September 2016



Mwandishi Wetu
Bandari ya Dar es Salaam imeandika historia mpya kwa kupokea meli kubwa kuliko zote zilizowahi kutia nanga Bandarini ikiwa na urefu wa mita 261.
Mv Hammonia Grenada ikiwasili katika bandari ya Dar Es Salaam

Meli hiyo inayoitwa MV Hammonia Grenada ambayo ina uwezo wa kubeba makasha 4,256 imetia nanga katika bandari ya Dar es Salaam ambapo imeshusha makasha 483 na kupakia makasha 656 kabla ya kuelekea nchini Thailand.

Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema kwamba ujio wa meli hiyo ni ushahidi tosha kwamba bandari ina uwezo wa kupokea meli kubwa za aina hiyo ambazo awali zilikuwa zikiishia bandari ya Mombasa tu.

Kakoko amesema kwamba wapo waliokuwa wakifikiri kwamba bandari yetu sasa haifanyi kazi lakini ukweli ni kwamba bandari yetu ipo sawa na inaendelea kupokea meli kama kawaida.

Na kuwathibitishia hilo, amesema kwamba hata Mhe. Rais John Pombe Magufuli wakati alipokuja kufanya ziara katika bandari ya Dar es Salaam kulikuwa na meli nyingine saba zimetia nanga.

“Napenda niwatoa hofu wateja wetu kwamba bandari yetu ina uwezo wa kuhudumia meli kubwa bila shida yoyote na ujio wa meli hii umefungua milango ya meli nyingine kubwa kuja katika bandari yetu,” alisema Kakoko.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu, bandari ya Dar es Salaam ina gati zenye uwezo wa kuhudumia meli kubwa za namna hiyo ambazo ni pamoja na gati namba 8,9 na 10.
Naye Rubani Mkuu wa Mamlaka, Capt. Abdullah Mwingamno ambaye ndiye aliyeengiza meli hiyo amesema kwamba hii ndio meli kubwa kuliko zote ambazo zimewahi kuingia katika bandari ya Dar es Salaam.
Mv Hammonia Grenada

Mwingamno amesema kwamba hapo mwanzo mlango wa bandari yetu ulitengenezwa kuweza kuhudumia meli zenye urefu wa mita 234 tu lakini kutokana na mabadiliko ya teknolojia na jinsi meli zenyewe zinavyojengwa imeweza kuingiza hata meli za urefu mkubwa zaidi.

Pamoja na suala la teknolojia, Capt Mwingamno amesema kwamba kwa sasa TPA ina wataalamu wa kutosha ambao wamepata mafunzo sehemu mbalimbali Duniani ili kuweza kuingiza meli kubwa za namna hiyo.

“Tumepeleka kundi la kwanza la vijana wetu nchini Afrika Kusini kupata mafunzo ya jinsi ya kuingiza meli kubwa katika bandari yenye lango kama la kwetu na kundi la pili la vijana hawa tumelipeleka Copenhagen, Denmark,” amesema.

Amesema kwamba kundi la tatu la vijana hao tulilipeleka Nantes nchini Ufaransa kupata mafunzo kama hayo, kwahiyo napenda kuwahakikishia wateja wetu kwamba tunao wataalamu wa kutosha kuifanya kazi hii.

Hapo awali, TPA ilishawahi kuingiza meli nyingine kubwa yenye urefu wa mita 250 na baadae ikaingiza meli nyingine yeenye urefu wa mita 255.

Kwa mujibu wa Capt. Mwingamno, meli zenye urefu wa mita 261 mara nyingi huishia Bandari ya Mombasa kutokana na udogo wa lango letu lakini ujio wa meli hii umefungua rasmi milango ya kibiashara.

“Ujio wa meli hii umefungua rasmi njia kwa meli nyingine kubwa za aina hii ambazo zilidhani zisingiweza kuingia katika bandari ya Dar es Saam na hivyo kufungua rasmi ushindani na bandari nyingine,” amesema.
Mwisho.
IMETOLEWA NA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA
S.L.P 9184
DAR ES SALAAM
         Barua Pepe: maoni@tanzaniaports.com
         Simu za Bure: 0800 110047 na 0800 110032



Mwandishi Wetu
Bandari ya Dar es Salaam imeandika historia mpya kwa kupokea meli kubwa kuliko zote zilizowahi kutia nanga Bandarini ikiwa na urefu wa mita 261.

Meli hiyo inayoitwa MV Hammonia Grenada ambayo ina uwezo wa kubeba makasha 4,256 imetia nanga katika bandari ya Dar es Salaam ambapo imeshusha makasha 483 na kupakia makasha 656 kabla ya kuelekea nchini Thailand.

Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema kwamba ujio wa meli hiyo ni ushahidi tosha kwamba bandari ina uwezo wa kupokea meli kubwa za aina hiyo ambazo awali zilikuwa zikiishia bandari ya Mombasa tu.

Kakoko amesema kwamba wapo waliokuwa wakifikiri kwamba bandari yetu sasa haifanyi kazi lakini ukweli ni kwamba bandari yetu ipo sawa na inaendelea kupokea meli kama kawaida.

Na kuwathibitishia hilo, amesema kwamba hata Mhe. Rais John Pombe Magufuli wakati alipokuja kufanya ziara katika bandari ya Dar es Salaam kulikuwa na meli nyingine saba zimetia nanga.

“Napenda niwatoa hofu wateja wetu kwamba bandari yetu ina uwezo wa kuhudumia meli kubwa bila shida yoyote na ujio wa meli hii umefungua milango ya meli nyingine kubwa kuja katika bandari yetu,” alisema Kakoko.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu, bandari ya Dar es Salaam ina gati zenye uwezo wa kuhudumia meli kubwa za namna hiyo ambazo ni pamoja na gati namba 8,9 na 10.
Naye Rubani Mkuu wa Mamlaka, Capt. Abdullah Mwingamno ambaye ndiye aliyeengiza meli hiyo amesema kwamba hii ndio meli kubwa kuliko zote ambazo zimewahi kuingia katika bandari ya Dar es Salaam.

Mwingamno amesema kwamba hapo mwanzo mlango wa bandari yetu ulitengenezwa kuweza kuhudumia meli zenye urefu wa mita 234 tu lakini kutokana na mabadiliko ya teknolojia na jinsi meli zenyewe zinavyojengwa imeweza kuingiza hata meli za urefu mkubwa zaidi.

Pamoja na suala la teknolojia, Capt Mwingamno amesema kwamba kwa sasa TPA ina wataalamu wa kutosha ambao wamepata mafunzo sehemu mbalimbali Duniani ili kuweza kuingiza meli kubwa za namna hiyo.

“Tumepeleka kundi la kwanza la vijana wetu nchini Afrika Kusini kupata mafunzo ya jinsi ya kuingiza meli kubwa katika bandari yenye lango kama la kwetu na kundi la pili la vijana hawa tumelipeleka Copenhagen, Denmark,” amesema.

Amesema kwamba kundi la tatu la vijana hao tulilipeleka Nantes nchini Ufaransa kupata mafunzo kama hayo, kwahiyo napenda kuwahakikishia wateja wetu kwamba tunao wataalamu wa kutosha kuifanya kazi hii.

Hapo awali, TPA ilishawahi kuingiza meli nyingine kubwa yenye urefu wa mita 250 na baadae ikaingiza meli nyingine yeenye urefu wa mita 255.

Kwa mujibu wa Capt. Mwingamno, meli zenye urefu wa mita 261 mara nyingi huishia Bandari ya Mombasa kutokana na udogo wa lango letu lakini ujio wa meli hii umefungua rasmi milango ya kibiashara.

“Ujio wa meli hii umefungua rasmi njia kwa meli nyingine kubwa za aina hii ambazo zilidhani zisingiweza kuingia katika bandari ya Dar es Saam na hivyo kufungua rasmi ushindani na bandari nyingine,” amesema.
Mwisho.
IMETOLEWA NA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA
S.L.P 9184
DAR ES SALAAM
         Barua Pepe: maoni@tanzaniaports.com
         Simu za Bure: 0800 110047 na 0800 110032


Alhamisi ya Septemba, 15 inaingia katika historia ya mjasiriamali, Jacqueline Mengi kwa kufanya uzinduzi wa duka la samani za ndani la Molocaho Amorette likiwa na vitu ambavyo ni vya pekee kutokana na aina ya malighafi ambayo wametumia kutengeneza.

Akizungumzia duka hilo, Bi.Mengi alisema kuwa ilikuwa ni ndoto yake ya muda mrefu ya kutaka siku moja kuwa na duka kama hilo ambalo litakuwa na samani ambazo ni ngumu kuzipata sehemu nyingine kutokana na kutengenezwa tofauti na samani nyingi ambazo zinapatikana madukani.

"Siamini kama ndoto yangu imetia, kwa kipindi cha miaka iliyopita kuna vitu nilikuwa nikitamani kuwa navyo nyumbani lakini sikuweza kuvipata nilipokuwa nikitafuta na hapo ndipo ndoto za kuwa na duka zilipoanzia,

"Nilikuwa nataka kitu cha tofauti ambacho ni ngumu kukikuta sehemu nyingine kutokana na kuwa na ubunifu wa kipekee ambao utawavutia wateja wa ndani ya nchi na nje ya nchi na ninaamini watafurahia," alisema Bi. Mengi.

Aidha Bi. Mengi alisema kuwa bidhaa ambazo zitakuwa zikipatikana katika duka la Molocaho - Amorette zimetengenezwa na malighafi kutoka Tanzania kama mbao za Mninga na hivyo kuwataka Watanzania kuwa wazalendo kwa kutumia bidaa ambayo imetengenezwa na malighafi za Tanzania.

Mmoja wa wageni waliohudhuria halfa ya uzinduzi, Faraja Nyalandu alisema kuwa kwa kijana kama Jacqueline Mengi kuwa na duka kama hilo ni hatua kubwa ambayo vijana wengi wanatamani kuifikia, kumpongeza kwa juhudi alizozifanya lakini pia kutoa ushauri kwa wengine ambao wanataka kufanikiwa.

"Kwanza nimpongeze Jacqueline amefanya uthubutu na amefanikiwa kuwa na kitu kama hiki, juhudi yake inaonyesha kuwa kila mtu tu anaweza kufanikiwa kama akiongeza juhudi katika jambo analotaka kulifanya," alisema Bi. Nyalandu.

Duka hilo la kisasa na la aina yake linapatikana Masaki karibu na hoteli ya Sea Cliff kwenye jengo la "Village Walk" gorofa ya kwanza.

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na wageni walikwa pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa duka lake la samani za ndani "Amorette" lililopo katika jengo la Village Walk gorofa ya kwanza karibu na Sea Cliff Hotel, Masaki jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa nje utaokutambulisha hili ndio duka la "Amorette"
Bi. Jacqueline Mengi akikata utepe kuzindua duka lake hilo.
Ha ha ha ha, sasa mko huru kuingia wageni waalikwa kujionea yaliyomo,.....Bi. Jacqueline Mengi akifurahi jambo mara baada ya kukata utepe.
Bi. Jacqueline Mengi akiongozana na baadhi ya wageni waalikwa kuingia ndani ya duka la "Amorette"
Balozi Juma Mwapachu na baadhi ya wageni waalikwa wakiangalia moja ya meza ya chakula (dining table) iliyotengenezwa kwa mbao aina ya Mninga baada ya kuzinduliwa duka hilo lililopo katika jengo la Village Walk, Masaki jijini Dar.
Wageni waalikwa wakiendelea kukagua samani mbalimbali katika duka hilo.
Bi. Jacqueline Mengi akiwaonyesha mambo mazuri yaliyomo katika duka la Amorette baadhi marafiki waliohudhuria uzinduzi huo.
Bi. Jacqueline Mengi akizungumza jambo na Balozi Juma Mwapachu wakati akiwatembeza wageni waalikwa katika maeneo mbalimbali ndani ya duka lake la Amorette.
Wageni waalika wakiangalia moja ya kitanda cha aina yake kinachouzwa katika duka la Amorette lililopo katika jengo la Village Walk, Masaki jijini Dar es Salaam.
Sehemu maalum ya kitanda hicho ya kuhifadhia mashuka, Blanket pamoja na mito.
Bi. Jacqueline Mengi akipozi katika moja ya samani ndani ya duka lake la Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi katika pozi matata ndani ya duka lake la Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuzindua duka lake la samani za ndani la Amorette.
Wanahabari na wageni waalikwa wakiwa ndani ya duka la Amorette kujionea bidhaa mbalimbali.
Wageni waalikwa wakiendelea kutazama kitanda hicho cha aina yake.
Sophia Byanaku akijinafasi katika moja ya samani zilizomo kwenye duka la Amorette.
Mmoja wa wageni waalikwa akitazama bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa kwa mbao aina ya Mninga ndani ya duka la Amorette.
Baadhi ya samani zilizomo ndani ya duka la Amorette.
Balozi Juma Mwapachu (kushoto) akibadilishana mawazo na mwalikwa mwenzake kwenye uzinduzi wa duka la Amorette.
Mwanadada Monica Joseph akipozi kwenye moja ya bidhaa zilizopo ndani ya duka la Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi akipozi kwenye samani moja wapo inayopatikana katika duka lake la Amorette.
Warembo wakiwa wamepozi kwenye samani zinazopatikana katika duka la Amorette lililopo ndani ya jengo la Village Walk, Masaki jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa wakibadilishana mawazo ndani ya duka la Molocaho-Amorette.
Bi. Jacqueline Mengi akiwa kwenye picha ya pamoja na rafiki zake.
Bi. Jacqueline Mengi akibadilishana mawazo na baadhi ya marafiki zake.
Mkurugenzi wa Dorice Mollel Foundation, Dorice Mollel (kulia) katika picha ya pamoja na Mdau Monica Joseph.
Bi. Jacqueline Mengi katika picha ya pamoja na Dorice Mollel.

 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Bi. Zulmira Rodriguez akizungumza kuhusu mradi ambao una malengo ya kurejesha watoto wa kike shuleni. Kushoto ni Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UNWOMEN), Hashina Begum na kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Maimuna Tarishi.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Maimuna Tarishi akizungumza kuhusu mipango ya serikali kukabiliana na tatizo la watoto wa kike kukatishwa masomo.
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UNWOMEN), Hashina Begum akizungumzia sababu ya watoto wa kike kutokuwepo shuleni na jinsi ambavyo UNWOMEN watashiriki katika mradi wa kusaidia watoto wa kike kurudi shuleni.
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Watu Duniani (UNFPA), Maria Karadenizli akielezea takwimu za watoto wa kike ambao hawapo shuleni. 
 Mkuu wa Ofisi wa Shirika hilo la Maendeleo la (KOICA), Joosung Park akielezea ushiriki wa KOICA katika kusaidia mradi huo kukamilika sawa na mipango iliyowekwa.


Na Mwandishi wetu

Katika kuhakikisha watoto wa kike wanakuwa shuleni na hatimaye kumaliza masomo yao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limetenga Dola 1,605,000 ambazo ni zaidi ya Bilioni 3 za Kitanzania ambayo zitatumika kuwasaidia watoto wa kike nchini kurejea katika shuleni kwa ajili ya kuendelea na masomo.

Akizungumzia mradi huo, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Bi. Zulmira Rodriguez alisema kuwa Tanzania bado inaonekana kuwa na tatizo la watoto wa kike kuachishwa masomo yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwepo kupata mimba za utoto na ndoa za utotoni hivyo kupitia mradi huo wataweza kuwasaidia watoto hao kuendelea na masomo.

Bi. Rodriguez alisema UNESCO imeamua kushirikiana na serikali ili kuwasaidia watoto wa kike kurejea masomoni na utafanyika kwa uhakika bila kumwacha mtoto yoyote na wana matumaini utaweza kusaidia watoto wa kike ambao wamekatishwa ndoto zao kimaisha kutokana na kukatishwa masomo.

“Tanzania kuna tatizo la watoto wa kike kusahaulika katika elimu na UNESCO imejitoa kushirikiana na serikali ya Tanzania ili kusaidia kukuza elimu ya watoto wa kike, “Baadhi ya mambo ambayo yanaonekana kuchangia ni pamoja na mambo ya asili, wamekuwa wakiwaozesha ndoa za utotoni na na watoto wengine wamekuwa wakipata mimba za utoto na hivyo kuacha masomo … mradi huu ni wa uhakika na utasaidia kukuza elimu,” alisema Bi. Rodriguez.

Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Maimuna Tarishi alisema serikali inafahamu kuwepo kwa changamoto hizo na imekuwa ikifanya jitihada ili kuhakikisha kuwa matatizo ya watoto wa kike kukatishwa masomo yakimalizika.

Alisema kuwa makabila mengi ya Tanzania yamekuwa yakiwaona watoto wa kike kama watu wa kukaa nyumbani na kulea watoto lakini kama jamii ikiwa na mtizamo tofauti na kuwawezesha watoto wa kike basi wanaweza kusaidia nchi kukuza uchumi.

“Tumeona kazi ambayo wameifanya UNESCO hata machifu huko Ngorongoro wameanza kuelewa umuhimu wa watoto wa kike kuwa shuleni na kwa mpango huu matarajio ya serikali ni kumaliza changamoto iliyokuwepo awali,

“Serikali inafahamu kuna changamoto nyingi ambazo zinawakuta watoto wa kike na sio katika elimu pekee bali ni maeneo mengi … serikali inataka kukuza thamani ya elimu kwa watoto wa kike ambao wengi wao wanakatishwa kwa sababu ya mimba na ndoa za utotoni,” alisema Bi. Tarishi.

Nae Afisa Mradi wa Maswala ya Afya ya Uzazi kwa Vijana (UNFPA), Fatina Kiruviya alisema mradi una malengo ya kuhakikisha watoto wa kike wanakuwa shuleni na kwa kuanza wanataraji kufanya mradi Ngorongoro, Pemba, Geita na Sengerema.

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.