VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliovuliwa nyadhifa zao hivi karibuni Dkt. Kitila Mkumbo na Zitto Kabwe wamesema kwamba njama zilizotumika kuwavua madaraka ni mkakati wa viongozi wa juu wa chama katika kujipanga kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa chama unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu. MOblog inaripoti. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo asubuhi jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Serena, aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Dkt. Kitila Mkumbo amesema waraka wa siri unaojulikana kama Mkakati wa Mabadiliko 2013 uliandaliwa na kuhaririwa na yeye kwa kuwa katika siasa za ushindani kuandaaa mkakati wa ushindi si uhaini.

“siamini hata kidogo kwamba kugombea nafasi yeyote iliyo wazi ndani ya chama cha siasa ni uhaini na hujuma. Msingi namba moja wa Chadema ni Demokrasia na hakuna namna ya kudhihirisha mapenzi kwa Demokrasia zaidi ya kuruhusu ushindani katika nafasi za uongozi na hasa uongozi wa juu kabisa,” amesema Dkt. Mkumbo
Amesema kwamba viongozi wa juu wa Chadema wana hofu ya siasa za ushindani baada ya kukaribia kwa uchaguzi mkuu ndani ya chama na yeye pamoja na Samson Mwigamba wanaamini kwamba madadiliko ya uongozi wa juu wa chama ni lazima.

IMG_5201

Dkt. Mkumbo aliendelea kusema kwamba mkakati kwa ajili ya uchaguzi iwe ndani ya chama au nje ya chama ni haki ya kikatiba kwa sababu ni mkakati wa uchaguzi hata viongozi wa juu wa sasa wa Chadema walikuwa na mkakati wao katika kujiandaa na uchaguzi ndani ya chama.

“Siasa za ushindania ndani ya chama cha siasa ni kujenga Demokrasia ya kweli na kama chama kikuu cha upinzani kinakataa kujenga Demokrasia kinachoililia kila siku kwenye chama tawala ni Udikteta usiokubalika katika dunia ya leo,” alisisitiza Dkt. Mkumbo
Amesema waraka wa Mkakati wa mabadiliko 2013 uliandaliwa na watu wanne tu bila Zitto Kabwe kujulishwa ingawa alikuwa mlengwa mkuu wa mkakati ambapo waandaji walipanga kumfuata na kumshawishi ajiunge.

Kwa upande wake Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amesema kwamba hatarajii kutoka ndani ya chama na hana mpango wa kuvunja chama chake kilichomlea na kumkuza miaka nenda rudi kwa sababu yeye ni muumini mwaminifu wa chama.

Amesema kuwa cha kushangaza ni waraka wa siri uliomuhusisha yeye na viongozi wa Chama cha Mapinduzi na wa Usalama wa Taifa kwamba anatumika kuhujumu chama chake na waraka huo ulisambazwa na viongozi wa juu wa chadema kama mkakati wao wa kumdhoofisha kisiasa kuelekea mbio za kugombea uongozi katika uchaguzi wa chama mwishoni mwa mwaka huu.

Amesema sababu ya pili ni kuwakosoa viongozi wa Chadema yakutokupeleka hesabu za chama kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kamati kuu ilidai alipaswa kuwatonya kwanza kabla ya kwenda kwa umma na waandishi wa habari.
“dhamira yangu ilikataa na nitaendelea kusimamia ukweli kwamba hesabu za vyama vya siasa lazima zikaguliwe na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa fedha za Serikali kama sheria inavyotaka,” amesema
Zitto aliendelea kusema kuwa kama kuchagua kati ya chama na nchi yake atachagua nchi kwanza kabla chama na kwamba ataendelea na msimamo wake pia wa kukataa posho ya kukaa yaani (Sitting Allowance) kwa sababu analipwa mshahara na fedha za kujikimu.  

IMG_5241

Mgogoro ndani ya Chadema ulipamba moto baada ya Kamati Kuu kuwavua uongozi Zitto Kabwe na Dk Kitila Mkumbo, huku Makamu Mwenyekiti Taifa, Said Arfi akiandika barua ya kujiuzulu Ijumaa ya wiki hii.

Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wakati Dk Mkumbo amevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu. Wawili hao wanatuhumiwa kukisaliti chama.

 IMG_5274

Taarifa zilisema hoja ya kukisaliti chama pia ilimkumba Arfi akidaiwa kumwezesha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita ubunge bila kupingwa, katika uchaguzi mkuu uliopita na ndiyo sababu ya kuamua kuachia ngazi nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa.

Mbali ya kuwavua uongozi Zitto na Dk Mkumbo, pia Kamati Kuu imewapa siku 14 wajieleze kwa nini wasifukuzwe uanachama. Kwa uamuzi huo Zitto amebaki na wadhifa wa ubunge wake wa Kigoma Kaskazini na wadhifa mwingine kwenye Kamati ya Bunge.

 IMG_5252

Kujiuzuru kwa Arfi

Makamu Mwenyekiti wa Taifa, Said Arfi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, Ijumaa ya wiki hii aliwasilisha barua ya kujiuzulu nafasi ya uongozi wa chama, akisema; “…kuchoshwa na unafiki unaoendelea ndani ya chama. Napenda ifahamike pia kwangu masilahi ya wapigakura, wakazi na wananchi wa Mpanda Mjini na Wilaya ya Mpanda ni muhimu katika kuwatumikia, hivyo basi sipo tayari kuchaguliwa marafiki.

Katika barua hiyo anasema amechochwa na tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake kuwa alimsadia Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita bila ya kupingwa  katika uchaguzi wa ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita.

“Kwa kipindi kirefu zimekuwepo shutuma dhidi yangu na kutiliwa shaka uhusiano wangu na Mhe Pinda Waziri Mkuu. Pamoja na kulijadili katika vikao kadhaa Mpanda na Dar es Salaam bado yapo mashaka kwa nini alipita bila kupingwa. Huo ulikuwa uamuzi wa Wanampanda kwenu imekuwa ni tatizo, lakini hamsemi kwa nini. Majimbo mengine 16 nchini yalipita bila kupingwa mlikuwa wapi na nani alaumiwe? Huu ni unafiki  wa kupindukia.

Vilevile, katika barua hiyo, Arfi anasema amechukizwa na kauli ya mwasisi wa chama hicho, aliyemtaja kwa jina moja la Mtei kuwachagulia marafiki.

“Aidha mmechukizwa sana kwa nini nilihoji kauli ya Mwasisi wa chama, Mhe Mtei kutuchagulia viongozi.  Naomba ifahamike wazi kwamba huu ni mtazamo wangu na utabakia hivyo siku zote kwa chama cha demokrasia kutoruhusu uongozi wa kiimla kwa kukidhi matakwa ya waasisi ambao huvigeuza vyama kuwa mali binafsi.
 IMG_5364



 IMG_5373



 IMG_5365

 IMG_5398

 IMG_5429

 IMG_5417

 IMG_5434
 Chanzo cha habari na www.dewjiblog.com.
















































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.