Staa wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa, Thierry Henry, ametangazwa rasmi kuwa balozi mpya wa kimataifa wa kampuni ya michezo ya kubashiri mtandaoni, Betway, wakati huu ambapo ligi kuu za barani Ulaya zinarudi dimbani kwa msimu mpya.

Thierry Henry 

Katika nafasi yake hiyo mpya, Henry anatarajiwa kuwa kiungo muhimu kati ya mashabiki wa soka na mchezo wenyewe, kupitia maudhui maalum na mitazamo ya kitaalamu atakayoshiriki kwa ushirikiano na kampuni hiyo.

Henry alianza soka lake la kulipwa nchini Ufaransa akiwa na AS Monaco, kabla ya kujiunga na Juventus kwa kipindi kifupi na kisha kutua Arsenal mwaka 1999, ambako alijizolea umaarufu mkubwa kwa kuwa mfungaji bora wa muda wote wa klabu hiyo. Aliisaidia Arsenal kutwaa mataji mawili ya Ligi Kuu England (EPL), ikiwemo msimu wa ‘Invincibles’ mwaka 2003/04, na mataji matatu ya FA Cup.

Baadaye alijiunga na Barcelona, alikoshinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) mwaka 2009 kama sehemu ya kikosi kilichotwaa mataji sita ndani ya msimu mmoja — rekodi ya aina yake barani Ulaya.

Katika ngazi ya kimataifa, Henry alikuwa sehemu ya kikosi cha Ufaransa kilichoshinda Kombe la Dunia mwaka 1998, na pia alitwaa taji la Euro 2000. Tangu astaafu soka, amekuwa kocha na mchambuzi maarufu wa soka katika vituo vya runinga mbalimbali.

“Soka siku zote limekuwa mchezo wa kasi na msisimko, na hayo ndiyo mambo ambayo Betway huwapatia mashabiki kwa namna ya kipekee,” alisema Henry. “Ninatarajia kushiriki kwenye kitu kikubwa kinachowaunganisha watu na mchezo wanaoupenda.”

Tangazo hilo limetolewa wakati ambapo Ligi Kuu England (EPL), La Liga na ligi nyingine kubwa barani Ulaya zinarejea, kipindi ambacho huwa na ushawishi mkubwa kwa mashabiki na wadau wa soka duniani kote.

Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni hiyo, uteuzi wa Henry unaonesha dhamira ya kuendelea kuwekeza kwenye soka la kimataifa. Betway tayari ni mshirika wa klabu kadhaa maarufu ikiwemo Arsenal, na inaendesha shughuli zake katika masoko mbalimbali ya Afrika, Ulaya na Amerika.

Mwisho

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.