ILIKUWA kama filamu fulani hivi. Leodgar Tenga alitumia saa nne, kuanzia saa tano asubuhi mpaka saa nane kumkabidhi ofisi Jamali Malinzi juzi Jumamosi. Baada ya kukabidhiwa rungu  Malinzi akawaambia wajumbe wote 18 wa Kamati ya Utendaji; “Tukutane mara moja.”
Angetile alipoulizwa alisema; “Nimepata taarifa hizo lakini sina cha kuzungumza kwa sasa, bado natafakari nitatoa tamko kesho (leo Jumatatu) au keshokutwa(Jumanne).”
Wakapanda gari wakaelekea kwenye hoteli moja iliyoko Kariakoo, jijini Dar es Salaam. Baada ya kufika hapo akataja ajenda halafu akashtua hadhira baada ya kutamka kwamba hana imani na Katibu Mkuu, Angetile Osiah. Hivyo akamtaka atoke nje ya kikao hicho ili ajadiliwe ndipo wajumbe walipomuunga mkono Malinzi kwa hoja na kutaka Angetile apigwe chini na nafasi yake akaimu Ofisa Habari, Boniface Wambura ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari na mwanasheria.
Ndipo jana Jumapili, Malinzi akatangaza rasmi uamuzi huo na kusema kwamba Angetile ambaye mkataba wake unamalizika Desemba amepewa likizo yenye malipo mpaka mkataba wake utakapokwisha Desemba. 
Malinzi alitwaa madaraka hayo baada ya kumshinda Athuman Nyamlani katika uchaguzi wa shirikisho hilo uliofanyika Jumapili ya wiki iliyopita.
Malinzi ambaye Fifa na CAF zimekubali ushindi wake, alisema uteuzi wa Wambura ulianza rasmi juzi Jumamosi na aliziomba klabu, vyama vya wilaya, vyama vya mikoa, vyama shiriki na wadau wa soka wampe ushirikiano  Wambura kwenye utendaji wake.
Angetile alipoulizwa alisema; “Nimepata taarifa hizo lakini sina cha kuzungumza kwa sasa, bado natafakari nitatoa tamko kesho (leo Jumatatu) au keshokutwa(Jumanne).”
 Awali baada ya kushinda hata kabla kukabidhiwa ofisi Malinzi alitangaza kufuta kamati zote za shirikisho hilo na kuunda nyingine mpya kwavile hana imani na ufanisi wake kwavile nyingi zilikuwa zikipepesuka kwenye uamuzi.
Malinzi ameahidi kusafisha vitengo mbalimbali vya TFF na kurejesha hadhi ya utendaji kwenye soka la Tanzania.

Chanzo: Gazeti la Mwanaspoti
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.