WABUNGE wa Seneti jimbo la Hawaii nchini Marekani limekuwa jimbo la kwanza nchini Marekani hivi karibuni kupitisha kwa kura moja muswada wa sheria ya ndoa za mashoga na kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja katika jimbo hilo.
Wafuasi wa ndoa za jinsia moja katika Hawaii sherehe katika mji wa Honolulu


Serikali ya jimbo la Seneti lapitisha kwa kura 19 kwa 4 za waliopiga muswada huo wa ndoa za mashoga nchini huo.


Gavana wa jimbo la Hawaii aliyechaguliwa kidemokrasia anasema atasaini muswada huo wA sheria za ndoa za mashoga bila kuchelewa Ili kutoa haki ya watu wanaoamini hivyo, sheria hiyo inatazamiwa kuanza rasmi kutumika tarehe 2 Desemba mwaka huu.
Wafuasi wanaodai ndoa za jinsia moja


Taarifa zinasema kuwa ndoa za jinsia moja nchini Marekani zimepitishwa katika majimbo 14 na wilaya moja ya Columbia.

Waandishi wanasema muswada huo wa sheria za ndoa ya jinsia moja itafanya jimbo la Hawaii kuwa maarufu kwa harusi za mashoga na wasagaji kupita majimbo yote nchini Marekani.


Watafiti katika Chuo Kikuu cha Hawaii wamesema kwamba sheria hiyo  itakuza utalii kwa mapato USD 217m (£ 136m ) ndani ya miaka mitatu ijayo.


"Natarajia kusaini kipande hii muhimu cha sheria, ambayo inatoa usawa wa haki za binadamu kwa watu wa jinsia moja kufunga ndoa kisheria na kulinda uhuru wa kuabudu na wa kidini,” amesema gavana wa jimbo la Hawaii Neil Abercrombie 


Rais wa Marekani Barack Obama amekaribisha kura ya Jumanne wiki hii kwa kusema “. Nimekuwa daima najisikia fahari kuzaliwa katika jimbo la Hawaii na kura hii ya leo inanifanya nijisikie fahari zaidi na zaidi ,’ amesema
Wengi wamepokeza baada ya kesi ya mwaka 1990 katika jimbo la Hawaii ambapo wanawake wawili waliomba kibali cha kufunga ndoa lakini wakazusha mjadala mkubwa kuhusu ndoa za jinsia moja nchini nzima.


Ilipelekea karibu majimbo 30 kupiga marufuku ndoa za jinsia moja na kusababisha baraza la Congress kupitisha sheria ya ulinzi wa ndoa mwaka 1996.
 same, sex, marriage:, 7, states, most, likely, to, legalize, gay, marriage, in, 2013,

Na sheria hiyo ya ulinzi wa ndoa ilifafanua kwamba ndoa ni kati ya mwanaume na mwanamke lakini sheria hiyo ya ndoa ilipigwa chini Mahakama Kuu nchini Marekani mwanzoni mwa mwaka huu.
 

Kura za jumanne katika jimbo la Hawaii limeongeza kasi ya haki za mashoga kuweza kufunga ndoa nchini Marekani.

Wakati huo huo, Maseneta wa jimbo la Illinois walipitisha muswada wa ndoa za jinsia moja mapema mwezi huu na gavana wa jimbo hilo, Pat Quinn amesema atasaini kuwa sheria tarehe 20 November mwaka huu.





Mwisho.



Na Damas Makangale, Moblog kwa Msaada kwa Mtandao
 
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.