Articles by "Fashions"

Showing posts with label Fashions. Show all posts

Mrembo wa Tanzania mwenye tamaa ya kuwa na himaya ya samani za kimataifa kupitia kampuni yake, kama alivyowahi kuelezwa na jarida la Forbes hivi karibuni, Jacqueline Ntuyabaliwe ametwaa tuzo mbili za ubunifu kupitia kampuni ya Molocaho by Amorette. Ushindi wake huo unamuingiza katika kundi la watu wenye ubunifu mkubwa wa bidhaa za majumbani na katika maofisi, muda mfupi tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo. Molocaho by Amorette kampuni ya kubuni na kutengeneza samani ilizinduliwa Septemba 2016. Miezi michache tu tangu kuundwa kwake inaonesha kukimbia na kufanikisha tuzo tatu za kimataifa. Katika tuzo zenye ushindani mkali na heshima kubwa kwenye ubunifu za kimataifa zijulikanzo kama A-Prime Design (A'Design) zilizofanyika mjini Roma mwishoni mwa wiki Jacqueline amepata tuzo katika kategori mbalimbali na kuwa wa pili kategori nyingine. 

Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi.

Bidhaa zilizompatia tuzo ni samani na pia za mwanga. Ngorongoro Settee ilimpatia medali ya shaba kwa upande wa samani na katika bidhaa za mwanga Sayari Lamp pia ilimpatia tuzo ya shaba. Nafasi ya pili ilipatikana katika kiti cha Flamingo. Taarifa zilizofikia thebeauty zinasema kategori ya Furniture, Decorative Items and Homeware Design Category ya mwaka 2016 na kiti cha Ngorongoro na kategori ya Lighting Products and Lighting Projects Design Category ya mwaka 2016 ilikuwa na Sayari lamp. Na Kiti cha Flamingo kilimpatia nafasi ya pili katika kategori ya Furniture, Decorative Items and Homeware Design Category ya mwaka 2016.


Muonekano wa kiti cha Ngorongoro Settee uliompatia tuzo Jacqueline Mengi kupitia kampuni yake ya Molocaho by Amorette.[/caption] A-Prime Design Shindano aliloshiriki Jacqueline Mengi akiwa na kampuni yake ya Molocaho by Amorette la A’Design hushirikisha wabunifu, wagunduzi na makampuni yanayotengeneza bidhaa mbalimbali za ubunifu wa ndani. Shindano la A' Design limeanzishwa kwa lengo la kuhakikisha kwamba wabunifu wanakuja na bidhaa bora kabisa zenye ushindani mkali katika soko la kimataifa. Kwa kawaida tuzo zake hutolewa katika kusanyiko kubwa la wabunifu linalofanyika Roma, Italia kwa kuratibiwa na OMC Design Studios SRL . Jacqueline, Miss Tanzania (2000) hivi karibuni alishiriki tuzo za rais za CTI na ana mafunzo ya Interior Design kutoka Rhodec International. Kampuni ya Molocaho by Amorette, kampuni ya Tanzania inajishughulisha na utengenezaji wa samani bora kwa namna mteja anavyohitaji, nyuzi, taa, urembaji, samani za nje na kwenye bustani.


Sayari Lamp iliyompatia tuzo katika kategori ya Lighting Products and Lighting Projects Design Category ya mwaka 2016.


Molocaho inatengeneza samani zenye mahadhi ya kiafrika ikichanganya utamaduni wa Tanzania katika mazingira ya kisasa na kumalizia na ubunifu wa kimataifa. Molocaho, moja ya makampuni ya Afrika Mashariki ya samani yanayokua kwa kasi, imejipatia nafasi kubwa ya heshima kwa kuhakikisha kwamba inatumia mali ghafi na mbao njema pekee za Tanzania kutengeneza samani zenye kwenda kimataifa. Katika mahojiano na jarida maarufu la Forbes alishawahi kusema kwamba anawania soko la kimataifa kutokana na ukweli kuwa bidhaa anazotengeneza zimejipambanua kwa wateja.


Muonekano wa kiti cha Flamingo kilimpatia nafasi ya pili katika kategori ya Furniture, Decorative Items and Homeware Design Category ya mwaka 2016.[/caption] Jacqueline Ntuyabaliwe, pamoja na kuwa na ratiba yenye changamoto sana (Yeye ni balozi wa WildAid na yumo ndani ya bodi kadhaa; mama wa watoto pacha wavulana; mke kwa mfanyabiashara mwenye mafanikio makubwa na akiendesha taasisi ya hisani ya elimu), huhakikisha anakagua kila samani inayozalishwa kiwandani kwake kabla ya kuuzwa au kusafirishwa. Mume wake, Reginald Mengi, ni tajiri mwenye mafanikio makubwa nchini Tanzania ambaye ameujenga utajiri wake kwa kufanya karibu kila kitu kuanzia uzalishaji wa kinywaji cha Coca-Cola hadi uchimbaji wa madini na kumiliki vituo vya televisheni na magazeti. Kwa tuzo hizo Amorette, inajidhihirisha kuwa chata yenye mafanikio makubwa nchini Tanzania na huku ikipanda kwa kasi kimataifa.


With Christmas just weeks away Myleene Klass has released her latest collection for Littlewoods.com and it's uber-glamorous.
Slipping into her own designs the 36-year-old showed off her slender figure in a string of dazzling outfits. The 10 piece collection features floor sweeping dresses in leopard print and sequins, a rose gold leather skirt and fitted bodycon dresses in studded leathers and prints.
The TV presenter is now on her ninth fashion collection for the retailer and the sexy range is the perfect partywear for the festive season.
Littlewoods.com Myleene Klass dazzles in shimmering sequins as
she models her latest fashion collection for
online retailer, Littlewoods.com
Myleene is a party teaser
Littlewoods.com Myleene Klass dazzles in shimmering sequins as
she models her latest fashion collection for
online retailer, Littlewoods.com
Time to sparkle
Myleene’s 10 piece collection features floor dresses in leopard print and sequins, a rose gold leather skirt and fitted bodycon dresses in studded leathers and prints.


Myleene says: “This collection is top to toe glamour. I’ve created short and floor length dresses that will see you through the party season no matter what your style is. The designs are striking, head turning pieces that I’m certain you will look and feel incredible in.”
Littlewoods.com Myleene Klass dazzles in shimmering sequins as
she models her latest fashion collection for
online retailer, Littlewoods.com
She's a winner in party frock

Kenyatte Nelson, Group marketing director, Littlewoods.com, said: “Myleene has put her magic touch on this collection. Her collections are always eagerly anticipated as Myleene is an expert on knowing exactly what the customer is looking for and we have no doubt our customer will love this range too.”


Littlewoods.com Myleene Klass dazzles in shimmering sequins as
she models her latest fashion collection for
online retailer, Littlewoods.com 
 


Mpigie Kura Miss Tanzania USA, Joy Kalemera anayeshiriki kinyang'ayiro cha kumtafuta Miss Africa USA. Mtangazaji wa Mimi Na Tanzania Hoyce Temu ambaye pia ni Miss Tanzania 1999 yupo nchini Marekani na amefanya mahojiano na mrembo huyo.
IMG-20140727-WA0011
Pichani ni  Miss Tanzania USA 2014, Joy Kalemera katika pozi kabla ya mahojiano na Mtangazaji wa kipindi cha "Mimi na Tanzania" Hoyce Temu nchin Marekani.

Usikose kuangalia marudio ya mahojiano hayo kwenye kipindi cha "Mimi na Tanzania" Jumamosi  ya tarehe 2 August ,2014 Saa saba mchana katika kituo cha Televisheni cha Channel Ten.

Namna ya kushiriki kumpigia kura moja kwa moja kwenye profile yake Bonyeza hapa utakuwa umeingia kwenye profile ya Joy Kalemera na bonyeza kitufe chenye alama ya mkono (sehemu iliyozungushiwa duara na wino mweusi) na moja kwa moja utakuwa umempigia kura Mtanzania mwenzetu anayeiwakilisha vyema nchini yetu kwenye kinyan'ganyito hicho.

 http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/07/Joy-Kelemera.jpg
NOTE: Unaweza kupiga kura mara nyingi uwezavyo kila baada ya dakika mbili kwa kubofya sehemu ile ile.




IMG-20140727-WA0013
Miss Tanzania 1999 ambaye pia ni Mtangazaji wa kipindi cha "Mimi na Tanzania" Hoyce Temu akipata ukodak na Miss Tanzania USA, Joy Kelemera baada ya mahojiano maalum nchini Marekani.


IMG-20140727-WA0014
Pichani ni Hoyce Temu, Joy Kalemera na camera crew/IskaJojo studios (katikati) aliyefanikisha kukerokodi maojiano hayo.



IMG-20140727-WA0015
Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu na Miss Tanzania USA 2014, Joy Kalemera katika pozi za madaha.






































































Na Damas Makangale, Moblog —

MBUNIFU wa mavazi Vida Mahimbo wa jijini Dar es Salaam Jumamosi ya wiki iliyopita amezindua ‘Collection’ yake ya ‘Face of Summer 2014’ yenye muonekano wa rangi za Kimataifa.

Event ilianza mchana majira ya saa Sita mchana ambapo wadau wa masuala ya urembo walipata nafasi ya kuangalia Collection mpya New Khanga T-shirts and Jeans yenye rangi za Kimataifa inayoitwa ‘Face of Summer 2014’ sambamba na kujipatia ushauri wa bure wa namna ya kupaka Make Up pamoja na utunzaji wa kucha kutoka kwa wataalam waliobeba kwenye fani ya urembo.


“Nimekuwa kwenye tasnia ya mitindo na mavazi kwa takribani miaka minne na leo nimezindua ubunifu mpya wa mavazi inaoendana na rangi za kimataifa hasa kwenye T-shirts na jeans,” amesema Mahimbo Mahimbo amesema kwamba yeye ana tengeneza nguo hasa za kike lakini ambazo zinaweza kuvaliwa karibu kila siku na watu wa rika mbalimbali wa kimataifa na watu wa kawaida.
 

Zipo Make Up za kila aina zinazoendana na ngozi ya mteja ambapo pia unaweza kupata kwa bei Jumla na reja reja. Pichani wageni mbalimbali wanaopenda urembo wakiangalia Make up wakati wa uzinduzi huo uliofanyika kwenye Duka la Atsoko Beauty and Cosmetic lililopo Mikocheni jijini Dar.
Amesema kwamba ameamua kumchangua (Sing Bird) Shaa kama balozi wake kwa sababu ni mtu anayeweza kuwakilisha vyema kwenye sanaa kutokana na mavazi, muonekano na uelewa wake mkubwa katika mambo ya mitindo hapa nchini. 


Mahimbo alisisitiza kwamba tukio hilo la Jumamosi iliyopita imetoa nafasi kwa wateja wake wa ndani na nje ya nchi kuweza kuona collection yake mpya ya 2014 hasa khanga na jeans.


Katika tukio hilo alishirikiana Atsoko wa duka la vipodozi kuandaa ‘Face of Summer 2014’ katika kuwapa watu waliotembelea nafasi ya kuona kazi zake mpya za sanaa ya ubunifu, amesema  

Shaa alichaguliwa kuwa balozi wa tukio hili na waandaaji kutokana na kuwa na sifa ambazo wao walizihitaji. Vida Mahimbo, Shaa, Rio Paul na Mary.

Kwa sasa wateja wa nchini wataweza kupata bidhaa ya T-shirts Khanga na Jeans katika duka la Atsoko Beauty and Cosmetics zilizotengenezwa na Vida Mahimbo


Muonekano wa Duka la Atsoko Beauty and Cosmetics lililopo Mikocheni jijini Dar palipofanyikia uzinduzi wa ‘Face of Summer 2014’ Collection mpya ya Mbunifu wa Mavazi Vida Mahimbo. 
(Picha na Zainul Mzige, MoBlog)

Wateja wakiangalia collection mpya ya nguo za mbunifu wa mavazi nchini,Vida Mahimbo. 


Add caption
 
 

Mmoja wa wateja akisoma brochures za bidhaa za Atsoko Beauty and Cosmetic.....She is so fine....!

BIdhaa mbalimbali za urembo
 

Flora Chacha akimpaka Make up mhudumu wa Peroni kuleta muonekano mzuri zaidi kwa wageni waalikwa.


 
 
Mbunifu wa Mavazi Vida Mahimbo (kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa ‘Face of Summer 2014’ (Song Bird) Shaa pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Atsoko Beauty and Cosmetic Marie Englesson (kushoto) pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Duka hilo.

 
 
Mtaalam wa kucha Maryciana Naivasha (katikati) Balozi wa ‘Face of Summer 2014’ (Song Bird) Shaa pamoja na Mtaalamu wa urembo Duka la Atsoko Beauty and Cosmetic Flora Chacha wakibadilishana mawazo (kulia)

 
 
 
 
 

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.