Tanzania ni nchi ya nne duniani kwa wagonjwa wa sikosel.

TAASISI ya Sikoseli Tanzania imewaomba wadau wengine wa afya nchini kujiunga katika mapambano ya ugonjwa wa seli moja yaani sikoseli kwa sababu utafiti unaonyesha kati ya watoto 8,000 hadi 11,000 kuzaliwa na ugonjwa huo nchi nzima.
Makamu Mwenyekiti wa Mfuko wa Sikoseli Tanzania, Dk Julie Makani akihojiwa na waandishi wa habari katika hafla ya kuhamsidha jamii kuhusu ufahamu wa ugonjwa wa sikoseli 'seli mundu' iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Ugonjwa  wa sikoseli hurithiwa kutoka kwa wazazi wote wawili wenye
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye kampeni ya kuhamasisha mapambano dhidi ya ugonjwa ambao uliandaliwa na taasisi mbili za Sikoseli Tanzania na Little Fingers Music mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Sikoseli Tanzania, Dkt Julie Makani alisema kwamba hospitali ya taifa Muhimbili kupokea wagonjwa mia kila wiki ambapo ni asilimia ishirini tu nchi nzima.

Alisema kwamba ugonjwa huo ni wakurithiwa kutoka kwa wazazi baba na mama kwenda kwa mtoto na Tanzania ni nchi ya nne duniani kuwa na wagonjwa wengi wa sikoseli na kama hatapata ufumbuzi wa kukabiliana nao mapemna asilimia tisini na tano ya watoto watakaozaliwa wanaweza kufa kabla ya umri wa miaka mitano.


“nadhani ni wakati muafaka kwa makampuni, wawakilishi wa nchi mbalimbali na wadau wa sekta ya afya kuja kuunga mkono mapambano haya ya sikoseli nchini,’ alisema

Dkt Makani aliongeza kuwa hospital ya Muhimbili wamefungua kitengo maalum kwa ajili ya kuhudumia watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kwa msaada wa mashirika mbalimbali ikiwemo la Welcome Trust kutoka Uingereza ambao wanawapatia kiasi cha dola za kimarekani 250,000 kwa mwaka

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Little Fingers Music, Veronica Eyakuze alisema kwamba shirika lake la mafunzo ya muziki limeamua kusaidia watoto wenye matatizo na ugonjwa huo kwa njia ya kufundisha kupiga muziki, piano, gitaa na kazi zingine za muziki katika kuhamasisha mapambano dhidi ya ugonjwa huo

“sisi katika Little Fingers Music tupo mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo kwa miaka mingi na kusaidia watoto wenye matatizo hayo kwa kuwafundisha kupiga muziki ili wajue kwamba wanaweza kufanya shughuli yeyote na kuibua vipaji vyao,’ alisisitiza 
Mkurugenzi wa Kituo cha Little Fingers Music, Veronica  Eyakuze akizungumza na waandishi wa habari katika hafla hiyo.

Naye Arafa Said Salim (27) binti aliyezaliwa na ugonjwa huo, alisema kwamba ameanzisha taasisi yake ya kupambana ugonjwa huo kwa ajili ya kuhamasisha jamii kwamba ugonjwa huo unaweza kuishi nao bila matatizo yoyote.
Mmoja wa wagonjwa wa sikoseli, Arafa Said Salim ambaye pia ni muasisi wa Jumuiya ya wagonjwa wa Sikoseli Tanzania (CDPCT) akizungumza kuhusu ni jinsi gani mtu anayeugua ugonjwa huo anaweza kuishi maisha ya kawaida.
Mmoja wa wagonjwa wa sikoseli, Arafa Said Salim akipozi kwa picha na mumewe, Salim Msaky ambaye yeye hana sikoseli hafla hiyo. Hiyo ni kuonyesha kuwa mgonjwa wa sikoseli anaweza kuolewa ama kuoa mwenza asiye na ugonjwa huo bila kuleta madhara kwake.

“nimeanzisha taasisi yangu ya Wagonjwa waishio na Sikoseli Tanzania katika juhudi zangu binafsi za kuelimisha jamii kwamba ni muhimu kujua mapema na kuweza kuishi na ugonjwa katika maisha ya raha na marefu,” alisema Arafa alisema kwamba yeye binafsi ameolewa na anaweza kuishi na mumewe bila matatizo yoyote na ana matumaini anaweza kupata mtoto asiye na ugonjwa huo.

Aliongeza pia kwa miaka takribani kumi tangu kitengo cha sikoseli kufunguliwa katika hospitali ya Muhmbili utafiti umeonyesha kwamba vifo vya watoto chini ya miaka mitano vinapungua.

Mwisho.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.