MJI WA SERIKALI, DODOMA –

Serikali ya Tanzania imepongezwa kwa mafanikio yake katika kuimarisha mifumo ya tahadhari na ufuatiliaji wa majanga kupitia Kituo cha Dharura cha Taifa (Situation Room) kilichopo Mtumba, Dodoma.

Pongezi hizo zimetolewa na wataalamu kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso waliopo nchini kwa mafunzo ya siku tatu ya kubadilishana uzoefu, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Menejimenti ya Maafa, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amesema kituo hicho kimeongeza uwezo wa taifa kutoa tahadhari mapema kwa wananchi na kuratibu mashirika mbalimbali kukabili majanga.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Kituo hicho, Bi. Jane Kikunya, amesema wageni hao wameonesha nia ya kuiga mfumo huo katika nchi zao kutokana na mafanikio waliyojionea.

Aidha, wageni hao wameeleza kufurahishwa na jinsi taarifa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kuwasilishwa kwa wananchi kwa haraka na kwa usahihi.










This is the most recent post.
Older Post

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.