2013

MADEREVA wa bajaji mkoani Singida,wameshauriwa kujenga utamaduni wa kutii bila shurti sheria za usalama barabarani,ili pamoja na mambo mengine,kuondoa uwezekano wa kutokea kwa ajali zinazosababisha vifo na uharibifu mkubwa wa mali.
 
Aidha, wametakiwa kutii bila shurti kanuni na taratibu zilizowekwa na SUMARTA,ili kupunguza uwezekano wa kutokea kwa migomo na kufunga barabara.
Usafiri wa Bajaji
 
Wito huo umetolewa juzi na meja Stan wa kitengo cha usalama barabarani mkoani Singida,wakati akizungumza na madereva wa bajaji wa kituo cha soko kuu mjini hapa ambao walifunga barabara ya mtaa wa Mukhandi kutumika.
 
Meja Stan aliwataka kuheshimu maamuzi ya SUMATRA kwa kuwapa vituo vya kupakia abiria,ili kuepuka kutokea kwa migongano baina yao na bodaboda na hata hiece.
 
“Kama wewe SUMATRA imekupangia kituo chako kuwa ni cha stand ya mabasi cha zamani,sheri,ukipakia abiria anakuja hapa soko kuu,sheria inakutaka ukimshusha tu,uondoke hapo mara moja kurudi kwenye kituo chako”,alisema.
 
Meja Stan alisema abiria huyo akimaliza shughuli zake soko kuu,atapanda bajaji au usafiri mwingine kwenda anakotaka.
 
Akifafanua zaidi,alisema kuwa sheria hairuhusu dereva wa bajaji ambaye soko kuu sio kituo chake asubiri abiria pale,ili amalize shughuli zake halafu ampeleke sehemu nyingine anakokwenda.Wajibu wake ni kumshusha na yeye kurudi kwenye kituo chake.
 
Wakati huo huo,meja Stan amewataka wajenge utamaduni wa kutumia viongozi wao kuwasiliana na uongozi wa halmashauri ya manispaa ya Singida,ili kujadiliana pamoja kutatua kero mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi wa kudumu,ikiwemo ya ufinyu wa maegesho.
 
MWISHO.


Picture
Rais Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete (kulia) wakihudhuria sherehe za miaka 50 ya Uhuru wa Kenya zilizofanyika katika Uwanja wa Michezo wa Kasarani mjini Nairobi leo. Kushoto ni Mwenyeji Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta. Watatu kushoto ni Naibu Rais wa Kenya, William Ruto, Watano Kushoto ni Waziri Mkuu wa Ethiopia, Haile Mariam Desalegn, na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi na mkewe. (picha: FREDDY MARO/Ikulu)


Picture



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Desemba 10, 2013, ameungana na viongozi wa mataifa mbali mbali duniani na maelfu ya wananchi wa Afrika Kusini Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha aliyekuwa kiongozi mashuhuri wa Afrika Kusini na duniani, Mheshimiwa Nelson R Mandela.
Picture
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe George W. Bush na Mkewe Laura Bush wakiwa jukwaa la viongozi na watu mashuhuri baada ya Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha aliyekuwa kiongozi mashuhuri wa Afrika Kusini na duniani, Mheshimiwa Nelson R Mandela leo Desemba 10, 2013 katika uwanja wa FNB jijini Johannesburg. (picha: Ikulu)


Maelfu kwa maelfu ya wananchi wamehimili mvua kubwa iliyokuwa inanyesha kwa nguvu kwenye Uwanja wa Michezo wa FNB mjini Johannesburg kumwaga Mzee Mandela ambaye alikuwa ishara kuu ya upinzani wa siasa za ubaguzi wa rangi za 
makaburu wa Afrika Mashariki.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe George W. Bush na Mkewe Laura Bush wakiwa jukwaa la viongozi na watu mashuhuri baada ya Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha aliyekuwa kiongozi mashuhuri wa Afrika Kusini na duniani, Mheshimiwa Nelson R Mandela leo Desemba 10, 2013 katika uwanja wa FNB jijini Johannesburg. (picha: Ikulu)

Mheshimiwa Mandela ambaye alifariki duniani Ijumaa iliyopita, Desemba 5, 2013, alikuwa Kamanda wa Jeshi la Ukombozi la Chama cha African National Congress la Umkhoto we Sizwe akafungwa jela kwa uhaini kwa miaka 27 na utawala wa Makaburu.

Baada ya kutoka jela mwaka Februari 1990, Mzee Mandela alichaguliwa kuwa Rais wa Kwanza wa Afrika Kusini ya mwaka 1994. Lakini Mheshimiwa Mandela alitumikia kipindi kimoja tu cha miaka mitano na kukataa kutumikia kipindi cha pili.

Kiasi cha viongozi 91 kutoka sehemu duniani wamehudhuria Kumbukumbu hiyo iliyokuwa na kila aina ya mchanganyiko wa hisia – wengine wakiwa na majonzi na wengine wakicheza na kuimba kwa muda wote wa shughuli hiyo iliyochukua kiasi cha jumla ya saa tano.

Mbali na Rais Kikwete ambaye amefuatana na Mama Salma Kikwete, marais wengine mashuhuri duniani waliohudhuria Kumbukumbu hiyo ni Mheshimiwa Barack Obama wa Marekani, Mheshimiwa Francois Hollande wa Ufaransa, Waziri Mkuu wa Uingereza, Mheshimiwa David Cameroun na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Ban Ki Moon.

Kumbukumbu hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi wa zamani wa Marekani wakiwemo marais watatu wa zamani wa Marekani – Mheshimiwa Jimmy Carter, Mheshimiwa Bill Clinton na Mheshimiwa George W Bush na mawaziri wakuu wawili wa zamani wa Uingereza, Mheshimiwa Tony Blair na Mheshimiwa Gordon Brown.

Rais Kikwete kesho, Jumatano, Desemba 11, 2013, ataungana na viongozi wenzake katia katika kutoa heshima za mwisho na kuuaga rasmi mwili wa Marehemu Mandela ambao utawekwa kwenye Majengo ya Urais wa Afrika Kusini ya Union Buildings mjini Pretoria.

Source: http://www.wavuti.com

Receptionist (Two Posts) (Ref.No.NHC/R)
National Housing Corporation(NHC)

Date Listed: Dec 2, 2013
Phone: No Phone Calls
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Dec 16, 2013

Position Description:
From Daily News December 2, 2013
National Housing Corporation (NHC) is inviting applications from suitably qualified .dynamic and good team player to fill the position of RECEPTIONIST in its Directorate of Regional Operations and Administration.
The Receptionist reports to the Senior Administration Officer and has overall responsibility of ensuring good customer services and prompt service delivery.
Specific Duties and Responsibilities include:
As the first point of contact for most customers, endeavors to answer telephone enquiries in an efficient, friendly and professional manner.
Ensures that all guests are received in a good manner and directs them to the appropriate officers/office. Makes and receives telephone calls for staff and transmit messages accordingly.
Keeps detailed and updated records of calls made through the switchboard including monitoring telephone bills to correspond with switchboard usage.
Operates the telephone Switchboard and ensure that the Switchboard functions at all times and to report promptly on all telephone defects.
Provides assistance in the administration and maintenance of corporation records
Participates in key result area and key performance indicator review processes to establish areas for improvement
Maintains a high professional and ethical profile in accordance with Corporation standards of core values May also provide administrative and secretarial support to the Administration Department..
Qualifications and Experience:
A holder of Diploma in front Desk /Office Management or Customer Service Management.
A Post Graduate study in relevant field will be an added advantage.
The applicant should have an age of between 24 to 35 years.
He /She must have working experience of at least 5 years as a receptionist in a reputable organization. Experience in the real estate industry shall be an added advantage
He/she must have strong administration skills and ability to communicate at all level.
Must have ability to create a positive, everlasting impression with the most professional, courteous and expedient manner.
Must have good communication skills in both English and Kiswahili Must be computer literate
Must be customer focus and flexible team player Must have good planning and organizational skills
Very attractive REMUNERATION is offered as per NHC scheme of service.


Application Instructions:
If you think you meet job requirement, please apply in strictly confidence to the undersigned enclosing an application letter, photocopies of relevant certified certificates and names of two referees to reach the undersigned before 16th December, 2013.
Director General,
National Housing Corporation
PO.BOX 2977,
Dar Es Salaam
NB: Only shortlisted candidates will be contacted.

Office Manager
Mott MacDonald

Date Listed: Dec 3, 2013
Email Address: Click to Email
Area: Kigoma
Application Deadline: Dec 05, 2013
Start Date: Dec 16, 2013


Position Description:
The DFID-funded Education Quality Improvement Programme in Tanzania (EQUIP-T) aims to support 36 districts in their efforts to produce a better quality of primary education for more than two million children in over 3700 primary schools.

We have an exciting opportunity for an Office Manager in the Kigoma region to provide office administration, logistics and financial management support to the programme. Reporting to the Regional Team Leader you will be responsible for the supervision of an Office Support Assistant and two drivers in the Regional programme office.

Duties will include:

  • Overseeing all the administrative, financial, logistics, and facilities needs in the region;
  • Ensure that the regional office meets all the pre-set IMS (Integrated Management Systems) requirements under the direction of the Programme Operations Manager;
  • Produce regular rolling quarterly and monthly forecasts, submitting monthly site returns to the  Finance Manager in Dar es Salaam to feed into the monthly reconciliation and invoicing processes of the programme;
  • Maintain up-to-date programme accounts on the system to ensure that timely, accurate and appropriate information is available to the programme management team;
  • Liaise with administrative and technical teams to ensure accurate financial forecasting and prompt disbursal and reconciliation of expenditure;
  • Support the Regional Team Leader and/or the Regional Technical Specialists in preparing budgets for training events and workshops;
  • Supervise preparation of all payment vouchers, journal vouchers and cheques and ensure the timely settlement invoices;
  • Monitor expenditure and advise the Regional Team Leader and Programme Finance Manager of potential issues with regards to financial forecasting, disbursement or accounting;
  • Maintain a petty cash register and supervise the imprest accounts for regional based staff.
  • Work closely with all immediate colleagues and Government staff within the region to provide a high quality service to internal and external customers;
  • Ensure the maintenance of a healthy and productive work environment within the regional office.
Essential competencies/skills and qualifications
  • Degree level or equivalent
  • Relevant professional qualification in administration and office skills/ICT
  • Demonstrable experience providing administrative management to a professional team
  • Proven people management experience
  • Pro-active attitude with the ability to work under pressure
  • Excellent communication skills
Desirable
  • Previously worked within an international organisation


Application Instructions:
Please send your CV to the email link above
We receive a large number of applications so should you not hear back within 2 weeks please assume at this time that your application has not been successful.
You can also view our vacancies on our website below

Specialist/Consultant Surgeon - (Two Posts )
Shree Hindu Mandal Hospital

Date Listed: Dec 3, 2013
Email Address: Click to Email
Phone: No phone Calls
Areas: Dar Es Salaam, Mwanza
Application Deadline: Dec 17, 2013


Position Description:
From the Daily News of 3rd December 2013.
One Post - Dar es Salaam
One Post - Mwanza
Attractive remuneration package based on qualification and experience would be offered to the suitable candidate


Application Instructions:
Applications accompanied by Curriculum Vitae (CV) indicating current telephone contact/E-mail address are invited to reach the undersigned within two weeks from the date of first appearance of this advert.
The Chief Executive Officer
Shree Hindu Mandai Hospital
P.O. Box 581
Dar es Salaam.
OR
Email your applications through the email link above

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Engineer Felchesmi Mramba kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar es Salaam leo, Jumatatu, Desemba 2, 2013, na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Florens Turuka inasema kuwa uteuzi huo umeanza leo hii.

Kabla ya uteuzi wake, Eng. Mramba alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo la TANESCO.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

2 Desemba, 2013

2014-2015 Amsterdam Excellence Scholarships is now open to international students outside of EU/EEA. The fully-funded scholarship is towards selected Masters Degree Programmes offered at University of Amsterdam in Netherlands. Deadline varies depending on Faculty but is 15 January 2014 or 1 February 2014 . Course starts September 2014.


Amsterdam Excellence Scholarship

In 2014, a new prestigious scholarship programme will be launched, targeting exceptionally talented Master’s students from outside Europe. The AES is a full scholarship of €25,000 (covering tuition and living expenses) for one academic year with the possibility of extension for a second year (for two-year Master’s programmes).

Who is eligible?

Students from any discipline belonging to the top 10% of graduates from their class may apply. Selection is on the basis of academic excellence, ambition and relevance for a student’s future career. Scholarship recipients will join extracurricular activities and become part of a select community.
The application process for the 2014-2015 academic year will open in November 2013 and the deadline for applications is 15 January 2014.
Published by  Studenten Services
29 November 2013.


Requirements for eligibility

Candidates wishing to apply for an AES scholarship must meet the following requirements:
  • Hold a non-EU/EEA passport and not be eligible for support under the Dutch system of study grants and loans (Studiefinanciering; for more information please refer to www.DUO.nl). The scholarship office should be notified as soon as possible of any change in nationality, type of residence permit, and/or possible Studiefinanciering support throughout the academic year.
  • Be (provisionally) admitted to an English-taught Master’s degree programme at the University of Amsterdam which is registered in the Central Register of Higher Education Programmes (CROHO; for more information refer to: www.DUO.nl).
    For more information about general application requirements, please consult the individual programme descriptions at www.uva.nl/education for Master’s study programmes taught in English.
  • Be (provisionally) admitted to a Master's programme at the UvA for the first time. AES will not be awarded to candidates who are admitted for a second Master's programme at the UvA.
  • Be able to comply with Dutch visa regulations as indicated by the IND (Dutch Immigration Service).
  • Be enrolled at the UvA as a full-time student for the academic year and the programme for which the scholarship is awarded. Scholarship continuation is not guaranteed when a candidate changes his or her Master’s programme.
  • The candidate should not receive another scholarship for the same period of study as the AES. Notify the scholarships office when another scholarship has been awarded and accepted.

Selection criteria

Eligible candidates are selected for a scholarship on the basis of their academic excellence and promise in the proposed field as evidenced by:
  • the candidate’s academic records. Students from any discipline belonging to the top 10% of graduates from their class can apply;
  • the academic quality of the educational institute where the undergraduate (or graduate) programme has been obtained;
  • a letter of recommendation by a dean, teacher or academic supervisor;
  • the quality of the letter of motivation (maximum 500 words) in which the candidate explains the reasons for choosing the specific Master’s programme (broader context, relevance for future career);
  • a description of extracurricular activities such as participation in student commissions, international experience, sports or music at a high level or volunteer work;
  • proof of English proficiency (IELS/TOEFL) :TOEFL (internet-based) -  overall score of 100 (with a minimum score of 22 in each of the different components), IELTS (academic) - overall score of 7.0 (with at least 7.0 in each of the four components);
  • the quality of the application as a whole (completeness, accuracy, consistency).

Conditions for maintaining the AES

AES recipients must maintain good academic standing. The scholarship will only be continued if the AES student is making satisfactory progress towards the degree, i.e. complete the courses of the first semester of the first year on time with a grade point average of 8 (out of 10). At the end of the academic year, the full credit load should have been earned with a grade point average of 8 (out of 10). If the AES recipient decides to quit studying, the AES payments already received must be reimbursed in full.
Students who receive the AES for a two-year Master’s programme will be evaluated after one year of study. The scholarship will only be continued for the second year if the AES student has completed all courses of the first year on time with a grade point average of 8.0.
It is expected that AES recipients will participate in activities with AES sponsors, will join the extracurricular activities and become part of a selective community, including the AES alumni network. AES students will form a strong international network during their study period, which will be stimulated by an interesting tailor-made extracurricular programme. Their special relationship with the UvA will continue to be fostered once they become alumni. The UvA’s Alumni Office is actively involved in setting up international alumni chapters. AES alumni would be ideal candidates to play an active role in those international UvA alumni chapters, and by doing so, they will maintain a special link with the UvA and pave the way for new AES students.
The scholarship may be terminated if the recipient unreasonably refuses to participate in such activities.


 How to apply

Faculties and graduate schools offering AES

The faculties and graduate schools award scholarships themselves; as such, regulations may vary. Students interested in an Amsterdam Excellence Scholarship may contact the faculty or international school offering the study programme of their choice for more information.
































































Chuo cha BBC cha Uandishi wa Habari, (BBC Academy, College of Journalism) chafungua upya tovuti ya Kiswahili kwa ajili ya waandishi wa habari duniani kote.

Chuo cha BBC cha Uandishi wa Habari kimeanzisha upya tovuti ya Kiswahili katika mfumo (mtindo) mpya na maswala mapya.
Tovuti yenyewe inaweza kupatikana kwenye simu ya mkononi, tabiti (tablet) na komputa kubwa.

Lengo la tovuti ya Kiswahili ni kuonesha mtindo wa uandishi katika idhaa za lugha mbali-mbali zinazotangaza katika Idhaa Kuu ya Dunia ya BBC, na ni sehemu ya jukumu la BBC la kuhudumia jamii na kusambaza ujuzi wake ili kunufaisha waandishi wa habari wa Kiswahili dunia nzima.

Ali Saleh, Mhariri wa Idhaa ya Kiswahili:

"Baada ya serikali za Afrika Mashariki kuruhusu vyombo vingi vya habari binafsi kuanzishwa, vinatoa ushindani mkubwa kwa vyombo vya habari vya kimataifa. Ingawa vyombo hivyo vimestawi na kuzidi kukua, vyombo vinavyojitegemea vinakabiliwa na tishio katika nchi kadha, ambako waandishi wa habari wamekimbia kwa sababu ya kulengwa kwa mashambulio na mashtaka. Serikali katika nchi ambako BBC inasikika zinatayarisha sheria kali kupunguza uhuru wa kujieleza, haki ya kutofichua chanzo cha taarifa, na kuwafunga waandishi wa habari kwa yale waliyotangaza."
Tovuti ina maeneo matatu muhimu, ufundi wa uandishi, lugha ya Kiswahili, na maadili ya BBC.

Kupitia sehemu hii ufundiutapata ushauri kuhusu televisheni, redio na mtandao, utangazaji, uandishi, mitandao ya jamii na mengi mengineyo.

Katika sehemu hii wahariri na waandishi wa BBC wanaeleza namna ya kutangaza na kuandika taarifa za televisheni na jinsi ya kuandika ripoti kuhusu michezo. Tovuti inatoa mwongozo jinsi ya kuthibitisha habari zilizoko kwenye mitandao ya jamii.

Katika sehemu yavigezo, kuna ushauri kuhusu msimamo wa kutopendelea upande wowote, ukweli, uhuru, maslahi ya jamii, uwajibikaji na sheria.

Lakini msingi wa kila tovuti ni lugha. Sehemu yalugha inatoa ushauri kuhusu lugha isiyopendelea upande wowote, lugha sahihi, tahajia, ufupisho, majina ya kigeni na ufundi wa kutafsiri na mengineyo.

Sehemu ya lugha ya tovuti ina vielelezo vilivyotengenezwa maalumu kulingana na utamaduni wa Kiswahili. Juhudi zimefanywa kuelezea sehemu hii kwa picha zinazoonesha Idhaa iliyohusika ya BBC pamoja na wasikilizaji na watazamaji.
Pamoja na tovuti ya Kiswahili, Chuo cha Uandishi wa Habari cha BBC, (College of Journalism) piya kinaanzisha lugha tatu nyengine,Burmese,Pashto naVietnamese. Tovuti hizo nne zinafanya jumla ya tovuti za chuo cha BBC zilizoanzishwa upya kufikia 11.

Katika miaka mitano iliyopita BBC College of Journalism, imeanzisha jumla ya tovuti 27 katika lugha tofauti.
Unaweza kusoma tovuti za BBC College of Journalism bila ya kutozwa pesa kokote uliko duniani.

KATIKA miaka mitano iliyopita BBC College of Journalism, imeanzisha jumla ya tovuti 27 katika l
ugha tofauti. Unaweza kusoma tovuti za BBC College of Journalism bila ya kutozwa pesa kokote uliko duniani.

Chanzo:BBC Swahili

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA  

TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA

S. L.P. 4865,                                                                                                          
Dar es Salaam. 

Simu: 2150043-6/2150360   
Nukushi: (022) 2150047
Baruapepe: dgeneral@pccb.go.tz 
                                                                                                                   
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU ACHAGULIWA KUWA MAKAMU WA RAIS WA SHIRIKISHO LA TAASISI ZA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA DUNIANI

Wajumbe 460 wa Mkutano Mkuu wa Saba wa Shirikisho la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Duniani (International Association of Anti-Corruption Authorities – IAACA), kwa sauti moja wamemchagua Dkt. Edward G. Hoseah, Mkurugenzi
Mkuu wa TAKUKURU kuwa Makamu wa Rais wa shirikisho hilo.

Mkutano huo ambao umehudhuriwa na zaidi ya washiriki 460 kutoka nchi mbalimbali duniani umefanyika nchini PANAMA – Amerika ya Kati kuanzia tarehe 22/11 – 24/11/2013. Wajumbe wa mkutano huu ni pamoja na Wakuu wa taasisi 98 za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Duniani ambapo kauli mbiu ya mkutano huu ni “Utawala wa Sheria na Rushwa: Changamoto na Fursa Zilizopo”.

Dkt. Hoseah ambaye kabla ya kuchaguliwa kwake alikuwa ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Utendaji ya Shirikisho hilo, anakuwa Mwafrika wa kwanza kushika wadhifa huo mkubwa katika tasnia ya mapambano dhidi ya rushwa duniani.

Uchaguzi huu ni heshima kubwa kwa Tanzania na Bara la Afrika kwa ujumla.  Hii pia ni fursa nzuri kwa Tanzania kuonesha uwezo wake wa kuongoza mapambano dhidi ya rushwa kimataifa.

Nyadhifa nyingine za kimataifa ambazo Dkt. Hoseah anashikilia au aliwahi kushikilia ni pamoja na kuwa Rais wa kwanza wa Shirikisho la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Afrika Mashariki (2007-2008); Rais wa kwanza wa Jukwaa la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa katika nchi za SADC (SAFAC – 2010 - 2011) na Mwenyekiti wa Bodi ya Umoja wa Afrika ya Ushauri wa Masuala ya Rushwa (AU-ABC 2011-2012). Shirikisho la Kimataifa la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Duniani ambalo linajumuisha Taasisi 298 pamoja na wanachama zaidi ya 2,000 kutoka katika Asasi mbalimbali zisizo za kiserikali, lilianzishwa Aprili 19, 2006 na Makao Makuu yake yapo Peking, China.

Lengo kuu la kuanzishwa kwa Shirikisho hilo ni kuziwezesha nchi wanachama kutekeleza Mkataba wa Umoja wa Mataifa Dhidi ya Rushwa uliopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Desemba 30, 2003.

Imetolewa na Doreen Kapwani, Afisa Uhusiano wa TAKUKURU, Panama. Novemba 26, 2013

VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliovuliwa nyadhifa zao hivi karibuni Dkt. Kitila Mkumbo na Zitto Kabwe wamesema kwamba njama zilizotumika kuwavua madaraka ni mkakati wa viongozi wa juu wa chama katika kujipanga kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa chama unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu. MOblog inaripoti. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo asubuhi jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Serena, aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Dkt. Kitila Mkumbo amesema waraka wa siri unaojulikana kama Mkakati wa Mabadiliko 2013 uliandaliwa na kuhaririwa na yeye kwa kuwa katika siasa za ushindani kuandaaa mkakati wa ushindi si uhaini.

“siamini hata kidogo kwamba kugombea nafasi yeyote iliyo wazi ndani ya chama cha siasa ni uhaini na hujuma. Msingi namba moja wa Chadema ni Demokrasia na hakuna namna ya kudhihirisha mapenzi kwa Demokrasia zaidi ya kuruhusu ushindani katika nafasi za uongozi na hasa uongozi wa juu kabisa,” amesema Dkt. Mkumbo
Amesema kwamba viongozi wa juu wa Chadema wana hofu ya siasa za ushindani baada ya kukaribia kwa uchaguzi mkuu ndani ya chama na yeye pamoja na Samson Mwigamba wanaamini kwamba madadiliko ya uongozi wa juu wa chama ni lazima.

IMG_5201

Dkt. Mkumbo aliendelea kusema kwamba mkakati kwa ajili ya uchaguzi iwe ndani ya chama au nje ya chama ni haki ya kikatiba kwa sababu ni mkakati wa uchaguzi hata viongozi wa juu wa sasa wa Chadema walikuwa na mkakati wao katika kujiandaa na uchaguzi ndani ya chama.

“Siasa za ushindania ndani ya chama cha siasa ni kujenga Demokrasia ya kweli na kama chama kikuu cha upinzani kinakataa kujenga Demokrasia kinachoililia kila siku kwenye chama tawala ni Udikteta usiokubalika katika dunia ya leo,” alisisitiza Dkt. Mkumbo
Amesema waraka wa Mkakati wa mabadiliko 2013 uliandaliwa na watu wanne tu bila Zitto Kabwe kujulishwa ingawa alikuwa mlengwa mkuu wa mkakati ambapo waandaji walipanga kumfuata na kumshawishi ajiunge.

Kwa upande wake Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amesema kwamba hatarajii kutoka ndani ya chama na hana mpango wa kuvunja chama chake kilichomlea na kumkuza miaka nenda rudi kwa sababu yeye ni muumini mwaminifu wa chama.

Amesema kuwa cha kushangaza ni waraka wa siri uliomuhusisha yeye na viongozi wa Chama cha Mapinduzi na wa Usalama wa Taifa kwamba anatumika kuhujumu chama chake na waraka huo ulisambazwa na viongozi wa juu wa chadema kama mkakati wao wa kumdhoofisha kisiasa kuelekea mbio za kugombea uongozi katika uchaguzi wa chama mwishoni mwa mwaka huu.

Amesema sababu ya pili ni kuwakosoa viongozi wa Chadema yakutokupeleka hesabu za chama kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kamati kuu ilidai alipaswa kuwatonya kwanza kabla ya kwenda kwa umma na waandishi wa habari.
“dhamira yangu ilikataa na nitaendelea kusimamia ukweli kwamba hesabu za vyama vya siasa lazima zikaguliwe na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa fedha za Serikali kama sheria inavyotaka,” amesema
Zitto aliendelea kusema kuwa kama kuchagua kati ya chama na nchi yake atachagua nchi kwanza kabla chama na kwamba ataendelea na msimamo wake pia wa kukataa posho ya kukaa yaani (Sitting Allowance) kwa sababu analipwa mshahara na fedha za kujikimu.  

IMG_5241

Mgogoro ndani ya Chadema ulipamba moto baada ya Kamati Kuu kuwavua uongozi Zitto Kabwe na Dk Kitila Mkumbo, huku Makamu Mwenyekiti Taifa, Said Arfi akiandika barua ya kujiuzulu Ijumaa ya wiki hii.

Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wakati Dk Mkumbo amevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu. Wawili hao wanatuhumiwa kukisaliti chama.

 IMG_5274

Taarifa zilisema hoja ya kukisaliti chama pia ilimkumba Arfi akidaiwa kumwezesha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita ubunge bila kupingwa, katika uchaguzi mkuu uliopita na ndiyo sababu ya kuamua kuachia ngazi nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa.

Mbali ya kuwavua uongozi Zitto na Dk Mkumbo, pia Kamati Kuu imewapa siku 14 wajieleze kwa nini wasifukuzwe uanachama. Kwa uamuzi huo Zitto amebaki na wadhifa wa ubunge wake wa Kigoma Kaskazini na wadhifa mwingine kwenye Kamati ya Bunge.

 IMG_5252

Kujiuzuru kwa Arfi

Makamu Mwenyekiti wa Taifa, Said Arfi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, Ijumaa ya wiki hii aliwasilisha barua ya kujiuzulu nafasi ya uongozi wa chama, akisema; “…kuchoshwa na unafiki unaoendelea ndani ya chama. Napenda ifahamike pia kwangu masilahi ya wapigakura, wakazi na wananchi wa Mpanda Mjini na Wilaya ya Mpanda ni muhimu katika kuwatumikia, hivyo basi sipo tayari kuchaguliwa marafiki.

Katika barua hiyo anasema amechochwa na tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake kuwa alimsadia Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita bila ya kupingwa  katika uchaguzi wa ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita.

“Kwa kipindi kirefu zimekuwepo shutuma dhidi yangu na kutiliwa shaka uhusiano wangu na Mhe Pinda Waziri Mkuu. Pamoja na kulijadili katika vikao kadhaa Mpanda na Dar es Salaam bado yapo mashaka kwa nini alipita bila kupingwa. Huo ulikuwa uamuzi wa Wanampanda kwenu imekuwa ni tatizo, lakini hamsemi kwa nini. Majimbo mengine 16 nchini yalipita bila kupingwa mlikuwa wapi na nani alaumiwe? Huu ni unafiki  wa kupindukia.

Vilevile, katika barua hiyo, Arfi anasema amechukizwa na kauli ya mwasisi wa chama hicho, aliyemtaja kwa jina moja la Mtei kuwachagulia marafiki.

“Aidha mmechukizwa sana kwa nini nilihoji kauli ya Mwasisi wa chama, Mhe Mtei kutuchagulia viongozi.  Naomba ifahamike wazi kwamba huu ni mtazamo wangu na utabakia hivyo siku zote kwa chama cha demokrasia kutoruhusu uongozi wa kiimla kwa kukidhi matakwa ya waasisi ambao huvigeuza vyama kuwa mali binafsi.
 IMG_5364



 IMG_5373



 IMG_5365

 IMG_5398

 IMG_5429

 IMG_5417

 IMG_5434
 Chanzo cha habari na www.dewjiblog.com.
















































1. Utangulizi

Katika kikao chake cha siku mbili kilichofanyika tarehe 20 - 22 Novemba 2013, Kamati Kuu ya CHADEMA, pamoja na mambo mengine, iliazimia kunivua nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama. Kwa mujibu wa taarifa ya chama iliyotolewa katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013, ilielezwa kwamba sababu za kuvuliwa uongozi mimi na Dk Kitila Mkumbo ni uhaini na hujuma kwa chama kutokana na waraka unaojulikana kama mkakati wa uchaguzi 2013. Ukweli ni kwamba waraka uliotajwa si sababu ya mimi kuvuliwa nafasi zangu za uongozi kama ilivyojadiliwa katika Kikao cha Kamati Kuu.

Sababu za kufukuzwa kwangu kama zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ni tuhuma lukuki ambazo si mara yangu ya kwanza kuzisikia zikijadiliwa ndani na nje ya vikao vya chama. Hitimisho la tuhuma hizi ni kwamba mimi nimekuwa nikikisaliti chama kwa kutumika na CCM na Usalama wa Taifa. Nitazianisha tuhuma hizi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vyama.

Ninatambua kwamba chama changu kinapita katika wakati mgumu sana sasa hivi. Nataka nitamke mapema sana kwamba mimi Zitto Zuberi Kabwe sitokuwa chanzo cha CHADEMA kuvunjika. Hiki ndicho chama kilichonilea na kunifikisha hivi nilivyo. Ningependa chama hiki mtoto wangu atakapokuwa mtu mzima na atakapoamua kujiunga na siasa aingie CHADEMA. Bado nina imani kubwa na chama changu na ninaamini ndicho kinachostahili kuendesha nchi jana, leo na kesho.

2. Kuhusu tuhuma mbalimbali zinazo elekezwa kwangu

Zipo tuhuma nyingi ambazo zimekuwa zikirudiwarudiwa katika vikao vya chama na nje ya vikao na baadhi ya viongozi wenzangu. Tuhuma hizi zinalenga kuonyesha kwamba mimi ni mbinafsi na kwamba ninapokea rushwa ili kukihujumu chama changu. Nitazianisha tuhuma kwa kifupi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vya chama.

i) Tuhuma kwamba sikushiriki kumpigia kampeni mgombea wetu wa urais katika uchaguzi wa mwaka 2010. Ningependa kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:


  • Mimi nilikuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Kaskazini huko Kigoma.
  • Pamoja na kuwa mgombea wa ubunge, nilifanya kampeni katika majimbo mengine 16 katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dar es Salaam, Mtwara, Pwani, Shinyanga, Mara na Rukwa. Hakuna kiongozi yeyote wa juu aliyefanya kampeni katika majimbo mengi kama mimi, ukiacha mgombea urais.
  • Kote nilipopita nilimpigia kampeni wagombea wetu wa udiwani, ubunge na Rais.
  • Katika Mkoa wa Kigoma nilizunguka na mgombea urais katika kata zote za Kigoma Kaskazini na majimbo yote manane ya Mkoa wa Kigoma.

ii) Tuhuma kwamba katika Mkoa wa Kigoma nilishindwa kuwapigia kampeni wagombea wetu kiasi kwamba peke yangu ndiye niliyeshinda katika uchaguzi huo. Ukweli ni kwamba niliwapigia sana kampeni wagombea wetu, na hivyo ndivyo wapiga kura wa Kigoma walivyoamua.

iii) Tuhuma kwamba nilishiriki kuwashawishi wagombea wetu katika baadhi ya majimbo kujitoa katika uchaguzi wa mwaka 2010 ili kuwapisha wagombea wa CCM wapite bila kupingwa kwa njia ya rushwa. Majimbo yanayotajwa ni pamoja na Sumbawanga, Musoma Vijijini na Singida Mjini. Kama nilivyokwisha kueleza katika vikao mbalimbali vya chama jambo hili si la kweli na hakuna popote ambapo watoa tuhuma hizi wamewahi kutoa ushahidi kwamba nilifanya jambo hili. Nipo tayari kwa uchunguzi ndani ya chama na watoa tuhuma waje na ushahidi bayana wa jambo hili. Si afya kwa chama kuendelea kurudiarudia tuhuma hizi kila mara tangu mwaka 2010 bila uchunguzi wowote kufanyika na jambo hili lifikie mwisho.

iv) Tuhuma kwamba nimekuwa sishiriki katika operesheni mbalimbali za chama: Ukweli ni kwamba nimeshiriki sana katika operesheni mbalimbali za chama ndani na nje ya nchi. Kwa mfano, mwaka 2011 tulikuwa na operesheni kubwa katika mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na nilikwenda katika mikoa yote tuliyotembelea. Mwaka 2012 baada ya hoja ya mkonge bungeni nilifanya ziara Mkoa wa Tanga. Mwaka 2012 kulikuwa na operesheni kubwa moja katika mikoa ya kusini ya Mtwara na Lindi. Operesheni hii sikushiriki kwa sababu nilikuwa nchini Marekani kufungua matawi kwa mwaliko wa Watanzania wanaoishi huko.

v) Tuhuma kwamba nimekidhalilisha chama kwa tamko la PAC kwamba Hesabu za Vyama hazijakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG): Katika jambo hili ninatuhumiwa kwamba mimi kama Naibu Katibu nilipaswa kuwasiliana kwanza na viongozi wa chama 'kuwatonya' ili wajiandae. Kwamba kutokuwatonya kumekidhalilisha chama na kukiweka kundi moja na CCM na nastahili kuadhibiwa vikali kwa kuwa katika taarifa yangu nilikuwa na nia mbaya na chama chetu. Maelezo yangu niliyoyatoa na ambayo ningependa kuyakariri hapa kuhusu jambo hili ni kama ifuatavyo:

  • Utawala bora hautaki mimi kutumia nafasi yangu ya uenyekiti wa PAC kulinda chama changu na kuonea vyama vingine. Kufanya hivyo ni kuendeleza tabia zile zile ambazo tunazipinga na ambazo tunapigania kuzibadilisha
  • Napenda kusisitiza kwamba hakuna chama ambacho kimewahi kukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). Natambua kwamba mahesabu ya chama changu yamekuwa yakikaguliwa na wakaguzi wa nje kwa utaratibu tuliojiwekea. Lakini matakwa ya kisheria ni kwamba mahesabu ya vyama vya siasa hayajakaguliwa na CAG, na hili ni kosa la kisheria, bila kujali kosa hili ni la nani.

vi) Tuhuma kwamba mimi ni mnafiki katika kukataa kwangu kuchukua Posho za Vikao
Mtakumbuka kwamba mimi nilikataa kuchukua posho tangu mwaka 2011 kama ishara ya kuonyesha kwa vitendo msimamo wa chama chetu wa kupinga posho za kukaa na matumizi mengine yasiyofaa katika fedha za umma kama ilivyoanishwa kwenye Ilani yetu ya mwaka 2010-2015. Mtakumbuka kwamba hivi karibuni Mheshimiwa Lema amenishutumu kwamba kukataa kwangu kuchukua posho ni unafiki kwa sababu ninapokea posho kubwa zaidi katika mashirika ya umma ambapo mimi ni mwenyekiti wa kamati husika. Ninapenda kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:

  • Sipokei posho yeyote ya vikao (sitting allowance) ndani na nje ya Bunge tangu mwaka 2011. Hii ni pamoja na vikao vyote katika Kamati za Bunge ninavyohudhuria. Mtu yeyote mwenye ushahidi vinginevyo auweke hadharani.
  • Swala la kukataa posho (sitting allowance) ni swala la kiilani katika chama chetu, na kwangu ni swala la kimisingi zaidi. Katika Wilaya yangu vifo vya kina mama wajawazito ni 1900 kati ya wanawake 100,000 wenye ujauzito. Vifo hivi vinatokana na ukosefu wa huduma kwa sababu ya bajeti finyu. Ndiyo maana nilifurahi sana kwa chama chetu kuliweka swala la kupunguza matumizi ya Serikali katika Ilani, na kuondoa posho za wabunge, ambao tayari wanapokea mishahara mikubwa, kungesaidia sana kupatikana fedha ambazo zingeokoa vifo vingi vya kina mama.
  • Jambo hili si suala la ugomvi baina yangu na Mheshimiwa Lema. Ni suala la msingi katika chama chetu.


3. Usambazaji wa Ripoti ya Siri kuhusu Zitto Kabwe
Hivi karibuni kulisambazwa waraka unaoitwa ripoti ya siri kuhusu mimi ukibeba lundo la tuhuma kwamba nimehongwa fedha nyingi ili kukihujumu chama changu. Waraka huu ulidaiwa kuwa umechomolewa kutoka makao makuu ya CHADEMA. Jambo hili pia lilijadiliwa katika kikao cha juzi kwa kifupi, na majibu ya viongozi wa chama ilikuwa ni kwamba waraka huu haukuandaliwa wala kusambazwa na makao makuu. Katika mchango wangu nililalamikia mambo matatu yafuatayo:

  1. Kwamba baadhi ya waliokuwa wanasambaza waraka ule walikuwa ni viongozi wa chama chetu. Bahati mbaya hadi leo hakuna hata mmoja ambaye amekwishachukuliwa hatua za kinidhamu. Ninaamini kwamba kuna siku watu hao watachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za chama chetu.
  2. Kwa kuwa chama kimekana rasmi kuhusika na waraka huu, nitaendelea na taratibu za kisheria ili kuhakikisha kwamba wote waliohusika kutengeneza hekaya ile wanachukuliwa hatua stahiki za kisheria.


4. Hitimisho
Ninatambua kwamba kuna watu walitegemea leo ningejibu mapigo na ningewazodoa watu kwa majina kama ilivyo kawaida katika siasa za Tanzania. Natambua pia kwamba, kama ilivyo kawaida wakati wa migogoro katika vyama vya siasa hapa Tanzania, kuna watu walitegemea leo ningetangaza 'maamuzi magumu'. Natambua kwamba wapo ambao wangependa kupata nafasi ya kuendelea kutumia suala hili katika harakati zao za kudhoofisha mapambano ya demokrasia na uthabiti wa siasa za ushindani nchini mwetu. Napenda wanachama wa CHADEMA na wapenda demokrasia na siasa safi wote nchini watambue kwamba mimi bado ni mwanachama mwaminifu wa chama hiki na nitakuwa wa mwisho kutoka kwenye chama hiki kwa hiari yangu. Nitafuata taratibu zote ndani ya chama katika kuhitimisha jambo hili.

Naomba wanachama waelewe kwamba mimi kama binadamu ninaumia ninapopigwa. Tuhuma ninazorushiwa ni kubwa na zinanikwaza. Tuache siasa za uzushi ili tujenge chama chetu na nchi yetu, ili hatimaye tuwakomboe Watanzania wenye matarajio na imani kubwa kwa chama chetu.

Kama mwanasiasa kijana niliyekaa katika siasa kwa muda sasa yapo mengi mazuri nimeyafanya. Lakini kuna maeneo nilipojikwaa na yapo makosa niliyofanya kisiasa katika maisha yangu ya siasa.

Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina, waumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa majitaka. Hii ni changamoto kubwa ndani ya chama chetu inayohitaji uongozi shupavu kuikabili. Nitasimama daima upande wa demokrasia. Kama alivyopata kunena mmoja ya wanasiasa maarufu, 'kiwango cha juu kabisa cha uzalendo katika nchi ni kukubali kutofautiana kimawazo', na ninatamani huu ndio uwe utamaduni wa chama chetu.


Kabwe Zuberi Zitto, Mb
Dar es Salaam.
24 Novemba, 2013

Baadhi ya wafanyakazi wa Airtel mwishoni mwa wiki wameitembelea shule ya msingi ya Kiromo iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani na  kutoa mafunzo ya awali juu  ya matumizi ya kompyuta kwa wanafunzi wa shule hiyo.
 
Mkurugenzi wa  Idara ya Fedha wa Airtel Tanzania, Bw. Kalpesh Mehta akiwafundisha matumizi ya kompyuta baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kiromo iliyopo wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani. Wanafunzi wa shule hiyo walipata nafasi ya kujifunza kompyuta katika hatua za awali baada ya wafanyakazi wa Airtel kuitembelea shule hiyo leo.
Wafanyakazi hao wamedai kuwa kujitolea kwenda kutoa mafunzo katika shule hiyo ambayo ilijengwa na kampuni yao kupitia mradi wa shule yetu sio jambo la msimu tu kwani wana mpango wa kuendelea kutoa huduma hiyo mara kwa mara katika shule mbalimbali nchini.

Mkurugenzi wa idara ya Fedha ya Airtel, Bw. Kalpesh Mehta alisema Airtel inaelewa wazi ni jinsi gani matumizi ya vifaa kama kompyuta hurahisisha kazi nyingi katika jamii na hivyo imeamua kwenda kutoa mafunzo ya ujumla kwa wanafunzi wa shule hiyo kwa dhumuni la kuleta mchango chanya kwenye jamii.

“Kompyuta ni kifaa muhimu sana ambacho hurahisisha kazi mbalimbali zinazofanywa kwa ajili ya maendeleo ya jamii hivyo inabidi wanafunzi waanze kujifunza juu ya umuhimu wa kifaa hiki mapema katika kusaidia maendeleo ya jamii huko mbeleni.” Alisema Mehta.

Kwa upande wake Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya Kiromo, Bw. Joseph Ngunangwa alisema masomo hayo yametoa hamasa kubwa sana kwa wanafunzi wa shule hiyo kwa sababu yamewafanya wahisi masomo hayo yana urahisi na sio magumu kama walivyokuwa wakifikiria.

“Wanafunzi walikuwa na mitazamo kwamba wanaojifunza kompyuta ni tabaka flani tu la watu na walikuwa wakihisi kwamba kompyuta ni somo gumu lakini leo  wametiwa moyo na wafanyakazi wa Airtel na wameanza kuona kuwa somo hilo ni rahisi na yeyote anaweza kulisoma na kufaulu vyema,” alisema Pangahela.

Mwalimu huyo aliongeza kuwa kupitia masomo hayo idadi ya wanafunzi watoro imepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na sababu kuwa wengi huja shule kwa ajili ya kujifunza kompyuta.

Kwa upande wao wanafunzi wa shule ya Kiromo waliwashukuru wafanyakazi wa Airtel kwa kuonesha ukarimu mkubwa sana na kusema kuwa wanatamani masomo hayo yangekuwa yanafanyika kila siku.

Si mara ya kwanza kwa wafanyakazi wa Airtel kuzitembelea shule na kutoa mafunzo kama hayo vile vile Kampuni hiyo hutoa misaada ya vitabu mbalimbali vya kiada nchini na kuchangia katika ujenzi wa taifa hususani katika sekta ya elimu.





























































Hadi tunawaletea habari hizi ni kwamba mkutano wa waandishi wa habari na aliyekuwa katibu mkuuu wa chama kikuu cha upinzani Tanzania Chadema unaendelea katika hoteli ya serena jijini Dar Es Salaam na habari zilitofikia kutoka ndani huko ni kwamba Mhe. Mbunge wa Kigoma Kaskazini Bwana Zito Kabwe ameapa kupambana akiwa ndani ya chama mpaka tone la mwisho.
 
Amesema atajiuzulu ngoo na huku akipinga shutuma zote za kuvuliwa madaraka yake ndani ya chama hicho moja baada ya nyingine.

Tutawaletea habari kamili hapo punde.


Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.