Baraza linapenda kuwaarifu wote walioomba kudahiliwa katika kozi za cheti na diploma na umma kwa ujumla kuwa muda wa nyongeza wa kutuma maombi kwa mwaka 2016/2017 umeongezwa hadi tarehe 13 Agosti 2016 ili kuruhusu ambao hawakukamilisha maombi yao kuyamaliza na ambao hawajafanikiwa kuomba kutuma maombi yao.

Baraza linaomba ifahamike kuwa vyuo na kozi zilizojaa hazitaonekana tena wakati wa maombi bali kozi zitakazoonekana ni zile zenye nafasi tu pia baraza linashauri waombaji wajipime na kuangali ushindani wa kozi ili kufanikisha kuchaguliwa kwao. Vyuo na kozi zilizo na nafasi zimeainishwa hapa.

Baraza pia linapenda kuwaarifu waombaji waliofanya maombi kwenye vyuo vya Ualimu vya Serikali kuwa uteuzi kwenye vyuo hivyo unasubiri mwongozo wa Serikali na hivyo watafahamishwa punde uteuzi utakapokamilika. Waombaji wa vyuo hivi wanashauriwa kusubiri na kutokubadili machaguo yao hadi kutangazwa kwa uteuzi kwa vyuo vya Ualimu vya Serikali.

Baraza pia linapenda kuwataarifu waombaji waliokwisha chaguliwa kwenye awamu ya kwanza na wanataka kuomba uhamisho kutoka kozi ama chuo kimoja kwenda kingine wavute subira utaratibu utatolewa mara tu majibu ya waombaji wa awamu ya pili yatakapotolewa.

Aidha Baraza linapenda kuwafahamisha waombaji wa Shahada ya Kwanza (Bachelor Degree) waliofanya maombi kupitia mfumo wa pamoja wa udahili wa Baraza kuwa utaratibu wa kukamilisha maombi yao utatolewa baada ya mashauriano kati ya Baraza na Tume ya Vyuo Vikuu yatakapokamilika.

Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
NACTE
Tarehe: 08th Agosti, 2016

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.