UMOJA wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wamejiunga pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania . Aidha kwa pamoja wamezuru miradi iliyofadhiliwa na EU. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Mkwawa kwenye semina iliyoelezea malengo hayo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani. Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania. 
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (kushoto) akisalimiana na mmoja wa wahadhiri wa chuo hicho alipowasili katika ofisi za Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akiwa ameambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez.(Picha zote na Zainul Mzige wa Moblog)

Semina katika vyuo hivyo ni sehemu ya mpango madhubuti wa Umoja wa mataifa uliozinduliwa Arusha Mei mwaka huu na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wenye lengo la kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia. Ujumbe huo wa EU na UN pia ulipata nafasi ya kutembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na EU ukiwamo wa Boma la Kijerumani ambalo lilikarabatiwa kwa ruzuku ya EU kupitia 'fahari yetu – Southern Highlands Culture Solutions'. Boma hilo ni moja ya majengo ya zamani katika mji wa Iringa na lilijengwa na Wajerumani mwaka 1900 kama hospitali ya kijeshi. Baada ya vita ya Kwanza ya Dunia, jengo hilo lilibadilishwa matumizi na watawala wapya, Uingereza, na kulifanya kuwa jengo la utawala. EU imesema inaona fahari kuwa mmoja wa wawekezaji wakubwa katika sekta ya sanaa na urithi wa kitamaduni nchini Tanzania, ikifadhili miradi 10 iliyo chini ya programu ya 10 ya EDF ya kusaidia masuala ya kitamaduni. 

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akiwa kwenye mazungumzo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (upande wa kushoto katikati) pamoja na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Hoyce Temu (kushoto) alipotembelewa ofisini kwake na ugeni huo. Kulia ni Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever pamoja na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, Henry Mditi.

Masuala yanayohusu urithi wa kitamaduni ni muhimu katika kuchagiza ukuaji wa uchumi, ajira na huku ikifuma mahusiano ya kijamii, na kutoa fursa ya kuboresha utalii endelevu mkoani Iringa huku ikileta faida kwa wakazi wa eneo hilo. Bw. Rodriguez, akizungumza katika kampeni hiyo alisema kwamba ajenda 2030 ambayo ni ajenda ya maendeleo endelevu inahitaji ushiriki wa kila mmoja.Aliwapongeza wanachuo hao na wanazuoni kwa kujikita kutambua malengo hayo ya dunia. Aidha aligusia umuhimu wa vijana kushiriki katika masuala ya maendeleo kutokana na ukweli kuwa, kwa taifa kama la Tanzania vijana ni asilimia 60 ya wananchi wote waliopo.Alisema kwamba vijana wanajukumu kubwa la kushiriki katika maendeleo hayo kwa lengo la kuipeleka nchi katika hatua nyingine ya maendeleo. 

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwa ameongozana na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, Henry Mditi kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano Chuo Kikuu cha Iringa.

Hata hivyo alisema kwamba ni wajibu wa kila mtu hasa vijana, kuhakikisha kwamba malengo hayo ya dunia yanafanikiwa . Alisema Umoja wa Mataifa kwa kusaidiwa na wadau wake muhimu kama Umoja wa Ulaya, utaendelea kusaidia Watanzania kuwajibika katika shughuli mbalimbali za maendeleo katika kuunga mkono malengo hayo ya dunia. Mmoja wa washiriki alipongeza Umoja na wa Mataifa kwa kuwafikia vijana wa vyuoni na kuwapa semina hiyo. “Ninajisikia mtu mwenye bahati kupata nafasi ya kujifunza maendeleo endelevu kutoka kwa Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini. Nikiwa kama kijana, naona faraja kuona kwamba viongozi wetu wanafuata maelekezo yaliyofafanuliwa kwenye malengo 17 ya maendeleo endelevu; naamini kama tukijitahidi kuyafikia ifikapo 2030, basi Tanzania na duniani kwa ujumla itakuwa eneo jema la kuishi. Na kwa kuwa sasa natambua kuhusu malengo hayo ya dunia, ninaweza kutoa mchango wangu kusaidia kuyafikia -najisikia kuwezeshwa sana.” amesema Mary, mmoja wa washiriki. 

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akisoma taarifa fupi ya Chuo Kikuu cha Iringa mbele ya ujumbe kutoka Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya wakati semina kuhusu malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akizungumza kwenye semina ya malengo ya dunia kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa ambapo aliwaasa wakawe mabalozi wazuri wa malengo hayo kwenye jamii zao na wanafunzi wenzao wa vyuo vingine.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akitoa salamu za Umoja wa Ulaya kwa niaba ya Balozi wa Umoja huo, Bw. Roeland Van De Geer wakati wa semina Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa wanachuo wa Iringa iliyowezeshwa na EU.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwapiga msasa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa kuhusu Malengo ya Dunia katika semina iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
Mwanafunzi wa mwaka wa tatu anayechukua Shahada ya Sayansi katika Uchumi na Fedha wa Chuo Kikuu cha Iringa, Sarafina Sayi akiuliza swali kwa mkufunzi wa malengo ya dunia Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (hayupo pichani) wakati wa semina hiyo.
Mwanafunzi wa Shahada ya Sayansi katika Uchumi na Fedha wa Chuo Kikuu cha Iringa, Geoffrey Kadori akiuliza swali kwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela wakati wa semina ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa wanafunzi wa Chuo hicho.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akijibu swali wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwenye semina kuhusu malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.

Pichani juu na chini ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa kutoka vitivo tofauti chuoni hapo waliohudhuria semina ya malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla makabrasha na majarida yenye ripoti na taarifa mbalimbali za Umoja wa Mataifa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ripoti na makabrasha mbalimbali ya Umoja wa Mataifa mara baada ya kuhitimisha semina kuhusu SGDs kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa tatu kulia) katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya pamoja na Balozi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs Champion), Sabinus Paul (kushoto) nje ya ukumbi kulikofanyika semina kuhusu SDGs kwa wanachuo wa Iringa.
Picha ya pamoja na sehemu ya washiriki wa semina hiyo huku wakiwa na mabango ya SDGs.
Muonekano wa nje wa jengo la Makumbusho ya Mkoa na Kituo cha Utamaduni -Iringa Boma ambalo limejengwa kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).
Kibao cha Makumbusho ya Mkoa wa Iringa kinachoratibiwa na Mradi wa Fahari yetu kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Iringa
Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever akielezea dhumuni la mradi Fahari Yetu unaolenga kuendeleza utamaduni nyanda za juu kusini kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (mwenye suti) ambao ndio wafadhili wa jengo hilo la Makumbusho ya Mkoa wa Iringa. Wengine katika picha ni wahadhiri na maprofesa kutoka Chuo Kikuu cha Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akisaini kitabu cha wangeni ndani ya Makumbusho ya mkoa wa Iringa.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa.
Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever akitoa maelezo picha mbalimbali zinazoelezea historia ya mkoa wa Iringa wakati wa utawala wa Chifu Mkwawa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro walipotembelea makumbusho ya mkoa wa Iringa
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akisoma historia mbalimbali za enzi za utawala wa kichifu ndani ya Makumbusho ya Mkoa wa Iringa.
Mwongoza wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Jacob Shenyagwa (mwenye miwani) akitoa maelezo ya picha mbalimbali kwa ugeni huo wa UN na EU uliotembelea makumbusho hiyo iliyojengwa chini ya ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).
Mwongoza wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Deonis Mgumba akitoa maelezo ya vifaa mbalimbali vilivyokuwa vikitumika enzi za utawala wa kichifu kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, Henry Mditi (katikati) walipotembelea makumbusho hayo mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro wakitwanga mahindi kienyeji katika moja ya kinu kilichokuwa kinatumika enzi hizo za utawala wa kichifu kilichopo katika makumbusho hayo.
Mwongoza wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Matatizo Kastamu akitoa maelezo ya picha mbalimbali zenye kumbukumbu za utawala wa kichifu na historia ya mji wa Iringa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (kushoto), Mtalaam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu na Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever wakipitia vipeperushi vyenye maelezo ya kina ya Mradi wa Fahari Yetu unaoendesha Makumbusho na Kituo cha Utamaduni mkoa wa Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro katika picha ya pamoja kwenye sanamu maalum za mavazi ya kipindi cha utawala wa Chifu Mkwawa walipotembelea Makumbusho ya mkoa wa Iringa.


Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) imeshirikiana na kampuni ya Getenrgy kuandaa mkutano wa Afrika wa Mafuta na Gesi (GETENERGY VTEC AFRICA 2016) ambao unafanyika nchini kwa siku tatu kuanzia Novemba, 21-23, 2016.

Katika hotuba yake ya utangulizi, Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida alisema kuwa mkutano huo umekutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya mafuta na gesi kutoka nchi mbalimbali Afrika ikiwepo serikali, viwanda, mashirika ya maendeleo na vyuo ambavyo vinatoa elimu ya mafuta na gesi.

Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida akitoa neno la utangulizi katika Mkutano wa Afrika wa Mafuta na Gesi.

"Malengo ya mkutano huu ni kuangalia changamoto gani ambazo zinalikabili Bara la Afrika katika sekta ya mafuta na gesi, kubadilisha ujuzi kwa wataalamu wa mataifa ambayo yameshiriki na kujadili hatua ya kuchukua ili kuboresha sekta hii lakini pia utasaidia kukuza ushirikiano baina ya nchi washiriki,

"Katika mkutano washiriki wataisaidia Serikali na wadau kuweka mikakati ya kutekeleza na yenye ufanisi kuhusu sekta ya mafuta na gesi na kama Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamiii tutaendelea kushirikiana na wadau kutafuta changamoto zinazokabili sekta na mbinu za kutumia ili kuyatatua," alisema Dkt. Kida.

Mgeni rasmi katika mkutano huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu akizungumza umuhimu wa mkutano huo na jinsi ambavyo unaweza kuwanufaisha Watanzania.

Kwa upande wa mgeni rasmi katika mkutano huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu alisema, Serikali kwa sasa inataka kuhakikisha kunakuwapo na wataalamu wengi ili kunapokuwepo na sehemu ambazo kunapatikana mafuta au gesi waweze kushiriki wenyewe ili kipato kinachopatikana kiwanufaishe wananchi na Taifa kwa ujumla.

"Nchi ina akiba nyingi ya gesi na tunategemea kupata mafuta baadae lakini tunangaalia upande wa wataalamu, tunahitaji kuwa na wataalamu katika sekta ya mafuta na gesi ili tutakapoanza shughuli ya uchimbaji tayari tuwe na wataalamu wanaohitajika hapa nchini,

"Huu ndiyo mchango wa ndani, hatuwezi kufanya sisi pekee lazima tuwe na wageni lakini pia tuwe na Watanzania wanaotumikia sekta hii na wanaofaidika na uchimbaji wa hayo mafuta," alisema Mama Samia.

Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo haonekani pichani akielezea jinsi ambavyo Serikali imejipanga kuinua sekta na mafuta na gesi ili Watanzania wengi wanufaike na uwepo wa mafuta na gesi nchini.

Nae Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo alisema Serikali imejipanga kuboresha sekta ya mafuta na gesi kwa kutoa elimu kuhusu sekta hiyo katika baadhi ya vyuo mbalimbali nchini ili wahitimu wanapomaliza waweze kuingia moja kwa moja katika sekta hii.

"Tupo katika orodha ya nchi 20 Afrika ambazo zinafanya vizuri, baada ya miaka mitano tutakuwa tumepiga hatua na mtaona ni jinsi gani tumefanikiwa, kwasasa tuna wanafunzi wamehitimu UDOM na tunashirikiana na China na Uingereza kwahiyo niwahakikishie kuwa tumejipanga," alisema Prof. Muhongo.

Mkurugenzi wa kampuni ya Getenergy, Virginia Baker akitoa taarifa kuhusu kampuni hiyo, malengo na umuhimu wa kufanyika kwa mikutano hiyo.

Mikutano ya GETENERGY VTEC kwa mwaka 2016 tayari imeshafanyika katika nchi ya Mexico na Uingereza na imekuwa ikikutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya mafuta na gesi ili kujadili jinsi sekta hiyo inaweza kuboreshwa na kuwa bora zaidi kuliko ilivyo sasa.

Wadau mbalimbali wa sekta ya mafuta na gesi kutoka mataifa mbalimbali wakifuatilia mkutano wa mafuta na gesi ambao mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu.



Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu akipewa maelekezo kutoka kwa msimamizi wa banda la Chuo cha AGR TRACS kuhusu masomo yanayotolewa na chuo hicho. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida.

By Damas Makangale, Dar es Salaam, Tanzania  
The government of Tanzania has hailed for its efforts on creating a conducive environment for investment as Belgians business community eyeing to invest in energy, sisal, transport and infrastructure sectors to give a boost to the country’s economy.
Speaking to the East African Business week at the Kings Function day held last week at the Ambassador Residence in Dar es Salaam, Belgian Ambassador to Tanzania, Paul Cartier said that the government has to create a conducive environment for sustainable investment development.
Image result for Belgian Ambassador to Tanzania, Paul Cartier
On left,Belgian Ambassador to Tanzania, Paul Cartier
“Nearly 42 business people are here in Tanzania for business and trade talks that will lead to the sustainable investments to the two countries, but I would like to call upon the government to reduce multiple taxes as a way to encourage Foreign Direct Investment (FDI),” He said.
Ambassador Cartier told the EABW that the bilateral and economic ties between the two countries will continue for the betterment of the people as his government will continue to support Tanzania in various areas as a path for social and economic development.
He said that at present, Belgian Development Cooperation is active in the domains of natural resource management, local government, agriculture, water and sanitation. 
However, he noted that the efforts made over the next few years will concentrate on a limited number of sectors because one assessment concluded that the scope of Belgian cooperation was too wide.
Ambassador Cartier underscored that for example that Belgium was spreading its resources too thinly over too many sectors and the geographical dispersion of projects also made it difficult to adopt a consistent approach.
Moreover, the development programme concluded between Belgium and Tanzania in late 2009 is focused on two sectors: reforming local authorities and managing natural resources. 
The budget for 2010-2013 stands at €60 million. Cross-cutting issues include gender, the environment and the rights of the child.
Tanzania is one of the poorest countries in the world. Most Tanzanians still depend on subsistence farming to survive.
Belgium is providing financial and technical assistance to the Tanzanian Local Government Reform Programme, which was set up to strengthen local authorities and transform them into effective instruments of social and economic development. 
The programme involves devolving government responsibilities and financial resources to the local level to give district councils more autonomy to set their own priorities and implement their own development plans.
Under the new system, local government administrations will be responsible for meeting local needs and be held accountable by local councils. In other words, local governments are becoming the driving force behind development.
Natural resources are key to long-term economic development and poverty reduction in general. Many communities in Tanzania depend on natural resources because they live off fishing, farming, hunting, keeping livestock or forestry.
Accordingly, Belgium is supporting those Tanzanian initiatives in which environmental conservation and economic development go hand in hand.

ETH Excellence Master Scholarship Programme for International Students in Switzerland, 2017
The ETH Zurich, Switzerland
Application Deadline: December 15, 2016
Apply Now

Scholarship Positions Newsletter
Psychology Free Online Course by University of Toronto
University of Toronto
Course Starts on December 12, 2016
Apply Now


64 London School of Economics and Political Science PhD Studentships in UK, 2017
The London School of Economics and Political Science, United Kingdom
Application Deadline: December 14, 2016 (Department of Economics only), January 9, 2017 (including consideration for ESRC funding) and April 26, 2017
Apply Now

12 Fully-funded Birkbeck Postgraduate Research Scholarships in UK, 2017-2018
Birkbeck University of London, United Kingdom
Application Deadline: January 16, 2017
Apply Now

Duke University Free Online Course on English Composition

Duke University and Coursera
Course Starts on December 5, 2016
Apply Now


Newcastle University MBA Scholarships for International Students in UK, 2017
Newcastle University, United Kingdom
Application Deadline: Contact Employer
Apply Now


JAUW International Fellowship Program for Women in Japan, 2017
Japanese Association of University Women (JAUW), Japan
Application Deadline: March 31, 2017
Apply Now


Masters Scholarships for International Students at Örebro University in Sweden, 2017-2018
Örebro University, Sweden
Application Deadline: January 31, 2017
Apply Now


KTH Master’s Challenge for Indian Students in Sweden, 2017
KTH Royal Institute of Technology
Application Deadline: November 21, 2016
Apply Now


Charles Wallace India Trust Long term Awards in UK, 2017-2018
Charles Wallace India Trust, United Kingdom
Application Deadline: 30 November 2016
Apply Now


15 Undergraduate Scholarships for International Students at University of Edinburgh in UK, 2017-2018
University of Edinburgh, United Kingdom
Application Deadline: April 14, 2017
Apply Now


UN Women National Committee Australia Global Executive MBA Scholarship in Australia, 2017
University of Sydney, Australia
Application Deadline: November 20, 2016
Apply Now


45 PhD Scholarships for International Students at University of Edinburgh in UK, 2017
University of Edinburgh, United Kingdom
Application Deadline: February 1, 2017
Apply Now


High Achiever Foundation Prize for African Students in UK, 2017
University of Nottingham, United Kingdom
Application Deadline: April 21, 2017
Apply Now


MSc Scholarships for International Students at University of Strathclyde in UK, 2017
University of Strathclyde, United Kingdom
Application Deadline: June 30, 2017
Apply Now


Geography Taught Master’s Merit Awards at University of Manchester in UK, 2017
University of Manchester in United Kingdom
Application Deadline: June 30, 2017
Apply Now


Humanitarian Scholarships for International Students at University of Dundee in UK, 2017
University of Dundee in United Kingdom
Application Deadline: January 1, 2017
Apply Now


University of Westminster Research Studentships for International Students in UK, 2017
University of Westminster, United Kingdom
Application Deadline: February 10, 2017
Apply Now


Faculty Postgraduate Scholarships for International Students at Lancaster University in UK, 2017-2018
Lancaster University, United Kingdom
Application Deadline: February 10, 2017 (for Law School) and March 3, 2017 for all other departments
Apply Now


Gerda Henkel Foundation Research Scholarships in Germany, 2016
The Gerda Henkel Foundation
Application Deadline: 15 June 2016
Apply Now


Short-Term Scholarships for Egyptian Students in Germany, 2017
DAAD, Germany
Application Deadline: February 15, 2017
Apply Now


School of Life Sciences and Bioengineering PhD Scholarships for Tanzanian Students, 2017
Nelson Mandela African Institution of Science and Technology (NM-AIST), Tanzania
Application Deadline: November 18, 2016
Apply Now

Postdoctoral Research Fellowship in North Atlantic Geodynamics at University of Oslo in Norway, 2017

University of Oslo, Norway
Application Deadline: February 1, 2017
Apply Now

Theodor Heuss Research Fellowship for Home/EU and Overseas Students in Germany, 2017

University of Oxford, United Kingdom
Application Deadline: February 3, 2017
Apply Now


Soon Young Kim Postdoctoral Fellowships at Harvard University in USA, 2017
Korea Institute, Harvard University, United States of America
Application Deadline: January 5, 2017
Apply Now


PhD Position in Mathematics at University of Southern Denmark, 2017
University of Southern Denmark
Application Deadline: December 8, 2016
Apply Now

Professional Diploma Full Scholarships for Developing Countries in Africa, 2017

London School of Hygiene & Tropical Medicine, United Kingdom
Application Deadline: January 15, 2017
Apply Now

Sir Jack Cater Scholarship for Postgraduate Students at University of Bath in UK, 2017-2018
University of Bath, United Kingdom
Application Deadline: June 1, 2017
Apply Now

Peace Revolution MENA Salam Fellowship in Turkey, 2017
Peace Revolution, Turkey
Application Deadline: November 30, 2016
Apply Now

Yiddish Book Center Fellowship Program in USA, 2017-2018

Yiddish Book Center, United States of America
Application Deadline: January 9, 2017
Apply Now


Computer Architecture Free Online Course by Princeton University
Princeton University
Course Starts on November 21, 2016
Apply Now

Open University Management and Leadership Free Course

Open University
Application Deadline: Course starts on February 20, 2017
Apply Now

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010 Genevieve Mpangala amejitosa kusaidia kurejesha heshima ya mkoa wa Tabora katika elimu hasa kwa wasichana ambao ndio nguzo kubwa kwa familia na maendeleo ya taifa.

Mrembo huyo ameamua kufanya hivyo kwa kutembelea shule mbili za Tabora Girls na Isevya kuongea na wanafunzi, kuwapa moyo na kuangalia matatizo yanayowasumbua katika kujipatia elimu.

Akizungumza na Moblog amesema kwamba amekuwa na masikitiko makubwa na matokeo ya mitihani ya kitaifa ya sekondari kwa miaka mitatu ilhali simulizi za Tabora miaka iliyopita ni za kufurahisha sana uikionesha kwamba mkoa huo ndio kitovu hasa cha elimu.

Anasema ukisoma nyaraka mbalimbali unaona jinsi Tabora ilivyokuwa ngome ya elimu huku watanzania wengi wakifika hapo pia kupata elimu ya sekondari.

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala akizungumza wa shule ya sekondari Tabora Girls hivi karibuni.

“Kwa kweli pamoja na masimulizi mazuri kuhusu elimu Tabora miaka ya 80 na 90 ,nilichagua Tabora girls kwa sababu ni shule aliyosoma mama yangu mzazi form 1 mwaka 1977 mpaka 1980 mpaka na aliisifia sana shule yake hiyo na nikapenda niweze kuwa karibu nao kuhakikisha wanafunzi wote wanamaliza,na Isevya ilikua chaguo la pili kwasababu ilikua ni shule ya kutwa (day) na nilipendelea kuongea na wanafunzi hao” alisema Genevieve.

Mkoa wa Tabora ambao unapatikana kati ya Magharibi ya Tanzania kwenye uwanda wa latitudo 40-70 Kusini na longitudo 310 - 340 mashariki ukipakana na mikoa ya Shinyanga, Katavi, Singida, Kigoma na Dodoma ni mji ulioanzishwa na wafanyabiashara wa Kiarabu kwenye miaka ya 1850 ukijulikana kama Kazeh .

Kihistoria Kazeh ambayo ilikuwa kitovu cha biashara ya utumwa, mwaka 1871 robo ya mji ilichomwa moto na kuvurugwa na mtawala wa wanyamwezi Mirambo .

Ingawa mwaka 1885 hadi 1891 wajerumani walijaribu kutawala, historia zinasema kwamba mji huo ulikuwa na vurugu kubwa lakini baadae ukatawaliwa na wajerumani wakafanya mji wa utawala kabla ya vita kuu ya kwanza kuingia na wao kung’olewa.
Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010 Genevieve Mpangala akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi na mwalimu wao alipofanya ziara shuleni hapo.

Pamoja na historia yenye misukosuko ya Mkoa wa Tabora ambao ni moja ya mikoa yenye eneo kubwa unategemea sana kilimo kufanikisha maisha lakini kwa miaka mingi mkoa umekuwa ukididimia kimaendeleo na kijamii.

Mkoa wa Tabora ambao umekua wa mwisho kwa miaka mitatu mfululizo mwaka 2013,2014 na 2015 unahitaji nguvu kubwa ya kujiondoa katika shida ya kuporomoka katika elimu

Mrembo Genevieve anasema ziara yake katika shule hizo imemfumbua macho na kuona haja kubwa ya kuendelea na programu za kufufua matumaini.

Pamoja na kuwashukuru walimu kwa ushirikiano waliompa aliwataka wanafunzi kuweka mkazo katika imani, matumaini na kutekeleza ndoto zao katika uwanda mkubwa zaidi.
Aidha pamoja na kuzungumza "HAVE FAITH,HOPE FOR MORE AND DREAM EVEN BIGGER", pia aliwaasa kuwa elimu ni msingi mzuri wa maisha na kuwa wasiharakishe na kupotoshwa na mambo ya kidunia kwani haya maisha yapo.

Akiwa na wasichana wa shule ya Tabora Girls walimweleza changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni pamoja na kutokuwepo na uzio kwenye shule yao hiyo, uhaba wa vitabu, upungufu wa walimu, uhaba wa upatikanaji wa habari mubashara, kwa wanafunzi kwamba hawana king'amuzi,kwa wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi wanauhitaji wa msaada wa kofia pamoja na mafuta ya kuwakinga na jua.

Matatizo hayo yanatokana zaidi na kwamba wengi wao wanatoka kwenye mazingira duni. Changamoto nyingine ni pamoja na kuwa na zahanati ambayo ina uhaba wa vifaa mfano:vyandarua vya kutosha pamoja na vitanda,pia kwa wanafunzi ambao wanaulemavu wa macho ambao ni hafifu na vipofu kabisa hivyo kuna uhaba wa brail paper.

Ziara fupi ya Mrembo wa Tanzania 2010 Genevieve Mpangala kwa shule mbili za jijini Tabora za Isevya Secondary School na shule ya vipaji maalum ya wanawake Tabora girls.

Amesema katika mazungumzo yake na wanafunzi hao amebaini pia kwamba kutofanya vyema kwa wanafunzi pia kunasababishwa na wanafunzi hao kutumia madawa ya kulevya, utoro, mimba za shuleni na wazazi kuozesha mabinti katika umri mdogo kabla ya wao kumaliza shule.

Naibu Waziri (Ofisi ya Waziri Mkuu), Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Dkt. Abdallah Possi amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) kwa kusaidia kutoa elimu kwa wananchi kuhusu watu wenye ualbino pamoja na kufanya tathmini jinsi wananchi walivyo na uelewa kuhusu watu hao.

Dk. Possi ameyasema hayo katika mkutano wa kuelezea tathmini ambayo imefanywa na UNESCO kwa wananchi wa wilaya nne ambazo tathmini ilifanyika na kusema kuwa ni jambo zuri ambalo limesaidia kuonyesha hali jinsi ilivyo na ni njia gani ambayo serikali inaweza kutumia ili kumaliza vitendo vya ukatili kwa watu wenye ualbino.

"Watu wenye ualbino wamekuwa wakiteseka kwa kipindi kirefu, wanakosa nafasi ya kusoma, kufanya biashara na mambo mengi yanawakabili, watu wa mashirika sio suluhisho ni jamii yenyewe, watu wengi bado hawana elimu ya kutosha kuhusu ualbino,

"Inabidi ifike hatua watu wenye ualbino waishi sawa na watu wengine na serikali imekuwa ikifanya jitihada kumaliza vitendo hivyo lakini inabidi jamii itambue hili sio jukumu la serikali peke yake ni muhimu kila mmoja akashiriki kuvitokomeza vitendo vya ukatili, UNESCO imetuonyesha njia ya kuiwezesha serikali kufanikisha nia yake," alisema Dkt. Possi.

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt Abdallah Possi kutoa hotuba kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. (Habari picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Kwa upande wa UNESCO kupitia Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues alisema UNESCO imnatambua kila mwanadamu ana haki ya kuishi kama binadamu wengine na kupitia utafiti wao ambao uliambatana na kutoa elimu wanaamini kuwa ni muda wa jamii kushirikiana ili kutokomeza vitendo vya kikatili kwa maalbino.

"UNESCO imeamua kujihusisha sana na hili jambo na kujitahidi kutoa elimu kwa jamii, tumeanza kulifanyia kazi jambo hili la kikatili kwa maalbino na mashambulizi ambayo wamekuwa wanakutana nayo sababu ya imani za kishirikina ambazo ni kinyume na haki za kibinadamu,

"Utafiti huu utaweza kusidia kumaliza vitendo vya kikatili kwa watu wenye ualbino, kila mtu ana haki za kimsingi na hilo ndilo ambalo UNESCO inalisimamia, na katika kufanikisha hili kila mtu katika jamii kwa nafasi yake ana wajibu wa kushiriki kumaliza vitendo hivi, ni lazima kushirikiana kumaliza jambo hili," alisema Rodrigues.

Tathmini hiyo imefanyika katika wilaya nne ambazo ni Misungwi na Sengerema kwa Mwanza, Msalala iliyopo Shinyanga na Bariadi mkoani Simiyu.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt Abdallah Possi akizungumza katika mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wenye Alibinism Tanzania (TAS) Nemes Temba akitoa neno kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kiongozi mkuu wa tathmini hiyo, Dkt. Nandera Mhando akiainisha mambo muhimu yaliyobainika kwenye tathmini wakati mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Sweden nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnitt akitoa maoni kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. Kulia ni Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp.
Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp akizungumza jambo kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini, Dr. Qasim Sufi akifafanua jambo wakati wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi akifafanua jambo kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Picha juu na chini ni Sehemu ya washiriki wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) wakiwemo wadau kutoka mashirika na taasisi mbalimbali uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.



Mshehereshaji wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism), Mathias Herman akiendesha mjadala kwa washiriki katika mkutano huo uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi akibadilishana mawazo na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnitt (wa pili kushoto), Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp (wa pili kulia) pamoja na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini, Dr. Qasim Sufi wakati wakijiandaa na zoezi la picha ya pamoja.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.