Ratiba ya Bunge Maalum la katiba kuanzia Septemba 16 hadi Oktoba 4, 2014
Mwenyekiti wa bunge Maalum la Katiba mh. Samuel Sitta amesema Oktoba 4 bunge maalum la Katiba litakamilisha rasmi kazi ya kutoa rasimu ya Pili ya Katiba itakayokabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar itakayopigiwa kura na wananchi katika Serikali ya awamu ya 5.
Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba

Amesema kamati ya uandishi wa KATIBA itaendelea kuanzia leo Septemba 16 hadi jumatatu Septemba 22 ambapo rasimu ya pili ya katiba itawasilishwa bungeni ambapo Septemba 23, 24 na 25 wajumbe wa bunge Maalum la KATIBA watahakiki rasimu hiyo kuangalia Kama masuala yote yaliyopendekezwa na wabunge hao yameingizwa Kama walivyokubaliana.

Kamati ya uandishi itaendelea kufanya marekebisho ya rasimu ya KATIBA hiyo Septemba 26 na 27 na Septemba 28 wajumbe wote wanatakiwa kukutana katika kamati zao kujielimisha kuhusu rasimu ya pili ya KATIBA mpya.

Septemba 29 ni siku ya wajumbe hao kupiga kura kuipitisha rasimu ya KATIBA hiyo ambayo itakabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar tayari kwa hatua ya kupelekwa kwa wananchi kupigiwa kura katika serikali ya awamu ya Tano baada ya uchaguzi Mkuu 2015.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.