Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam 

Bank of Africa Tanzania Limited imewahikisha wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati kwamba itaendelea kutoa mafunzo kuhusu matumizi ya fedha, kuweka kumbukumbu za biashara na elimu ya kodi kwa wateja wake ili kuhakikisha wanakua pamoja.

Akizungumza na waandishi wa Habari hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bi Esther Cecil Maruma alisema kwamba warsha hiyo yenye kauli mbiu “TUKUE PAMOJA” ilikuwa ni ahadi ya benki hiyo kutoa huduma na msaada kwa wafanyabishara wadogo na wa kati (SME) nchini.

Mwezeshaji mada kwenye program ya “TUKUE PAMOJA” Bw Eric Crispin akiteta jambo baada ya kuwasilisha mada kuhusu nidhamu ya matumizi ya fedha kwa wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati wa soko la Kariakoo , semina iliyoandaliwa na BANK OF AFRICA hivi karibuni ililenga kuwa elewa wafanyabiashara hao kuhusu maswala ya fedha 

Mkurugenzi Mtendaji huyo Aliongeza kwamba katika kufanikisha ukuaji wa kifedha na uthabiti wa biashara zao. Warsha hiyo ililenga kutoa elimu ya kifedha kwa kina, ambapo mada kama vile uwasilishaji wa rekodi za biashara, masuala ya kodi, na mikakati ya kuongeza uwezo wa huduma za kibenki ili kuchochea ukuaji wa mtaji zilijadiliwa kwa nia ya kuwainua wafanyabiashara

Baadhi ya wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa kwao kwenye programu ya “TUKUE PAMOJA” iliyoandaliwa na BANK OF AFRICA hivi karibuni jijini Dar es Salaam 
"Katika mipango wetu wa kimkakati ya miaka mitatu, sekta hii nyeti ya wajasiriamali imepewa kipaumbele kwa njia ya kipekee, ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya kifedha kwa wateja wetu. Takwimu zinaonyesha kuwa sekta hii inachangia karibu asilimia 30 ya mapato ya taifa na katika biashara 10, 9 ni biashara zinazomilikiwa na wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati  (SME), hivyo ni muhimu kuhakikisha tunawajengea uwezo,”

Aliogeza “Tangu tulipoanza rasmi programu hizi mnamo mwaka 2021, benki tayari imefikia wateja 500 wafanyabiashara wadogo wadogo (SME) na lengo la mwaka huu ni kufikia wateja 170. Matunda ya kile tunachofanya yanaonyeshwa katika matokeo mazuri tunayoshuhudia, ambapo faida ya benki imeongezeka kwa asilimia 33 kutoka Tsh 6.03 Bilioni hadi Tsh 9 Bilioni, kwa kulinganisha matokeo ya Juni mwaka jana na Juni mwaka huu." alisema Bi. Maruma.

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa benki hiyo alifafanua kwamba "benki pia imeweza kupata matokeo mazuri katika mikopo chechefu, na katika kipindi kilichofikia Juni benki imefikia asilimia 1.5 ya mikopo chechefu, hii ni chini ya kiwango kinachohitajika na Benki Kuu ya Tanzania cha asilimia 5." Matokeo haya yanatuambia kuwa wateja wetu ni wazuri na wanalipa mikopo yao vizuri."

"Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa wateja wetu wote wa Bank of Africa Tanzania kwa kuendelea kutuunga mkono na pia naomba kwa wajasiriamali wa Tanzania, hasa wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati ((SME); kwamba benki iko tayari kuhakikisha mafanikio yao, kama kauli mbiu ya programu yetu "TUKUE PAMOJA" benki ina azma ya kuendelea kuwekeza katika sekta hii. Hii inaelezewa kwa uwazi katika mpango wa kimkakati wa miaka mitatu wa benki yetu, ukiwa na bajeti ya Tsh 62.23 Bilioni iliyopangwa kwa sekta ya wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati (SME) pekee kwa mwaka 2022-2024, na kwa kipindi cha mwaka jana tumetoa mikopo ya takriban Tsh 47.87 bilioni, huku zaidi ya Tsh 20.67 bilioni tayari zikiwa zimekopeshwa mwaka huu hadi Juni, zikifaidisha zaidi ya wateja 16,000 wa SME." alisema Bi. Maruma

Kaimu Mkuu wa Huduma za Kibenki kwa wateja wa Binafsi na Reja Reja, Bi. Mwamvua Majeshi aliwahakikishia wafanyabiashara kwamba huduma za mikopo zitapewa kwa wakati bila kuchelewa kulingana na kanuni za kbenki hapa nchini.

“Kwa Bank of Africa, wateja wetu kuhudumiwa kupitia matawi yetu, hata hivyo, benki pia imewekeza katika huduma za kidijitali kama vile huduma za benki kwa simu (B-Mobile), huduma za benki za mtandao (BOAWeb-Internet Banking) na hivi karibuni tumezindua huduma ya Bank of Africa WAKALA yenye mawakala zaidi ya 200 nchini.” alisema Bi. Majeshi.

Kwa upande wao , mfanyabiashara , Bw Frank Chaula aliyehudhuria programu hiyo aliipongeza BANK OF AFRICA kwa jinsi ilivyo wawezesha kupitia mikopo na kuinua biashara zao na kuomba benki iendelee kuboresha huduma zake ili kufaidisha Watanzania wengi zaidi.

“Tunashukuru BANK OF AFRICA kwa semina hii muhimu na leo nimejifunza nidhamu ya matumizi ya fedha , kuweka kumbukumbu, mauzo na manunuzi kwenye biashara kwa kweli nimepanua uelewa kwenye biashara nawashukuru sana,” alisema Bw Chaula

Naye, Elia Komba ambaye ni msafirishaji alisema kwamba mafunzo waliyopata kuhusu biashara na elimu ya mambo ya kodi yatawasaidia katika kufanya biashara zao kwa kushirikiana na Mamlaka Kodi Tanzania (TRA) jinsi ya kuweka hesabu vizuri ili kuongeza tija kwenye biashara zao.

Naye mwezeshaji kwenye semina hiyo ya siku moja , Bw Eric Crispin alisisitiza muhimu wa kuwa na nidhamu kwenye matumizi ya fedha kwenye biashara zao za kila siku ili kuweza kukua kibiashara.

“ni muhimu kuwa na nidhamu kwenye matumizi ya fedha na kuwa na utaratibu wa kuwa na kuweka malengo na bajeti kwa kila matumizi yako ya kila siku na kuweka mifumo ya kutunza kumbukumbuku ya fedha,” aliongeza.

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.