Wiki moja kabla ya kusitishwa huduma za programu ya kompyuta (OS) ya Windows Xp, imefahamika kuwa waathirika wakubwa watakuwa ni benki na taasisi za fedha ambazo hutumia mfumo huo katika mashine za kutolea fedha (ATMs) Shirika la Microsoft limethibitisha kuwa benki ni miongoni mwa taasisi nyingi zitakazoathirika na mabadiliko hayo.
Mfano wa Windows XP

Baadhi zimeanza kufanyia kazi tatizo hilo, ikiwamo benki moja ambayo jana alasiri ilituma ujumbe kwa wateja wake kuwa, “Ndugu mteja, kuanzia Jumamosi saa 2:00 usiku Aprili 5, mpaka Jumapili saa 12:00 asubuhi tutakuwa tunaboresha mashine zetu za ATM, hivyo kadi yako haitafanya kazi kwa kipindi hiki. Asante.”

Kwa mujibu wa Microsoft asilimia kubwa ya benki katika nchi zinazoendelea zinatumia programu ya Windows XP katika kuendesha ATM, hivyo kuwa moja ya waathirika wa mpango huo.
File:Windows XP SP3.png
muonekano (interface) ya programu ya windows XP

Katikati ya Machi, Microsoft ilitangaza kusitisha huduma zote zinazohusiana na bidhaa zake za Windows Xp kufikia Aprili 8, mwaka huu. Pia shirika hilo litasitisha ufanisi wa programu ya kuzuia na kupambana na virusi ya Microsft Security Essentials katika mfumo wa Windows Xp, hivyo kufanya urahisi wa kompyuta zinazoitumia kukosa ulinzi.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Twiga Hosting, Jacob Urassa alisema Watanzania hawatakiwi kupuuza onyo hilo kwa kuwa ikifika Aprili 9 usalama wa taarifa zao utakuwa hatarini.

“Windows XP ni dhaifu mara tano zaidi ya Windows 7 na 8, kwa hiyo Microsoft wameona ni bora wakaitoa sokoni. Kwa maana hiyo ATM na kompyuta zote zinazotumia programu hizo hazitakuwa na ulinzi wa uhakika,” alisema Urassa ambaye ni mtaalamu wa masuala ya Teknolojia ya Mawasiliano (IT).

Alisema kuwa kuna idadi kubwa sana ya Watanzania wanaoendelea kutumia bidhaa hizo zikiwemo taasisi kubwa nchini hivyo kuna haja kubwa ya kuchukua hatua za kubadilika na teknolojia.

Naye, Ofisa Uhusiano wa Benki ya Posta, Noves Moses aliwatoa wasiwasi wateja wake kuwa licha ya kusitishwa kwa matumizi ya Windows XP, bado benki hiyo itaendelea kutoa huduma zenye kiwango kile kile.




Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.