Mwana wa Malkia wa Uingereza, Prince Charles matatani kwa kukwepa kodi anakabiliwa na uchunguzi juu ya fedha zake ambazo hazilipi kodi 

Wabunge wataka achunguzwe na malipo ya fedha zake ziwe wazi kwa umma



Mwana wa malkia wa Uingereza, Prince Charles matatani anakabiliwa na shutuma kali za kukwepa kulipa kodi na upendeleo katika kulipa kodi za nchi na sasa wabunge wanataka achunguzwe kwa mapato yake halisi na yawe wazi kwa umma wa Uingereza.


Wabunge wa Uingereza wanadai kwamba malipo yake si wazi na kodi yake anayolipa pia haipo wazi kama inavyotaka sheria za nchi hiyo ya Uingereza.


Prince Charles anakabiliwa uchunguzi wa mapato yake na wabunge wanadai uchunguzi wa mwana huyo wa malkia uwe wazi na safi na njia yeye kufadhiliwa katika vitu mbalimbali viwe wazi kwa umma.

Kamati ya fedha za umma ya bunge imesema kuwa mali za kampuni ya  Duchy wa Cornwall inayomilikiwa na Prince Charles,  ardhi na faida kubwa  kutoka kampuni ya Holdings ambayo kumlipa Prince Charles zaidi ya Paundi 19milion kwa kila mwaka, hazina kodi za biashara.


Na wakati huo huo, Taarifa zinasema kama mrithi mtarajiwa wa malkia wa Uingereza alipaswa kuwa makini na malipo ya kampuni zake kwenye kodi, ongezeko la thamani na sheria zingine za kodi, kamati hiyo ya bunge inahoji.


Margaret Hodg , Mwenyekiti wa Kamati huru ya Hesabu za Serikali , amesema idadi ya hatua zinahitajika kuchukuliwa ili kuleta wamiliki wa kampuni ya  Duchy ' ili waieleze vizuri kamati ya bunge.

Duchy , ni kampuni ya majengo inayomilikwa na Prince Charles  yenye thamani ya Paundi za Kiingereza 847million ,

Bibi Hodge amesema: ' Duchy inafurahia msamaha wa kulipa kodi hata kama inafanya kazi kwa faida kubwa na biashara za aina mbalimbali. Lakini Bibi Hodge anadai kutoa msamaha wa kodi  kwa kampuni kama hiyo ni kuwaumiza  washindani wake ambao hulipa kodi kwa mujibu wa sheria za nchi.


Mwisho 


Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.