Articles by "Jamii"

Showing posts with label Jamii. Show all posts


Travis Kalanick, the chief executive and co-founder of Uber Technologies Inc., apologized late Tuesday after a video surfaced of him getting into a shouting match with one of his company’s drivers, and said that he needed leadership help.
Travis Kalanick, chief executive officer of Uber Technologies Inc.

The argument was captured on the dash cam of Uber driver Fawzi Kamel during a drive in San Francisco on Feb. 5. In it, Kamel complains about how Uber’s lower fares have hurt his income.

“I lost money — $7,000 — because of you,” Kamel said. “I’m bankrupt because of you.”

“Bulls—,” Kalanick replied. “You know what. . . some people don’t like to take responsibility for their own s—,” Kalanick said before slamming the door on his way out. “They blame everything in their life on someone else.”

“To say that I am ashamed is an extreme understatement,” Kalanick said in a statement to employees Tuesday. “My job as your leader is to lead…and that starts with behaving in a way that makes us all proud. That is not what I did, and it cannot be explained away.

“It’s clear this video is a reflection of me — and the criticism we’ve received is a stark reminder that I must fundamentally change as a leader and grow up. This is the first time I’ve been willing to admit that I need leadership help and I intend to get it.

“I want to profoundly apologize to Fawzi, as well as the driver and rider community, and to the Uber team.”
The apology caps a rough month for Uber and Kalanick. Early in February, an estimated 200,000 people deleted its app in an online protest over Uber’s actions during protests at New York’s JFK airport, pressuring Kalanick to quit President Donald Trump’s economic advisory board.

On Feb. 19, a former Uber engineer accused the company of rampant sexual harassment and bias, and more stories of an out-of-control workplace soon emerged. Kalanick announced an investigation, led by former U.S. Attorney General Eric Holder, into its corporate climate. And Monday, Uber fired a software executive for failing to disclose sexual harassment allegations against him at his former job.



























































Shirika la kisheria lisilo la kiserikali la Legal Services Facility (LSF) wiki hii litatoa msaada wa komputa 176 zenye thamani ya shilingi million 146 kwa ajili ya vituo 160 vya wasaidizi wa kisheria vilivyoko mikoani—kama sehemu ya mkakati wake wa kuongeza ufanisi na kuboresha utoaji wa huduma za kisheria nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari hivi karibuni, komputa hizo zitatolewa wakati wa warsha (itakayofanyika Ijumaa hii Dar es Salaam) kwa viongozi wa mashirika yasiyo ya kiserikali yanayotoa msaada wa sheria na yanayofadhiliwa na LSF—kutekeleza miradi ya wasaidizi wa kisheria nchini.

Bw Kees Groenendijk, Meneja wa LSF, alisema komputa ni zana muhimu kwa vituo vya wasaidizi wa kisheria na wasaidizi wa kisheria wenyewe wanaotoa msaada wa kisheria nchini. Tangu kuanzishwa kwake miaka mitano iliyopita, LSF imekwishatoa ufadhili wa mabilioni ya fedha, ambazo, pamoja na mambo mengine, zimerahisisha kuanzishwa kwa vituo vya wasaidizi wa kisheria sehemu mbalimbali nchini.
Image result for legal services facility tanzania-Kees Groenendijk,
Mkurugenzi wa Shirika la Legal Services Facility (LSF), Bwana. Kees Groenendijk akizungumza  leo Jijini Dar es Salaam

“Ni ukweli usiopingika kwamba wasaidizi wa kisheria wamekuwa wakifanya vizuri sana linapokuja suala la kuwasaidia wanaohitaji msaada wa kisheria hasa vijijini. Ndiyo maana tumeamua kutoa hizi zana, ambazo naamini vitaongeza ufanisi wa huduma za kisheria. Naamini zitaongeza ufanisi na utendaji wa wasaidizi wa kisheria na vituo vya wasaidizi wa kisheria,” alisema Bw Groenendijk.

Komputa zitatolewa kwa mashirika yasiyo ya kiserikali 27 yanayotoa msaada wa sheria, ambayo ndiyo yatakayotoa hizo komputa kwa vituo vya wasaidizi wa kisheria katika maeneo yao ya kazi. Mashirika yasiyo ya kiserikali yanayotoa msaada wa sheria yametoa mchango mkubwa sana katika uanzishwaji wa vituo vya wasaidizi wa kisheria kupitia ufadhili wa LSF.

Kwa mujibu wa taarifa ya LSF, warsha inayofanyika wiki hii itatoa nafasi kwa washiriki kujadili mambo mbalimbali na changamoto zake katika kutekeleza miradi inayofadhiliwa na LSF na kupata suluhisho.

Pamoja na hayo, warsha hiyo itawezesha LSF kuelezea njia mkakati yake ya 2016-2021, nini LSF inataka kupata na matokeo yake kwa mashirika yasiyo ya kisherikali yanayotoa ushauri wa kitaalam (RMOs). Masuala mengine yanahudu namna ya kutatua migongano kati ya malengo ya kitaasisi ya RMOs na malengo mkakati ya LSF na namna ya kuongeza matokeo.

Kutakuwa na majadiliano pia juu ya kuyajengea uwezo mashirika yanayofadhiliwa na LSF/yanayotoa ushauri wa kitaalam, namna ya kujenga uwezo kwa wasaidizi wa kisheria na LSF, umuhimu wa kupima kazi na matokeo yake na kuripoti kwa njia ya mtandao.


PRISCA Shaaban Mpesya (29), mkazi wa Kitongoji cha Kikonde, Kijiji cha Kaoze katika Kata na Tarafa ya Kipeta wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, alikuwa analia kimya kimya.
Bi Prisca akiwa na jeraha kichwani.JPG
Alimtazama mwanaye Baraka (6) aliyening’iniza mkono wa kulia huku akilia kwa maumivu baada ya kukatwa kitanga cha mkono na ‘watu wasiojulikana’ wanaosaka utajiri, kwa sababu yeye ni albino na wanadai viungo vyake ni ‘dili’.

Kwa Prisca, kuzaa watoto wenye albinism inaonekana ni majanga kwake na kizazi chake, hasa katika kipindi ambacho matukio ya mauaji, kutekwa nyara na kukatwa viungo vya albino yameshamiri Tanzania na Afrika Mashariki na Kati.
Barakaaa.JPG
Anajaribu kukumbuka tukio hilo la usiku wa Jumamosi, Machi 7, 2015 alivyonusurika kufa yeye na mwanaye Baraka.

“Nilikuwa natoka nje kwenda kujisaidia, sijui ilikuwa saa ngapi kwa sababu sikuwa na saa, nje juu ya mlango tuliweka taa ya Mchina ya solar ambayo ilikuwa inaangaza, hivyo sikuwa na hofu,” ndivyo anavyoanza kumsimulia mwandishi wa makala haya wakati alipokuwa amelazwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Anasema ghafla tu alipofika mlangoni akashtuka kuona mtu akija mbio, akaipiga taa na kuivunja, kukawa giza.

“Nikajua huyu hakuwa mwema, hivyo nikajiandaa kupambana naye, alikuwa mwanamume mwenye nguvu kunishinda, lakini nilimdhibiti kwa sababu alitaka kuingia ndani kwa nguvu nami sikutaka kwa sababu wanangu walikuwa wamelala chini angeweza kuwaumiza.

“Mara nikasikia kitu kikinipiga kichwani pa! Nikaanguka na kupoteza fahamu. Nilipozinduka nikamwona mwanangu Baraka analia, kitanga cha mkono kimekatwa.” Akaongeza: “Natamani watu wanaofanya mambo haya wauawe hadharani.”

Anasema, mumewe Cosmas Yoramu Songoloka hakuwepo kwani alikuwa ameaga tangu mchana kwamba anakwenda kilabuni kunywa pombe, na mpaka majira hayo hakujua kama alikuwa kilabuni ama alikwenda kwa mke mdogo ingawa haikuwa zamu yake.

Baraka Cosmas Yoramu alikatwa kitanga cha mkono wa kulia na watu ‘wasiojulikana’ Machi 7, 2015 majira ya saa 2 usiku kwa imani za kujipatia utajiri wa kishirikina.

Jitihada za kupata tiba katika kituo cha afya Kamsamba wilayani Sumbawanga zilishindikana, hivyo kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya.

Prisca anasema, pamoja na ujauzito aliokuwa nao wakati huo, lakini hakuhisi chochote zaidi ya kuwalinda wanawe, zawadi pekee aliyopewa na Mwenyezi Mungu.

“Nimehangaika na mimba zao kwa nyakati tofauti, sikuwa tayari kuona wanapata madhara, ndiyo maana niliisahau hata hali yangu nikaamua kupambana,” anasema.

Maumivu ya jeraha lake la kichwani alilopata kwa kupigwa na ‘kitu kizito’ yalionekana siyo kitu kwa wakati huo, kwa sababu binti yake Lucia (3) ambaye ana albinism pia alikuwa anamsumbua hospitalini, na kwa umri wake, alikuwa hajui kinachoendelea.

Lakini kubwa zaidi ni kwamba, mwanaye mchanga wa kiume aliye albino, ambaye ndiyo kwanza alikuwa ametoka kujifungua, naye alikuwa analia akitaka kunyonya.

Sasa anao watoto watatu wenye albinism kati ya wanne, akiwemo huyo mdogo ambaye kwa sasa ametimiza mwaka mmoja na nusu tangu alipozaliwa Aprili 2015 kwenye Hospitali ya Rufaa Mbeya wakati akiuguza jeraha lake kichwani pamoja na kumuuguza mwanaye Baraka jeraha la mkono.

Bi. Prisca alifikishwa hospitalini hapo Machi 8, 2015 huku akiwa amembeba mwanaye Lucia na mimba ya miezi karibu nane ikiwa imemuelemea.

“Nisingeweza kumwacha Lucia kule porini kwa sababu watu wabaya wangeweza kumjia,” alisema.

Mtoto wake mkubwa, Shukuru (8), alimwacha kijijini huku mumewe Cosmas akiwa mahabusu kuhusiana na tukio hilo.

Mwandishi wa makala haya, ambaye amefanya utafiti wa mauaji ya albino kwa miezi nane mfululizo, alipiga kambi mjini Sumbawanga kwa takriban miezi miwili na kushuhudia maofisa wa polisi walivyowakamata wahusika wa tukio hilo, akiwemo Sajenti Kalinga Malonji, ‘tajiri’ ambaye ndiye aliyepelekewa kiganja hicho na kuahidi kuwapatia wenzake mamilioni ya fedha

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Mushi (kushoto) akimkabidhi mmoja wa watoto wa kituo cha yatima 'Yatima Group Trust Fund Mbagala Chamazi mfuko wa unga, . TTCL imekabidhi msaada wa bidhaa mbalimbali vikiwemo mchele, sukari, mafuta ya kupikia, soda, maji ya kunywa na mbuzi kwa ajili ya sherehe za Siku Kuu ya Chrismass. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa  Kituo cha Yatima Group Trust Fund Mbagala Chamazi.


Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Mushi (wa pili kushoto) akimkabidhi mbuzi Mkurugenzi Msaidizi wa  Kituo cha Yatima Group Trust Fund Mbagala Chamazi. TTCL imekabidhi msaada wa bidhaa mbalimbali vikiwemo mchele, sukari, mafuta ya kupikia, soda, maji ya kunywa na mbuzi kwa ajili ya sherehe za Siku Kuu ya Chrismass. 


Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Mushi (wa tatu kulia) akimkabidhi mmoja wa watoto wa kituo cha watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi cha Kimara SUCA maji ikiwa ni moja ya bidhaa zilizotolewa. TTCL imekabidhi msaada wa bidhaa mbalimbali vikiwemo mchele, sukari, mafuta ya kupikia, soda, maji ya kunywa na mbuzi kwa ajili ya sherehe za Siku Kuu ya Chrismass. 


Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Mushi (kushoto) akimkabidhi mfuko wa unga Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi cha Kimara SUCA, Evans Tegete ikiwa ni baadhi ya msaada uliotolewa na kampuni hiyo. TTCL imekabidhi msaada wa bidhaa mbalimbali vikiwemo mchele, sukari, mafuta ya kupikia, soda, maji ya kunywa na mbuzi kwa ajili ya sherehe za Siku Kuu ya Chrismass. 


Picha ya pamoja ya baadhi ya watoto kutoka vituo vyote vilivyosaidiwa na viongozi wao. 


Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Mushi (wa pili kushoto) akimkabidhi mbuzi mmoja wa watoto wa kituo cha watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi cha Kimara SUCA. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho, Evans Tegete.


Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Mushi (kushoto) akimkabidhi mmoja wa watoto wa kituo cha yatima 'Yatima Group Trust Fund Mbagala Chamazi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya TTCL kwa ajili ya sherehe za Siku Kuu ya Chrismass. 


Picha ya pamoja baada ya shughuli ya kukabidhi misaada hiyo.


Baadhi ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu wakibeba sehemu ya misaada waliyokabidhiwa na TTCL.


Mchungaji mmoja huko nchini Afrika Kusini, Lethebo Rabalago anatumiwa dawa ya mbu ya kupuliza kama njia ya uponyaji kwa waumini wake wanaokwenda kanisani kwake kwa ajili ya maombi ya matatizo mbalimbali ya kiroho.Image result for lethebo rabalago
 
Mchungaji anaamini kwamba dawa hiyo ya mbu ya kupuliza inaweza kumponya mwanadamu na kumwezesha mtu kupata upako wa bwana baada ya kuombewa na kupuliziwa kama sehemu ya ufunuo wa kutoka kwenye dimbwi la dhambi na mikosi.
 
Lethebo Rabalago, kutoka kwenye kanisa la Mount Zion General Assembly (MZGA) katika mji wa Limpopo, alituma picha kwenye mitandao ya kijamii kama vile Facebook na kuonyesha akitumia dawa hiyo kali ya kuua mbu kama nyenzo yake ya uponyaji.
 
Siku chache zilizopita kwenye mitandao ya kijamii kulijaa taarifa za mchungaji huyo anayetumia dawa hiyo ya mbu kama njia ya uponyaji kwa waumini wake hapo kanisani, baada ya kutuma picha hizo mijadala ilikuwa ikiendelea kwenye mitandao sehemu kubwa ya Afrika kuhus aina hiyo ya maombezi.
 
Mmoja wa waumini aliyepitia huduma alinukuliwa akisema kwamba “Nilikuja hapa na maumivu sehemu ya nyuma na tumbo, lakini sasa baaada ya maombezi ya mchungaji nimepata uponyaji wa kutosha na pua yangu iliumia tangu wiki iliyopita na baada ya mchungaji kuniombea na kunipuliza dawa nimepata nafuu kubwa,” alinukuliwa akisema.

SPIKA Mstaafu, Anna Makinda ameiomba serikali na mamlaka husika kuanza mchakato wa kusukuma mabadiliko ya sheria ya ndoa ili kupanua wigo wa haki za wanawake na watoto nchini.
 
Image result for ndoa
 
Akizungumza katika kongamano la wanawake lilioandaliwa na Mfuko wa msaada wa kisheria nchini (LSF) jana jijini Dar es Salaam, Makinda alisema kwamba sheria ya ndoa ya mwaka 1971 imepitwa na wakati na inahitaji marekebisho makubwa ili kutoa haki kwa wanawake nchini.
 
“Hii sheria ya ndoa inawatenga sana wanawake nchini katika swala la mirathi na kuacha watoto wengi wakiteseka ni wakati muafaka sasa kwa wanaharakati kusaidia na wabunge ili kuleta marekebisho hayo kwa manufaa ya nchini nzima,” alisema Makinda ambaye ni spika mstaafu.
 
Alisema kwamba marekebisho hayo makubwa au kuandikwa upya kwa sheria ya ndoa itakuwa hatua moja kubwa katika kulinda haki za wanawake za kumiliki mali, kama vile mashamba na kadhalika.
 
Alisisitiza kwamba swala la mirathi ni tatizo kubwa sana nchini ambapo wanawake wengi wamepoteza mali zao walizochuma na wenzi wao wakati wa ndoa.
 
“Nikiwa mbunge, waziri na baadaye spika tulipambana vikali katika kubadilisha sheria ya ardhi ili kuwapa watu wa hali ya chini kupata nafasi ya kumiliki ardhi, sasa na hii sheria ya ndoa inapaswa kushughulikiwa kwa haraka ili kuweza kutoa matokeo chanya kwa jamii,” aliongeza.
 
Alifafanua kwamba marekebisho hayo ya sheria ya ndoa yatasaidia kunusuru maelfu ya wanawake ambao wanateseka kutokana na kila aina ya unyanyasaji wa kijinsia na vipigo ambavyo vinaongezeka kila kona ya nchini.
 
Aliomba mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kushirikiana na serikali katika majadiliano hasa katika mambo ya mirathi na ndoa ili kuhakikisha upatikanaji wa marekebisho hayo yanapatikana haraka.
 
“ni muhimu pia maswala haya ya haki za wanawake na watoto kufundishwa katika shule za msingi na sekondari ili kupeleka elimu hiyo ya uraia kwa wanafunzi nchini nzima, ila ni muhimu kushirikiana na serikali ili kufanikisha hayo,” aliongeza 
 
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu, Mfuko wa Msaada wa Kisheria (LSF), Bw, Kees Groenendijk alisema kwamba mfuko lengo lake kuu ni kuongeza haki na usawa kwa wanawake nchini kupitia uwezeshaji wa fedha na mafunzo.
 
“Kutokana na mustadha huo, mfuko uliamua kwamba mfuko kusaidia mashirika yasiyo kuwa ya kiserikali yanayotoa msaada wa kisheria kwa jamii hasa wanawake ambao wapo katika wilay zote za Tanzania Bara,” alisisitiza.
 
Alisema tangu mfuko huo uanze zaidi ya wanawake 2,000 walifikiwa kwa msaada wa kisheria ambao ni asilimia 60% ya wanawake nchini nzima.
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) Bi, Tike Mwambipile alisema kwamba serikali ni lazima kuanzisha kitengo maalum cha kushughulikia matatizo ya ndoa na mirathi katika mifumo ya utoaji haki nchini.

UMOJA wa Nchi za Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wameweka nguvu ya pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Ruaha kwenye semina iliyoelezea malengo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani ambapo kati ya hao, vijana 50 wamepata semina ya mwongozo wa kuwa mabalozi wa malengo hayo (Global Goals Champions). Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania. 


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa misaada ya maendeleo UNDAP II 2016-2021 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akifafanua jambo juu ya ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Mpango wa misaada ya Maendeleo 2016-2021 (UNDAP II) kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa
Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa, Martin Noel akiwa ameongozana Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano chuoni hapo sambamba Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendesha semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia.

Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akielezea fursa za ufadhili wa masomo nje ya nchi katika tovuti ya Umoja wa Ulaya Tanzania wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia iliyofadhiliwa na EU.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akiwapiga msasa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia kwenye semina hiyo iliyofadhiliwa na EU.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akiwa amejumuika na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia ambapo semina hiyo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) nchini.
Pichani juu na chini ni vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha walioshiriki semina maalum ya kuwa mabalozi wa malengo ya dunia (Global Goals Champions) iliyoandaliwa na UN na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) akimkabidhi cheti Rais wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa Athman Waziri aliyehitimu kuwa balozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champion).
Picha juu na chini Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendelea na zoezi la kutunuku vyeti kwa mabalozi wa malengo ya dunia kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champions) baada ya kuhitimisha semina maalum iliyoshirikisha vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Martin Noel baada ya kuhitimisha semina ya malengo ya dunia mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Afisa Habari wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU), Muazarau Matola
Baadhi ya Global Goals Champions katika picha ya kumbukumbu na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akibadilishana mawazo na wahitimu wa semina malengo ya dunia (Global Goals Champions) mara baada ya kuhitimisha semina hiyo iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Ruaha mjini Iringa ambapo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).


Alhamisi ya Septemba, 15 inaingia katika historia ya mjasiriamali, Jacqueline Mengi kwa kufanya uzinduzi wa duka la samani za ndani la Molocaho Amorette likiwa na vitu ambavyo ni vya pekee kutokana na aina ya malighafi ambayo wametumia kutengeneza.

Akizungumzia duka hilo, Bi.Mengi alisema kuwa ilikuwa ni ndoto yake ya muda mrefu ya kutaka siku moja kuwa na duka kama hilo ambalo litakuwa na samani ambazo ni ngumu kuzipata sehemu nyingine kutokana na kutengenezwa tofauti na samani nyingi ambazo zinapatikana madukani.

"Siamini kama ndoto yangu imetia, kwa kipindi cha miaka iliyopita kuna vitu nilikuwa nikitamani kuwa navyo nyumbani lakini sikuweza kuvipata nilipokuwa nikitafuta na hapo ndipo ndoto za kuwa na duka zilipoanzia,

"Nilikuwa nataka kitu cha tofauti ambacho ni ngumu kukikuta sehemu nyingine kutokana na kuwa na ubunifu wa kipekee ambao utawavutia wateja wa ndani ya nchi na nje ya nchi na ninaamini watafurahia," alisema Bi. Mengi.

Aidha Bi. Mengi alisema kuwa bidhaa ambazo zitakuwa zikipatikana katika duka la Molocaho - Amorette zimetengenezwa na malighafi kutoka Tanzania kama mbao za Mninga na hivyo kuwataka Watanzania kuwa wazalendo kwa kutumia bidaa ambayo imetengenezwa na malighafi za Tanzania.

Mmoja wa wageni waliohudhuria halfa ya uzinduzi, Faraja Nyalandu alisema kuwa kwa kijana kama Jacqueline Mengi kuwa na duka kama hilo ni hatua kubwa ambayo vijana wengi wanatamani kuifikia, kumpongeza kwa juhudi alizozifanya lakini pia kutoa ushauri kwa wengine ambao wanataka kufanikiwa.

"Kwanza nimpongeze Jacqueline amefanya uthubutu na amefanikiwa kuwa na kitu kama hiki, juhudi yake inaonyesha kuwa kila mtu tu anaweza kufanikiwa kama akiongeza juhudi katika jambo analotaka kulifanya," alisema Bi. Nyalandu.

Duka hilo la kisasa na la aina yake linapatikana Masaki karibu na hoteli ya Sea Cliff kwenye jengo la "Village Walk" gorofa ya kwanza.

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na wageni walikwa pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa duka lake la samani za ndani "Amorette" lililopo katika jengo la Village Walk gorofa ya kwanza karibu na Sea Cliff Hotel, Masaki jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa nje utaokutambulisha hili ndio duka la "Amorette"
Bi. Jacqueline Mengi akikata utepe kuzindua duka lake hilo.
Ha ha ha ha, sasa mko huru kuingia wageni waalikwa kujionea yaliyomo,.....Bi. Jacqueline Mengi akifurahi jambo mara baada ya kukata utepe.
Bi. Jacqueline Mengi akiongozana na baadhi ya wageni waalikwa kuingia ndani ya duka la "Amorette"
Balozi Juma Mwapachu na baadhi ya wageni waalikwa wakiangalia moja ya meza ya chakula (dining table) iliyotengenezwa kwa mbao aina ya Mninga baada ya kuzinduliwa duka hilo lililopo katika jengo la Village Walk, Masaki jijini Dar.
Wageni waalikwa wakiendelea kukagua samani mbalimbali katika duka hilo.
Bi. Jacqueline Mengi akiwaonyesha mambo mazuri yaliyomo katika duka la Amorette baadhi marafiki waliohudhuria uzinduzi huo.
Bi. Jacqueline Mengi akizungumza jambo na Balozi Juma Mwapachu wakati akiwatembeza wageni waalikwa katika maeneo mbalimbali ndani ya duka lake la Amorette.
Wageni waalika wakiangalia moja ya kitanda cha aina yake kinachouzwa katika duka la Amorette lililopo katika jengo la Village Walk, Masaki jijini Dar es Salaam.
Sehemu maalum ya kitanda hicho ya kuhifadhia mashuka, Blanket pamoja na mito.
Bi. Jacqueline Mengi akipozi katika moja ya samani ndani ya duka lake la Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi katika pozi matata ndani ya duka lake la Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuzindua duka lake la samani za ndani la Amorette.
Wanahabari na wageni waalikwa wakiwa ndani ya duka la Amorette kujionea bidhaa mbalimbali.
Wageni waalikwa wakiendelea kutazama kitanda hicho cha aina yake.
Sophia Byanaku akijinafasi katika moja ya samani zilizomo kwenye duka la Amorette.
Mmoja wa wageni waalikwa akitazama bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa kwa mbao aina ya Mninga ndani ya duka la Amorette.
Baadhi ya samani zilizomo ndani ya duka la Amorette.
Balozi Juma Mwapachu (kushoto) akibadilishana mawazo na mwalikwa mwenzake kwenye uzinduzi wa duka la Amorette.
Mwanadada Monica Joseph akipozi kwenye moja ya bidhaa zilizopo ndani ya duka la Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi akipozi kwenye samani moja wapo inayopatikana katika duka lake la Amorette.
Warembo wakiwa wamepozi kwenye samani zinazopatikana katika duka la Amorette lililopo ndani ya jengo la Village Walk, Masaki jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa wakibadilishana mawazo ndani ya duka la Molocaho-Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi akiwa kwenye picha ya pamoja na rafiki zake.
Bi. Jacqueline Mengi akibadilishana mawazo na baadhi ya marafiki zake.
Mkurugenzi wa Dorice Mollel Foundation, Dorice Mollel (kulia) katika picha ya pamoja na Mdau Monica Joseph.
Bi. Jacqueline Mengi katika picha ya pamoja na Dorice Mollel.

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.