N a Mwandishi Wetu Lindi

Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) limewataka viongozi wa Mkoa wa Lindi kutengeneza mkakati kabambe utakaozuia mimba za utotoni kwa wasichana ambazo zinawasabishia kukatisha masomo na badaye kushindwa kujishughulisha na shughuli za kiuchumi kutimiza ndoto zao.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Bi. Beng’i Issa wakati baraza hilo lilipozindua  programa ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA)mkoani humo  kuwa kunahitajika kuweka mkakati wa kuzuia mimba za utotoni ili wasichana waweze kutimiza ndoto zao za kiuchumi baada ya kuhitimu masomo yao.

“Mkoa huu unamatatizo ya wasichana kuacha masomo hata wakiwa wamefaulu kujiunga na shule za sekondari hawaendi na inakadiliwa asilimia 30 hukatisha masomo kutokana na mimba za utotoni,” mimba za utotoni zinakatisha ndoto za kiuchumi za wasichana.

Alisema program ya IMASA imekuja kuwezesha Makundi ya kinamama, vijana na makundi maalum hivyo makundi ya vijana yakipata elimu ni nyenzo kubwa  ya kufikia malengo yao ya kiuchumi na ukizingatia mkoa huo unfursa nyingi za kiucumi.

Bi. Beng’i alisema mkoa huo wananchi wanajishughulisha na kilimo cha korosho,alzeti,uvuvi, mazao ya mwani, hivyo programa hiyo itashirikiana na mkoa huo kuweka vipaumbele ili kuandaa programa kwa ajili ya uwezeshaji wake.

Alisema program ilipokelewa  vizuri  mkoani humo na wananchi walitamani sana program ianze haraka na washiriki wengi walikuwa ni wafanya biashara, wakulima , wakulima wa kuongeza thamani mazao na madalali wa kilimo.

Pia aliutaka mkoa huo kuendelea na program zao za kawaida katika kilimo cha korosho, ubanguaji korosho kuongeza thamani  mazao na uvuvi  na zile za uwezeshaji za asilimia kumi na kuendelea kufuata maelekezo ya serikali.

Katibu wa Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu Manispaa ya Lindi, Bi.Zuhura Meza alisema anamshukuru Rais mama samia kuanzisha program hiyo ambayo imekuja kuwainua kiuchumi wanawake kupitia mafunzo ya ujasirimali na uwezeshaji watakao pewa.

“Nikilirudi nyummbani naenda kuwaelimisha watu wenye ulemavu wale ambao hawajajisajili na program ili nao waende kujishajili kupata fursa ya mafunzo na uwezeshaji,” alidai fursa hii imekuja kuwakomboa watu wenye ulemavu.

Naye Mkulima wa Mwani kutoka kata ya Lindi Mjini ya Kitumbi Kwela Manispaa Lindi, Rukia Selemen alisema yeye ni mkulima na mchakataji wa bidhaa za mwani  anashukuru ujio wa program hiyo kufika katika manispa yao  kutoa  elimu ya ujasirimali na itamwezesha kufanya vizuri zaidi.

Mjasilimali toka Kilwa Masoko Bi. Fatuma Juma alisema anajishughuli na usindikaji wa mzao mbalimbali yakiwemo ya maziwayogati, juice ya mwani na anatengeneza bidhaa za urembo kama nguo na alidai kwa kusema kuwa program hiyo imewaingiza katika mfumo na kufanya kazi kwa ubora,

“Program hii imetupatia elimu ya ujasairimali na pia inalenga kutupatia uwezeshaji,” na alisema wao  wamejipanga kupokea uwezshaji huo ili waweze kukuza mitaji yao pamoja na biashara na ujasiriamali. 

 Mkuu wa Wilaya la Lindi Shaibu Ndemanga akifuatilia jambo wakati Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumiu (NEEC) lilipozindua  programa ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA)mkoani humo, kushoto ni Katibu Mtendaji wa baraza hilo,Bi. Beng’i Issa na kulia ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa huo, Bw. Majid Myao. Picha na mwandishi wetu.


Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.