Image result for nkrumah hall university of dar es salaam
Nkurumah Hall
Karibuni katika Mdahalo (Debate) wa Kitaifa utakaofanyika Nkrumah siku ya Jumapili tangu saa 8 mchana hadi saa 12 jioni.

Kwa muda mrefu sasa, tumekuwa tukiandika, tukijadiliana na kulumbana kuhusu matumizi ya lugha ya Kiswahili. Iwe katika kuitumia kama lugha ya kufundishia, au kutolea hotuba katika mikutano au hata mawasiliano rasmi katika maofisi ya Serikali na Mashirika yake n.k.
Katika mijadala hiyo kuna wanaosema kuwa, tutumie Kiswahili na kuna wanaosema tuachane na Kiswahili tutumie Kiingereza.

Siku ya Jumapili tarehe 19, ni mara ya kwanza ambapo pande mbili zinazokinzana zitakutana ili kubishana kwa HOJA.
Ukumbi wa Nkrumah umekuwa na sifa ya kuwa na mijadala yenye kuleta tija na mabadiliko mioyoni au vichwani mwa watu, wawe viongozi au waongozwaji. Karibu ili ushiriki katika utamaduni huu wa Nkrumah na utoe mchango wako, kwa hoja za kitaaluma.

Kwa wale ambao mtashindwa, Mdahalo huo utarushwa mubashara na Vyombo vyetu vya habari vya TBC, ITV, Azam TV, Star TV, na Clouds, ikiwa ni pamoja na radio zake.

Karibuni

Aldin
Mratibu


Prof. Aldin K. Mutembei   (PhD)                       
Taasisi ya Taaluma za Kiswahili                
Kampasi ya Mwalimu J.K. Nyerere           
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam                 
+255 715 426 162+255 715 426 162      [Kiganjani]                +255 715 426 162

b-pepe: kaimutembei@gmail.com          Alternative e-mail: <kaimutembei@gmail.com>
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.