April 2014


The University of Luxembourg seeks to hire an outstanding doctoral researcher at its Interdisciplinary Centre for Security, Reliability and Trust (http://wwwen.uni.lu/snt [1]) (SnT).



The successful candidate will participate in the activities of the SaToSS (http://satoss.uni.lu [2]) research group led by Prof. Dr. Sjouke Mauw. The SaToSS group is working on formalizing and applying formal reasoning to real-world security problems and trust issues. The research topics of the group include: security protocols, security modeling, formal methods for security, socio-technical aspects of security, risk management, privacy, verification, etc. 



Your role

--------------

The position is within the national project Attack-Defense Trees: Theory Meets Practice (ADT2P). ADT2P is a follow-up project of a recently finalized project Attack Trees (http://satoss.uni.lu/projects/atrees/ [3]). The main tasks of

The Ph.D. student will be to

- Develop techniques for efficient representation of large-scale

 security models,

- Introduce algorithms for quantitative analysis of such models,

- Integrate the developed techniques with existing risk assessment

  methods and tools,

- Implement the obtained results in a computer tool,

- Conduct case studies together with the project partners from

 industry,

- Co-supervise master students.



Your Profile

----------------

The candidate is expected to have:

- A Master degree in computer science or mathematics,

- A proven interest in security,

- Background in formal methods,

- Excellent written and oral English skills.



  We offer

-----------

The University offers a three year appointment (extension up to 4 years in total is possible). The University offers highly competitive salaries and is an equal opportunity employer. You will work in an exciting International environment and will have the opportunity to participate in the development of a newly created research center.



Application

---------------

Applications should be written in English and include the following

documents:

- Cover letter indicating the research area of interest and your

  motivation,

- Curriculum Vitae (including your contact address, work experience,

  list of publications),

- A research statement addressing the topic of the position (max 1

  page),

- A short description of your Master work (max 1 page),

- Transcript of grades from all university-level courses taken,

- Contact information for 3 referees.



Applications should be submitted electronically via the on-line

recruitment portal of the University of Luxembourg at




Deadline for applications: June 22, 2014.



Contact information

-----------------------

For further inquiries please contact: 

Prof. Dr. Sjouke Mauw (sjouke.mauw@uni.lu [5]) or 

Dr. Rolando Trujillo Rasua (rolando.trujillo@uni.lu [6])



For more information about this vacancy please check 




Links:

------





[5] mailto:sjouke.mauw@uni.lu


Mabingwa watetezi na mbingwa wa ligi kuu ya Ujeruman timu ya Bayern Munich jana usiku ilijutia ushiriki wake katika mashindano ya mwaka huu mara pale baada ya kukutana na kipigo kikali toka timu ya Real Madrid ya Uhispania mara baada ya kufungwa magoli 4-0 katika mchezo wa marudiania ya mashindano ya Klabu Bingwa ya Ulaya katika hatua ya Nusu Fainali.

Itakumbukwa juma moja lilipita mabingwa hao wa bavarian walikubali kipigo cha bao moja pasipo majibu katika mchezo wao wa kwanza wa mashindano hayo uliochezwa mjini madrid na hivyo kuhitimisha kwa kutolewa kwa jumla ya mabao 5-0.

Alikuwa ni mchezaji bora wa dunia na timu ya taifa ya Ureno Christiano Ronaldo na Sergio Ramos beki toka Brazili waliopelekea kipigo hicho ambacho ni moja kati ya ushindi iliyoupata timu hiyo tokea mwaka 2002.

Iliwachukua dakika 34 Real Madrid kuandika bao lao tatu kupitia kwa nyota wake Christiano Ronaldo mara baada ya kupata pasi murua toka kwa Gareth Bale na kufanya kuongoza kwa mabao 3-0 mara baada ya beki Sergio Ramos kuwa tayari ameshaidakia timu hiyo mabao amwili kupitia kwa kichwa na kufanya mabingwa wao kulitazama taji lao la kumi ya mshindano hayo.


Ronaldo scored his 15th and 16th Champions League goals of the campaign


Ramos rises high to bullet a header past Neuer










































TIMU ZILIKUWA HIVI:
 
NYOTA WA MCHEZO— SERGIO RAMOS (Real Madrid)
Bayern Munich: Neuer 4, Dante 0, Ribéry 4 (Götze 72, 5), Mandzukic 5 (Martínez 46, 6), Robben 6, Boateng 3, Lahm 3, Müller (Pizarro 72, 5), Alaba 3, Schweinsteiger 5, Kroos 5.Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Van Buyten, Rafinha, Raeder, Hojbjerg.

Kadi ya njano: Dante.
Real Madrid: Casillas 7, Pepe 8, Ramos 9 (Varane 75, 6), Coentrão 8, Ronaldo 9, Benzema 8 (Isco 80, 6), Bale 9, Alonso 8, Carvajal 8, Modric 8, Di María 8 (Casemiro 84, 5). Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Diego López, Marcelo, Morata, Illarra.
Kadi ya njano: Alonso.
Ref: Pedro Proença (Portugal
















































AFISA Mmoja wa polisi mwanamke nchini Kenya amepewa onyo kali kwa kuvalia sketi iliyokuwa imembana kiasi cha kuonyesha umbo lake.

Wakuu wake walichukua hatua ya kumuonya polisi huyo baada ya picha yake kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii na kupigiwa gumzo kubwa.
Alipigwa picha akiwa amevalia sketi yake fupi na yenye kumbana akiwa anashika doria katika eneo ambako mashindano ya magari yalikuwa yanafanyika eneo la Kati mwa Kenya.
 
Afisa Linda Okello akiwa kazini
Afisa huyo kwa jina Linda Okello, alitakiwa kufika mbele ya Mkuu wake James Mugeria na kuonywa vikali dhidi ya kuvalia hivyo kwa mara nyingine, kitendo ambacho alifahamishwa kuwa ni utovu wa nidhamu kwa kuvalia nguo isiyo ya heshima kwa polisi

Maafisa mjini Kiambu wamesema kuwa kupewa onyo kwa afisa Linda na kuonywa dhidi ya kuvalia sketi yake iliyokuwa imembana sana ni jambo la kawaida na kwamba ameruhusiwa kuendelea na majukumu yake.
Waliongeza kuwa afisa huyo ameamrishwa kuanza kuvalia kiheshima.
Alipigwa picha na mwanahabari mmoja wa gazeti moja maarufu nchini Kenya akiwa na wenzake kazini mjini Kiambu. Lakini punde si punde picha hiyo ikaanza kusambazwa kwa mitandano ya kijamii na baadhi wakiikejeli.

Taarifa ya polisi huyo kuonywa ilizua hasira kwenye mitandao ya kijamii baadhi wakihoji ikiwa ni makosa kwa afisaa wa polisi kuvalia sketi ya kumbana. Nini Kauli yako?


ASKARI Polisi wanne wa kituo cha Polisi Singida mjini na wakazi 14 wa kijiji cha Utaho tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi mkoani Singida,wamefariki dunia baada ya kugongwa na basi la kampuni ya summry T.799 BET aina ya nissan.
 
Miili ya marehemu wa ajali hiyo
Tukio hilo limetokea aprili 28 mwaka huu saa 2.45 usiku katika barabara kuu Singida-Dodoma eneo la kijiji cha Utaho wilaya ya Ikungi.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida,SACP.Geofrey Kamwela askari hao ni F.849 D/CPL Boniface Magubika,F.6837 Pc Jumanne Mwakihamba,G.7993 Pc Novatus Tarimo na G.8948 Pc Michael Mwakihaba.
Alitaja wengine waliofariki kuwa ni pamoja na Ramadhani Mjengi afisa mtendaji wa kijiji cha Utaho,Paul Hamisi mwenyekiti wa kijiji cha Utaho,Ernest Salanga,mwenyekiti wa kitongoji cha Utaho,Saidi Rajabu,Usirika Itambu,Chima Mughenyi,Slim Juma,Abeid Ramadhani,Mwinyi Hamisi na Issa Husein wote wakazi wa kijiji cha Utaho.


Aidha.Kamwela amesema kuwa miili ya watu wengine bado haijatambuliwa na imehifadhiwa kwenye chumba cha maiti cha hospitali ya mkoa mjini Singida.
Akizungumuzia juu ya ajali hiyo,kamanda huyo amesema kuwa awali kijana Gerard Zephania (24) akiwa ametoka kusaga nafaka aligongwa na gari la mizigo ambalo bado halijafahamika na kufariki papo hapo.
"Askari wa polisi wakitumia gari PT 1424,walifika eneo la tukio kwa ajili ya kuubeba mwili wa Gerard kuuleta katika hospitali ya mkoa kwa uchunguzi,kundi la wananchi wa kijiji cha Utaho nao walifika eneo la tukio",amesema na kuongeza;


"Wakati askari polisi wakiwa kwenye harakati ya kuupakia mwili huo ghafla basi la summry liliacha njia na kuingia kushoto mwa barabara kwa nia ya kulikwepa gari la polisi na ndipo lilipovamia na kugonga kundi la watu hao wakiwemo askari polisi.Watu 15 walifariki papo hapo",amesema Kamwela.
Kamanda Kamwela amesema kuwa dereva wa basi hilo Paulo Njilo mkazi wa Dar-es-salaam hakuweza kusimamisha basi hilo nadi kilomota 25 alipolisimamisha na yeye kutorokea kusikojulikana.

Aidha,amesema ajali hiyo imesababisha majeruhi nane ambapo wawili kati yao wamelazwa katika hospitali ya mkoa na hali zao zinaendelea vizuri.Majeruhi wengine sita wamelazwa katika hospitali ya misioni ya Puma na hali zao sio nzuri.

"Uchunguzi zaidi juu ya ajali hiyo unaendelea ili kujua chanzo halisi cha tukio pamoja na kumtafuta dereva wa basi ili aweze kuhojiwa na kisha hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake",amesema Kamanda Kamwela.
Na Nathaniel Limu, Singida

MWISHO.

Askari sita wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika wilaya za Rungwe na Mbeya waliofahamika kwa majina Coplo Johnson, PC Raymond, PC Simona, PC Shaaban, PC Kajolo na Sajini Hezron, wamefukuzwa kazi kwa tuhuma za kushawishi, kuomba na kupokea rushwa, blogu ya Mbeya Yetu imeripoti.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ahmed Msangi amenukuliwa akisema kuwa askari hao walifikishwa katika Mahakama ya Kijeshi na Hukumu kutolewa Aprili 24 mwaka huu na adhabu yao ikawa ni kufukuzwa kazi.

Aidha, askari wengine waliofukuzwa kazi hivi karibuni ni pamoja na PC James Kagomba aliyehukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa kosa la wizi wa kutumia silaha.

WP Prisca Kilwai anayekabiliwa na kesi ya wizi wa mtoto.

DC Marcelino Venance Na. 8084, PC Juma Idd Na. 3117 na askari mgambo MG Jackson Mwakalobo waliohukumiwa kifungo cha mwaka 1 kwa kosa la kusababisha kifo cha Dentho Kajigili, aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Ivumwe, Mbeya. 


Chanzo cha habari na mtandao wa www.wavuti.com

HOTUBA YA MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI WA KUWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA HOSPITALI YA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI MUHIMBILI, KAMPASI YA MLOGANZILA, TAREHE 24 APRILI 2014

Mheshimiwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini;
Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi;
Waheshimiwa Mabalozi;
Waheshimiwa Mawaziri;
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam,
Professa Ephata Kaaya, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili.
Viongozi na Watendaji wa Serikali,
Viongozi na Wanajumuia wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;



Shukrani
Awali ya yote, napenda kukushukuru Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kunialika kuja kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya kisasa ya kufundishia na kutolea huduma katika eneo hili la Kampasi mpya ya Chuo Kikuu cha Afya Sayansi Shirikishi Muhimbili, Mloganzila. Leo ni siku ya aina yake katika historia ya Chuo Kikuu cha Muhimbili na taifa kwa jumla. Kitendo hiki cha leo kinaashiria kuanza rasmi kwa kazi ya ujenzi wa Kampasi mpya ya Mloganzila ya MUHAS na ni kubwa katika uboreshaji wa huduma ya afya nchini. Shughuli hii kufanyika leo kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wetu ni jambo stahiki kabisa. Ujenzi huu ni moja ya kielelezo thabiti cha juhudi na mafanikio ya Serikali yetu, katika kuwapatia Watanzania huduma bora zaidi za afya.


Hali ya Sekta ya Afya Wakati Tunaungana
Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana;

Utoaji wa huduma bora za afya ni wajibu wa msingi wa Serikali yetu na uhai wa taifa letu. Wakati tulipoungana tarehe 26 Aprili, 1964, hali ya huduma ya afya ilikuwa duni na afya ya wananchi wetu haikuwa ya kuridhisha. Kulikuwa na hospitali chache mno, halikadhalika, vituo vya afya na zahanati zilikuwa chache sana. Iliwalazimu wananchi kutembea umbali mrefu sana kutafuta huduma za afya. Katika vituo hivyo vya kutolea huduma za afya vifaa vya uchunguzi na vifaa tiba vilikuwa haba na duni. Wataalamu wa fani mbalimbali za afya walikuwa wachache sana. Watu walikuwa wanakufa siku si zao kwa maradhi yanayoweza kuzuilika na kutibika. Umri wa wastani wa kuishi ulikuwa miaka 35. Kwa ajili hiyo, Serikali zetu zilitangaza maradhi kuwa moja ya maadui watatu wakubwa, wengine wakiwemo umaskini na ujinga. 


Katika kipindi cha miaka 50 ya muungano, Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimepambana na adui maradhi kwa nguvu kubwa. Tumetoa kipaumbele cha juu katika kupanua na kuboresha huduma za afya. Hii imejidhihirisha kwa sera na mikakati mbalimbali ya afya inayotekelezwa, ukubwa wa bajeti za afya zinazotengwa, idadi ya miradi inayotekelezwa na matokeo mazuri yanayopatikana kutokana na juhudi hizo za Serikali. 


Mafanikio ya Miaka 50 ya Muungano katika Sekta ya Afya


Ndugu Wananchi;
Jitihada zilizofanyika katika miaka 50 iliyopita zimewezesha kuongezeka kwa zahanati, vituo vya afya na hospitali, vifaa vya uchunguzi, vifaa tiba na wataalamu wa kada mbalimbali za afya. Kutokana na juhudi hizo, idadi ya Watanzania wanaopata huduma bora za afya katika ngazi zote imeongezeka sana na ushindi dhidi ya maradhi mengi unaonekana. Uwezo wetu wa kupambana magonjwa yanayoua watu wengi nchini umefikia mahali pazuri, na ule wa kuchunguza na kutibu maradhi yanayotulazimu kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi unaendelea kuimarika. Kwa mfano, maambukizi ya ugonjwa wa malaria kwa watoto na akina mama wajawazito yamepungua kwa asilimia 50, na kule Zanzibar maambukizi ya malaria ni asilimia 0.3. Maambukizi ya UKIMWI yamepungua kutoka asilimia 18 mwaka 1986 hadi kufikia asilimia 5.1 hivi sasa. 


Tunaendelea kuimarisha vituo vya kutoa huduma ya afya kuanzia zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya, mikoa, kanda na taifa kwa majengo, vifaa tiba, vifaa vya uchunguzi na wataalamu. Katika ngazi ya taifa kwa mfano, tumepiga hatua ya kutia moyo kwa maradhi ya moyo, figo, saratani, mifupa, ubongo na mishipa ya fahamu. Kwa upande wa maradhi ya moyo tumejenga kituo cha tiba na mafunzo ya magonjwa ya moyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili yenye vitanda 100. Kituo hiki kinawezesha wagonjwa wa moyo wengi kupata matibabu hapa hapa nchini badala ya kupelekwa nje. Katika kipindi cha mwaka mmoja cha ufanyaji kazi wake, kituo hiki kimeweza kufanyia upasuaji wagonjwa 347, kuwawekea mashine za kuongeza nguvu kwenye moyo (pacemaker) wagonjwa 3 na mwaka huu wameanza uwekaji wa vyuma vidogo (stent) katika mishipa ya damu ya moyo ambayo imebana. Haya ni mafanikio makubwa na ya kutia moyo.
Kwa upande wa figo, hivi sasa tunatoa huduma za magonjwa ya figo katika Hospitali ya Muhimbili, Hospitali ya Kanda, Mbeya na Shule ya Tiba ya Chuo Kikuu cha Dodoma. Pale Chuo kikuu cha Dodoma pia tunajenga kituo kikubwa kitakachobobea kwenye maradhi ya figo. Lengo letu ni kwamba, kitakapokamilika chuo hiki kiweze kufanya matibabu ya kubadilisha figo (kidney transplant). 


Aidha, tumeboresha taasisi ya saratani ya Ocean Road kwa mejengo, vifaa na wataalamu. Tumeongeza maradufu uwezo wa taasisi hiyo kulaza wagonjwa kutoka wagonjwa 120 mwaka 2011 hadi wagonjwa 290 hivi sasa. Halikadhalika, tumenunua mashine mpya kwa ajili ya uchunguzi na tumeongeza wataalamu waliobobea wa magonjwa ya saratani. Vilevile, tunakamilisha ujenzi wa jengo la Taasisi ya Mifupa, Ubongo na Mishipa ya Fahamu. Litakapokamilika tutaliwekea vifaa vya kisasa vya uchunguzi na tiba ili kuongeza uwezo wetu wa kukabiliana na maradhi haya.
Ujenzi wa Hospitali ya Kufundishia ya Kampasi ya Mlonganzila


Ndugu Wananchi;

Jiwe la msingi tunaloweka leo, ni mwendelezo wa juhudi hizi za Serikali za kupambana na adui maradhi. Hospitali hii itakuwa na vitanda 600, itakuwa na vifaa tiba vya kisasa kabisa kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya mishipa ya fahamu. Ujenzi wa Hospitali ya Kampasi hii utasaidia sana kupunguza msongamano kwenye hospitali ya rufaa ya Taifa ya Muhimbili na za rufaa zilizopo nchini, ambazo hutoa huduma za utaalamu wa juu. Aidha, itasaidia kupunguza ulazima wa kupeleka wagonjwa nchi za nje kwa ajili ya matibabu. Matibabu nje ya nchi ni gharama kubwa kwa Serikali, lakini pia fursa zenyewe ni chache na wengi wengi hawapati nafasi ya kupelekwa nje kwa matibabu. Hivyo ujenzi wa hospitali hii ya Chuo Kikuu cha Muhimbili ni ishara ya wazi ya dhamira ya serikali katika kukabiliana na tatizo hili.

Hatua Zilizochukuliwa na Serikali Katika Ujenzi wa Kampasi na Hospitali ya Kufundishia


Ndugu Wananchi;

Baada ya Chuo Kikuu cha Muhimbili kutafuta eneo la kupanua huduma zake, mwaka 2006 nilifanya uamuzi wa kuwapatia eneo hili lenye ukubwa wa ekari 3,800 kwa ajili ya kujenga Kampasi mpya na hospitali ya kisasa ya kufundishia na kutolea huduma. Tulianza kutafuta fedha za ujenzi wa hospitali ya kufundishia, tukafanikiwa kupata mkopo wa riba nafuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini wenye thamani ya dola za Marekani milioni 76.5. Mkopo huo ungetosheleza kujenga jengo la hospitali hiyo pamoja na vifaa vya kisasa vya kutosheleza mahitaji ya hospitali.
Ujenzi haukuweza kuanza kwa wakati kutokana na mgogoro wa ardhi uliokuwepo katika eneo hili. Matokeo ya ucheleweshaji huo umepandisha gharama za ujenzi kwa dola za Marekani milioni 18. Maana yake ni kuwa fedha za mkopo tulizopata hazitoshi tena kukamilisha jengo hilo na kununulia vifaa kama ilivyokusudiwa. Viongozi wa Chuo Kikuu cha Muhimbili waliponijia nilikubali bila kusita kwamba Serikali itaongeza hizo dola milioni 18 zinazohitajika. Niwahakikishie kuwa tutatoa fedha hizo ili ujenzi ukamilika kwa kiwango kilichotarajiwa.


Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana;

Ni mategeneo ya Serikali kuwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Kampasi hii, Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili kitakuwa na uwezo wa kuongeza udahili wa wanafunzi wa fani mbalimbali za afya kutoka takribani wanafunzi 3,000 na kufikia wanafunzi 15,000. Hii itapunguza kwa kaisi kikubwa, kama si kumaliza kabisa uhaba mkubwa wa wataalam wa fani za afya ulioko nchini kwa sasa. Aidha, ni mategemeo yangu pia kuwa wakati ujenzi utakapokamilika idadi ya wanafunzi wa shahada za uzamili na uzamivu itaongezeka kwa kiasi kikubwa na hivyo kuongeza idadi ya wataalamu waliobobea wa fani mbalimbali za afya.


Hitimisho
Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana;


Kwa kumalizia, napenda kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini kwa kutupatia mkopo wa ujenzi na vifaa vya hospitali hii. Mkopo uliotolewa ni mkopo wenye riba nafuu ambao kama usingepatikana ingebidi tutumie fedha iliyopangwa kwa ajili ya miradi mingine kwenye ujenzi wa hospitali hii. Napenda kuwashukuru wananchi wa maeneo ya Kwembe na Mloganzila kwa kutoa ushirikiano katika mradi huu. Mradi huu ni moja ya kielelezo cha mafanikio ya Muungano wetu wa Miaka 50, tuutunze utakapokamilika ili utufae kwa miaka 50 mingine. Nawatakieni kila la heri katika kusherehekea miaka 50 ya Muungano wetu.

POSITION DESCRIPTION:

From the Daily News of 25th April
The Cooperative Audit and Supervision Corporation (COASCO) is a public organization which was established under the parliament Act No. 15 of 1982. The main objective of establishing the Corporation is to provide Auditing and supervision service to cooperative societies in Tanzania Mainland until 2005 when the law was amended to allow COASCO to provide Auditing and Consultancy services to iQclude Non Cooperative entities. COASCO has 15 regional offices in Arusha, Mara, Kaqera, Mwanza, Mbeya, Iringa, Dar es Salaam, Mtwara, Ruvuma, Kilimanjaro, Tabora. Shinyanga, Morogoro, Dodoma and Tanga with Headquarter in Dodoma.
COASCO invites applications from suitable qualified Tanzanians to fill the following vacancies.

Assistant Auditor Grade II (5 VACANCIES)
i) Qualifications and Experience
Holder of a Degree or Advanced Diploma in Accounting from recognized institutions.
Capable of undertaking external audits of different clients including Cooperatives, Must be computer literate.
ii) Duties and Responsibilities
Conduct audits of clients and issue audit reports Provide supervisory and advisory services to clients Periorm any other duties as directed by the employer
iii) Remuneration:
According to COASCO salary scales (Le. COASS 4)

iv) Age Limit: Not above 35 years



APPLICATION INSTRUCTIONS:

Applications should be accompanied with Curriculum Vitae (Cv), copies of educational and professionals' certificates, two passport size, names of three referees, email addresses and reliable telephone/mobile phone numbers should be sent to under mentioned address in two weeks time from the first day of this advertisement. Statements of results are not allowed.
Director General, COASCO,
P. O. Box 761,
DODOMA.




if you are qualified for this position
Please Follow the Application Instructions

Mchezaji wa timu ya Barcelona na timu ya Taifa ya Brazil, Dani Alves jana usiku alijibu kwa aina yake ubaguzi wa rangi uliolekezwa dhidi yake kwa kuila ndizi iliyokuwa amerushiwa wakati akijiandaa kupiga mpira wa kona katika mchezo ulioshirikisha timu yake ya Barcelona na Villareal na kutoa washindi wa mabao 3-2.

Katika kuelezea tukio hilo mchezaji huo alitabanaisha ya kuwa anamshukuru sana mtu huyo aliyerusha ndizi hiyo kwa kusema ya kwamba ilimpa nguvu zilizomsaidia kupiga mipira niwili ya krosi zilizoisaidia timu yake kupata mabao.



Tanzania ni nchi ya nne duniani kwa wagonjwa wa sikosel.

TAASISI ya Sikoseli Tanzania imewaomba wadau wengine wa afya nchini kujiunga katika mapambano ya ugonjwa wa seli moja yaani sikoseli kwa sababu utafiti unaonyesha kati ya watoto 8,000 hadi 11,000 kuzaliwa na ugonjwa huo nchi nzima.
Makamu Mwenyekiti wa Mfuko wa Sikoseli Tanzania, Dk Julie Makani akihojiwa na waandishi wa habari katika hafla ya kuhamsidha jamii kuhusu ufahamu wa ugonjwa wa sikoseli 'seli mundu' iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Ugonjwa  wa sikoseli hurithiwa kutoka kwa wazazi wote wawili wenye
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye kampeni ya kuhamasisha mapambano dhidi ya ugonjwa ambao uliandaliwa na taasisi mbili za Sikoseli Tanzania na Little Fingers Music mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Sikoseli Tanzania, Dkt Julie Makani alisema kwamba hospitali ya taifa Muhimbili kupokea wagonjwa mia kila wiki ambapo ni asilimia ishirini tu nchi nzima.

Alisema kwamba ugonjwa huo ni wakurithiwa kutoka kwa wazazi baba na mama kwenda kwa mtoto na Tanzania ni nchi ya nne duniani kuwa na wagonjwa wengi wa sikoseli na kama hatapata ufumbuzi wa kukabiliana nao mapemna asilimia tisini na tano ya watoto watakaozaliwa wanaweza kufa kabla ya umri wa miaka mitano.


“nadhani ni wakati muafaka kwa makampuni, wawakilishi wa nchi mbalimbali na wadau wa sekta ya afya kuja kuunga mkono mapambano haya ya sikoseli nchini,’ alisema

Dkt Makani aliongeza kuwa hospital ya Muhimbili wamefungua kitengo maalum kwa ajili ya kuhudumia watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kwa msaada wa mashirika mbalimbali ikiwemo la Welcome Trust kutoka Uingereza ambao wanawapatia kiasi cha dola za kimarekani 250,000 kwa mwaka

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Little Fingers Music, Veronica Eyakuze alisema kwamba shirika lake la mafunzo ya muziki limeamua kusaidia watoto wenye matatizo na ugonjwa huo kwa njia ya kufundisha kupiga muziki, piano, gitaa na kazi zingine za muziki katika kuhamasisha mapambano dhidi ya ugonjwa huo

“sisi katika Little Fingers Music tupo mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo kwa miaka mingi na kusaidia watoto wenye matatizo hayo kwa kuwafundisha kupiga muziki ili wajue kwamba wanaweza kufanya shughuli yeyote na kuibua vipaji vyao,’ alisisitiza 
Mkurugenzi wa Kituo cha Little Fingers Music, Veronica  Eyakuze akizungumza na waandishi wa habari katika hafla hiyo.

Naye Arafa Said Salim (27) binti aliyezaliwa na ugonjwa huo, alisema kwamba ameanzisha taasisi yake ya kupambana ugonjwa huo kwa ajili ya kuhamasisha jamii kwamba ugonjwa huo unaweza kuishi nao bila matatizo yoyote.
Mmoja wa wagonjwa wa sikoseli, Arafa Said Salim ambaye pia ni muasisi wa Jumuiya ya wagonjwa wa Sikoseli Tanzania (CDPCT) akizungumza kuhusu ni jinsi gani mtu anayeugua ugonjwa huo anaweza kuishi maisha ya kawaida.
Mmoja wa wagonjwa wa sikoseli, Arafa Said Salim akipozi kwa picha na mumewe, Salim Msaky ambaye yeye hana sikoseli hafla hiyo. Hiyo ni kuonyesha kuwa mgonjwa wa sikoseli anaweza kuolewa ama kuoa mwenza asiye na ugonjwa huo bila kuleta madhara kwake.

“nimeanzisha taasisi yangu ya Wagonjwa waishio na Sikoseli Tanzania katika juhudi zangu binafsi za kuelimisha jamii kwamba ni muhimu kujua mapema na kuweza kuishi na ugonjwa katika maisha ya raha na marefu,” alisema Arafa alisema kwamba yeye binafsi ameolewa na anaweza kuishi na mumewe bila matatizo yoyote na ana matumaini anaweza kupata mtoto asiye na ugonjwa huo.

Aliongeza pia kwa miaka takribani kumi tangu kitengo cha sikoseli kufunguliwa katika hospitali ya Muhmbili utafiti umeonyesha kwamba vifo vya watoto chini ya miaka mitano vinapungua.

Mwisho.

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.