Wanawake wajasiriamali waaswa kuzingatia ubora wa bidhaa wanazozalisha 


.watanzania wahimizwa kununua bidhaa zinazotengenezwa na wazawa 


WANAWAKE Wajasirimali nchini wameaswa kuzingatia umuhimu wa ubora kwenye bidhaa zao wanazozalisha kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa ili kupata soko la uhakika ndani na nje ya nchi. Moblog linaripoti.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akifunga rasmi Maonyesho ya Wanawake Wajasirimali (MOWE) katika viwanja vya mnazi mmoja jijin Dar es Salaam, maonyesho hayo ya wanawake wajasirimali yalikuwa ya wiki nzima ambapo wakinamama wanapata nafasi ya kuonyesha na kuuza bidhaa mbalimbali usindikaji, mvinyo, batiki kwa wakazi wa jijini


Akizungumza kwenye kilele cha wiki ya Wajasirimali Wanawake Tanzania (MOWE) Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda amesema wanawake wanaweza kufanikiwa endapo watazingatia ubora wa vifungashio (Packaging) wanavyotumia kwenye bidhaa zao.
Mama Tunu Pinda, Mke wa Mheshimiwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda



“Nimedokezwa kwamba baadhi ya wajasirimali wamejisajili na kupata kiandishi-anuani yaani Barcodes, hapa Tanzania, mfumo huu umeanza kutumika hivi karibuni na wajasirimali wengi wameshawishiowa kujiunga ili bidhaa zao ziweze kutambuliwa kitaifa na kimataifa,’ amesema

Mama Pinda amesema kwamba watanzania wote wake kwa waume lazima wapende kununua bidhaa zinazotengenezwa hapa nyumbani ili kuweza kuwainua wajasirimali wazawa hasa wakinamama kwa kuunga mkono kampeni ya “Be Tanzanian, Buy Tanzanian” inayohimiza kuwa Mzalendo, Nunua bidhaa za kitanzania.

Amesema hata hivyo, kuna baadhi ya bidhaa zinazozalishwa na baadhi ya vikundi vya hapa nyumbani bado hazijaweza kumudu ushindani wa soko na kukubalika kuuzwa kwenye maduka makubwa yaani supermarkets.
Mama Pinda aliongeza kuwa changamoto nyingine kubwa inayowakabili wajasirimali wenhi ni kutozingatia viwango vinavyotambulika katika soko la ndani la nje ili bidhaa za wazawa ziweze kupenya kwenye soko la kitaifa, kikanda na kimataifa kwa maslahi mapana ya wajasirimali na nchi kwa ujumla.

“kwenu akinamama wajasirimali na wale waliohidhuria wasio wajasirimali ni matumaini yangu kuwa mmetumia fursa hii kubadilishana mawazo na kujenga mitandao ya kusaidiana na kuendelezana,” alisisitiza 

Kwa upande wake, Mratibu wa kitaifa wa Programu ya kuendeleza Ujasirimali kwa Wanawake Tanzania kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO) Noreen Toroka amesema shirika la kazi linafarijika kuchangia katika mipango na program za serikali za kuchangia ukuaji wa ajira kwa kupitia program za ILO katika kumuendeleza mjasirimali mwanamke nchini.

“kwa takribani miongo miwili ILO imekua ikifanya kazi kuhakikisha ujasirimali unachangia ajira na kipato kwa kina mama na tunajivunia kuwa kati ya wadau wengi walio katika kujengea uwezo washirika wetu idara za serikali, asasi za kifedha na zisizo za kifedha katika kuwainua wajasirimali wakinamama Tanzania,” amesema
Toroka amesema katika kuendeleza wakinamama nchini ILO imetoa mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake zaidi ya 500 na kuwaunganisha na huduma za kifedha na wataalamu wa ujasiriamali kwa elimu ya biashara na stadi za kazi.

“Kupitia washirika wetu ILO imefikia wakina mama 100 Mkoani Lindi na tunashukuru wadau wtu WAMA Foundation na program yao ya village savings and loan, wakinamama hao walipata mafunzo ya ujasiriamali na tunategemea watapata mikopo nafuu ili waweze kuanzisha, kuboresha na kupanua biashara zao,” aliongeza 

Mwisho
  

Habari na Damas Makangale
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.