MVUA zinzazoendelea kunyesha katka maeneo mbalimbali ya nchi na takribani jijini Dar Es Salaam katika  siku tatu zilizopita na za leo hii zimezidi kuharibu miundombinu ya sehemu kubwa la jijini Dar es Salaam na vitongoji vyake achilia mbali sehemu nje kidogo ya jiji hili mkoa wa pwani ambao daraja la Ruvu liliharibika na kuleta adha kubwa watumiaji wa barabara hiyo ya morogoro road.

zikiwa zikichagizwa pia na miundo mbinu hafifu au mibovu hasa katika ya jiji la Dar Es Salaam kama ilivyoshuhuhudiwa leo hii na mwandishi wa habari hii katikati ya jiji katika  eneo la Posta mpya karibu na stendi za mabasi yaendayo mwenge ambapo mvua iliyoshesha kwa takribani  dakika kumi (saa sita na dakika 20 hadi sita na nusu) na kuacha maeneo hayo yakiwa taabu tupu kwa waendao kwa miguu na waendeshao vyombo vya moto.
Mvua iliyoyesha leo majira ya sita mchana kwa takribani dakika 15 na kufanya eneo hili la posta mpya kushindwa kupitika


Kimsingi kero imekuwa kubwa kuingia katika ya jiji la Dar es Salaam na kutoka kwa sababu ya foleni ya magari na mifereji yote ya maji imezibuka kwa hiyo ni maji kila kona ya mtaa kati kati ya Posta na Kariakoo.


Ingawaje, wizara ya Ujenzi imesema kuwa asilimia kubwa ya miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko haikujengwa chini ya kiwango kama inavyodaiwa, bali ni matokeo ya uharibifu wa mazingira.


Akizungumza na moja ya gazeti la kila siku hapa nchini, Msemaji wa wizara hiyo, Martin Ntemo amesema madaraja mengi yaliyoharibiwa na mvua zinazoendelea nchini yameliwa katika makutano na barabara na si kumeguka.


“Mito mingi imechepuka katika mikondo yake ya zamani kutokana na uharibifu wa mazingira unaofanywa na wakazi wa maeneo hayo kila kukicha.,” amesema na kuongeza:


“Pia asilimia kubwa ya madaraja hayo yameshuka katika urefu wake wa awali kutokana na mchanga unaosababishwa na mmonyoko wa udongo, hivyo kupunguza sehemu iliyokuwa imekadiriwa kwa maji kupita.”
Mvua ya dakika kumi tano iliyonyesha leo na huu nndiye hali halisi ilivyokuwa kwa watumia barabara hiyo wa miguu na wa magari


Aliongeza kuwa madaraja na barabara hizo nyingi zilikuwa zimeshakabidhiwa muda mrefu kwa Serikali na kwamba Wizara inaendelea kutafuta suluhu ya kuyarudisha katika hali yake ya kawaida.

Mvua zinazoendelea kunyesha nchini zimeendelea kuharibu miundombinu mbalimbali ya barabara ambapo mawasiliano kati ya Jiji la Dar es Salaam na mikoani yalikatika kutokana na madaraja kuharibika na kufurika maji.
Mvua iliyonyesha leo jumatano majira ya sita mchana, uonekano wa eneo hili maaruf kwa magari ya mwenge posta


“Tulikuwa na wakati mgumu katika Daraja la Mpiji kutokana na uhaba wa mawe, lakini tayari tumeshapata sehemu ambayo malori yatakuwa yakichukua na kupeleka eneo la ujenzi,” amesema Ntemo.


Amesema walifanikiwa kupata mawe eneo la Wazo Hill na viunga vyake ambayo yatasaidia kukamilisha ujenzi wa daraja hilo lililopo Barabara ya Bagamoyo kufikia leo asubuhi au mchana.










Mwisho
















































































































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.