Asasi zaidi ya 500 zaunga mkono rasimu ya pili ya Jaji Warioba 

KAULI ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa ufunguzi wa Bunge la Katiba na Waziri wa Nchi,  Ofisi  ya Waziri Mkuu, Sera na Uratibu, William Lukuvi kwamba muundo wa serikali tatu utatoa mwanya kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuchukua nchi ni vitisho dhidi ya maoni ya wananchi wanaotaka serikali tatu.

Akizungumza na Makangale Satellite blog Tanzania hivi karibuni jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya mkutano wa waandishi wa habari uliondaliwa na Asasi za Kiraia kuhusu mwenendo wa mchakato wa kutunga katiba Mpya, Mkurugenzi Mtendaji wa Youths Partnership Countywide (YPC), Israel Ilunde amesema kwamba kauli ya Rais Kikwete wakati wa uzinduzi wa Bunge la Katiba ni kutisha wananchi dhidi ya maoni yao kuhusu serikali tatu.

“kimsingi baada ya Rais kutoa maoni yake kwamba serikali tatu itatoa nafasi kwa jeshi kuchukua nchi ni kutisha wananchi wa Tanzania dhidi ya maoni yao ambayo yapo kwenye rasimu ya pili iliyowasilishwa na jaji warioba,” amesema
Ilunde amesema kwamba si kweli kwamba muundo wa serikali tatu italifanya jeshi la wananchi wa Tanzania kuchukua madaraka bali ilikuwa mbinu ya Rais kikwete kutisha na kuwatia hofu wananchi ambao wanataka serikali tatu.

Aliongeza kwamba Waziri Lukuvi aliongeza chumvi kwenye mkutano na baadhi ya viongozi wa dini kwamba serikali tatu itakuwa rahisi kwa JWTZ kuchukua nchi wakati kimsingi ni upotoshaji mkubwa.

“viongozi wakuu wa serikali wamewatisha wajumbe wa bunge maalum la katiba na wananchi kwa ujumla kuhusu swala la serikali tatu ni kinyume kabisa na katiba ya mwaka 1977,” alisisitiza
Kwa upande wake, Mratibu wa Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu, Onesmo Olengurumwa amesema kwamba Bunge la katiba linatumia mamlaka yake vibaya kwa kutaka kuhodhi kila kitu.

“Tume ya Jaji warioba imefanya kazi nzuri ya kuandika rasimu na bunge maalum ya katiba na kuijadili na kuibariki tu rasimu ili iende kwa wananchi na si kubadilisha rasimu yenye maoni ya wananchi,” amesema
Amesema kwamba bunge la katiba halina mamlaka ya kisheria kubadili rasimu ya pili iliyotengenezwa na Tume ya warioba kwa sababu ni kinyume na matakwa ya kisheria.

Awali, Mwenyekiti wa Umoja wa AZAKI wa kutetea Rasimu ya wananchi, Irinei Kiria amesema kwamba asasi za kiraia zaidi ya 500 wanaunga mkono rasimu ya pili ya katiba mpya kwa kuwa imekidhi mahitaji ya watanzania.

“kwamba hatujafurahishwa na mijadala ndani ya bunge maalum la kutunga katiba mijadala ambayo imepoteza utaifa na badala yake imejikita kwenye kutoheshiminiana, ubabe, ubaguzi, vijembe na vitisho,” aliongeza
 Amesema asasi za kiraia wamehuzunishwa na tabia ya kudhihaki na kudharau rasimu ya pili pamoja na Tume ya Mabadiliko ya katiba pamoja na Mwenyekiti wake.

Mwisho
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.