Meneja Mkuu wa Multichoice Tanzania Bw. Peter Fauel akifafanua ujio wa Super Sport nchini Tanzania na kuipongeza TFF kwa kuonyesha ushirikiano na kuwa Chaneli hiyo itaonyesha mechi tano za Ligi ya Tanzania kuanzia leo Ijumaa Septemba 28 hadi Jumatano Oktoba 3 mwaka 2012.



Mkuu wa Super Sport barani Afrika Bw. Andre Venter akielezea furaha yake kuja Tanzania na kupata fursa ya kulitangaza soka la Tanzania kimataifa kupitia chaneli ya Super Sport amesema chaneli hiyo imechafanya kazi katika nchi za Kenya na Uganda na Sasa ni wakati wa Tanzania kuonyesha kiwango chake cha soka Kimataifa.



Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini (TFF) Bw. Leordgar Tenga akitoa nasaha zake wakati wa uzinduzi wa wiki ya Soka Tanzania ambapo amevitaka vilabu vitakavyopata bahati ya kuonekana katika chaneli hiyo kuonyesha kiwango cha soka la Tanzania na kuzingatia nidhamu haswa mechi ya Watani wa Jadi Yanga na Simba ambao wanatambulika barani Afrika kama timu zenye upinzani mkali.




Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania Bi. Furaha Samalu akifurahi jambo na watangazaji wa kipindi cha Africa Soccer Show wakati wa halfa hiyo.




Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo kuwa Super Sport wakishirikiana na TFF wapo hapa nchini na kwa mara ya kwanza wanaonyesha mechi za Ligi ikiwemo timu ambazo hata siku moja hazijawahi kuonekana kwenye Chaneli ya Super Sport na kuwataka wachezaji wa timu hizo kuonyesha uwezo wao kwa sababu ni fursa ya pekee kuonekana katika nyanja ya Kimataifa. Aidha amewataka Watanzania ambao hawajaunganishwa na DStv wafanye hima kununua ving'amuzi ili waweze kushuhudia mechi hizo pamoja na chaneli nyinginezo zinazopatikana katika DStv.




Meneja Mkuu wa Multichoice Tanzania Bw. Peter Fauel akisalimiana na baadhi ya wageni waalikwa katika hafla fupi ya uzinduzi wa wiki Soka Tanzania iliyofanyika jijini Dar kwenye Hoteli ya Southern Sun.




Dada Levina kutoka Multichoice Tanzania anayetazama kamera akifurahi jambo na wadau



Meneja wa fedha wa Multichoice Tanzania Bw. Senguti (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Multichoice Tanzania Bw. Peter Fauel.




Baadhi ya Wadau wa michezo wakipata viburudisho wakati wa uzinduzi wa wiki ya soka Tanzania.



Mkurugenzi Mkuu wa Multichoice Tanzania Bw. Peter Fauel (katikati) katika akiteta jambo na Rais wa TFF Bw. Leordgar Tenga na Mkuu wa Super Sport Afrika Bw. Andre Venter.



Mtangazaji wa Jahazi ya CLOUDS FM Arnold Kayanda (wa pili kulia) na wadau wa tasnia ya michezo akiwemo mchambuzi wa masuala ya michezo nchini, Bwana Edo Kumwembe mwenye fulana kulia wakiwa kwenye pozi la picha



Barbara Kambogi akibadilishana mawazo na waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo.



'Crew' nzima ya Super Sport iliyotua nchini kwa ajili ya wiki ya Soka Tanzania



Kipindi cha Africa Soccer Show kwa mara ya kwanza kilifanyika LIVE nchini Tanzania. Pichani ni Watangazaji wakifanya mahojiano na Katibu Mkuu wa TFF Bw. Angetile Oseah (katikati).






































































































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.