilot project in Temeke district.
In the wake of increasing number of urban poor needing legal assistance in different parts of the country, LSF came up with urban legal empowerment—a new and strategic model which guides paralegals and legal aid organizations on how to assist urban dwellers to access their social and economic rights.

Nchi za Afrika zinaweka mikakati inayolenga kukomesha uzalishaji na matumizi ya dawa bandia na sizizo na viwango, tatizo kubwa linalorudisha nyuma maendeleo ya nchi za Africa.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Dr. Agnes Kijo, akiongeza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Jukwaa la Kudhibiti Ubora wa Madawa Afrika (African Medicines Quality Forum-AMQF) jijini Dar es Salaam. Aliyekaa katika ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dr. Faustine Ndungulile, na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo Afrika (NEPAD), Margareth Ndomondo—wadau walijadili mbinu za kukomesha uzalishaji na usambaji wa dawa bandia na zisizo na viwango—mkutano uliandaliwa na NEPAD,  The United States Pharmacopeia convention (USP), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA),

“Lengo letu kuu ni kuhakikisha ubora wa dawa zinazotumiwa na waafrika,” amesema Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dr. Faustine Ndungulile, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Jukwaa la Kudhibiti Ubora wa Madawa Afrika (African Medicines Quality Forum—AMQF).  Kongamano hili limeandaliwa na Shirika la Maendeleo Afrika (NEPAD), The United States Pharmacopeia convention (USP), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA),
Kwa mujibu wa Waziri Ndungulile, dawa bandia na sizizo na viwango ni tatizo kubwa barani Afrika, linalohitaji mikakati madhubuti, na kusisitiza kuwa Afrika mikakati haiwezi kufanikiwa bila ushiriakiano wa wadau wote.
“Dawa bandia na sizizo na viwango zinagharimu pesa nyingi nchi za Afrika. Kuna watu wanakufa kwa ajili ya dawa hizi, pia kuna watu walazimika kutumia dawa nyingine za ziada. Zote hizi ni gharama kwa mwananchi mmoja mmoja na Serikali zetu kwa ujumla,” amesema Waziri Ndungulile.
Kama njia ya kudhibiti ongezeko la madawa bandia na sisizo na viwango, nchi za Afrika sasa hivi zinaweka mpango mkakati wa pamoja unaolenga kudhibiti usambaji na matumizi wa dawa bandia. Ameutaka Mkakati huo kama AMQF—jukwaa jipya la Africa lengo lake kuu ni kuweka mikakati mipana itakayotatua matatizo na changamoto zinazotokanazo na madawa yenye ubora hafifu yanayosambazwa kwa matumizi barani Afrika.  Kuanza kwa Jukwaa la AMQF kunakuja wakati kukiwa na ongezeko kubwa la matumizi ya madawa bandia na yasiyo na kiwango, yaliyokwisha muda wake katika sehemu mbalimbali barani Afrika, ikiwemo Tanzania.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani yaani ‘WHO’ asilimia 42 ya taarifa zinahusu madawa bandia na madawa yaliyokwisha muda wake, huripotiwa katika nchi za Afrika.

“Kupitia jukwaa hili matatizo ya ubora ya madawa yatashughulikiwa kikamilifu na hatimae kukomesha kabisa uzalishaji na usambazaji wa madawa bandia na zisizo na viwango katika masoko ya Afrika,” amesema Waziri.

Kwa mujibu wa Waziri Tanzania Tanzania ni moja ya nchini iliyofanikiwa kwa kiasi kikubwa katika udhibiti wa dawa bandia, jambo lilosababisha “Mkutano huu ufanyike hapa kwetu ili nchi zingine za Afrika zipate nafasi ya kujifunza kutoka kwetu.”
Aliongeza kwamba Tanzania imeweza kujitosheleza kwa dawa za kutosha na zenye viwango vya kimataifa na changamoto kubwa ilikuwa na kudhibiti dawa zinazoingia kwa njia ya panya ambapo tayari mamlaka husika (TFDA)  imeanza kushughulikia, kwa kufungua ofisi za kanda zinazolenga kupunguza mianya ya dawa zinazoingia kwa njia ya panya.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Bi Agnes Kijo alisema “Tanzania ina mahabara ya kisasa, zilizosambaa sehemu mbalimbali nchini…yote haya ni kuhakikisha ubora na viwango vya dawa zinazosambazwa katika masoko yetu na kutumiwa na watu.”
“Katika mkutano huu jambo kuu litakuwa na kwa namna ngani tunaweza kudhibiti dawa bandia kwenye masoko na kuhakikisha kwamba wazalishaji pia wanatoa dawa zenye ubora unaokubalika katika soko,” alisisitiza Bi Kijo.
Mkuu wa Mipango wa NEPAD, Margareth Ndomondo, amesema “Mamlaka za uthibiti lazima zitengeneze mifumo ya pamoja ikayosaidia kudhibiti usambazaji na matumizi katika nchi za Afrika kwa urahisi.”
Mkutano huo imekutanisha washiriki kutoka nchi 18 za Afrika –ikiwa ni pamoja na Nigeria, Ghana, Ethiopia, Uganda, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Cameron, Ivory Coast, Mali, Burkina Faso, Mauritania, Senegal, Sierra Leone, Sudan, Guinea, and South Africa pamoja na mawakala barani Afrika kama vile Wakala wa Afya Afrika Magharibi (WAHO) na wafadhili wa maendeleo kama vile Shirika la Afya duniani yaani WHO, Shikla la misaada la Marekani yaani USAID pamoja na Benki ya Dunia.
Wawakirishi kutoka nchi zaidi ya 18 za Afrika wakifutia mijadala katika Mkutano wa Jukwaa la Kudhibiti Ubora wa Madawa Afrika (African Medicines Quality Forum-AMQF) jijini Dar es Salaam—unaolenga kukomesha uzalishaji, usambazaji na matumizi ya dawa bandia na zisizo na viwango.

Mwakilishi wa Shirika la United States Pharmocopeia Convention (USP, Bi. Emily Kaine, akiongea wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Kudhibiti Ubora wa Madawa Afrika (African Medicines Quality Forum-AMQF) jijini Dar es Salaam—unaolenga kukomesha uzalishaji, usambazaji na matumizi ya dawa bandia na zisizo na viwango.

Mkuu wa Kitengo cha Mipango katika Shirika la Maendeleo Afrika (NEPAD), Bi. Margareth Ndomondo akiongea wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Kudhibiti Ubora wa Madawa Afrika (African Medicines Quality Forum-AMQF) jijini Dar es Salaam—unaolenga kukomesha uzalishaji, usambazaji na matumizi ya dawa bandia na zisizo na viwango.

Mwakilishi wa Shirika la United States Pharmocopeia Convention (USP, Bi. Emily Kaine, akiongea wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Kudhibiti Ubora wa Madawa Afrika (African Medicines Quality Forum-AMQF) jijini Dar es Salaam—unaolenga kukomesha uzalishaji, usambazaji na matumizi ya dawa bandia na zisizo na viwango.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dr. Faustine Ndungulile (katikati), akiongea na waandishi wa habari baada ya kufungua Mkutano wa Jukwaa la Kudhibiti Ubora wa Madawa Afrika (African Medicines Quality.

WATAALAMU na wanazuoni wamekubaliana haja ya kupitia mpango wa maendeleo endelevu wa viwanda, SIDP (1996-2020), ili kwenda na wakati kwa kubadili kilimo na kuiweka nchi katika njia bora ya kufikia uchumi wa viwanda. Kauli hiyo imetamkwa kwa namna tofauti na wataalamu hao ambao wamekutana jijini hapa kuangalia uhusiano uliopo kati ya viwanda, mabadiliko ya tabia nchi na kilimo; na ni namna gani sera ya viwanda inaweza kupitiwa upya kuakisi mahusiano haya. Warsha hiyo iliyoandaliwa na ESRF na CUTS International imelenga katika kuelezea umuhimu wa kuangalia mahusiano ya sera ya maendeleo ya viwanda na mabadiliko ya tabia nchi, usalama wa chakula na biashara. 

Wakijadili mada mbalimbali zilizowasilishwa katika semina hiyo iliyofanyika ESRF, wataalam hao walitambua umuhimu wa pekee wa kupitia upya sera hiyo ili iweze kuonesha muunganiko fasaha uliopo kati ya viwanda, kilimo na biashara; na hatua/mikakati ipi iwepo kukinga adhma hii ya viwanda dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi. Wamesema kwamba kwa kuunganisha sera ya maendeleo endelevu ya viwanda na uchakataji wa bidhaa za kilimo na kilimo chenyewe kunaleta mwanya wa kuweka msingi imara katika mchakato wa maendeleo na hasa viwanda. Pia, kwa kuwa na sera madhubuti, nchi itaweza kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika sekta ya Viwanda, hususani viwanda vinavyotegemea maligafi za sekta ya kilimo.


Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene akitoa neno la ukaribisho kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida wakati wa mkutano wa awamu ya pili ya kuangalia Tabia nchi, Uboreshaji kilimo, na mahusiano yake na biashara kwa jumuiya ya Afrika Mashariki (PACT EAC2), uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 
Katika mkutano huo ilikubalika haja ya kuwa na mikakati ya utetezi kwa kuangalia tafiti zitakazofanywa juu ya kinachojiri katika maendeleo kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi, usalama wa chakula na biashara. Zaidi ya yote, pia wadau waliona kuna haja kubwa ya kuwa na tafiti itayoweza kuonesha ni kwa kiasi gani sera ya SIDP (1996-2020) imeweza kuchangia katika ukuaji wa viwanda Tanzania, na changamato zipi imekumbana nazo ambazo zinapaswa kutatuliwa na kuanishwa wakati wa mapitio ya sera hii. Akiwasilisha hoja yake ndugu Solomon Baregu, Mtafiti wa ESRF na Meneja wa Mradi wa PACT EAC 2, amesema kwa kuangalia hali halisi ya sasa ipo haja kwa wataalamu kutambua changamoto zinazojitokeza katika maendeleo endelevu ya viwanda na kukiangalia kilimo kama msingi wa uimarishaji wa viwanda. 

Aidha alisema kwamba kwa kuangalia hali ya sasa ipo haja kubwa ya kubadili kilimo cha Tanzania ili kuboresha maisha ya wananchi na kuimarisha viwanda kwa kuvipatia mali ghafi ya kutosha na yenye ubora. Alisema ni vyema kuelewa uhusiano uliopo katika sera za maendeleo ya viwanda na kilimo ili kuwa na mpango mahsusi wa utetezi kwa lengo la kuimarisha viwanda. Katika mkutano huo washiriki pia walipitia mambo mbalimbali na hatua zinazochukuliwa kupitia sera ya mpango wa maendeleo wa viwanda unaomalizika 2020.


Mkurugenzi Msaidizi wa idara ya Ushirikishaji Kikanda kutioka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bi. Sekela Mwaisela akisoma hotuba ya ufunguzi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo wakati wa mkutano wa awamu ya pili ya kuangalia Tabia nchi, Uboreshaji kilimo, na mahusiano yake na biashara kwa jumuiya ya Afrika Mashariki (PACT EAC2), uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano ESRF jijini Dar es Salaam.

Miongoni mwa mambo yaliyojitokeza kwenye mazungumzo ya tafiti ni umuhimu wa kuoanisha sera mbalimbali katika kilimo na viwanda kuzihuisha na kuzipa mwelekeo wenye maana kama chachu katika kuimarisha uchumi wa viwanda. Walisema ipo haja ya kuangalia sera hizo ili ziwe msaada katika kuimarisha kilimo na kutoa ushindani kwa viwanda vinavyotegemea bidhaa za kilimo ili kujiimarisha. Aidha katika mazungumzo kwenye mkutano huo imeelezwa kuwa ingawa serikali kupitia wizara zake mbalimbali na Ofisi ya Makamu wa Rais wamechukua hatua kadhaa kuwa na matokeo bora katika utetezi wa bidhaa za viwanda zinazotokana na kilimo, kukosekana kwa uangalizi na utekelezaji wa pamoja kumeleta shida kwa wananchi. Sera ya sasa ya maendeleo endelevu ya viwanda (SIDP) imetengenezwa mwaka 1996 na itaisha 2020 lakini bado ipo haja ya kuweka mahusiano katika utekelezaji wa mpango huo wa maendeleo, kwani kwa mazingira ya sasa hakuna mahusiano na kuna vikumbo katika sera mbalimbali. Wamesema kwamba sera hiyo haitoi mwanya wala mahusiano kati ya viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, mabadiliko ya tabia nchi, biashara na usalama wa chakula.


Mtafiti wa ESRF na Meneja wa Mradi wa PACT EAC 2, Solomon Baregu akiwasilisha namna bora ya kufanya utafiti wenye lengo la kuoanisha mpango wa maendeleo endelevu ya viwanda na mabadiliko ya tabia nchi na kilimo wakati wa mkutano huo wa kuzungumzia mradi wa PACT-EAC2 uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.

Aidha walisema kwamba mpango wa pili wa maendeleo (2016/17-2020/21) unaonesha haja ya kuweka Tanzania katika njia ya viwanda kwa kuijengea nchi uwezo wa kuzalisha katika kilimo na pia katika ufugaji. Haja ya kubadilisha Kilimo inatokana na ukweli kuwa ni moja ya sekta zinazoingiza kipato cha kigeni kwani inachangia asilimia 29.1 ya pato la taifa, huku ikichangia asilimia 30 ya fedha za kigeni. Aidha ndio chanzo pekee cha uhakika cha biashara ikitoa asilimia 65 ya mahitaji ya viwanda (ghafi) na asilimia 90 ya chakula cha taifa huku ikiajiri asilimia 66.9 ya nguvu kazi ya Taifa. 

Ndugu Peter Lanya, aliekua Makamu Mwenyekiti wa TCCIA, akitoa ufafanuzi zaidi alisema kwamba kunatakiwa mabadiliko katika sera hiyo ili kuupa usasa kwa kuwekeza kwenye mahusiano ya kilimo, mali ghafi kama taifa likitaka kuendelea kuelekea uchumi wa viwanda. Naye ndugu, Joseph Kihaule, Afisa Mkuu wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Raisi, alisema kwamba kuna haja ya kubadilika katika kilimo ili kuweza kufanya vyema huku akisema mazungumzo ya kimataifa ya kupata muafaka, hususani yahusuyo mabadiliko ya tabia nchi, ni muhimu yakaunganishwa na sera mbalimbali ili kuimarisha kilimo na upatikanaji wa chakula.


Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa TCCIA, Peter Lanya akizungumzia SIDP 1996-2020 wakati wa mkutano wa awamu ya pili ya kuangalia Tabia nchi, Uboreshaji kilimo, na mahusiano yake na biashara kwa jumuiya ya Afrika Mashariki (PACT EAC2), uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa idara ya Ushirikishaji Kikanda kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bi. Sekela Mwaisela.

Awali akifungua semina hiyo Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na uwekezaji (viwanda) Adelhelm Meru alishukuru taasisi za ERSF na CUTS International kwa kuona umuhimu wa kuwa na mkutano huo wanne wa kitaifa kuzungumzia mradi wa PACT-EAC. Katika hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi msaidizi Wizara ya Viwanda Ushirikishaji Kikanda, Bi. Sekela Mwaisela alisema kwamba wizara inatambua haja ya kuweka pamoja viwanda na uchakataji wa mazao ya kilimo kwa kuwa inasaidia kuweka sawa maendeleo ya viwanda. Alisema kwamba kazi iliyofanywa na ESRF inaiweka wizara hiyo katika nafasi bora zaidi ya kufanya mabadiliko ya muhimu kufikia mwaka 2020. Alisema sera hiyo iliyoanza 1996-2020 imepita katika maeneo matatu ambayo yalilenga kuimarisha uwezo wa viwanda (1996-2000), matumizi ya teknolojia (2000-2010) na uimarishaji wa viwanda 2010-2020. Alisema SIDP imesaidia kuimarisha viwanda na sasa lazima kuwepo na uangalizi ili kuwepo na mahusiano mazuri kati ya sera zote zinazotegemewa kuwezesha maendeleo endelevu ya viwanda.


Afisa Mkuu wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Joseph Kihaule akichangia maoni katika mkutano huo uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida katika hotuba yake iliyosomwa na Prof. Fortunata Makene amesema ipo haja kubwa ya kuwepo kwa mabadiliko katika SIDP kutokana na mahusiano yake na sekta nyingine hasa yenye uhusiano na kilimo. Katika mkutano huo wa awamu ya pili ya kuangalia Tabia nchi, Uboreshaji kilimo, na mahusiano yake na biashara kwa jumuiya ya Afrika Mashariki (PACT EAC2), Dk Kida alisema kwamba taasisi yake imefurahi kutoa mchango kwa ajili ya kusaidia kuimarisha viwanda nchini. Alisema mkutano huo unaoangalia namna ya kuboresha sera ya viwanda, SIDP (1996-2020), kabla ya utafiti utakaoanza baadae ni muhimu katika kuona kwamba kilimo kinaboreshwa sanjari na SIDP kwa kuweka mahusiano ambayo awali yalikosekana katika sera ya SIDP.


Pichani juu na chini sehemu ya washiriki wakichangia maoni wakati wa mkutano huo uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa mikutano ESRF jijini Dar es Salaam.

Alisema kwa taifa la Tanzania ili lisonge mbele ni vyema masuala muhimu katika SIDP yakaangaliwa ili kutekeleza mipango ya maendeleo ya viwanda kwa kuhusisha na uchakataji wa mazao ya kilimo. Aidha alisema katika utafiti utakaosaidia kuboresha SIDP majukumu ya biashara ya kimataifa katika maendeleo ya viwanda na tabia nchi haviwezi kudharaulika. Alisema utafiti utakaofanywa utasaidia kuongeza ‘nyama’ zaidi katika mikakati ya maendeleo kwa kufanya utetezi kwenye mabadiliko ya tabia nchi, biashara na usalama wa chakula kwa kufanya mabadiliko makubwa katika uchakataji bidhaa za kilimo kwa kutambua pia makubaliano ya kimataifa ambayo Tanzania ni mshiriki, hususani UNFCCC na WTO.





Picha juu na chini washiriki kutoka taasisi mbalimbali za serikali na sekta binafsi walioshiriki kwenye mkutano huo.[





Picha ya pamoja ya washiriki.

SHIRIKA la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) limekabidhi vifaa vya radio kwa radio za jamii nne vyenye thamani ya mamilioni ya shilingi. Unesco imesema kwamba utoaji wa vifaa hivyo umelenga kuongeza usikivu wa mawimbi ya radio katika maeneo ya vijijini. Shughuli ya kukabidhiana imefanyika Agosti 17 mwaka huu. Akizungumza wakati wakukabidhiana vifaa hivyo Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues alisema kwamba UNESCO inatambua kazi nzuri zinazofanywa na radio hizo za jamii za kuwafikia wananchi wengi zaidi.


Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kushoto) akizungumza jambo wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya radio jamii iliyofanyika katika ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.

Aidha alisema ni muhimu sana kwa radio hizo za jamii kujiangalia na kujitunza zenyewe ili wasiingie katika matata na kuchapisha au kutangaza stori baada ya kukamilika kwake. Alisema ipo haja kwa vyombo vya habari kufanyakazi kwa mujibu wa taratibu zao na kuhakikisha kwamba hawachapishi habari ambazo zinahatarisha uwapo wa uandishi unaozingatia maadili. Meneja wa radio ya Jamii ya Baloha FM, Samada Maduhu aliishukuru UNESCO kwa kusaidia kituo chake na kwamba wanatarajia kufikia wilaya tano.


Meneja wa radio ya Jamii ya Baloha FM ya Kahama, Samada Maduhu, akitoa neno la shukrani kwa ofisi za Unesco wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo yaliyofanyika katika ofisi za Shirika hilo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa mtaalamu wa Mawasiliano Unesco, Nancy Kaizilege Angulo.


Alishukuru UNESCO kwa kuwawezesha kufika katika wilaya tano na kwamba kwa msaada huo wataokoa shilingi laki saba kwa mwezi kuazima transmita. “Radio yetu inawafikia watu 500,000 lakini kwa kupatiwa hivi vifaa tutaweza kufikia watu milioni 1 katika wilaya zaidi ya tano za Kahama, Shinyanga Vijijini, Nyang’wale na Mbogwe mkoani Geita na pia Nzega na Uyui mkoani Tabora ,” alisema meneja huyo .

 Kwa mujibu wa Maduhu, kama wasingelipata transmita hiyo wangelikuwa wanatumia sh milioni 8.4 kwa mwaka.


Ofisa Utawala na Rasilimali Watu wa Radio Jamii ya Pangani FM, Rehema Kilapilo akitoa shukrani kwa uongozi wa Unesco wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa vya redio iliyofanyika katika ofisi za Unesco jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Ayubu Kalufya wa radio ya jamii Uvinza alisema kwamba kituo chake kilikuwa kinakodisha transmita kwash laki tano na kufanya kwa mwaka mzima kutumia sh milioni 6. Alisema kwa kupata vifaa hivyo walikuwa wanaachama na ukodishaji huo. Kwa mujibu wa Kalufya, transmita hiyo mpya itawafikisha mbali zaidi katika pwani za Ziwa Tanganyika na hivyo kuleta mabadiliko yanayokusudiwa. Kalufya alisema wananchi wakisikia mambo mbalimbali ya kuwaelimisha na wao wakapata nafasi ya kutoa maneno yao haki za binadamu zitakuwa zimeheshimiwa sana nchini.


Mkurugenzi wa Radio Jamii Uvinza FM, Ayubu Kalufya (kulia) akitoa neno la shukrani kwa hivyo Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kushoto) wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa vya radio hizo yaliyofanyika kwenye ofisi za shirika hilo jijini Dar es Salaam.

Aliishukuru Unesco kwa kuendelea kuwasaidia na kusema kama si kwa msaada wa UNESCO jamii zilizopo pembezoni zisingepata nafasi ya kutoa madukuduku yao. Radio nyingine zilizonufaika na msaada huo ni Pangani FM. Radio hiyo sasa inaweza kusikika Tanga nzima badala ya Pangani pekee. Katika orodha ya redio zilizopatiwa vifaa ipo pia Mkoani FM ya kutoka Zanzibar.


Picha juu na chini ni Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues na Ofisa Utawala na Rasilimali Watu wa Radio Jamii ya Pangani FM, Rehema Kilapilo wakisaini hati za makabidhiano ya vifaa katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za UNESCO jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Maofisa kutoka sekta ya mawasiliano UNESCO.





Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akikabidhi hati ya makubaliano na moja kati ya vifaa hivyo kwa Ofisa Utawala na Rasilimali Watu wa Radio Jamii ya Pangani FM, Rehema Kilapilo wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ofisi za shirika hilo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Maofisa kutoka sekta ya mawasiliano Unesco Dar es Salaam.


Picha juu na chini ni Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues na Meneja wa radio ya Jamii ya Baloha FM ya Kahama, Samada Maduhu kwa pamoja wakisaini hati za makabidhiano ya vifaa hivyo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za UNESCO jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Maofisa kutoka sekta ya mawasiliano UNESCO Dar es Salaam.
 


Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akikabidhi hati ya makubaliano na moja kati ya vifaa hivyo kwa Meneja wa radio ya Jamii ya Baloha FM ya Kahama, Samada Maduhu wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ofisi za shirika hilo jijini Dar es Salaam.


Picha juu na chini ni Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues na Mkurugenzi wa Radio Jamii Uvinza FM, Ayubu Kalufya kwa pamoja wakisaini hati za makabidhiano ya vifaa hivyo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za UNESCO jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Maofisa kutoka sekta ya mawasiliano UNESCO.

 


Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akikabidhi hati ya makubaliano na moja kati ya vifaa hivyo kwa Mkurugenzi wa Radio Jamii Uvinza FM, Ayubu Kalufya wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ofisi za shirika hilo jijini Dar es Salaam.





Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akigonga 'cheers' na wawakilishi wa redio jamii zilizopokea vifaa hivyo kwenye hafla fupi iliyofanyika katika ofisi za shirika hilo Unesco jijini Dar es Salaam.

MWENYEKITI wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi amezitaka Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kushirikiana katika kutumia utajiri wake mkubwa wa raslimali kunufaika kiuchumi. Ushirikiano huo ni pamoja na kuzindeleza raslimali hizo na kutumia nembo moja ya kibiashara ili kuzalisha mabilionea wakubwa duniani. Mwenyekiti huyo alisema hayo katika mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili.

 
Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi akizungumza wakati akifungua mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Pamoja na kutoa wito huo Dk Mengi pia amempongeza Rais wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli pamoja na serikali yake kwa kuwa mstari wa mbele kuboresha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya. Aidha alisema dhamira yake ya kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya viwanda itasaidia kuwakwamua Watanzania kutoka katika umaskini. Katika mazungumzo hayo ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania –TPSF Dr Reginald Mengi na Ujumbe wa Kenya umeongozwa na Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor. 

 
Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor akimpongeza Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi kwa kutoa risala nzuri ya ufunguzi wa mkutano huo. 

 Akizungumza katika mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye amesema mkutano huo umeitishwa kutokana na kujitokeza vikwazo vya kufanya biashara baina ya Wafanyabiashara wa Tanzania na Kenya, jambo linalokwamisha malengo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya kujenga uchumi unaoongozwa na sekta Binafsi. Kwa upande wake Kiongozi wa Ujumbe wa KEPSA Bw. George Owuor amesema Wafanyabiashara wa Kenya wanapenda sana kushirikiana kibiashara na wenzao wa Tanzania, na wangependa kuona vikwazo vinavyokwamisha mahusiano ya kibiashara vinaondolewa.


Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor akiwasilisha mada kuhusu kupunguza pengo la biashara kati ya Tanzania na Kenya na kutumia fursa zilizopo na kutanua biashara nje ya mipaka katika mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Meneja anayeshughulikia Utafiti, Uchambuzi na Sera wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA, Victor Ogalo (kushoto) akitoa mada kuhusu changamoto za kisera za Tanzania na Kenya katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia walioketi ni Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor na Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi wakifuatilia kwa umakini mada hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Alaska Tanzania, Jennifer Bash wakifuatilia mada mbalimbali zikizokuwa zikiwasilishwa ukumbini hapo katika mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili uliofanyika jijini Dar es Salaam.


Pichani juu na chini ujumbe wa Tanzania na Kenya ulioshiriki mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili uliofanyika jijini Dar es Salaam.



Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor na mwenyeji wake Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi katika mkutano huo.
  Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye akijibu maswali kwa waandishi wa habari (hawapo pichani). Kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi.

 

The Ngorongoro District Authorities, in collaboration with the UNESCO Dar es Salaam Office, will welcome the Permanent Secretary of the Ministry of Health (MoHCDGEC), Dr. Mpoki Ulisubisya, the Vice-Chancellor of the Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), Prof. Ephata Kaaya and the UNESCO Representative, Ms. Zulmira Rodrigues on 23 June 2017 for a visit to the first Tele-health Centre in the country. The mission is taking place in the context of the preparations of the handover from UNESCO to Government of this innovative model for provision of specialised health care to remote rural populations. 

The Tele-Clinic is part of a UNESCO/Samsung Digital Village programme in a remote Maasai village in Ngorongoro, Arusha. It is an innovation platform, testing health services provision in maternal and infant care, dental and Ear, Nose and Throat (ENT) services that utilizes connectivity and smart technologies. It will be the first tele-health pilot to connect all levels of the Tanzanian healthcare system reaching out to the remotest communities. The pilot is in the initial service trial phase, focusing first on the operationalization of remote maternal consultations.

   

The Digital Village is a pioneering example that demonstrates how remote communities can be empowered by modern technology improving their access to quality health and education services and build capacities to generate decent income. UNESCO’s innovation approach is unique in its focus on incorporating the cultural specifics in the programme by working in close collaboration with the local community, traditional leaders and healers and by building on traditional Maasai livelihoods such as Maasai crafts to tap into the opportunities for sustained development of the Northern Circuit. The visitors will also be introduced to other Digital Village programme components including e-learning, livelihoods development and cultural tourism development activities.

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam 
                
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la pili la Uwezeshaji  wananchi kiuchumi litakalofanyika Juni 10, 2017 mjini Dodoma ambalo litazileta pamoja sekta ya umma na binafsi kujadili suala la uwezeshaji kama njia ya kuongeza chachu ya uwezeshaji na kufikia uchumi wa viwanda.
Image result for majaliwa kassim majaliwa
Mh. Waziri Mkuu Ndugu, Kassim Majaliwa Kassim
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi. Beng’I Issa alisema hayo wakati akizungumza na wanandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuwa kongamano hilo litawaleta pamoja sekta ya umma na binafsi kujadili masuala ya uwezeshaji kama njia ya kuongeza chachu ya u wezeshaji wananchi kiuchumi na kufikia uchumi wa viwanda.

“Kongamano hili linalenga kupata michango kutoka kwa wadau sekta hizo na hii itasaidia katika kuongeza chachu ya utekelezaji masuala ya uwezeshaji wananchi Kiuchumi,”.Kongamano hilo ni la siku moja lenye kauli mbiu isemayo Wezesha Watanzania Kushiriki Uchumi wa Viwanda, aliongeza kusema ,Bi.Issa.

Alisema kongamano hilo la pili lina malengo mbalimbali yakiwemo ya kukutanisha wadau wa sekta ya umma na binafsi kujadili masuala hayo, kupokea ripoti ya utekelezaji wa uratibu wa masuala ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ngazi ya taifa na pia waziri Mkuu atakuwa Mwenyekiti wa Kongamano hilo.

Malengo mengine ni kutambua wizara, Idara, Taasisi, Serikali za Mikoa na Wilaya nchini zilizofanya vizuri katika kuratibu masuala ya uwezeshaji katika maeneo yao, kuchochea kasi ya utekelezaji wa mikakati ya uwezeshaji wananchi kiuchumi na kujifunza kutoka kwa wadau mbalimbali namna bora zaidi ya kusukuma mbele gurudumu la uwezeshaji. 

Kongamano hilo pia litawezesha wananchi kujifunza na kujitambua kupitia wengine waliofanya vizuri, na pia  Waziri Mkuu atazindua taarifa ya uwezeshaji ya mwaka ambayo inatokana na tathimini ya utekelezaji uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Bi. Beng’I alifafanua kwamba taarifa hiyo inatekelezwa na wadau mbalimbali na atatoa zawadi kwa washindi waliofanya vizuri katika kupeleka mbele ajenda ya uwezeshaji kutoka makundi ya wizara, Idara, na taasisi za umma, mikoa, sekta binafsi na mifuko ya uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.

Pia alisema baraza limealika wadau 300 toka sekta ya umma na binafsi, wadau wa maendeleo, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, tasisi za utafiti na elimu ya juu kushiriki kongamano hilo.

Bi. Issa pia alisaini Makubaliano na Kampuni ya Magazeti ya Tanzania Standard Newspaper (TSN) katika kuhamasisha na uelimishaji umma kuhusu uwezeshaji wananchi kiuchumi na katika kongamano hilo watafanya kazi pamoja.

Naye Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya TSN, Dk. Jim Yonazi alisema magazeti ya serikali yatafanya kazi kubwa ya kuelimisha wananchi katika kushiriki  uchumi unaokusudiwa na serikali ya awamu ya tano yenye dhamira uchumi wa viwanda.

”Tumejipanga kuhakikisha shughuli hii inafanikiwa na hii ni fursa nzuri kwetu kuwafikishia wananchi taarifa sahihi na kwa wakati ili wazitumie,” na kwa kufanya hiyo itasaidia kukuza uchumi wao na uchumi wa taifa,aliongeza kusema,Dk. Yonazi.

 Kongamano hilo hufanyika kila mwaka mara moja chini ya baraza hilo na limetokana na mwongozo wa uratibu wa masuala ya uwezeshaji wananchi kiuchumi katika Wizara, idara za umma, serikali za mikoa na wilaya na sekta binafsi nchini. Pia ulizinduliwa rasmi Feburuary 9, 2016 na waziri Mkuu Kassim Majawaliwa.

Mwongozo huu umekuwa kichocheo cha uratibu utekelezaji wa sera ya Taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi katika sekta ya umma kwa kuwezesha kuundwa kamati ya uwezeshaji na uteuzi wa waratibu katika wizara mikoa 26 na halmashauri zote 185 nchini.

Ofisa wa Benki ya NMB Tawi la Temeke, Latifa Ayoub Dadah (kushoto) akimkabidhi mpira wa miguu mmoja wa viongozi wa michezo wa Shule ya Msingi Wailes kwa ajili ya shule hiyo. Mpira huo umetolewa na Benki ya NMB kama zawadi kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes mara baada ya elimu ya masuala ya fedha na akiba iliyotolewa na benki hiyo. Wa kwanza kusho to ni Mwalimu wa Taaluma wa Shule ya Msingi Wailes, Zabibu Wasia akishuhudia


Ofisa wa Benki ya NMB Tawi la Temeke, Latifa Ayoub Dadah (kushoto) akitoa elimu ya masuala ya kifedha na akiba kwa wazazi na wanafunzi walioshiriki mafunzo ya programu ya wajibu ya NMB katika Shule ya Msingi Wailes ya jijini Dar es Salaam.



Mmoja wa wachezaji vijana (kulia) wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Azam kupitia kituo chao cha michezo akimkabidhi mpira wa pete mmoja wa viongozi wa michezo wa Shule ya Msingi Wailes kwa ajili ya shule hiyo. Mpira huo umetolewa na Benki ya NMB kama zawadi kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes mara baada ya elimu ya masuala ya fedha na akiba iliyotolewa na benki hiyo.


Mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes akijibu swali kwenye mafunzo ya programu ya wajibu iliyotolewa na Benki ya NMB shuleni hapo.



Mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes akijibu swali kwenye mafunzo ya programu ya wajibu iliyotolewa na Benki ya NMB shuleni hapo.


BENKI ya NMB imetoa elimu ya masuala ya kibenki na umuhimu wa kujijengea utamaduni wa uwekaji akiba kwa wanafunzi na baadhi ya wazazi wa Shule ya Msingi Wailes iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam. Akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes walioshiriki mafunzo hayo ya kifedha, Ofisa wa Benki ya NMB Tawi la Temeke, Latifa Ayoub Dadah alisema NMB inaendelea kutoa elimu ya masuala ya kifedha ikiwa ni pamoja na kujifunza mbinu za kuweka akiba kwa ajili ya maisha ya baadae. Alisema elimu hiyo inatolewa kupitia Programu maalum ya Wajibu ambayo hutoa fursa kwa watoto, vijana na wazazi kujifunza masuala ya kifedha ili kumjengea mtoto utamaduni wa kujiwekea akiba, elimu ambayo watoto wengi hawapati fursa ya kujifunza. 

Akizungumza katika mafunzo hayo, alisema vijana wengi wamekuwa hawana utaratibu wa kujiweka akiba tangu wadogo hivyo NMB kupitia programu ya Wajibu inaendelea kutoa elimu kwa watoto, vijana pamoja na wazazi wao kuelewa umuhimu wa kujiwekea akiba ya fedha kupitia akaunti mbali mbali za benki hiyo, kama vile Mtoto Account, Chipukizi Account na Mwanachuo Account. NMB katika ziara hiyo ambapo ilikuwa imeongozana na wachezaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Azam kupitia kituo chao cha michezo, mbali na anafunzi na wazazi kupata elimu ya masuala ya kifedha na uwekaji akiba kwa manufaa ya baadaye, wachezaji wa Azam walicheza mpira na wanafunzi hao pamoja na kugawa zawadi mbalimbali toka NMB na kampuni ya Azam.  



Picha ya pamoja ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes na wageni wao baada ya mafunzo ya programu ya wajibu iliyotolewa na Benki ya NMB.


Ofisa wa Benki ya NMB Tawi la Temeke, Latifa Ayoub Dadah (kushoto) akimkabidhi zawadi mmoja wa wazazi wa wanafunzi walioshiriki mafunzo ya programu ya wajibu ya NMB.


Ofisa wa Benki ya NMB Tawi la Temeke, Latifa Ayoub Dadah (kulia) akimkabidhi moja ya zawadi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes baada ya kujibu vizuri swali kwenye mafunzo ya programu ya wajibu. Akifafanua zaidi, Bi. Latifa alisema elimu hiyo ni mwendelezo wa programu ya wajibu ambapo NMB imekuwa akizunguka katika shule mbalimbali za msingi na sekondari nchi nzima huku ikitoa elimu ya kifedha na masuala mazima ya uwekaji akiba. Alisema elimu hiyo itawasaidia watoto na vijana kufanya matumizi mazuri ya fedha kwa sasa na baadae, elimu ambayo wengi wameikosa. Alisema elimu hiyo ambayo imepokelewa vizuri kwa wanafunzi na wazazi ambao wameshiriki itaendelea kutolewa na benki hiyo hivyo kuwashauri wazazi na vijana kufungua akaunti mbalimbali ya NMB kulingana na maitaji yao ili waweze kunufaika. 

"...Mwitikio kwa waliopata fursa ya kushiriki katika mafunzo haya ni mzuri kwa kwli hasa katika wilaya yetu ya Temeke, tumekuwa tukipokea watoto mbalimbali wakija kufungua akaunti jambo ambalo linaonesha wamevutiwa na elimu hii," alisema ofisa huyo wa Benki ya NMB Tawi la Temeke. Naye Mwalimu wa Taaluma wa Shule ya Msingi Wailes, Zabibu Wasia aliishukuru Benki ya NMB kwa kutoa mafunzo hayo kwa wanafunzi pamoja na baadhi ya wazazi/walezi wa shule hiyo na kuahidi kuendelea kuwa mabalozi kueneza elimu hiyo kwa wengine kutokana na umuhimu wake.

 "..Tunaishukuru sana NMB kwa kuamua kuleta elimu hiyo kwa wanafunzi na wazazi wa Wailes tunaamini hii ni fursa ya kipekee kwetu maana shule za msingi Dar es Salaam zipo nyingi lakini umeona muanze na sisi...tunashukuru sana kwa kutupendelea," alisema Bi. Wasia. Mbali na elimu hiyo NMB ilitoa mipira miwili kama zawadi kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes, yaani mpira wa miguu kwa wanafunzi wa kiume na mpira wa pete kwa wanafunzi wa kike.  

Mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes akijibu swali kwenye mafunzo ya programu ya wajibu iliyotolewa na Benki ya NMB shuleni hapo.



Baadhi ya wachezaji vijana wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Azam kupitia kituo chao cha michezo wakiwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes.

Ofisa wa Benki ya NMB Tawi la Temeke, Latifa Ayoub Dadah (kulia) akitoa elimu ya masuala ya kifedha na akiba kwa wazazi na wanafunzi walioshiriki mafunzo ya programu ya wajibu ya NMB katika Shule ya Msingi Wailes ya jijini Dar es Salaam.


Mmoja wa wachezaji vijana (kulia) wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Azam akipiga mpira alipokuwa akicheza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes ya jijini Dar es Salaam.

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.