Huku zikionekana  dalili za hakuna uwezekano wa kumpata mshambuliaji wa Liverpool, Louis Suarez timu ya Arsenal mara baada ya jana kuanza ligi vibaya ina mpango wa kumgekia mshambuliaji wa kiispania anayeichezea Swansea City, Michu.

 Habari zaidi zinazidi kunatabaisha ya kwamba klabu ya Swansea iko tayari kumwachia mshambuliaji wao huyo hatari ikiwa timu ikifikia dau la paundi za kiingereza la million 25.

MIWANI PANA YA EDO ~ TATHMINI YA MECHI YA KWANZA YA MAN UNITED KATIKA LIGI

nikiwa mmojawapo wa mashabiki wa mabingwa wa England Manchester United leo nimeamua kuielekeza MIWANI YANGU PANA kuangazia mechi ya kwanza katika ligi ya kocha mpya David Moyes na kilichotokea katika mchezo huo ugenini dhidi ya Swansea
RVP akifunga goli la kwanza

Najua mashabiki wengi wa United walilalamika kuona baadhi ya wachezaji wakianza katika mechi ya Jana huku wale wanaowapenda wakianzia benchi hii ni kawaida kwani mashabiki wanachojua ni ushindi tu bila kufikiria unakujaje huo ushindi.

Lakini kwa miwani yangu pana nilichogundua ni kwamba kuna baadhi ya wachezaji uwepo wao Uwanjani mara nyingi hufanya timu pinzani kuingia hofu hata kutoka kabisa kimchezo. Kuna timu zikisikia mchezaji kama  Ryan Giggs au Rio au Vidic wanaanza huingiwa na hofu na kufungwa hata kabla ya mchezo na hii hutokea katika timu nyingi na kubwa mfano Barcelona jaribu tu kuangalia ikicheza bila kuwa na mastaa wake kama Messi,Iniesta na Xavi.

Hapo ndipo utakubaliana nami kwamba uwepo wa Ryan Giggs katika kikosi kilichoanza jana ni tofauti na angeanza Januzaj au uwepo wa Valencia uwanjani ni tofauti na kama angeanza Wilfred Zaha vivyo hivyo kuanza kwa Danny Welbeck ni tofauti na angeanza Jesse Lingard au Evra ni tofauti kabisa na Buttner. Sio kama Nawadharau wachezaji hao hapana hapa nazungumzia umuhimu wa kuanza na wakongwe.
Kunaweza kukawa na potential katika vijana lakini ni vizuri kama wakianzia benchi na nadhani makocha wenye akili hulitambua hilo na hapa nampa credit David Moyes.

Turudi katika mchezo husika

Magoli Manne katika mchezo wa kwanza si haba kama tukiendelea hivi kwa mechi sita za mwanzo ambazo mimi nadhani ndizo zitakazotufanya tuwe katika nafasi ya kutetea ubingwa itakua poa sana.
Danny Welbeck anaonekana amekua kimchezo japo anahitaji kufanya mengi ili kufata nyayo za aliyekua akivaa namba 19 Dwight Yorke ila ni kati ya wachezaji watakaoisaidia United msimu huu sina shaka na hili.

Wayne Rooney bado anahitajika katika Kikosi na sioni sababu ya Kumuuza au kumruhusu aondoke hapa naziangalia dakika chache alizoingia na kutoa pasi mbili za magoli. Huyu ni aina ya wachezaji ambao United wanawahitaji msimu huu hasa kwa mchango wake katika timu na kuongeza morale katika timu.

Safu ya Ulinzi ilionekana kuimarika japokua niliona kabisa jinsi Jones alivyokua akihangaika kuziba nafasi ya Rafael na sina shaka kama alifanikiwa huku muunganiko wa Vidic na Rio Ferdinand ukionekana kua imara tuombee tu wasipate majeruhi.
Upande wa ufungaji sina shaka na Robin Van Perse kwani anajua nini anachokifanya ikifikia chance za kufunga ila hofu yangu iko katika upande wa Kiungo na mchezaji gani anayeweza kumtengenezea Van Perse pasi za magoli na hapa ndo nimeanza kumwelewa Moyes na mpango wake wa kumnunua Cesc Fabrigas kwani mipira ilikua haikai eneo hilo.

Zaidi ya yote huu ni ushindi muhimu kwa benchi zima la ufundi na timu hasa ili kuanza msimu mpya na kumsahau Ferguson kama bado yupo United.

Mechi inayofuata ni dhidi ya Chelsea Jumatatu Ijayo Nyumbani Old Trafford badae United itasafiri mpaka Liverpool kuikabili Liverpool kabla ya kurudi Old Trafford kuikaribisha Crystal Palace.

Kwa leo haya ndo niliyoyaona katika mechi hiyo na ni mawazo binafsi hayana uhusiano au hayabadilishi chochote kilichotokea.

Chanzo cha habari na blogu ya wapendasoka.blogspot.com

The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular
universities and higher learning institutions in Africa. This is according
to 4icu.org University web ramming.

The aim of this website is to provide an approximate popularity ranking of
world Universities and Colleges based upon the popularity of their
websites. This is intended to help international students and academic
staff to understand how popular a specific University/College is in a
foreign country.

This has made UDSM to be the first popular high learning institution in
East Africa followed by Makerere University which ranked 11th and
University of Nairobi which ranked 20th. South African Universities are
top in the rank. SUA ranks 59th (8th in EA) while MUHAS ranked 98th (11th
in EA).  More in http://www.4icu.org/topAfrica/

Marca has reported that the Portuguese has tied down his future at the Bernabeu until 2018, increasing his salary to 17million euros (£14.8million) per year after tax and negotiating a new arrangement over the sale of his image rights in the process.

Ronaldo has two years to run on his deal at Madrid, who paid a world record £80million fee to prise him away from Manchester United in 2009, but has courted speculation over his future by revealing that he misses English football. United have subsequently been heavily linked with the player.
Ronaldo said: "I'm not going to confirm anything - I'm just going to do my job like I always do.

"My future - I don't know. At this moment I'm a player of Madrid, the future, I really don't know.
"Let's see what's going to happen - but for the moment, I'm good where I am."

He also gave little away about his thoughts on Madrid's pursuit of the Tottenham star, who is expected to break the record Ronaldo set for being the most expensive player in the world.

Madrid are believed to be ready to pay £95m for Gareth Bale but Ronaldo added: "I'm not going to speak about that because I'm not the right person to say if he deserves that money - if it's a good deal or not.

"I'm happy here - I think the players I have beside me, they are great - I'm not going to speak about other players."

KOCHA wa zamani wa Bayern Munich Felix Magath amedai kuwa meneja mpya wa Mabingwa wa Bavarian almaarufu kama Bayern Munich, Josep " Pep" Gardiola amejitakia mwenyewe matatizo kwa kumsaini  kiungo kinda Thiago Alcantara kuichezea Bayern Munich msimu huu mpya.
 
Alcantara, Kiungo wa Spain mwenye Miaka 22, aliihama Barcelona Mwezi uliopita na kuhamia Bayern Munich kwa Dau la Euro Milioni 20 na kuungana na Kocha Mhispania mwenzake aliekuwa Barcelona, Pep Guardiola, ambae pia ndie alimwinua Alcantara kutoka Timu B hadi Kikosi cha Kwanza cha Barca.

Lakini Felix Magath, aliekuwa kocha wa Bayern Munich kati ya wwaka 2004 na 2007, amesema uamuzi wa Guardiola kumchukua Alcantara utamletea matatizo na atajutia.

Magath ametamka: “naona ni tatizo kwa kocha Mhispania kumsaini Mhispania mwenzake. Pep atapata matatizo na Thiago. Ama wachezaji wenzake watakasirika kwa kuwa anachezeshwa mara kwa mara au watu watahoji uhamisho wake wa dau kubwa ikiwa hachezi! Kocha Josep Gurdiola almaarufu kama Pep angeweza kuepuka hili,"

Mbali ya utata huo, Felix Magath, ambae Msimu uliopita alikuwa Kocha wa Klabu ya Bundesliga Wolfsburg, pia anaamini Pep Guardiola hatashinda ile vita ya kupiku mafanikio ya Msimu uliopita ya Kocha Jupp Heynckes ambae aliiwezesha Bayern Munich kuweka Historia ya kuwa Klabu ya kwanza ya Germany kutwaa ‘Trebo’ yaani, Ubingwa wa Germany, Ubingwa wa Ulaya na kubeba German Cup.

Magath amedai: “Pep ana tatizo kubwa la kurithi Timu ambayo ilishinda kila kitu Msimu uliopita. Hivyo hawezi kuwafanya wawe bora zaidi ya hapo!”

Dar es Salaam. Rais wa Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton jana alifanya ziara katika makazi ya watu duni eneo la Vingunguti, wilayani Ilala Dar es Salaam, ambapo alikagua miradi midogomidogo ya wananchi inayofadhiliwa na mfuko wake (Bill Clinton Foundation).
Rais Jakaya Kikwete akimpokea mgeni wake rais Mstaafu wa Marekani Bill Clinton anayepanda kwenye gari
Clinton alitembelea eneo hilo akitokea moja kwa moja Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam (JNIA), alipowasili akiwa katika ziara ya nchi mbalimbali za Afrika kukagua miradi inayoendeshwa na mfuko wake.
Katika eneo hilo rais huyo mstaafu alipokewa kwa shamrashamra mbalimbali ikiwamo ngoma za kiasili huku baadhi ya wananchi wakipigwa butwaa na kutoamini macho yao kwa kiongozi huyo kutembelea makazi yao.
Aidha, Clinton alipata wasaa wa kusalimiana na wakazi wa Vingunguti wakiwamo watoto ambao walishindwa kuzuia hisia zao wakijaribu kumsogelea, hali iliyomsukuma Clinton kuwasogelea na kuwasalimia kwa kuwashika mikono.
Maneno ya ‘Welcome Vingunguti Clinton‘ yalisisika kutoka kwa wananchi kuashiria kumkaribisha rais huyo wa 42 wa Marekani wakati alipowasalimia akitumia takriban dakika 15.
Clinton alikagua miradi ya midogomodogo ya wananchi iliyo chini ya mfuko wake ikiratibiwa na kutekelezwa na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (Plan) pamoja na Benki ya Barclays kupitia Vikoba.
Miradi aliyokagua ni pamoja na saluni za kinamama, ushonaji na chips ambapo pia alishuhudia mmoja wa wanachama wa vikundi hivyo akikabidhiwa mkopo wa Sh100,000 ambaye alieleza mbele ya Clinton kuwa atazitumia kwa mradi wa maandazi, hali iliyomfanya rais huyo na umati wa watu uliohudhuria kucheka.
Akizungumza katika ziara hiyo Clinton alizishauri benki nchini, kuwekeza kwenye vikundi vya kuweka na kukopa (Vikoba) akieleza kuwa ndiyo mkombozi kwa wananchi hasa wanawake.
“Nimekuwa kwenye miradi hii kwa miaka 30 kabla sijawa rais, hivyo basi najua umuhimu wake. Benki zinatakiwa zisaidie Vikoba kwani vikundi hivyo huwafikia wananchi kwa haraka na wepesi hivyo basi kunahitajika njia mbadala za kuhakikisha vinakuwa imara,” alisema Clinton na kuongeza;
“ Raha ya maendeleo ni kuona watu wanajitegemea wenyewe katika shughuli za kujiingizia kipato.”
Mmoja wa wananchi walionufaika, Zainab Paul ambaye ni mwanachama wa Kikundi cha Amani Hisa alisema kuwa kupitia Mfuko wa Bill Clinton na Vikoba ameweza kujikwamua kimaisha ikiwamo kumlipa mtoto wake karo ya shule.
“Kikundi chetu kina wanachama 30 na huwa tunanunua hisa kwa Sh2000 na kila mwanachama anaruhusiwa kukopa zaidi ya mara tatu,” alisema Paul.

 Clinton alieleza kufurahishwa kwake na hatua walizofikia wakazi hao wa Vingunguti akiwapongeza kinamama kwa jitihada zao na baada ya ziara hiyo alielekea Ikulu kwa mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete.
Awali, Mtendaji Mkuu wa Plan, Tanzania, Jorgen Haldorsen alisema shirika lake limekuwa likihudumia nyanja za kiuchumi na kijamii kwa lengo la kuhakikisha wananchi wa kada ya chini wanapata huduma mbalimbali ikiwamo afya.
Naye, Mshauri wa Mambo ya Kujikimu wa Plan Stella Tungaraza aliwataka wananchi kujiunga zaidi na Vikoba na kwamba shirika lake limepanga kuanza kutoa mafunzo ujasiriamali kwa vijana ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Baadaye Rais Clinton alitia saini makubaliano ya taasisi yake ya Bill Clinton Foundation kusaidia sekta ya kilimo nchini.
Makubaliano hayo yalitiwa saini Ikulu jijini Dar es Salaam na Sophia Kaduma ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Chakula pamoja na mwakilishi wa taasisi ya rais huyo mstaafu, Walker Morris.
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Clinton alisema wakulima wa Tanzania wanatakiwa kutambua kuwa kuna nchi nyingine zinashindwa kuendesha shughuli za kilimo kutokana na uhaba wa ardhi au kuwa na ardhi isiyokuwa na rutuba na kuwataka watumie fursa hiyo kukuza uzalishaji wa kilimo .
Alisema kama wakulima hao watajituma Tanzania inaweza kuzalisha chakula ambacho kinaweza kulisha dunia.


 Chanzo cha habari na gazeti la Mwananchi.












































The Sun:


  • Spurs players asked Gareth Bale to autograph their shirts in an emotional farewell yesterday.
  • Arsene Wenger has warned Luis Suarez that more bad behaviour won't be tolerated if he does join Arsenal this summer.
  • Arsenal expect to complete the £8million sale of striker Gervinho to Roma within the next 48 hours.
  • Newcastle are set to finally break their summer transfer duck with a double swoop for James McCarthy and Bafetimbi Gomis.
  • Juventus are set to offer Manchester City £10million for left-back Aleksandar Kolarov.
  • Crystal Palace boss Ian Holloway has moved to bring winger Scott Sinclair back to the club on loan.
  • Carlo Ancelotti is ready to give Cristiano Ronaldo the freedom of the park in a bid to prevent Manchester United from turning his head.
  • Darren Bent's future remains in limbo after Fulham failed to match Aston Villa's asking price. 


  • Daily Mirror:
  • Harry Redknapp is planning a surprise move for Spurs striker Jermain Defoe.
  • Arsene Wenger last night labelled Gareth Bale's £105million move to Real Madrid "a joke".
  • Newcastle look set to break their summer transfer duck after agreeing a fee for Lyon striker Bafetimbi Gomis and QPR's Loic Remy.
  • Tottenham have agreed a deal to sell Clint Dempsey to MLS club Seattle Sounders.
  • Middlesbrough manager Tony Mowbray hopes to land Bristol City star Albert Adomah for £1million.
  • Arsene Wenger could go back to Swansea with an offer for Ashley Williams.
  • Gareth Barry is considering joining Rafa Benitez at Napoli.


  •  Daily Star:


  • Gareth Bale hopes his move to Real Madrid will be completed on Tuesday - and the Spanish giants will then follow it up by landing Luis Suarez.
  • Steven Gerrard has revealed he turned down a big move last season.
  • Jose Mourinho wants Fernando Torres to stay at Chelsea and banish his Stamford Bridge hell. 

  • Daily Mail:


  • Arsene Wenger has described Real Madrid's word-record £87million bid for Gareth Bale "a joke".
  • Matt Phillips looks to be heading to QPR despite facing a further two months out with a broken arm.
  • Fulham have made an improved £4.75million offer for Darren Bent.
  • Arsenal have intensified their bid to sign Ashley Williams to ease their defensive injury crisis.
  • Clint Dempsey is a target for MLS side Seattle Sounders.
  • Stoke are in talks over a deal for USA international forward Juan Agudelo.
  • Newcastle have edged closer to breaking their summer transfer duck by agreeing a fee for Bafetimbi Gomis .

  •  Daily Express:


  • Steven Gerrard rejected interest from Bayern Munich last summer to stay at Liverpool.
  • Gareth Bale now looks certain to take flight to Real Madrid.
  • Emmanuel Frimpong is back in Martin Jol's sights at Fulham.
  • Alan Pardew hopes to make Bafetimbi Gomis his first signing of the summer 


  •  The Guardian:

    Arsene Wenger believes that Real Madrid's world record move for Gareth Bale stands to make a mockery of the incoming financial fair play regulations as he pointed out that Arsenal's continuing pursuit of Luis Suarez was driven by self-generated funds. 

    The Daily Telegraph: 

    Real Madrid are ready to step up their world record bid for Gareth Bale, with his future is likely to be decided next week in Miami


















































































































    Real Madrid wapo tayari kumuuza Cristiano Ronaldo kwenda Manchester United mwezi huu baada ya nahodha huyo wa Ureno kukataa kuanza mazungumzo ya mkataba mpya.

    Gazeti la Daily Star limesema United na Real Madrid wametumia siku 12 zilizopita kuzungumza juu ya ada ya uhamisho ya paundi millioni 80 - na mabingwa wa Premier League wamezidi kupata uhakika wa kumrudisha kipenzi chao Old Trafford. 

    Raisi wa Real Florentino Perez mwanzoni alitaka kwamba uhakika kutoka kwa Ronaldo kama yupo tayari kusaini mkataba mpya - na alishangazwa kwamba mchezaji kuwa alikuwa tayari kurudi United. 

    Hilo lilipelekea Madrid kufungua mazungumzo rasmi na United, wakitambua kwamba wanaweza wakamuuza kwa fedha kidogo ikiwa winga huyo atabakia kwamwaka mmoja zaidi ndani ya Bernabeu kwa kuwa atakuwa amebakisha mkataba wa mwaka mmoja tu.  

    Lakini pia imeonekana wazi kwamba Madrid wanataka kumpata mbadala wa Ronaldo - Gareth Bale ambaye tayari wameshatoa ofa ya £85m kwa Spurs.
    Mapema wiki hii aliyekuwa raisi wa Madrid - Ramon Calderon alikaririwa akisema kwamba Madrid wanajiandaa kumuuza Ronaldo na ndio maana wanafanya kila liwezekanalo kumsajili Gareth Bale kutoka Tottenham.

    Ikumbukwe pia wakati akiwa bado kocha wa Man United Sir Alex Ferguson alikarriwa akisema kila kipo sawa kwa ajili ya usajili wa mchezaji mkubwa wakati wa dirisha kubwa la usajili litakapofunguliwa. Pia Wakati akihojiwa na BBC hivi karibuni aliyekuwa msaidizi wa Ferguson - Mike Phelan aliulizwa kama boss wake alikuwa akimzungumzia Ronaldo aliposema kuhusu usajili wa mchezaji mkubwa? Phelan alishindwa kukataa wala kukubali kuhusu suala hilo, akisema "no comment'. 


















     

    According to reports, Cristiano Ronaldo is moving closer to a return to Manchester United.
     
    Ronaldo, who was playing for Real Madrid against LA Galaxy last night, is apparently stalling on signing a new contract, leaving his future at the Bernabeu in doubt.The Portuguese forward is demanding £330,000-a-week to stay in the Spanish capital - a figure Real Madrid are not prepared to offer. 

    With the imminent arrival of Gareth Bale, the Daily Star have reported that Madrid are willing to sell Ronaldo in an attempt to raise the £105million they will pay Tottenham for the Welshman.

    The paper is reporting that United and Madrid have spent the last two weeks negotiating an £80m deal with David Moyes increasingly confident that he can bring the player to Old Trafford.
    His teammate Mesut Ozil has now revealed that he is concerned about the possibility of Ronaldo leaving the club and insists he is important to any future success they will have.

    Ozil is quoted as saying in the Evening Standard: “Ronaldo is very important to the team, just look at all the goals he has scored.
    “He’s a great person. I hope he can stay here for a long time because he can help us win important titles.
    “We have come very close to winning the Champions League and that leaves a very bitter taste.
    “What we hope is that we can go further this season. I believe we are good enough to make the final.”

    Ronaldo at United uniform


     Cristiano Ronaldo after netting a hat-trick for Real Madrid.
















    Dar/Dodoma. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimemfungulia mashtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kutokana na kauli yake aliyoitoa bungeni hivi karibuni kwamba wanaokaidi maagizo ya dola wapigwe.
    Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba akiwaonyesha waandishi wa habari, stakabadhi na hati ya mashtaka yaliyofunguliwa dhidi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika Mahakama Kuu ya Tanzania Dar es Salaam jana. Picha na Michael Jamson
    Hatua hiyo ya LHRC imepingwa vikali na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Dk Elieza Feleshi akisema hakuna uhalali wa mashtaka yoyote dhidi ya kiongozi huyo sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.

    Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo Bisimba alifungua mashtaka hayo katika Mahakama Kuu jana akisema kuwa wanamshtaki Waziri Mkuu kwa maelezo kuwa amekiuka kifungu cha Katiba Ibara 13 (1). Pinda ametajwa kuwa ni mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo namba 24.
    Mkurugenzi wa Maboresho na Utetezi wa LHRC, Harold Sungusia alisema jana kwamba, mwingine aliyeunganishwa katika kesi hiyo ya kikatiba iliyofunguliwa na LHRC na Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.
    Alisema katika kesi hiyo, kuna jopo la mawakili wasiopungua 20 na kwamba wamepata saini za wananchi 2,029 wanaopinga kauli hiyo ya Pinda na kuunga mkono kufunguliwa kwa kesi hiyo.
    Mjumbe wa Bodi ya LHRC, Wakili Dk Ringo Tenga alisema katika kesi hiyo wameangalia zaidi sheria na hasa haki za msingi za binadamu na kwamba kauli hiyo ya Waziri Mkuu Pinda inahatarisha haki hizo.

    Kauli yenyewe
    Wakati wa Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu bungeni, Juni 19, mwaka huu, Waziri Mkuu akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu aliyeuliza: “Serikali ipo tayari kiasi gani kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”
    Waziri Mkuu alijibu: “Ni lilelile nililosema... mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria.
    “Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.” Kesi hiyo itakayosikilizwa na majaji watatu, haina uhusiano na kesi nyingine ambazo wajibu maombi hupewa siku 90 kujibu hoja zilizowasilishwa. Kesi hiyo imefunguliwa kwa mujibu wa Katiba Sura ya Tatu.

    Akizungumza juzi kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma baada ya kufungwa kwa Warsha ya Wapelelezi na Waendesha Mashtaka wa Serikali ngazi ya mikoa, Dk Feleshi alisema hakuna uhalali wa mashtaka hayo kwa sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.
    “Hii haikuwa kuchochea apige watu, alichosema ni kupiga wale wasiotaka kutekeleza amri halali na zaidi alisema piga lakini si kupiga na kuua,” alisema.
    Mkutano huo uliendeshwa chini ya ulinzi mkali huku kukiwa na udhibiti wa kuvuja siri kwa kiwango cha juu. Pamoja na mambo mengine, ulikuwa ukijadili mbinu za kisasa katika kuendesha kesi pamoja na kujiuliza sababu za Serikali kushindwa katika kesi nyingi.
    “Kwa sababu lile neno kupiga ni lazima lipewe maana pana huwezi kumpiga tu mtu hivihivi ambaye hakuvunja sheria lakini nilivyoelewa, ilikuwa ni hivyo, ni sawa na mtu ambaye anamshambulia askari,” alisema Dk Feleshi.
    Alisema kuna sheria ya kutumia nguvu pale ambako kuna mkusanyiko usiokuwa wa halali pindi raia wanapokaidi kutawanyika kwa hiari hivyo hakuna shaka kauli ya Waziri Mkuu ililenga hivyo.
    Hata hivyo, alisema hajapata taarifa za LHRC kumshtaki Waziri Mkuu kimaandishi na kwamba akizipata atatoa ufafanuzi baada ya kuona lengo la mashtaka.
    Msimamo
    Akizungumza baada ya kufungua mashtaka hayo, Dk Bisimba alisema Waziri Mkuu anaweza kushtakiwa kwa kuwa alizungumza kwa nafasi yake ya Waziri Mkuu na si mbunge na kusisitiza kwamba hakuna aliye juu ya sheria na kudai kwamba kauli hiyo ni kinyume cha Katiba.
    Alisema kuwa kila anayevunja Katiba lazima ashughulikiwe kisheria na kwamba mahali pake ni mahakamani tu. Alisema kwa mujibu wa hati hiyo ya madai, kauli na amri kama hizo zinapotolewa na kiongozi mwenye hadhi kama ya mdaiwa wa kwanza (Waziri Mkuu) huchukuliwa kama sheria inayopaswa kutekelezwa na wakala wa utekelezaji wa sheria kama vile polisi. Wadai hao wanadai kuwa kwa ufahamu wao polisi wanaweza kuchukulia kauli hiyo kama amri halali kutoka kwa mkubwa wao na hivyo kuwapiga na kuwatesa watu wasio na hatia, kinyume cha Katiba.
    Pia wanadai wanatambua kuwa Ibara ya 100 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa kinga kwa wabunge na uhuru wa maoni bungeni. Hata hivyo, wanatambua kuwa Ibara ya 100 (2) ya Katiba hiyo inawawajibisha wabunge wote chini ya masharti ya Katiba na kwamba kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Pinda inakiuka Ibara ya 12(12).
    Hivyo wanaiomba Mahakama hiyo itamke kuwa kauli na amri hiyo aliyoitoa Pinda inavunja Katiba.


    Mkurugenzi wa taasisi inayofuatilia Mwenendo wa Bunge (Watch), Marcos Albania alidai kwamba wamegundua kuwa kauli hiyo ya Pinda ni moja kati ya matamko makubwa yanayovunja Katiba.
    Alisema mbali na shtaka hilo, kuna la pili dhidi ya Waziri Mkuu Pinda, ambalo hawajalifikisha mahakamani ambalo pia linatokana na kauli hiyo aliyoitoa bungeni kwamba: “Sasa wamechoka.”.

    Chanzo na Gazeti la Mwananchi




    Dar/Dodoma. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimemfungulia mashtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kutokana na kauli yake aliyoitoa bungeni hivi karibuni kwamba wanaokaidi maagizo ya dola wapigwe.
    Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba akiwaonyesha waandishi wa habari, stakabadhi na hati ya mashtaka yaliyofunguliwa dhidi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika Mahakama Kuu ya Tanzania Dar es Salaam jana. Picha na Michael Jamson 
    Hatua hiyo ya LHRC imepingwa vikali na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Dk Elieza Feleshi akisema hakuna uhalali wa mashtaka yoyote dhidi ya kiongozi huyo sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.

    Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo Bisimba alifungua mashtaka hayo katika Mahakama Kuu jana akisema kuwa wanamshtaki Waziri Mkuu kwa maelezo kuwa amekiuka kifungu cha Katiba Ibara 13 (1). Pinda ametajwa kuwa ni mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo namba 24.
    Mkurugenzi wa Maboresho na Utetezi wa LHRC, Harold Sungusia alisema jana kwamba, mwingine aliyeunganishwa katika kesi hiyo ya kikatiba iliyofunguliwa na LHRC na Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.
    Alisema katika kesi hiyo, kuna jopo la mawakili wasiopungua 20 na kwamba wamepata saini za wananchi 2,029 wanaopinga kauli hiyo ya Pinda na kuunga mkono kufunguliwa kwa kesi hiyo.
    Mjumbe wa Bodi ya LHRC, Wakili Dk Ringo Tenga alisema katika kesi hiyo wameangalia zaidi sheria na hasa haki za msingi za binadamu na kwamba kauli hiyo ya Waziri Mkuu Pinda inahatarisha haki hizo.

    Kauli yenyewe
    Wakati wa Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu bungeni, Juni 19, mwaka huu, Waziri Mkuu akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu aliyeuliza: “Serikali ipo tayari kiasi gani kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”
    Waziri Mkuu alijibu: “Ni lilelile nililosema... mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria.
    “Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.” Kesi hiyo itakayosikilizwa na majaji watatu, haina uhusiano na kesi nyingine ambazo wajibu maombi hupewa siku 90 kujibu hoja zilizowasilishwa. Kesi hiyo imefunguliwa kwa mujibu wa Katiba Sura ya Tatu.

    Akizungumza juzi kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma baada ya kufungwa kwa Warsha ya Wapelelezi na Waendesha Mashtaka wa Serikali ngazi ya mikoa, Dk Feleshi alisema hakuna uhalali wa mashtaka hayo kwa sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.
    “Hii haikuwa kuchochea apige watu, alichosema ni kupiga wale wasiotaka kutekeleza amri halali na zaidi alisema piga lakini si kupiga na kuua,” alisema.
    Mkutano huo uliendeshwa chini ya ulinzi mkali huku kukiwa na udhibiti wa kuvuja siri kwa kiwango cha juu. Pamoja na mambo mengine, ulikuwa ukijadili mbinu za kisasa katika kuendesha kesi pamoja na kujiuliza sababu za Serikali kushindwa katika kesi nyingi.
    “Kwa sababu lile neno kupiga ni lazima lipewe maana pana huwezi kumpiga tu mtu hivihivi ambaye hakuvunja sheria lakini nilivyoelewa, ilikuwa ni hivyo, ni sawa na mtu ambaye anamshambulia askari,” alisema Dk Feleshi.
    Alisema kuna sheria ya kutumia nguvu pale ambako kuna mkusanyiko usiokuwa wa halali pindi raia wanapokaidi kutawanyika kwa hiari hivyo hakuna shaka kauli ya Waziri Mkuu ililenga hivyo.
    Hata hivyo, alisema hajapata taarifa za LHRC kumshtaki Waziri Mkuu kimaandishi na kwamba akizipata atatoa ufafanuzi baada ya kuona lengo la mashtaka.
    Msimamo
    Akizungumza baada ya kufungua mashtaka hayo, Dk Bisimba alisema Waziri Mkuu anaweza kushtakiwa kwa kuwa alizungumza kwa nafasi yake ya Waziri Mkuu na si mbunge na kusisitiza kwamba hakuna aliye juu ya sheria na kudai kwamba kauli hiyo ni kinyume cha Katiba.
    Alisema kuwa kila anayevunja Katiba lazima ashughulikiwe kisheria na kwamba mahali pake ni mahakamani tu. Alisema kwa mujibu wa hati hiyo ya madai, kauli na amri kama hizo zinapotolewa na kiongozi mwenye hadhi kama ya mdaiwa wa kwanza (Waziri Mkuu) huchukuliwa kama sheria inayopaswa kutekelezwa na wakala wa utekelezaji wa sheria kama vile polisi. Wadai hao wanadai kuwa kwa ufahamu wao polisi wanaweza kuchukulia kauli hiyo kama amri halali kutoka kwa mkubwa wao na hivyo kuwapiga na kuwatesa watu wasio na hatia, kinyume cha Katiba.
    Pia wanadai wanatambua kuwa Ibara ya 100 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa kinga kwa wabunge na uhuru wa maoni bungeni. Hata hivyo, wanatambua kuwa Ibara ya 100 (2) ya Katiba hiyo inawawajibisha wabunge wote chini ya masharti ya Katiba na kwamba kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Pinda inakiuka Ibara ya 12(12).
    Hivyo wanaiomba Mahakama hiyo itamke kuwa kauli na amri hiyo aliyoitoa Pinda inavunja Katiba.


    Mkurugenzi wa taasisi inayofuatilia Mwenendo wa Bunge (Watch), Marcos Albania alidai kwamba wamegundua kuwa kauli hiyo ya Pinda ni moja kati ya matamko makubwa yanayovunja Katiba.
    Alisema mbali na shtaka hilo, kuna la pili dhidi ya Waziri Mkuu Pinda, ambalo hawajalifikisha mahakamani ambalo pia linatokana na kauli hiyo aliyoitoa bungeni kwamba: “Sasa wamechoka.”.

    Chanzo na Gazeti la Mwananchi


































    Imenukuliwa kutoka kwenye gazeti la MWANANCHI-- Shirika la Viwango (TBS) limetangaza orodha ya bidhaa 48 ambazo hazitakiwi kuwepo sokoni kutokana na muda wa kuitumia nembo ya kampuni hiyo katika bidhaa zao kumalizika na wahusika kushindwa kuwasilisha bidhaa zao kwa ajili ya uhakiki kabla ya kuruhusiwa tena.

    Hatua hiyo ya TBS inatokana na watengenezaji wa bidhaa hizo ambazo awali zilithibitishwa na TBS na kuruhusiwa kutumia nembo yao hiyo ya ubora kumalizika na wahusika kushindwa kuwasiliana na shirika hilo kwa ajili ya uhakiki wa bidhaa zao hizo .

    Ofisa Uhusiano wa TBS, Rhoida Andusamile aliliambia Mwananchi kuwa bidhaa hizo kuanzia hivi sasa hazitakiwi kuonekana sokoni na msako utaanza wakati wowote kuziondoa na zile ambazo zitakamatwa wahusika watachukuliwa hatua kali za kisheria.

    “Tumetoa tangazo lakini kabla ya hapo tuliwapa muda wawe wameleta bidhaa zao kwa ajili ya kuhakikiwa kabla ya kuruhusiwa kuendelea kutumia nembo yetu,akini wamekaidi ndio maana tumewatangazia kama utaratibu unavyoagiza” alisema Rhoida.

    Imenukuliwa kutoka kwenye gazeti la MWANANCHI-- Shirika la Viwango (TBS) limetangaza orodha ya bidhaa 48 ambazo hazitakiwi kuwepo sokoni kutokana na muda wa kuitumia nembo ya kampuni hiyo katika bidhaa zao kumalizika na wahusika kushindwa kuwasilisha bidhaa zao kwa ajili ya uhakiki kabla ya kuruhusiwa tena.

    Hatua hiyo ya TBS inatokana na watengenezaji wa bidhaa hizo ambazo awali zilithibitishwa na TBS na kuruhusiwa kutumia nembo yao hiyo ya ubora kumalizika na wahusika kushindwa kuwasiliana na shirika hilo kwa ajili ya uhakiki wa bidhaa zao hizo .

    Ofisa Uhusiano wa TBS, Rhoida Andusamile aliliambia Mwananchi kuwa bidhaa hizo kuanzia hivi sasa hazitakiwi kuonekana sokoni na msako utaanza wakati wowote kuziondoa na zile ambazo zitakamatwa wahusika watachukuliwa hatua kali za kisheria.

    “Tumetoa tangazo lakini kabla ya hapo tuliwapa muda wawe wameleta bidhaa zao kwa ajili ya kuhakikiwa kabla ya kuruhusiwa kuendelea kutumia nembo yetu,akini wamekaidi ndio maana tumewatangazia kama utaratibu unavyoagiza” alisema Rhoida.

    Bidhaa ziliazoainisha katika tangazo hilo ni pamoja na na
    majina ya watengenezaji /wasambazaji katika mabano ni pamoja na karatasi laini ‘tissue’ za Alawi Supplies ya Zanzibar, Milk Marie Biscut za Britania, Maji ya Great Zone, Mishipi na nyavu za kuvulia samaki za Imara Fishnet, maji ya Raha na fulana za Kibo Trade.

    Bidhaa zingine ni matofali ya GM Gross, taulo za watoto za Hengan Sanitary, baadhi ya rangi za Chui, beteri za Dry Cell, magodoro ya Jumbo foam, sabuni za Mbasira Investment ya Shinyanga, mifuko ya plastiki ya Centaza na mafuta ya kupikia ya Sun Flower Seed (Sun Shine) na korosho zinazosambazwa na Frabho Enterprises.

    Pia taulo za wanawake za Sythentic Detergent (ARIEAL) za Procter&Gambler, mifuko ya B-Twill Jute na A-Twill, mifuko ya plastiki ya Tropical, mafuta ya kupikia ya Sun Flower ya A TO Z Oil Mills, Korosho za Munawar ya Mbeya, Sabuni za kunawia za Brite Chemicals, pipi, lawalawa, mipira ya kutafuna ya rangi mbili.

    Vilainisha vya injini (Saud Oil) za Star Composed, betri za 777 kutoka China, maji ya kunywa ya Shia yanayotengenezwa na Siha Beverage, mtindi wa Morani Dairy ya Tanga, pikipiki za Star Shineray, vigae vya Mbezi, sabuni ya Liquid Detergent, mbao zilizotiwa dawa za Mombo, Jam iliyochanganywa ya Les Group ya Musoma.

    Orodha hiyo pia inataja Jusi za nanasi za Unnat Fountain ya Morogoro, Maji Uluguru, springi za magari za kampuni ya TASIA, Gypsum zinazotengenezwa na Tanzania Gypsum ya Dar es Salaam, Maji ya Uzima, magodoro ya Plyfoam,Mvinyo wa nanasi wa Kivumbui ya Arusha na mabati ya RD Roofing & Wire Product.

    Bidhaa zingine ni unga wa sembe wa Kweniml ya Machame Kilimanjaro, boriti za Ravji Manufacturing, mafuta ya breki za magari ya Automotive Packed ya Dar es Salaam, maJi ya kunywa ya AAMFA, pikipiki za Foshan Fost za China na mvinyo wa matunda wa Victoria Food Product ya Mara pia Jibini, mtindi na maziwa ya Kyaka Milk Processing , Sabuni za kufulia za Jamii za Kampuni ya Mbasira ya Shinyanga.

    Author Name

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Powered by Blogger.