Siku moja baada ya nguli ya sheria za katiba nchini, Dakta Sengodo Mvungi kuaga dunia nchini Afrika Kusini, Jeshi la Polis Kanda Maalum Ds, linamshikilia mtuhumiwa mmoja John Ikondia Mayunga (56) kwa kosa la kushiriki kikamilifu kwenye mauaji ya mwanasheria huyo na mjumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba.
Marehemu, Dakta Sengodo Mvungi wakti wa uhai wake


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova amesema mtuhumiwa huyo ni mkazi wa kiwalani walipata taarifa kwa raia wema kwamba alishiriki kikamilifu kwenye tukio hilo lilosababisha kifo cha Dakta Sengodo Elibariki Mvungi.
Kamanda wa Kanda Maalumu Dsm, Kamishna msaidizi wa jeshi la  Polisi, Suleman Kova


“mnamo tarehe 12/11/2013 Polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kwamba kuna mtu ambaye amehusika na tukio la mauaji ya Dakta Mvungi na kwamba kipindi hicho mnamo saa 12 jioni mtuhumiwa alikuwa maeneo ya mtaa wa Twiga jangwani akiwa anaangalia Televisheni,” amesema Kamishina Kova

Kova amesema kwamba mtuhumiwa alitambuliwa na kukamatwa kisha kuhojiwa na Polisi na alikubali kwamba alihusika na akawaongoza askari hadi nyumbani kwake kiwalani Migombani.


Alifafanua kwamba taratibu za upekuzi zilifanyika na katika upekuzi vilipatikana silaha ambayo ni bastola aina ya REVOLVER N0. BDN 6111 pamoja na risasi ishirini na moja.


Kova amesema kuwa mtuhumiwa alikiri kwamba katika vitu vitu vilivyoibwa nyumbani kwa dakta Mvungi ni pamoja na bastola hiyo aidha siku ya tukio hilo walitumia milipuko kutishia ili kufanikisha uporaji huo.


Kamanda Kova alisisitiza kwamba mtuhumiwa huyo ni wa kumi kukamatwa kuhusiana na tukio hilo na bado operesheni kali inaendelea ili kuhakikisha kuwa yeyote aliyehusika na tukio hilo anakamatwa kwa nguvu za dola.


Mwisho.


Na Damas Makangale, Moblog
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.