November 2013



Chuo cha BBC cha Uandishi wa Habari, (BBC Academy, College of Journalism) chafungua upya tovuti ya Kiswahili kwa ajili ya waandishi wa habari duniani kote.

Chuo cha BBC cha Uandishi wa Habari kimeanzisha upya tovuti ya Kiswahili katika mfumo (mtindo) mpya na maswala mapya.
Tovuti yenyewe inaweza kupatikana kwenye simu ya mkononi, tabiti (tablet) na komputa kubwa.

Lengo la tovuti ya Kiswahili ni kuonesha mtindo wa uandishi katika idhaa za lugha mbali-mbali zinazotangaza katika Idhaa Kuu ya Dunia ya BBC, na ni sehemu ya jukumu la BBC la kuhudumia jamii na kusambaza ujuzi wake ili kunufaisha waandishi wa habari wa Kiswahili dunia nzima.

Ali Saleh, Mhariri wa Idhaa ya Kiswahili:

"Baada ya serikali za Afrika Mashariki kuruhusu vyombo vingi vya habari binafsi kuanzishwa, vinatoa ushindani mkubwa kwa vyombo vya habari vya kimataifa. Ingawa vyombo hivyo vimestawi na kuzidi kukua, vyombo vinavyojitegemea vinakabiliwa na tishio katika nchi kadha, ambako waandishi wa habari wamekimbia kwa sababu ya kulengwa kwa mashambulio na mashtaka. Serikali katika nchi ambako BBC inasikika zinatayarisha sheria kali kupunguza uhuru wa kujieleza, haki ya kutofichua chanzo cha taarifa, na kuwafunga waandishi wa habari kwa yale waliyotangaza."
Tovuti ina maeneo matatu muhimu, ufundi wa uandishi, lugha ya Kiswahili, na maadili ya BBC.

Kupitia sehemu hii ufundiutapata ushauri kuhusu televisheni, redio na mtandao, utangazaji, uandishi, mitandao ya jamii na mengi mengineyo.

Katika sehemu hii wahariri na waandishi wa BBC wanaeleza namna ya kutangaza na kuandika taarifa za televisheni na jinsi ya kuandika ripoti kuhusu michezo. Tovuti inatoa mwongozo jinsi ya kuthibitisha habari zilizoko kwenye mitandao ya jamii.

Katika sehemu yavigezo, kuna ushauri kuhusu msimamo wa kutopendelea upande wowote, ukweli, uhuru, maslahi ya jamii, uwajibikaji na sheria.

Lakini msingi wa kila tovuti ni lugha. Sehemu yalugha inatoa ushauri kuhusu lugha isiyopendelea upande wowote, lugha sahihi, tahajia, ufupisho, majina ya kigeni na ufundi wa kutafsiri na mengineyo.

Sehemu ya lugha ya tovuti ina vielelezo vilivyotengenezwa maalumu kulingana na utamaduni wa Kiswahili. Juhudi zimefanywa kuelezea sehemu hii kwa picha zinazoonesha Idhaa iliyohusika ya BBC pamoja na wasikilizaji na watazamaji.
Pamoja na tovuti ya Kiswahili, Chuo cha Uandishi wa Habari cha BBC, (College of Journalism) piya kinaanzisha lugha tatu nyengine,Burmese,Pashto naVietnamese. Tovuti hizo nne zinafanya jumla ya tovuti za chuo cha BBC zilizoanzishwa upya kufikia 11.

Katika miaka mitano iliyopita BBC College of Journalism, imeanzisha jumla ya tovuti 27 katika lugha tofauti.
Unaweza kusoma tovuti za BBC College of Journalism bila ya kutozwa pesa kokote uliko duniani.

KATIKA miaka mitano iliyopita BBC College of Journalism, imeanzisha jumla ya tovuti 27 katika l
ugha tofauti. Unaweza kusoma tovuti za BBC College of Journalism bila ya kutozwa pesa kokote uliko duniani.

Chanzo:BBC Swahili

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA  

TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA

S. L.P. 4865,                                                                                                          
Dar es Salaam. 

Simu: 2150043-6/2150360   
Nukushi: (022) 2150047
Baruapepe: dgeneral@pccb.go.tz 
                                                                                                                   
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU ACHAGULIWA KUWA MAKAMU WA RAIS WA SHIRIKISHO LA TAASISI ZA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA DUNIANI

Wajumbe 460 wa Mkutano Mkuu wa Saba wa Shirikisho la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Duniani (International Association of Anti-Corruption Authorities – IAACA), kwa sauti moja wamemchagua Dkt. Edward G. Hoseah, Mkurugenzi
Mkuu wa TAKUKURU kuwa Makamu wa Rais wa shirikisho hilo.

Mkutano huo ambao umehudhuriwa na zaidi ya washiriki 460 kutoka nchi mbalimbali duniani umefanyika nchini PANAMA – Amerika ya Kati kuanzia tarehe 22/11 – 24/11/2013. Wajumbe wa mkutano huu ni pamoja na Wakuu wa taasisi 98 za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Duniani ambapo kauli mbiu ya mkutano huu ni “Utawala wa Sheria na Rushwa: Changamoto na Fursa Zilizopo”.

Dkt. Hoseah ambaye kabla ya kuchaguliwa kwake alikuwa ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Utendaji ya Shirikisho hilo, anakuwa Mwafrika wa kwanza kushika wadhifa huo mkubwa katika tasnia ya mapambano dhidi ya rushwa duniani.

Uchaguzi huu ni heshima kubwa kwa Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla.  Hii pia ni fursa nzuri kwa Tanzania kuonesha uwezo wake wa kuongoza mapambano dhidi ya rushwa kimataifa.

Nyadhifa nyingine za kimataifa ambazo Dkt. Hoseah anashikilia au aliwahi kushikilia ni pamoja na kuwa Rais wa kwanza wa Shirikisho la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Afrika Mashariki (2007-2008); Rais wa kwanza wa Jukwaa la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa katika nchi za SADC (SAFAC – 2010 - 2011) na Mwenyekiti wa Bodi ya Umoja wa Afrika ya Ushauri wa Masuala ya Rushwa (AU-ABC 2011-2012). Shirikisho la Kimataifa la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Duniani ambalo linajumuisha Taasisi 298 pamoja na wanachama zaidi ya 2,000 kutoka katika Asasi mbalimbali zisizo za kiserikali, lilianzishwa Aprili 19, 2006 na Makao Makuu yake yapo Peking, China.

Lengo kuu la kuanzishwa kwa Shirikisho hilo ni kuziwezesha nchi wanachama kutekeleza Mkataba wa Umoja wa Mataifa Dhidi ya Rushwa uliopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Desemba 30, 2003.

Imetolewa na Doreen Kapwani, Afisa Uhusiano wa TAKUKURU, Panama. Novemba 26, 2013

VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliovuliwa nyadhifa zao hivi karibuni Dkt. Kitila Mkumbo na Zitto Kabwe wamesema kwamba njama zilizotumika kuwavua madaraka ni mkakati wa viongozi wa juu wa chama katika kujipanga kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa chama unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu. MOblog inaripoti. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo asubuhi jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Serena, aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Dkt. Kitila Mkumbo amesema waraka wa siri unaojulikana kama Mkakati wa Mabadiliko 2013 uliandaliwa na kuhaririwa na yeye kwa kuwa katika siasa za ushindani kuandaaa mkakati wa ushindi si uhaini.

“siamini hata kidogo kwamba kugombea nafasi yeyote iliyo wazi ndani ya chama cha siasa ni uhaini na hujuma. Msingi namba moja wa Chadema ni Demokrasia na hakuna namna ya kudhihirisha mapenzi kwa Demokrasia zaidi ya kuruhusu ushindani katika nafasi za uongozi na hasa uongozi wa juu kabisa,” amesema Dkt. Mkumbo
Amesema kwamba viongozi wa juu wa Chadema wana hofu ya siasa za ushindani baada ya kukaribia kwa uchaguzi mkuu ndani ya chama na yeye pamoja na Samson Mwigamba wanaamini kwamba madadiliko ya uongozi wa juu wa chama ni lazima.

IMG_5201

Dkt. Mkumbo aliendelea kusema kwamba mkakati kwa ajili ya uchaguzi iwe ndani ya chama au nje ya chama ni haki ya kikatiba kwa sababu ni mkakati wa uchaguzi hata viongozi wa juu wa sasa wa Chadema walikuwa na mkakati wao katika kujiandaa na uchaguzi ndani ya chama.

“Siasa za ushindania ndani ya chama cha siasa ni kujenga Demokrasia ya kweli na kama chama kikuu cha upinzani kinakataa kujenga Demokrasia kinachoililia kila siku kwenye chama tawala ni Udikteta usiokubalika katika dunia ya leo,” alisisitiza Dkt. Mkumbo
Amesema waraka wa Mkakati wa mabadiliko 2013 uliandaliwa na watu wanne tu bila Zitto Kabwe kujulishwa ingawa alikuwa mlengwa mkuu wa mkakati ambapo waandaji walipanga kumfuata na kumshawishi ajiunge.

Kwa upande wake Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amesema kwamba hatarajii kutoka ndani ya chama na hana mpango wa kuvunja chama chake kilichomlea na kumkuza miaka nenda rudi kwa sababu yeye ni muumini mwaminifu wa chama.

Amesema kuwa cha kushangaza ni waraka wa siri uliomuhusisha yeye na viongozi wa Chama cha Mapinduzi na wa Usalama wa Taifa kwamba anatumika kuhujumu chama chake na waraka huo ulisambazwa na viongozi wa juu wa chadema kama mkakati wao wa kumdhoofisha kisiasa kuelekea mbio za kugombea uongozi katika uchaguzi wa chama mwishoni mwa mwaka huu.

Amesema sababu ya pili ni kuwakosoa viongozi wa Chadema yakutokupeleka hesabu za chama kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kamati kuu ilidai alipaswa kuwatonya kwanza kabla ya kwenda kwa umma na waandishi wa habari.
“dhamira yangu ilikataa na nitaendelea kusimamia ukweli kwamba hesabu za vyama vya siasa lazima zikaguliwe na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa fedha za Serikali kama sheria inavyotaka,” amesema
Zitto aliendelea kusema kuwa kama kuchagua kati ya chama na nchi yake atachagua nchi kwanza kabla chama na kwamba ataendelea na msimamo wake pia wa kukataa posho ya kukaa yaani (Sitting Allowance) kwa sababu analipwa mshahara na fedha za kujikimu.  

IMG_5241

Mgogoro ndani ya Chadema ulipamba moto baada ya Kamati Kuu kuwavua uongozi Zitto Kabwe na Dk Kitila Mkumbo, huku Makamu Mwenyekiti Taifa, Said Arfi akiandika barua ya kujiuzulu Ijumaa ya wiki hii.

Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wakati Dk Mkumbo amevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu. Wawili hao wanatuhumiwa kukisaliti chama.

 IMG_5274

Taarifa zilisema hoja ya kukisaliti chama pia ilimkumba Arfi akidaiwa kumwezesha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita ubunge bila kupingwa, katika uchaguzi mkuu uliopita na ndiyo sababu ya kuamua kuachia ngazi nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa.

Mbali ya kuwavua uongozi Zitto na Dk Mkumbo, pia Kamati Kuu imewapa siku 14 wajieleze kwa nini wasifukuzwe uanachama. Kwa uamuzi huo Zitto amebaki na wadhifa wa ubunge wake wa Kigoma Kaskazini na wadhifa mwingine kwenye Kamati ya Bunge.

 IMG_5252

Kujiuzuru kwa Arfi

Makamu Mwenyekiti wa Taifa, Said Arfi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, Ijumaa ya wiki hii aliwasilisha barua ya kujiuzulu nafasi ya uongozi wa chama, akisema; “…kuchoshwa na unafiki unaoendelea ndani ya chama. Napenda ifahamike pia kwangu masilahi ya wapigakura, wakazi na wananchi wa Mpanda Mjini na Wilaya ya Mpanda ni muhimu katika kuwatumikia, hivyo basi sipo tayari kuchaguliwa marafiki.

Katika barua hiyo anasema amechochwa na tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake kuwa alimsadia Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita bila ya kupingwa  katika uchaguzi wa ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita.

“Kwa kipindi kirefu zimekuwepo shutuma dhidi yangu na kutiliwa shaka uhusiano wangu na Mhe Pinda Waziri Mkuu. Pamoja na kulijadili katika vikao kadhaa Mpanda na Dar es Salaam bado yapo mashaka kwa nini alipita bila kupingwa. Huo ulikuwa uamuzi wa Wanampanda kwenu imekuwa ni tatizo, lakini hamsemi kwa nini. Majimbo mengine 16 nchini yalipita bila kupingwa mlikuwa wapi na nani alaumiwe? Huu ni unafiki  wa kupindukia.

Vilevile, katika barua hiyo, Arfi anasema amechukizwa na kauli ya mwasisi wa chama hicho, aliyemtaja kwa jina moja la Mtei kuwachagulia marafiki.

“Aidha mmechukizwa sana kwa nini nilihoji kauli ya Mwasisi wa chama, Mhe Mtei kutuchagulia viongozi.  Naomba ifahamike wazi kwamba huu ni mtazamo wangu na utabakia hivyo siku zote kwa chama cha demokrasia kutoruhusu uongozi wa kiimla kwa kukidhi matakwa ya waasisi ambao huvigeuza vyama kuwa mali binafsi.
 IMG_5364



 IMG_5373



 IMG_5365

 IMG_5398

 IMG_5429

 IMG_5417

 IMG_5434
 Chanzo cha habari na www.dewjiblog.com.
















































1. Utangulizi

Katika kikao chake cha siku mbili kilichofanyika tarehe 20 - 22 Novemba 2013, Kamati Kuu ya CHADEMA, pamoja na mambo mengine, iliazimia kunivua nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama. Kwa mujibu wa taarifa ya chama iliyotolewa katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013, ilielezwa kwamba sababu za kuvuliwa uongozi mimi na Dk Kitila Mkumbo ni uhaini na hujuma kwa chama kutokana na waraka unaojulikana kama mkakati wa uchaguzi 2013. Ukweli ni kwamba waraka uliotajwa si sababu ya mimi kuvuliwa nafasi zangu za uongozi kama ilivyojadiliwa katika Kikao cha Kamati Kuu.

Sababu za kufukuzwa kwangu kama zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ni tuhuma lukuki ambazo si mara yangu ya kwanza kuzisikia zikijadiliwa ndani na nje ya vikao vya chama. Hitimisho la tuhuma hizi ni kwamba mimi nimekuwa nikikisaliti chama kwa kutumika na CCM na Usalama wa Taifa. Nitazianisha tuhuma hizi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vyama.

Ninatambua kwamba chama changu kinapita katika wakati mgumu sana sasa hivi. Nataka nitamke mapema sana kwamba mimi Zitto Zuberi Kabwe sitokuwa chanzo cha CHADEMA kuvunjika. Hiki ndicho chama kilichonilea na kunifikisha hivi nilivyo. Ningependa chama hiki mtoto wangu atakapokuwa mtu mzima na atakapoamua kujiunga na siasa aingie CHADEMA. Bado nina imani kubwa na chama changu na ninaamini ndicho kinachostahili kuendesha nchi jana, leo na kesho.

2. Kuhusu tuhuma mbalimbali zinazo elekezwa kwangu

Zipo tuhuma nyingi ambazo zimekuwa zikirudiwarudiwa katika vikao vya chama na nje ya vikao na baadhi ya viongozi wenzangu. Tuhuma hizi zinalenga kuonyesha kwamba mimi ni mbinafsi na kwamba ninapokea rushwa ili kukihujumu chama changu. Nitazianisha tuhuma kwa kifupi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vya chama.

i) Tuhuma kwamba sikushiriki kumpigia kampeni mgombea wetu wa urais katika uchaguzi wa mwaka 2010. Ningependa kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:


  • Mimi nilikuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Kaskazini huko Kigoma.
  • Pamoja na kuwa mgombea wa ubunge, nilifanya kampeni katika majimbo mengine 16 katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dar es Salaam, Mtwara, Pwani, Shinyanga, Mara na Rukwa. Hakuna kiongozi yeyote wa juu aliyefanya kampeni katika majimbo mengi kama mimi, ukiacha mgombea urais.
  • Kote nilipopita nilimpigia kampeni wagombea wetu wa udiwani, ubunge na Rais.
  • Katika Mkoa wa Kigoma nilizunguka na mgombea urais katika kata zote za Kigoma Kaskazini na majimbo yote manane ya Mkoa wa Kigoma.

ii) Tuhuma kwamba katika Mkoa wa Kigoma nilishindwa kuwapigia kampeni wagombea wetu kiasi kwamba peke yangu ndiye niliyeshinda katika uchaguzi huo. Ukweli ni kwamba niliwapigia sana kampeni wagombea wetu, na hivyo ndivyo wapiga kura wa Kigoma walivyoamua.

iii) Tuhuma kwamba nilishiriki kuwashawishi wagombea wetu katika baadhi ya majimbo kujitoa katika uchaguzi wa mwaka 2010 ili kuwapisha wagombea wa CCM wapite bila kupingwa kwa njia ya rushwa. Majimbo yanayotajwa ni pamoja na Sumbawanga, Musoma Vijijini na Singida Mjini. Kama nilivyokwisha kueleza katika vikao mbalimbali vya chama jambo hili si la kweli na hakuna popote ambapo watoa tuhuma hizi wamewahi kutoa ushahidi kwamba nilifanya jambo hili. Nipo tayari kwa uchunguzi ndani ya chama na watoa tuhuma waje na ushahidi bayana wa jambo hili. Si afya kwa chama kuendelea kurudiarudia tuhuma hizi kila mara tangu mwaka 2010 bila uchunguzi wowote kufanyika na jambo hili lifikie mwisho.

iv) Tuhuma kwamba nimekuwa sishiriki katika operesheni mbalimbali za chama: Ukweli ni kwamba nimeshiriki sana katika operesheni mbalimbali za chama ndani na nje ya nchi. Kwa mfano, mwaka 2011 tulikuwa na operesheni kubwa katika mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na nilikwenda katika mikoa yote tuliyotembelea. Mwaka 2012 baada ya hoja ya mkonge bungeni nilifanya ziara Mkoa wa Tanga. Mwaka 2012 kulikuwa na operesheni kubwa moja katika mikoa ya kusini ya Mtwara na Lindi. Operesheni hii sikushiriki kwa sababu nilikuwa nchini Marekani kufungua matawi kwa mwaliko wa Watanzania wanaoishi huko.

v) Tuhuma kwamba nimekidhalilisha chama kwa tamko la PAC kwamba Hesabu za Vyama hazijakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG): Katika jambo hili ninatuhumiwa kwamba mimi kama Naibu Katibu nilipaswa kuwasiliana kwanza na viongozi wa chama 'kuwatonya' ili wajiandae. Kwamba kutokuwatonya kumekidhalilisha chama na kukiweka kundi moja na CCM na nastahili kuadhibiwa vikali kwa kuwa katika taarifa yangu nilikuwa na nia mbaya na chama chetu. Maelezo yangu niliyoyatoa na ambayo ningependa kuyakariri hapa kuhusu jambo hili ni kama ifuatavyo:

  • Utawala bora hautaki mimi kutumia nafasi yangu ya uenyekiti wa PAC kulinda chama changu na kuonea vyama vingine. Kufanya hivyo ni kuendeleza tabia zile zile ambazo tunazipinga na ambazo tunapigania kuzibadilisha
  • Napenda kusisitiza kwamba hakuna chama ambacho kimewahi kukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). Natambua kwamba mahesabu ya chama changu yamekuwa yakikaguliwa na wakaguzi wa nje kwa utaratibu tuliojiwekea. Lakini matakwa ya kisheria ni kwamba mahesabu ya vyama vya siasa hayajakaguliwa na CAG, na hili ni kosa la kisheria, bila kujali kosa hili ni la nani.

vi) Tuhuma kwamba mimi ni mnafiki katika kukataa kwangu kuchukua Posho za Vikao
Mtakumbuka kwamba mimi nilikataa kuchukua posho tangu mwaka 2011 kama ishara ya kuonyesha kwa vitendo msimamo wa chama chetu wa kupinga posho za kukaa na matumizi mengine yasiyofaa katika fedha za umma kama ilivyoanishwa kwenye Ilani yetu ya mwaka 2010-2015. Mtakumbuka kwamba hivi karibuni Mheshimiwa Lema amenishutumu kwamba kukataa kwangu kuchukua posho ni unafiki kwa sababu ninapokea posho kubwa zaidi katika mashirika ya umma ambapo mimi ni mwenyekiti wa kamati husika. Ninapenda kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:

  • Sipokei posho yeyote ya vikao (sitting allowance) ndani na nje ya Bunge tangu mwaka 2011. Hii ni pamoja na vikao vyote katika Kamati za Bunge ninavyohudhuria. Mtu yeyote mwenye ushahidi vinginevyo auweke hadharani.
  • Swala la kukataa posho (sitting allowance) ni swala la kiilani katika chama chetu, na kwangu ni swala la kimisingi zaidi. Katika Wilaya yangu vifo vya kina mama wajawazito ni 1900 kati ya wanawake 100,000 wenye ujauzito. Vifo hivi vinatokana na ukosefu wa huduma kwa sababu ya bajeti finyu. Ndiyo maana nilifurahi sana kwa chama chetu kuliweka swala la kupunguza matumizi ya Serikali katika Ilani, na kuondoa posho za wabunge, ambao tayari wanapokea mishahara mikubwa, kungesaidia sana kupatikana fedha ambazo zingeokoa vifo vingi vya kina mama.
  • Jambo hili si suala la ugomvi baina yangu na Mheshimiwa Lema. Ni suala la msingi katika chama chetu.


3. Usambazaji wa Ripoti ya Siri kuhusu Zitto Kabwe
Hivi karibuni kulisambazwa waraka unaoitwa ripoti ya siri kuhusu mimi ukibeba lundo la tuhuma kwamba nimehongwa fedha nyingi ili kukihujumu chama changu. Waraka huu ulidaiwa kuwa umechomolewa kutoka makao makuu ya CHADEMA. Jambo hili pia lilijadiliwa katika kikao cha juzi kwa kifupi, na majibu ya viongozi wa chama ilikuwa ni kwamba waraka huu haukuandaliwa wala kusambazwa na makao makuu. Katika mchango wangu nililalamikia mambo matatu yafuatayo:

  1. Kwamba baadhi ya waliokuwa wanasambaza waraka ule walikuwa ni viongozi wa chama chetu. Bahati mbaya hadi leo hakuna hata mmoja ambaye amekwishachukuliwa hatua za kinidhamu. Ninaamini kwamba kuna siku watu hao watachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za chama chetu.
  2. Kwa kuwa chama kimekana rasmi kuhusika na waraka huu, nitaendelea na taratibu za kisheria ili kuhakikisha kwamba wote waliohusika kutengeneza hekaya ile wanachukuliwa hatua stahiki za kisheria.


4. Hitimisho
Ninatambua kwamba kuna watu walitegemea leo ningejibu mapigo na ningewazodoa watu kwa majina kama ilivyo kawaida katika siasa za Tanzania. Natambua pia kwamba, kama ilivyo kawaida wakati wa migogoro katika vyama vya siasa hapa Tanzania, kuna watu walitegemea leo ningetangaza 'maamuzi magumu'. Natambua kwamba wapo ambao wangependa kupata nafasi ya kuendelea kutumia suala hili katika harakati zao za kudhoofisha mapambano ya demokrasia na uthabiti wa siasa za ushindani nchini mwetu. Napenda wanachama wa CHADEMA na wapenda demokrasia na siasa safi wote nchini watambue kwamba mimi bado ni mwanachama mwaminifu wa chama hiki na nitakuwa wa mwisho kutoka kwenye chama hiki kwa hiari yangu. Nitafuata taratibu zote ndani ya chama katika kuhitimisha jambo hili.

Naomba wanachama waelewe kwamba mimi kama binadamu ninaumia ninapopigwa. Tuhuma ninazorushiwa ni kubwa na zinanikwaza. Tuache siasa za uzushi ili tujenge chama chetu na nchi yetu, ili hatimaye tuwakomboe Watanzania wenye matarajio na imani kubwa kwa chama chetu.

Kama mwanasiasa kijana niliyekaa katika siasa kwa muda sasa yapo mengi mazuri nimeyafanya. Lakini kuna maeneo nilipojikwaa na yapo makosa niliyofanya kisiasa katika maisha yangu ya siasa.

Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina, waumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa majitaka. Hii ni changamoto kubwa ndani ya chama chetu inayohitaji uongozi shupavu kuikabili. Nitasimama daima upande wa demokrasia. Kama alivyopata kunena mmoja ya wanasiasa maarufu, 'kiwango cha juu kabisa cha uzalendo katika nchi ni kukubali kutofautiana kimawazo', na ninatamani huu ndio uwe utamaduni wa chama chetu.


Kabwe Zuberi Zitto, Mb
Dar es Salaam.
24 Novemba, 2013

Baadhi ya wafanyakazi wa Airtel mwishoni mwa wiki wameitembelea shule ya msingi ya Kiromo iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani na  kutoa mafunzo ya awali juu  ya matumizi ya kompyuta kwa wanafunzi wa shule hiyo.
 
Mkurugenzi wa  Idara ya Fedha wa Airtel Tanzania, Bw. Kalpesh Mehta akiwafundisha matumizi ya kompyuta baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kiromo iliyopo wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani. Wanafunzi wa shule hiyo walipata nafasi ya kujifunza kompyuta katika hatua za awali baada ya wafanyakazi wa Airtel kuitembelea shule hiyo leo.
Wafanyakazi hao wamedai kuwa kujitolea kwenda kutoa mafunzo katika shule hiyo ambayo ilijengwa na kampuni yao kupitia mradi wa shule yetu sio jambo la msimu tu kwani wana mpango wa kuendelea kutoa huduma hiyo mara kwa mara katika shule mbalimbali nchini.

Mkurugenzi wa idara ya Fedha ya Airtel, Bw. Kalpesh Mehta alisema Airtel inaelewa wazi ni jinsi gani matumizi ya vifaa kama kompyuta hurahisisha kazi nyingi katika jamii na hivyo imeamua kwenda kutoa mafunzo ya ujumla kwa wanafunzi wa shule hiyo kwa dhumuni la kuleta mchango chanya kwenye jamii.

“Kompyuta ni kifaa muhimu sana ambacho hurahisisha kazi mbalimbali zinazofanywa kwa ajili ya maendeleo ya jamii hivyo inabidi wanafunzi waanze kujifunza juu ya umuhimu wa kifaa hiki mapema katika kusaidia maendeleo ya jamii huko mbeleni.” Alisema Mehta.

Kwa upande wake Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya Kiromo, Bw. Joseph Ngunangwa alisema masomo hayo yametoa hamasa kubwa sana kwa wanafunzi wa shule hiyo kwa sababu yamewafanya wahisi masomo hayo yana urahisi na sio magumu kama walivyokuwa wakifikiria.

“Wanafunzi walikuwa na mitazamo kwamba wanaojifunza kompyuta ni tabaka flani tu la watu na walikuwa wakihisi kwamba kompyuta ni somo gumu lakini leo  wametiwa moyo na wafanyakazi wa Airtel na wameanza kuona kuwa somo hilo ni rahisi na yeyote anaweza kulisoma na kufaulu vyema,” alisema Pangahela.

Mwalimu huyo aliongeza kuwa kupitia masomo hayo idadi ya wanafunzi watoro imepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na sababu kuwa wengi huja shule kwa ajili ya kujifunza kompyuta.

Kwa upande wao wanafunzi wa shule ya Kiromo waliwashukuru wafanyakazi wa Airtel kwa kuonesha ukarimu mkubwa sana na kusema kuwa wanatamani masomo hayo yangekuwa yanafanyika kila siku.

Si mara ya kwanza kwa wafanyakazi wa Airtel kuzitembelea shule na kutoa mafunzo kama hayo vile vile Kampuni hiyo hutoa misaada ya vitabu mbalimbali vya kiada nchini na kuchangia katika ujenzi wa taifa hususani katika sekta ya elimu.





























































Hadi tunawaletea habari hizi ni kwamba mkutano wa waandishi wa habari na aliyekuwa katibu mkuuu wa chama kikuu cha upinzani Tanzania Chadema unaendelea katika hoteli ya serena jijini Dar Es Salaam na habari zilitofikia kutoka ndani huko ni kwamba Mhe. Mbunge wa Kigoma Kaskazini Bwana Zito Kabwe ameapa kupambana akiwa ndani ya chama mpaka tone la mwisho.
 
Amesema atajiuzulu ngoo na huku akipinga shutuma zote za kuvuliwa madaraka yake ndani ya chama hicho moja baada ya nyingine.

Tutawaletea habari kamili hapo punde.




International Doctoral School in Functional Materials (IDS-FunMat) for
Energy, Information Technology and Health is looking for potential candidates to fill up to seventeen PhD positions for the call 2014.

The school offers scholarships for PhD projects in Functional Materials Science, carried out in co-supervision between universities from two different countries (see list of partners). In most projects an industry partner is also involved. The PhD candidates must spend at least 6 months in each university. The projects start around October and take 3-4 years.

The European Union finances each year a number of ERASMUS MUNDUS PhD scholarships in our school, and in addition we have PhD projects funded by other sources.

There is also an exciting opportunity for those who are interested to work on LCA for sustainability assessment of materials (2014-10-LF Towards sustainable, economic and effective materials: development of a universal assessment model).

Further information about the positions can be found at: http://www.idsfunmat.u-bordeaux1.fr/


Wazazi na walezi  wa kijiji cha Jendele na Vijiji jirani wameshauriwa kuwapeleka watoto wao Skuli za Maandalizi mapema wakiwa na umri wa miaka mitatu ili kuwajengea  uwezo na ufahamu wakiwa na umri mdogo.

Hayo yameelezwa leo na Mratibu wa Jumuiya ya Skuli za Maandalizi za Madrasa Mohamed Othman Dau wakati alipokuwa akizungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa Skuli ya Maandalizi Nuru Islamia iliyopo Kijiji cha Jendele.

Amesema kumpeleka  mtoto Skuli katika umri huo  ni kumkuza mtoto kiakili na kimwili kwani kufanya hivyo inampekea kuwa na ufahamu nzuri katika masomo yake.

“ Ni vyema  wazazi  waone ni muhimu kuwapeleka Skuli za Maandalizi watoto wao kwani kufanya hivyo ni kuwaandaa katika msingi bora wa kielimu,alisema Mratibu wa Jumuiya Mohamed Othman Dau”.

Afisa Lishe Shemsa Nasour Mselem  amesema ni vyema wazazi kuzungumza na watoto wao wakati wakiwa tumboni kwani kufanya hivyo humjengea mtoto huyo kufahamu  haraka wakati akisha zaliwa.  

Aidha amesema ni bora wazazi  kuwapatia watoto wao chakula chenye mchanganyiko wa virutubisho mbali mbali kwa ajili ya kuwajenga watoto hao miili yao kwani kufanya hivyo huwafanya kuwa na Afya  bora .

Nao wazazi wa watoto hao wamesema wamefarajika kwa kupatiwa mafunzo hayo kwani wengi walikuwa hawafahamu namna ya kuwaandaa watoto wao na kuwapatia lishe bora.

Hata hivyo wamesema  kwamba wameshukuru Jumuiya ya Maendeleoya ukuwaji wa Mtoto (CCD)  kwa kupatiwa mafunzo ya naman ya kuwaandaa watoto wao wakiwa na umri mdogo jinsi ya kujifunza kucheza  kabla kupelekwa Skuli za Maandalizi.

Sales Manager
ACL HR Services

Date Listed: Nov 14, 2013
Email Address: Click to Email
Phone: No calls Please
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Nov 21, 2013
Start Date: Nov 14, 2013


Position Description:
Degree in related field
Minimum of 5 years of working experience in related field


Application Instructions:
HOW TO APPLY
Please interested candidates with the required qualification should send their
cv and certificate to acl.hrservices@gmail.com (Please write SALES MANAGER in subject line)
ACL HR Services

Receptionist One post
MIC Global Risks

Date Listed: Nov 13, 2013
Email Address: Click to Email
Phone: No Calls Please
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Nov 30, 2013


Position Description:
From The Daily News of 13th November 2013
Major Duties and Responsibilities
Handle the diary of the Chairman / CEO.
Handle all administrative matters.
Assist Finance Department.
Backup for Receptionist.
Qualifications, Experience and Skills:
Relevant academic qualification.
At least 2-3 years' work experience post relevant academic qualification
MIC Global Risks is a top ranking insurance broking company operating in Tanzania. We are also associated with MARSH the world's leading risk and insurance services firm and have entered into a strategic relationship with them. Following a major expansion plan, we invite applications from suitably qualified candidates for the following job opportunities from experienced and dynamic insurance specialists.


Application Instructions:
Interested candidates should forward their detailed resume stating age, qualifications, experience, e-mail address, daytime telephone contact and names and addresses of three referees to the contact address indicated below by 30 November, 2013
General Manager
MIC Global Risks (Tanzania) Limited
Approved Representatives of MARSH
8th Floor, Amani Place, Ohio Street
P.O. Box 10936,
Dar es Salaam, Tanzania
or
Applications can also emailed through the link above

Accountant
ARM Cement Ltd

Date Listed: Nov 13, 2013
Email Address:

info@armafrica.com   

Phone: No Calls Please
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Nov 27, 2013


Position Description:
From The Guardian of 13th November 2013
Qualification - Graduate (Preferably Commerce)
Experience - 3-5 years in accounting for stores, purchase, sales, cash, bank etc. Experience in dealing with banking operations will beaded advantage


Application Instructions:
Candidates should apply their resumes in English, copy of all educational certificates and work experience certificates from previous employers, two photographs, last three salary slips two references, copy of photo identity cards and character certificate from police. Applications without the above documents wont be entertained.
Send your applications through the email link above

Administrative Assistant/Receptionist
ARM Cement Ltd

Date Listed: Nov 13, 2013
Email Address: info@armafrica.com 
 Phone: No Calls Please
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Nov 27, 2013


Position Description:
From The Guardian of 13th November 2013
Qualification : Graduate with pleasant personality and good communication skills
Experience : Minimum 5 years related experience.
Brief Job Description : Manage plant administration jobs Applicants must be fluent in English and Swahili.


Application Instructions:
Candidates should apply their resumes in English, copy of all educational certificates and work experience certificates from previous employers, two photographs, last three salary slips two references, copy of photo identity cards and character certificate from police. Applications without the above documents wont be entertained.
Send your applications through the email link above.


Hadi kufikia raundi ya kumi na moja ya michezo ya Ligu kuu ya Uingereza al maarufu kama Barclay’s Premier League tumeshuhuddia ya kuwa hakuna timu ambayo unayoweza kusema ina uhakika wa kutoka na point tatu.

Mchezaji mahiri wa mabingwa watetezi Manchester united  na mfungaji bora wa Msimu uliyopita, Robin Van Persie

Hii ni mara baada ya timu ya Machester United kuifunga timu inayoonekana imedhamiria kulitwaa taji hilo kwa msimu huu kwa goli moja na huku timu ambayo imetumia hela nyingi katika usajili , matajiri wa Etihad Machester City kupokea kipigo toka kwa timu ya Sunderland.
Mchezaji mpya na wa ghali wa timu ya Arsenal, Mezut Ozil
Kwa hiyo mtu yeyoye anaweza kupata majibu ya kwamba hakunambabe halisi wa ligi hii kwani timu yoyote inaweza kuifunga timu yoyote pasipo kujali inacheza na timu ndogo au kubwa nah ii inatoa taswiara ya kwamba kiwango cha timu za ligu kuu vimepanda na hivyo kutoa ushindani halisi.
Kocha wa Chelsea mreno Jose Mourinho aliyerudi klabuni hapo kwa mara ya pili akitokea mabingwa wa zamani wa La Liga timu ya Real Madrid
Matokeo ya kushangaza kabisa yalikuwa ya Sunderalnd kuifunga Manchester City lakini pia matokeo kama hayo pia yalishaonekana ndani ya Old Trafford pale Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Manchester United walipopokea kipigo cha bao 1-0 toka kwa Westbromwich Albion, pia Aresnal kufungwa na Aston Villa 3-2 uwanja wake wa Emirates, na pia Liverpool walipofungiwa nyumbani kwake na Southanpton na vile vile pale Cheslea walipofungwa 2-0 na Newcastle United.
Mlinzi mahiri  na nahodha wa Manchester City, Vicent Kompany ambaye msimu huu umekuwa mbaya kwake kutokana na kuandamwa na majeruhi ya mara kwa mara.

Kwa hiyo tulichojifunza ni kwamba si kwamba Manchester United anaweza kufiunga Arsenal tuu bali timu yoyote inaweza kufungwa na timun yoyote ile pasipo kujali ule u nne bora.
Kocha mpya wa matajiri wa Machester City, Manuel Pellegrini
Lakini tukirudi nyuma kuna ukweli sahihi ya kuwa timu tatu za juu, Manchester United, Manchester City and Chelsea kumeleta utofauri kwa mfano tukingalia kwa upande wa Manchester United, kustaafu kwa Sir. Alex Ferguson na jinsi timu hizi gamin timu hizi zilivyoruhusu kupoteza pointi mpaka sasa.
Mchezaji wa Arsenal aliye kwenye kiwango cha juu msimu huu, Aaron Ramsey

Kutokea kuanzishwa kwa mfumo mpya wa Ligi mnamo mwaka 1992, kumekuwepo na msimu mmoja tuu  kuwepo kwa timu bora nane kubanana hadi kufikia hatua hii nah ii ilikuwa msimu wa 2001/2002 wakati waliokuwa wakiongoza Aston Villa wakiwa mbele point nne mbele ya Totenham na Arsenal kwenda kuchukua ubingwa kwa kuizidi Liverpool kwa pointi saba.
 
Kukiwa kumebakia na michezo 27 tunaweza kusema timu zote nane zinavyoweza kuleta ushindani  wa kugombea taji hilo katika muongo mmoja ambao haujapata kutokea.

Wafungaji bora mpaka kufkia sasa:-

        1. Sergio Agüero…………………    Manchester City….…..8
           Daniel Sturridge………………..   Liverpool……….…..…8
           Luis Suárez………………………. Liverpool…………...…8
       4.  Robin Van Persie…………………Manchester United 7
            Loïc Remy………………………...Newcastle United…..  7
       6. Aaron Ramsey…………………….Arsenal………………  6
       7. Wayne Rooney…………………... Manchester United…. 5
           Yaya Touré………………………. Manchester City…….  5
           Olivier Giroud…………………….Arsenal………………..5
           Romelu Lukaku…………………... Everton……………….5

 












































Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.