July 2015

By Fidelis Butahe na Mbonile Borton, Mwananchi
 
Dar es Salaam. Kada mpya wa Chadema, Edward Lowassa jana alichukua tena fomu ya kuwania urais lakini safari hii si kwa tiketi ya CCM, katika hafla ambayo ilishuhudiwa na umati mkubwa wa watu uliosababisha Mtaa wa Ufipa kufungwa kwa saa tatu.
Hafla hiyo pia ilitawaliwa na matukio mengi, likiwamo la waziri huyo mkuu wa zamani kuanza rasmi kutumia kaulimbiu ya Chadema ya People’s Power huku akinyoosha juu mkono uliokunja ngumi na kusababisha umati huo kulipuka kelele za shangwe.
Lowassa, ambaye Jumanne wiki hii alitangaza rasmi kujiondoa CCM na kujiunga na Chadema, alikabidhiwa fomu ya kugombea urais na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ambaye alifanya kazi hiyo badala ya Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa ambaye kwa mara nyingine hakuonekana kwenye tukio kubwa la chama hicho.
Katika hafla hiyo fupi, Lowassa ambaye wanachama walimchangia Sh1 milioni kwa ajili ya kuchukua fomu za kuwania urais, alitumia dakika nne kuzungumza, huku akiwashukia wanaomshambulia kuwa kujiunga kwake Chadema kunatokana na uroho wake wa madaraka.
“Wanapoteza muda na hawataniyumbisha,” alisema mbunge huyo wa Monduli.
Lowassa, aliyekuwa amevaa shati jeupe na suruali nyeusi na aliyekuwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser VX, alifika makao makuu ya Chadema saa 6:40 mchana akiwa pamoja na mkewe, Regina na familia yake na alipokewa na umati mkubwa wa watu waliokuwa wakiimba “rais, rais, rais… tuna imani na Lowassa, oya oya oya”.
Mara baada ya kushuka, Lowassa aliwapungia watu hao mkono huku akitabasamu, hali iliyosababisha kila mtu kutaka kumshika mkono jambo ambalo liliwapa wakati mgumu walinzi wa chama hicho, wanaojulikana kwa jina la Red Brigade.
Mbali na familia yake, Lowassa alisindikizwa na mbunge wa Arumeru Magharibi (CCM), Goodluck Ole Medeye na kada mkongwe wa CCM, Madson Chizii.
Watu wa rika mbalimbali walijaa kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho zilizopo Mtaa wa Ufipa na baadhi walitumia simu za mkononi kuchukua picha za tukio hilo.
Hali hiyo ilisababisha mtaa huo kufungwa huku wenye magari wakitakiwa na walinzi wa chama hicho kutafuta njia nyingine, kwa maelezo kuwa “rais wa nchi” anachukua fomu.
Wakati Lowassa akiwa ndani, watu hao waliendelea kushangilia na kuimba nyimbo mbalimbali nje ya ofisi hiyo, hasa walipomuona akizungumza na Tundu Lissu.
‘Yes We Can’
Katika hotuba yake Lowassa, alisema wakati wa kuing’oa CCM ni sasa na kutumia kaulimbiu ya “Yes We Can (Ndio Tunaweza)” iliyotumiwa na Rais wa sasa wa Marekani, Barack Obama wakati akiomba kura za Wamarekani kwa mara ya kwanza kuongoza nchi hiyo
.
“Nashukuru kwa mapokezi mliyonipa ninawashukuru walionichangia fedha za kuchukua fomu. Ninafurahi kwa heshima mliyonipa, heshima hii haina maelezo ya shukrani kusema nashukuru tu haitoshi ila kazi nitakayowatendea ndiyo itakuwa shukrani,” alisema Lowassa ambaye alijiuzulu uwaziri mkuu mwaka 2008.
“Najiandaa kufanya kazi iliyotukuka na itakayotuletea ushindi sisi (Chadema) na Watanzania.”
Lowassa aliwataka wananchi kujiandikisha katika daftari la wapigakura ili waweze kumchagua kiongozi wanayempenda.
“Mliojiandikisha mnatakiwa kutunza shahada zenu kungoja tarehe ya uchaguzi. Uchaguzi huu utakuwa ni namba tu (wingi wa kura), kama alivyosema (mwanasheria wa Chadema, Tundu) Lissu kuhusu kushinda ubunge na urais. Tunaweza kupata kura hizo mimi nina uhakika huo,” alisema.
Alisema anachokifanya sasa ni kutekeleza maelezo ya Mwalimu Julius Nyerere kuwa Watanzania wasipoyapata mabadiliko ndani ya CCM, watayatafuta nje ya chama hicho. “Mimi nimeridhika kwamba ndani ya CCM mabadiliko hayo hayawezekani kupatikana, lakini nimeridhika kuwa Watanzania wanataka mabadiliko na watayapata kwa kura zetu. Watanzania wanaotaka mabadiliko ni wengi naamini tukijipanga vizuri tutashinda uchaguzi huu bila matatizo yeyote,” alisema.
Alisema ushindi huo utapatikana bila kutumia lugha za matusi, kejeli na kwamba ustaarabu na kutoa hoja za msingi ndio chachu ya ushindi huo.
“Rais Barack Obama alipokuwa akigombea urais kwa mara ya kwanza aliwauliza wenzake ‘can we (tunaweza)?’, wakamjibu ‘yes we can (ndio tunaweza)’. Na mimi nataka kuwambia wenzangu ndio tunaweza,” alisema.
Kauli ya kuunganisha Chadema
Kabla ya Lowassa kuzungumza, Mbowe alisema kuwa kada huyo wa zamani wa CCM hawezi kueleweka kwa wanachama iwapo hatasema kaulimbiu ya chama hicho ya People’s Powe, inayomaanisha Nguvu ya Umma, akisema ndiyo inayowaunganisha wana-Chadema.
Baada ya Lowassa kutamka neno hilo, alishangiliwa na watu waliojazana eneo hilo ambao walimtaka arudie. Baadaye Mbowe alisema sasa amekuwa kamanda rasmi ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini.
“Tunaendelea kuwa pamoja kuandika historia,” alisema Mbowe. “Naomba kuwahakikishia jambo moja la msingi, Chadema ni chama makini na kitaendelea kuwa chama makini chenye kusheshimu, katiba, kanuni na maadili yake.”
Akizungumzia vikao vya kikatiba vya chama hicho, Mbowe alisema Agosti 2 kitafanyika kikao cha Kamati Kuu ambacho kitaanza kujadili fomu za mgombea na Agosti 3 kutakuwa na mkutano wa Baraza Kuu ambalo pamoja na mambo mengine litachambua ilani ya chama kuelekea uchaguzi mkuu, ushirikiano wa vyama vinavyounda Ukawa na kuchambua fomu za mgombea urais.
Alisema Agosti 4 utafanyika Mkutano Mkuu ambao utapitisha jina la mgombea urais na mgombea mwenza pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chadema, na ilani ya uchaguzi ya vyama vinavyounda Ukawa ambavyo ni NCCR-Mageuzi, Chadema, NLD na CUF.
Agosti 5, 6 na 7 Kamati Kuu itakutana mfululizo kuchambua na kuidhinisha wagombea ubunge kwa niaba ya Chadema, akisema vitafanya kazi kwa umakini kwa kuwa Chadema inajiandaa kuongoza dola.
Lissu
Akizungumzia mchakato uliotumika kumpata mgombea mwenye sifa, Lissu alisema ilifanyika kazi kubwa.
“Tumefanya hivyo kwa sababu tunataka Oktoba 25 iwe ndiyo mwisho wa utawala wa zaidi ya nusu karne wa CCM na mfumo wao wa utawala. Tumefanya utafiti wa kina na mpaka kupata jina la Lowassa,” alisema.
Alisema utafiti wa miezi mitatu wa Kamati Kuu ulihusisha viongozi wote wakuu wa chama hicho na wajumbe wa kamati kuu na sekretarieti.
“Utaratibu wa kumpata Lowassa ulimhusisha katika hatua zote Mbowe, Dk Slaa, makamu wenyeviti wote wawili, naibu makatibu wakuu na wajumbe wote wa kamati kuu. Baada ya kazi hiyo kamati kuu ilikaa kikao Jumapili (Julai 26) na kufanya uamuzi kwamba Lowassa atapeperusha bendera ya Chadema,” alisema.
“Kwa mila na desturi za chama chetu, uamuzi unapofanywa na vyombo halali vya chama kwa kufuata njia zilizowekwa na katiba na kanuni kila kiongozi na mwanachama anapaswa kuheshimu na kutekeleza maamuzi hayo,” alisema.
Umati wa watu
Watu walianza kufika eneo hilo kuanzia saa 4:00 asubuhi na mpaka kufika saa 6:00 mchana mtaa wa Ufipa ulikuwa umefungwa kutokana na idadi kubwa ya watu.
Watu waliofika eneo hilo walionekana wavumilivu kusubiri ujio wake kwa saa tatu, kwani awali ilielezwa awali kuwa angewasili saa 5:00 asubuhi. Eneo hilo lilikuwa na vituo vya aina yake, hasa kijana aliyejitambulisha kwa jina la Juma David ‘Ngosha’ aliyekuwa amevaa sare za kijani zinazotumiwa na CCM na ambaye baadaye alichangiwa fedha ili anunue sare zinazotumiwa na Chadema.
Alipoulizwa sababu za kwenda eneo hilo na sare za CCM alisema: “Nilitaka kupima jazba ya watu, nilitaka kuona mapokeo yao.”
Wakati Lowassa akiondoka eneo hilo, mtu aliyekuwa amevalia sare zinazotumiwa na CCM alibebwa juu juu na kuwekwa chini ya ulinzi mkali kabla ya kupewa sare za Chadema, kisha kuzipokea na kuzivua sare za chama hicho tawala.
Sare zinazotumiwa na Chadema ziliuzwa kwa wingi eneo hilo.
“Hali ya kisiasa sasa imekuwa na manufaa makubwa kwetu,” alisema mmoja wa wauzaji hao, Ester Rwambano.
Dk Slaa, Mnyika wakosekana
Lakini shamrashamra hizo zilifanyika bila ya kuwapo kwa Dk Slaa, ambaye pia alikosekana Jumanne wiki hii wakati wa kumtambulisha Lowassa, na pia Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika.
Hakuna taarifa zilizotolewa kuhusu kutokuwapo kwao, ingawa Lissu, ambaye pia hakuwapo kwenye kikao cha kwanza alijizungumzia akisema kuwa bado yupo na ataendelea kuwapo.
Ole Medeye yupo Chadema ‘kiana’
Kwenye shughuli hiyo pia alikuwapo mbunge wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye, ambaye alieleza kuwa anahudhuria shughuli hiyo kwa kazi maalum.
 “Mimi ni mshauri wa Lowassa katika masuala ya kupambana na rushwa,” alisema. Alisema alijiondoa katika mchakato wa ubunge wa CCM baada ya kubaini unaendeshwa kwa rushwa.
 “Mchakato wa Chadema bado unaendelea, tusubiri ila siwezi kusema kama nipo Chadema,” alisema.
Dk Slaa mafichoni
Jitihada za kumtafuta Dk Slaa hazikuzaa matunda licha ya gazeti hili kufika nyumbani kwake, Mbweni na kuweka kambi kwa zaidi ya saa tatu.
Wakati waandishi wetu wakiendelea kumsubiri Dk Slaa, gari la Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee lilipita karibu na makazi ya kiongozi huyo (Dk Slaa) na alipoulizwa alipo alijibu: “Dk yupo honeymoon (fungate), hana neno, anasubiri tuchukue nchi, amepumzika.”
Mdee pia alijibu tetesi za Dk Slaa kujiuzulu mara baada ya Lowassa kujiunga na chama hicho na kusema: “Hana matatizo kuhusu hilo na yupo vizuri.”
Mlinzi wa nyumbani kwa Dk Slaa aliyefahamika kwa jina moja la Abel alisema tangu migogoro ianze, kiongozi huyo wa Chadema na mkewe, Josephine Mushumbusi, wamekuwa mafichoni na kukataa kuzungumza na wanahabari. Alipoulizwa ni migogoro gani hiyo, alikataa kufafanua.

Chanzo na Gazeti laMwananchi


Ndugu waandishi wa habari na ndugu Watanzania wenzangu.
Yamepita majuma mawili tangu mchakato wa kuchagua mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) ukamilike. Nimetumia muda huu kutafakari kwa kina yaliyotokea Dodoma na hatima yangu katika siasa nchini. Ninajua marafiki wengi na wananchi wenzangu wanaoniunga mkono wamekuwa wakisubiri kwa hamu nitoe kauli.
Waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa akionyesha
Waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa akionyesha kadi yake ya uanachama wa Chadema baada ya kujiunga rasmi Dar es Salaam jana. Picha na Edwin Mjwahuzi
Nilipokuwa natangaza nia ya kugombea urais kule Arusha, nilieleza nia yangu ya kuanza mchakamchaka wa maendeleo ya nchi yetu na kuondokana na umaskini. Pamoja na yaliyotokea Dodoma, azma hii bado iko palepale.
Lakini nianze kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema aliyetupa sisi pumzi ya kuendelea kuwa wazima wa afya njema hadi hivi sasa. Nawashukuru pia mke wangu Regina, wanangu, wanafamilia na marafiki wote kwa mapenzi, msaada na uvumilivu wao wakati wa kipindi hiki kigumu tunachopitia. Nawashukuru sana pia maelfu ya wanachama wa CCM walionidhamini na mamilioni zaidi walioniunga mkono.
Katika safari zangu za mikoani wakati wa kuomba udhamini, nilitiwa hamasa na umati mkubwa wa watu waliojitokeza kuniunga mkono.Aidha, ninawashukuru sana wana kamati wangu, makundi mbalimbali na mamilioni ya vijana wakiwamo; “For You Movement”, “Friends of Lowassa” “Team Lowassa”, Umoja wa Bodaboda na wengine wengi ambao walijitolea kwa hali na mali katika Safari yetu ya Matumaini.
Nitakuwa sijahitimisha orodha ya shukrani iwapo nitaacha kuwashukuru viongozi wa dini zote nchini ambao waliungana na waumini wao wengi katika maombi na kwa kuniunga mkono. Najua sote tumevunjika moyo kwa yaliyotokea Dodoma na mazingira yaliyopelekea matokeo yale.
Kama ilivyokwishaelezwa, mchakato wa kuteua wagombea uligubikwa na mizengwe, ukiukwaji wa maadili, uvunjaji wa Katiba na taratibu za uchaguzi za CCM.
Zaidi ya hayo uchaguzi ulisimamiwa kwa upendeleo dhahiri na chuki iliyokithiri dhidi yangu. Kikatiba, Kamati ya Maadili si chombo rasmi na haina madaraka ya kuchuja na kupendekeza majina miongoni mwa wale wanaoomba kugombea Urais kupitia CCM.
Kilichotokea Dodoma ni kupora madaraka ya Kamati Kuu na kukiuka katiba ya CCM. Aidha, Kamati Kuu na Halmashauri Kuu viliitishwa na kuburuzwa ili vitekeleze azma ya watu binafsi pasipo kujali demokrasia, katiba, kanuni na taratibu za uchaguzi ndani ya CCM. Niliwekewa mizengwe na kuzushiwa majungu na uongo mwingi, kuhakikisha kuwa jina langu halifikishwi mbele ya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu kujadiliwa licha ya ukweli usiopingika kuwa nilikuwa mgombea anayeungwa mkono na wananchi na wanachama wengi wa CCM kuliko wenzangu wote. Kibaya zaidi ni kile kitendo cha kuwanyima wagombea wote 38 haki ya kujieleza mbele ya Kamati Kuu.
Ni dhahiri kwamba njama dhidi yangu ndani ya CCM si jambo jipya.Kumekuwa na mkakati wa siku nyingi wa kulichafua jina langu kwa uzushi na uongo usio na kifani. Aidha, mmeshuhudia jinsi vijana kadhaa walivyotumika kunikashifu na kunitukana na bila aibu na uongozi wa CCM na Serikali kuwazawadia madaraka makubwa.
Kwa namna ya kipekee napenda kuwapongeza na kuwashukuru wazee wetu akiwamo Mzee Kingunge Ngombale Mwiru na baadhi ya  wajumbe wa Kamati Kuu ikiwa ni pamoja na waheshimiwa Emmanuel Nchimbi, Sophia Simba na Alhaj Adam Kimbisa kwa uadilifu na ushujaa wao mkubwa wa kuisimamia katiba ya CCM na misingi ya haki na kukataa maamuzi batili ya Kamati ya Maadili na Kamati Kuu kuhusu uteuzi wa wagombea.
Cha msingi kuzingatia ni kuwa ili kuhitimisha njama za kunipora mimi na wagombea wengine haki zetu za msingi za kusikilizwa, viongozi wachache walikuwa tayari kupanda mbegu ya chuki na mfarakano ambao ni mfano mbaya kwa CCM na hata Taifa letu. Watanzania walitarajia chama kinachoongoza nchi kiwe ni mfano wa utawala wa sheria na kinara katika kutetea misingi ya haki na demokrasia na siyo kuihujumu. Yaliyotokea Dodoma yameitia dosari nchi yetu.
Kwa kifupi, ninaamini sikutendewa haki katika mchakato mzima wa kupendekeza majina na kuteua mgombea wa urais kupitia CCM. Nilinyimwa haki yangu ya msingi ya kusikilizwa na kuchaguliwa.
Kwa mantiki hii nitakuwa mnafiki kama nitaendelea kujidanganya mimi mwenyewe na umma wa Watanzania kwa kusema kuwa bado nina imani na CCM au kuwa CCM ni chama kitakachowaletea ukombozi wa kweli wa kiuchumi, kisiasa na kijamii. CCM niliyoiona Dodoma siyo tena kile chama nilichokulia na kilichonipa malezi na maadili ya siasa yaliyojengwa kwenye misingi ya haki, usawa na uadilifu.
Ni dhahiri kwamba CCM imepotoka na kupoteza mwelekeo na sifa ya kuendelea kuiongoza Tanzania yetu. Mimi kama Mtanzania aliye na uchungu na nchi yake nasema imetosha na SASA BASI!
Kama Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alivyosema, CCM siyo baba yangu wala mama yangu na kwamba kama Watanzania hawapati mabadiliko ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM. Sasa tuyatafute mabadiliko nje ya CCM.
Hivyo basi, baada ya kutafakari kwa kina nimeamua kuwa kuanzia leo ninaondoka CCM na kuitikia wito wa Ukawa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuungana nao katika kuleta mabadiliko ya kweli ya nchi yetu. Navishukuru vyama vyote vya siasa chini ya Ukawa, yaani Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD kwa mwaliko wao na imani yao na kuthamini mchango ninaoweza kutoa kufanikisha azma ya kuleta mabadiliko na maendeleo ya kweli ya Taifa letu. Waheshimiwa Freeman Mbowe, Profesa Ibrahim Lipumba, Mheshimiwa James Mbatia na Emmanuel Makaidi asanteni sana.
Ndugu zangu, sikuufanya uamuzi huu kwa pupa, lakini unafika wakati wa kuchukua maamuzi hata kama ni magumu  kwa kuamini fika kuwa ni kwa masilahi ya Taifa letu.
Nimejiridhisha kuwa ndani ya Ukawa Taifa letu linayo fursa ya pekee na ya kihistoria kushinda Uchaguzi Mkuu ujao na ya kuleta mabadiliko ya msingi katika nchi yetu. Kwa uamuzi na ushiriki wangu huu, ninaamini kwa dhati kuwa tutaondoa uhodhi wa madaraka wa chama kimoja na kujenga demokrasia yenye ushindani wa kweli kisiasa.
Namalizia kwa kutoa wito kwa Watanzania wenye nia njema na nchi yetu na wanaotaka kujenga demokrasia na kuleta mageuzi na maendeleo ya kweli, kujiunga nasi katika safari hii mpya ya kuinusuru nchi yetu.
Safari ya Matumaini inaendelea kupitia Ukawa lakini haitafanikiwa iwapo sote hatutajiandisha kupiga kura. Natoa wito kwa wakazi wa Dar es salaam, kutumia fursa iliyopo kujiandikisha kwa wingi.
Aidha, nawakumbusha Watanzania kote nchini waliojiandikisha kutunza shahada zao na kukumbushana kupiga kura ili ifikapo Oktoba mwaka huu tupate ushindi wa kishindo.
Ndugu zangu Watanzania, tuungane pamoja kuuondoa umaskini na kuleta mabadiliko ya kweli.
NARUDIA CCM SIYO MAMA YANGU

Chanzo na Gazeti la Mwanannchi

Moshi. Mbunge wa Kahama, James Lembeli ameiweka njiapanda CCM baada ya kutangaza kutogombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho.
 
Uamuzi wa Lembeli umekuja wakati wanachama kutoka sehemu mbalimbali wakitangaza uamuzi wao wa kujiengua CCM na kujiunga na vyama vya upinzani, hasa Chadema ambayo imesomba asilimia kubwa ya wahamaji hao.
Akizungumza na gazeti hili jana baada ya kuzagaa kwa taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa amekihama chama chake na kuhamia Chadema, Lembeli alisema taarifa hizo ni uvumi uliozagaa jimboni kwake, lakini hajajiunga na chama chochote.
“Ni uvumi tu na uvumi wenyewe umechangiwa na swali nililoulizwa leo na wananchi kwamba ‘mbona toka mchakato wa kuchukua fomu umeanza hatujakuona’ na mimi nikawajibu kuwa ‘sitachukua fomu’,” alisema.
Lembeli (pichani) alisema amechukua uamuzi huo kutokana na rafu inayoendelea jimboni humo na maneno ya baadhi ya wanachama, wakiwemo viongozi kuwa hatakiwi na vigogo ndani ya CCM.
Lembeli, mmoja wa wabunge waliokuwa mstari wa mbele wakati wa kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, alisema sababu za kutotakiwa huko zinatokana na dhana potofu ya baadhi ya viongozi kwamba michango yake ndani na nje ya Bunge inaivua nguo Serikali.
“Tangu mchakato wa uchukuaji wa fomu umeanza baadhi ya wanachama wengi tu wameitwa kwenye vikao visivyo halali karibu kata zote wakiwa na kadi zao na kuorodheshwa na kupewa maagizo ya kunikataa kwenye kura ya maoni na wengine wanapewa Sh5,000,” alisema mwandishi huyo wa habari.
Lembeli alidai kuwa mbaya zaidi ni kwamba zipo kadi mpya za CCM zinazotolewa kiholela bila kufuata utaratibu na licha ya kulalamikia hali hiyo hakuna hatua zilizochukuliwa.
Alisema kutokana na yote hayo, aliwahi kusema kwenye mkutano wa hadhara kuwa kuna njama hizo, lakini badala ya CCM kufanyia kazi madai hayo, wakamuita mbele ya Kamati ya Maadili.
“Kwenye kamati ya maadili nilituhumiwa kuwa nakidhalilisha chama na kutakiwa niwataje nani walioniambia sitakiwi. Niliwajibu, tena kwa maandishi na kuwapa orodha, lakini mpaka leo kimya ina maana mimi bado ni mtuhumiwa,” alidai.
“Mimi siyo mtoto mdogo. Naelewa nini kinaendelea na ndiyo maana nimesema sitachukua fomu ya kugombea ubunge kwa mazingira haya. Bado sijatangaza kuhama CCM”.
Wakati Lembeli akisisitiza suala la kuhama kwake ni fununu tu, habari nyingine zilidai huenda akagombea ubunge kwa tiketi ya Chadema kutokana na kutokubaliana na mchakato huo anaodai ni batili.
Lembeli anaonekana kuwa mwiba ndani ya Serikali ya CCM baada ya kuiongoza Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ya Bunge katika uchunguzi wa uendeshaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili na kuibuka na taarifa iliyoonyesha kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.
Mawaziri hao ni Balozi Hamis Kagasheki, Dk. David Mathayo, Dk. Emmanuel Nchimbi, Shamsi Vuai Nahodha na Ezekiel Maige.
Lembeli pia nusura ajikute nje ya mchakato wa uchaguzi wa mwaka 2010 wakati alipopigiwa simu na katibu mkuu wa CCM wa wakati huo, akiambiwa achukue fomu za kuwania ubunge wa jimbo jipya la Ushetu.
Wakati huo, Lembeli alidokezwa siku ya mwisho na ofisa mmoja wa Tume ya Uchaguzi kuwa hakukuwapo na jimbo hilo na kulazimika kufanya jitihada katika muda mfupi kuchukua fomu kwenye Jimbo la Kahama na kufanikiwa kushinda kiti hicho.
Hivi karibuni, Lembeli alitofautiana na taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue ya kuwasafisha mawaziri na katibu wa wizara waliowajibika kutokana na kashfa ya escrow na Operesheni Tokomeza.
Lembeli alisema kitendo cha kuwasafisha viongozi hao ni kuipeleka nchi gizani.
“Yuko hapa (waziri mkuu wa zamani, Edward)Lowassa. Japo mimi sipendi wizi na ufisadi, katika kashfa ya Richmond nilikuwa mmoja wa waliopiga kelele awajibike. Lakini wengine wamesafishwa, kwanini naye asisafishwe,” alisema baada ya taarifa hiyo ya Ikulu.
“Kama ni kusafishana tusafishwe wote, tuanze upya ndipo nchi hii itatawalika, vinginevyo huko mbele kuna giza nene.”

Chanzo gazeti la Mwananchi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Charles Mkumbo.
Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza linamshikilia mfanyabiashara maarufu Jijini humo Juma Mahende, anayemiliki Mabasi ya J4 kwa tuhuma ya kuwapiga risasi watu wawili na kuwapotezea maisha, katika eneo la Boma lililopo kata ya Nyakato Jijini humo.

Ni nyumbani kwa Marehemu Cloud Skalwanda, eneo la Nyasaka kata ya Kiloleli wilayani Ilemela Jijini Mwanza, ambako ndugu, jamaa na marafiki wa Marehemu, wamekutana kuomboleza msiba huo.

Tukio hilo limetokea majira ya saa nne usiku wa kuamkia leo katika eneo la Boma lililopo kata ya Nyakato, baada ya mtuhumiwa Juma Mahende kumuita Marehemu Cloud Skalwanda, na mwenzake Ally Mohamed mkazi wa kata ya Igoma kuzungumza masuala ya kibiashara.

Baada ya tukio hilo nyumbani kwa Marehemu Ally Mohamed kata ya Igoma, simanzi na vilio pia vikatawala, huku chanzo cha mauaji hayo kikielezwa kuwa marehemu hao walikuwa wakimdai mtuhumiwa shilingi milioni 25/=.

Wakizungumzia mauaji hayo kwa masikitiko makubwa huku wakibubujikwa na machozi, kaka wa marehemu Ally Mohamed Abeid aitwaye Ramadhan Mohamed Abeid pamoja na dada wa marehemu Claude, Bi. Aziza Steven Sikalwanda wamevitaka vyombo vya dola kuhakikisha vinatenda haki katika uchunguzi wa suala hilo.
Mjane wa marehemu Ally Mohamed Abeid, Bi. Dominata Gabriel pamoja na mmiliki wa nyumba aliyokuwa anaishi marehemu Ally Mohamed Abeid iliyoko eneo la Igoma Bw. Roger Rwegasira wanaeleza walivyopokea taarifa za kuuawa kwa watu hao.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Charles Mkumbo, amesema kuwa tayari Jeshi la Polisi mkoani hapa, linamshikilia mtuhumiwa Juma Mahende kwa uchunguzi zaidi.

The Department of Biotechnology (DBT) of the Ministry of Science and Technology, India, and TWAS have established a fellowship programme for foreign scholars from developing countries who wish to pursue postdoctoral research in biotechnology… More

The Melbourne International Research Scholarships (MIRS) is awarded to international students wishing to undertake graduate research degree studies at the University of Melbourne… More

Ulm University offers the following scholarships to foreign students… More

This programme is designed to further qualify future leaders in politics, law, economics and administration according to the principles of Good Governance and to prepare them in a praxis-oriented course for their professional life… More

Hamburg University of Applied Sciences awards scholarships to academically strong international students studying in Bachelor degree programmes… More

The Social Science Research Council (SSRC) and the Japan Foundation Center for Global Partnership (CGP) announce the annual Abe Fellowship Program competition… More

Columbia Law School is pleased to announce its 2016–2017 Human Rights LL.M. Fellowship Program for individuals with extraordinary potential in the field of international human rights… More

The Carl Duisberg Scholarship is open to students of or young professionals with up to two years work experience in… More

The Jeff Schell Scholarship is open to students of of or young professionals with up to two years work experience in… More

The Hasso-Plattner-Institute in Computer Science for Africa (HPI in CS4A), affiliated with the Department of Computer Science at the University of Cape Town, is offering PhD studentships in the field of Computer Science to students from the African continent… More

The Abus Salam International Center for Theoretical Physics (ICTP) and the OPEC Fund for International Development (OFID) announce a joint program offering fellowships and research/training opportunities to PhD students enrolled in universities in developing countries within areas of ICTP’s scientific and technical competence… More

The Fondazione "Ing. Aldo Gini", based at the University of Padova, in pursuance of its institutional aims, calls for applications for grants for a total amount of Euro 22,000.00 according to the following procedures… More

The ESSO Education Committee offers a number of Training Fellowships to support trainees in Surgical Oncology… More

The Faculty of Sciences of the University of Geneva offers an outstanding research environment for studies in the Biomedical and Life Sciences… More

The International Council of Ophthalmology (ICO) Fellowships Program was organized to help promising young ophthalmologists from developing countries improve their practical skills and broaden their perspectives of ophthalmology… More

Curtin University strives to give high achieving students around the world the opportunity to pursue their ambitions and gain a world-class education… More

Nationals from sub-Saharan Africa are invited to apply for the Africa’s Land and Food Fellowships at the Royal Agricultural University (RAU) in UK… More

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.