Na Mwandishi wetu, Arusha

Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kupitia Program ya Imarisha Uchumi na Mama (SAMIA) linalenga kuyaongeze uwezo wa biashara na ujasirimali makundi ya Kinamama, Vijana na makundi maalum wa Mkoani Arusha hasa wanaofanya shughuli za kitalii na biashara za nafaka zinazosafirishwa kwenda nchi za Afrika Mashairi.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Bi. Beng’i Issa wakati wa Baraza hilo lilipozindua Program ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA) inayotekelezwa na baraza hilo kuwa MKoa wa rusha kuwa makundi hayo yataongezewa uwezo w kibiashara hasa katika maeneo ya utalii na nafaka zinazounzwa nje ya nchi.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC}, Bi. Beng’i Issa akizungumza na mwakundi ya kinamama, vijana na makundi maalum wakati baraza hilo lilipozindua Program ya Imarisha Uchumi na Mama (SAMIA} mkoani Arusha. Picha na Mwandishi wetu, Arusha.

“Mkoa huu wa Arusha ni wa kimataifa na umeshamili shughuli za kitalii na ni mpaka wa kusafirisha mazao ya nafaka kwa nchini za Afrika Mashariki,” na alioneza kusema program hiyo inalenga kuwaongezea ujuzi na uwezeshaji ili waweze kutumia fursa kama hizo kwa mafanikio makubwa zaidi.

Alisema Royal Toure aliyofanya Rais Mama Samia Samia ilikuwa na mafanikio makubwa katika mkoa huo ambao ni Jijiji kwa hiyo program zote zinazolisha utalii zitatapata mafanikio kupitia utalii na IMAMA imejielekeza kwa fanya biashara wadogowadogo na wajasirimali katika sekta hiyo wanufaike na kufikia viwango vya kimataifa.

Alifafanuwa kwamba Arusha ni jiji na makundi ya kinamama, vijana na makundi maalum yamekuwa na mwamuko na shughuli zao hasa akimama kwa vile jiji linapokea watalii wanaposhuka, mikutano ya kitaifa na kimataifa inafanyika hapo.

Pia alisema akinamana wengi wanafanya shughuli za kuuza nafaka nje ya nchi na Tanzania ndiyo inayolima mazao ya nafaka na kulisha nchi za Afrika Mashiriki kati ya Tanzania na Kenya na hiyo ni fursa nzuri kwa watanzania kuvuka mpaka na kufanya biashara nchi nyingine.

Alisema mkoa huo makundi hayo yalionyesha mwitikio mkubwa wa kuipokea  programa ya IMASA na inakadiliwa kulikuwa zaidi ya washiriki 1500 wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na wanaume.

Mshauri wa wa Rais Masuala ya Wanawake, Bi. Sophia Mjema alisema wale wote walioanjiandikisha wataingizwa katika kanzidata na aliyataka makundi hayo kuchaangamki fura hiyo kupitia IMASA.

Mshauri wa Rais Masuala ya akiwa na mwakundi ya kinamama, vijana na makundi maalum wakati Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) lilipozindua Program ya Imarisha Uchumi na Mama (SAMIA} mkoani Arusha kulia kwake ni Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Bi.Beng’i Issa. Picha na Mwandishi wetu, Arusha.

“IMASA imejipanga kutoa uwezeshaji kwa akinamama, vijana na makundi maalum na hasa akinamama na hakuna atakaye achwanyuma,” na aliongeza kusema kila mmoja katika mtaa wake, kitongozi chake, wilaya yake anahitajika kujiandikisha kuingia katika mfumo.

Naye Bi. Sophia Amiri Makazi wa Arusha alisema wamepokea mafunzo kutoka IMASA na wanaona kuwa inalenga kuwakwamua watanzania akinamama ambao bado wapo chini.

” Program inataka kutunyanyuma akimama na makundi mengine na itamwezesha mwanamke anayeishi katika nyuma ya nyasi kuishi katika nyuma ya bati,” na aliongeza kusema anampongeza Rais Mama Samia kupitia baraza hilo kwa kupelekea programa hiyo

Alisema katika mkoa huo akinamama wanajishughulisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi na ujio wa program hiyo inawawezesha kupata maarifa na uwezeshaji kukuza biahara na ujasirimali.

 Baraza la Uwezahaji Wananchi Kiuchumi NEEC kupitia programa IMASA lipo katika hatua ya kutoa mafunzo kwa makundi ya kinamama, vijana na Makundi Maalumu na kuwaingiza katika kanzidata na badaye watapatiwa uwezeshaji ili waweze kukuza shughuli za biashara na ujasiriamali,

MWISHO


This is the most recent post.
Older Post

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.