RAIS Jakaya Kikwete amewahakikisha watanzani serikali ipo katika hatua za mwisho kuandaaa sheria, kanuni na utaratibu kwenye sekta ya gesi na mafuta kwa ajili ya uwekezaji wenye tija nchini.


Akizungumza kwenye kongamano la 19 la mwaka kwenye uzinduzi wa ripoti ya ya utafiti wa Shirika Lisilo kuwa la Kiserikali la (REPOA)  linalofanyika jijini Dar es Salaam kwa siku mbili, Rais kikwete alisema mpaka mwezi oktoba mwaka huu serikali itakuwa imeweka sheria, kanuni kwenye sekta ya gesi na mafuta ili wazawa washiriki kikamilifu.
Rais wa Tanzania Mheshimiwa, Dakta Jakaya Kikwete


“mpaka ukifika mwezi Oktoba basi sheria na taratibu zote zitakuwa tayari na kufungua milango pia kwa wawekezaji wa ndani kushiriki kwenye sekta ya gesi na mafuta nchini,” alisema

Alisema kwamba kwenye uwekezaji wa gesi na mafuta taifa litapata manufaa makubwa na mabilioni ya pesa yataingia kwa hiyo ni nafasi muhimu pia kwa watanzania wenye biashara za kati na ndogo ndogo kunufaika na uwekezaji huo.


Rais Kikwete alisisitiza kwamba katika uwekaji wa sheria na taratibu lazima mambo ya urasimu na rushwa viondolewe mara moja ili kuhakikisha sekta hiyo inakuwa na manufaa kwa wananchi wote.

Aliongeza kwamba lazima serikali na wadau wote muhimu wajiridhishe kwamba hakuna wizi wala utapeli katika sekta gesi na mafuta ili kumletea mwananchi wa kawaida maendeleo.

Kikwete alifafanua kwamba lazima serikali ihakikishe inajipanga vizuri ili kuzuia vitendo vyovyote vya hujuma, wizi na rushwa ili kuleta matokeo chanya kwa nchi na watu wake.

Alisema kwamba kwa muda mrefu watafiti wa ndani wamekuwa na msaada mkubwa katika kuisaidia serikali kutambua maeneo yenye mahitaji zaidi na hasa katika kuboresha maisha ya wananchi na kupambana na tatizo la ajira nchini.


“tafiti hizi za kila mwaka zimekuwa na msaada mkubwa kwa wafanyabiashara wadogo wadogo, wakulima na wananchi wa kawaida katika kufanya uamuzi sahihi kwenye maeneo,” aliongeza, Alisema kwamba nchini Tanzania zipo ajira ndogo ndogo milioni tatu lakini wanaofanya ajira hizo ni milioni tano na laki mbili kati hao asilimia 64 ni wanawake.
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA, Profesa Samwel Wangwe alisema kwamba tafiti hizi zinalenga kuwasaidia wananchi wanaojishughulisha na biashara ndogo ndogo ili kupunguza umaskini.


Profesa Wangwe alisema kwamba malengo ya tafiti pia ni kuongeza tija kwa kupata uzoefu kutoka nchi mbalimabali ulimwenguni ya jinsi ya kujenga viwanda, kusindikaji wa chakula na kupambana na tatizo la ajira hasa kwa vijana na wanawake.


Aliongeza pia kwamba REPOA wamewaalika wataalamu mbalimbali kutoka nchini ya Japan ili watanzania waweze kujifunza kutokana na nchi zao katika harakati za kupambana umaskini Afrika. 


Mwisho.

Habari na  Mtandao wa Habari wa Makangale Satellite Tanzania
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.