Askari sita wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika wilaya za Rungwe na Mbeya waliofahamika kwa majina Coplo Johnson, PC Raymond, PC Simona, PC Shaaban, PC Kajolo na Sajini Hezron, wamefukuzwa kazi kwa tuhuma za kushawishi, kuomba na kupokea rushwa, blogu ya Mbeya Yetu imeripoti.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ahmed Msangi amenukuliwa akisema kuwa askari hao walifikishwa katika Mahakama ya Kijeshi na Hukumu kutolewa Aprili 24 mwaka huu na adhabu yao ikawa ni kufukuzwa kazi.

Aidha, askari wengine waliofukuzwa kazi hivi karibuni ni pamoja na PC James Kagomba aliyehukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa kosa la wizi wa kutumia silaha.

WP Prisca Kilwai anayekabiliwa na kesi ya wizi wa mtoto.

DC Marcelino Venance Na. 8084, PC Juma Idd Na. 3117 na askari mgambo MG Jackson Mwakalobo waliohukumiwa kifungo cha mwaka 1 kwa kosa la kusababisha kifo cha Dentho Kajigili, aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Ivumwe, Mbeya. 


Chanzo cha habari na mtandao wa www.wavuti.com
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.