MAHAKAMA ya Mwanzo Tarime Mjini, imempa Zablon Kinogo siku tano kuhakikisha anampeleka chuo binti yake Deborah Zablon aliyegoma kuolewa ilihali alifaulu kidato cha Sita na kutakiwa kujiunga Chuo cha Ualimu Marangu, mkoani Kilimanjaro.

Kwa amri hiyo ya Mahakama iliyotolewa na Hakimu Jarome Migera, ni sawa na ‘ushindi’ kwa binti huyo mwenye umri wa miaka 20 aliyesisitiza kuipenda elimu kuliko ndoa.

Akitoa agizo hilo juzi, Hakimu Migera alimtaka Kinogo kuhakikisha analipa ada na gharama nyingine zitakazomfanya Deborah kujiunga na masomo yake ndani ya siku tano kuanzia juzi; Kinyume cha hapo, alionya hatua kali dhidi ya mzazi huyo zitachukuliwa kwa kuteketeza familia.

Akitoa agizo hilo alisema: “Mahakama yangu imekupa siku tano kuanzia leo Ijumaa (juzi) hadi Jumanne(keshokutwa) uwe umewasiliana na Mkuu wa Chuo cha Ualimu Marangu Moshi kuhusu sababu zilizofanya mwanao huyu achelewe kuripoti chuoni hadi ushitakiwe na kufikishwa hapa mbele ya mahakama hii. Mwanao alitakiwa kuripoti Agosti 21 mwaka huu, lakini umemchelewesha kwa kutaka ashindwe kwenda chuoni kwa nia ya kutaka umuoze anavyodai binti yako huyu hapa mbele ya mahakama hii.” alisema Hakimu Migera na kumtaka kuhakikisha anaripoti keshokutwa akiwa na vielelezo vya kulipa ada.

Hata hivyo, mzazi huyo alisema alikwenda mahakamani hapo akiwa na Shilingi 200,000 kama nauli na matumizi ya bintiye aweze kwenda chuoni, hivyo ameahidi kujipanga zaidi.Nje ya mahakama, Kinogo alisema: “Nilifika hapa na Shilingi 200,000 nimpe binti yangu huyu aende huko chuoni kwani naona mambo ya kuolewa yameshaharibika.”
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.