Wazazi na walezi  wa kijiji cha Jendele na Vijiji jirani wameshauriwa kuwapeleka watoto wao Skuli za Maandalizi mapema wakiwa na umri wa miaka mitatu ili kuwajengea  uwezo na ufahamu wakiwa na umri mdogo.

Hayo yameelezwa leo na Mratibu wa Jumuiya ya Skuli za Maandalizi za Madrasa Mohamed Othman Dau wakati alipokuwa akizungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa Skuli ya Maandalizi Nuru Islamia iliyopo Kijiji cha Jendele.

Amesema kumpeleka  mtoto Skuli katika umri huo  ni kumkuza mtoto kiakili na kimwili kwani kufanya hivyo inampekea kuwa na ufahamu nzuri katika masomo yake.

“ Ni vyema  wazazi  waone ni muhimu kuwapeleka Skuli za Maandalizi watoto wao kwani kufanya hivyo ni kuwaandaa katika msingi bora wa kielimu,alisema Mratibu wa Jumuiya Mohamed Othman Dau”.

Afisa Lishe Shemsa Nasour Mselem  amesema ni vyema wazazi kuzungumza na watoto wao wakati wakiwa tumboni kwani kufanya hivyo humjengea mtoto huyo kufahamu  haraka wakati akisha zaliwa.  

Aidha amesema ni bora wazazi  kuwapatia watoto wao chakula chenye mchanganyiko wa virutubisho mbali mbali kwa ajili ya kuwajenga watoto hao miili yao kwani kufanya hivyo huwafanya kuwa na Afya  bora .

Nao wazazi wa watoto hao wamesema wamefarajika kwa kupatiwa mafunzo hayo kwani wengi walikuwa hawafahamu namna ya kuwaandaa watoto wao na kuwapatia lishe bora.

Hata hivyo wamesema  kwamba wameshukuru Jumuiya ya Maendeleoya ukuwaji wa Mtoto (CCD)  kwa kupatiwa mafunzo ya naman ya kuwaandaa watoto wao wakiwa na umri mdogo jinsi ya kujifunza kucheza  kabla kupelekwa Skuli za Maandalizi.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.