RAIS na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuanzia Septemba 21.

Katika vyeo vipya hivyo ni pamoja na cheo kimoja cha Luteni Jenerali, Meja Jenerali 15 na Brigedia Jenerali 33.

Akizungumza Makao Makuu ya Jeshi muda mfupi kabla ya kuwavisha cheo kipya maofisa hao, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange alisema: “Rais amempandisha cheo Meja Jenerali Samuel Ndomba kuwa Luteni Jenerali”.

Rais pia amemteua Luteni Jenerali Ndomba kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ kuziba  nafasi  iliyoachwa wazi na Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo aliyestaafu utumishi jeshini kwa umri Septemba 21.

Kwa mujibu wa kanuni na sheria za Majeshi katika Juzuu la kwanza (Utawala) Jenerali Mwamunyange alimvisha cheo cha Luteni Jenerali, Ndomba kwa niaba ya Rais na Amir Jeshi Mkuu. Kabla ya uteuzi huo mpya, Luteni Jenerali Ndomba alikuwa Mkuu wa Jeshi la KujengaTaifa (JKT).

Katika hafla hiyo fupi, Jenerali Mwamunyange alisema kuwa Rais Kikwete alimpandisha cheo Brigedia Jenerali Rafael Muhuga kuwa Meja Jenerali kuanzia Septemba 21 na kumteua kuwa Mkuu mpya wa JKT.

Kabla ya madaraka hayo mapya, Meja Jenerali Muhuga alikuwa Mkuu wa Utawala wa JKT na amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Jenerali Ndomba. Jenerali Mwamunyange alimvisha cheo hicho kipya kwa niaba ya Rais na Amir Jeshi Mkuu.

Wakati huo huo, makamanda wengine waliopandishwa vyeo kutoka Brigedia Jenerali na kuwa Meja Jenerali wakiwamo maofisa wanawake; Grace Mwakipunda ambaye kwa sasa ni Kaimu Mkuu wa Utumishi Jeshini na Lilian Kingazi ambaye ni Mkurugenzi wa Utumishi Jeshini. Wengine ni Farah Mohamed, Kevin Msemwa,  Patrick Mlowezi, Charles Jitenga, Charles Mzanila na Daniel Igoti.

Makamanda wengine ni Vincent Mritaba, Ipanda Ipanda, Adam Mwabulanga, Ezekiel Kyunga, Projest Rwegasira na Juma Kapwani.

Aidha, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi aliwavisha vyeo vipya makamanda 33 waliokuwa na cheo cha Kanali kuwa Brigedia Jenerali ambao ni Pellegrin Mrope, Ryakitimbo Ryakitimbo, Mimy Abdallah, John Chacha, Ezira Ndimbwambo na Augostino Gailanga.

Wengine ni Gaudence Milanzi, Masumbuko Mndeme, Daniel Laswai, Sarah Rwambali, Mathew Sukambi, Narcis Lubamba, Mwapipo Kyalaliko, O. S. Mateka na   Jairo Mwaseba.

Mabrigedia Jenerali wengine ni Abdullah Mwenjudi, Cosmas Kayombo, Honoratus Lyamba, Ramadhani Kimweri, Nicodem Mwangela, Abbas Mnyani,  R.A. Rukyaa,  Elias Athanas, Fabiani Mangore,  George Mashamba,  Zoma Kongo, Harison Masebo, Paul Masao, Clemence Kahama,  Jacob Mohamed,  Mbazi Msuya, Alfred  Kapinga na George Ingrim.

Akitoa neno la shukurani kwa niaba ya makamanda wenzake wa ngazi za juu waliopandishwa vyeo, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi Luteni Jenerali Ndomba alimweleza Mkuu wa Majeshi kuwa kwa pamoja walitambua majukumu yaliyo mbele yao na aliahidi kuwa watayatekeleza kikamilifu.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.