Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema Jamhuri ya Kiislamu inalipa umuhimu mkubwa suala la uhusiano wake na nchi za Afrika ikiwemo Afrika Kusini.


Zarif ameyasema hayo akiwa mjini Pretoria Jumatano usiku na kuongeza kuwa, ‘Afrika Kusini ni moja ya nchi muhimu katika bara la Afrika na moja kati ya nchi zenye ushawishi mkubwa kimataifa.’ 


Amesema Iran inataka kuboresha uhusiano wake na nchi hiyo ya Afrika huku akielezea matumaini aliyonayo kuwa sekta binafsi na za kiserikali za nchi mbili zitatoa msukumo mkubwa katika uhusiano wa kiuchumi, kibiashara na kiufundi. 


Zarif yuko Afrika Kusini kuhudhuria kikao cha 11 cha Tume ya Pamoja ya Ushirikiano ya Iran na Afrika Kusini. Kikao hicho kinafanyika leo na Zarif ameelezea matumaini yake kuwa kitakuwa na natija nzuri itakayopelekea kukurubisha uhusiano wa nchi mbili katika nyanja za viwanda na biashara.


 Kikao hicho kitafanyika chini ya uenyekiti wa Zarif pamoja na Waziri wa Ushirikiano na Uhusiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini Bi. Maite Emily Nkoana-Mashabane. Zarif pia anatazamiwa kukutana na maafisa wa ngazi za juu wa Afrika Kusini akiwemo Rais Jacob Zuma.


Mwisho.


Picha ya Mohammad Javad Zarif 


Chanzo: Iran Swahili Radio

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.