July 2025

 Washindi 20 wa kwanza katika kampeni ya ‘Miamala ni Fursa’ wazawadiwa

Bank of Africa -Tanzania imetoa zawadi kwa washindi wake 20 wa kwanza wa wiki kupitia kampeni ya huduma za kibenki kwa njia ya kidigitali iitwayo “MIAMALA NI FURSA”, ambapo kila mmoja amepokea zawadi ya Sh50,000 kwa kutumia huduma za kibenki kwa njia ya simu za mkononi kupata huduma za huduma za kifedha.

Akizungumza kuhusu maendeleo ya kampeni hiyo iliyozinduliwa Juni 4, 2025, Afisa Mkuu wa Huduma za Kidigitali wa Bank of Africa-Tanzania, Bw Lameck Mushi, alisema kuwa mwezi mmoja tangu kuanza kwa kampeni hiyo ya miezi mitatu, imepokelewa vyema na umma wa Watanzania.

Bw Mushi alieleza kuwa kampeni hiyo inalenga kuhamasisha matumizi ya jukwaa la benki kupitia simu kwa kuwazawadia wateja wanaofanya miamala ya kila siku. Juhudi hizi ni sehemu ya dhamira ya benki yao kuendeleza matumizi ya huduma za benki kidigitali na kuendeleza ujumuishwaji wa kifedha nchini Tanzania.

Afisa Mkuu wa Huduma za Kidigitali wa Bank of Africa-Tanzania, Bw Lameck Mushi, akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu kampeni ya “Miamala ni Fursa” kwa wateja wao kwa kutumia huduma za kibenki kwa kupitia simu zao za kiganjani , kushoto ni Afisa Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa RejaReja Asupya Nalingigwa na kulia ni Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano Nandi Mwiyombella.

“Tunafurahia mwitikio mkubwa tulioupokea hadi sasa. MIAMALA NI FURSA tayari imefanya huduma za kibenki kupitia simu kuwa za kuvutia na muhimu katika maisha ya kila siku ya wateja wetu,” alisema Bw Mushi.


Akiendelea, alisema ukweli kwamba “Wateja wanashinda zawadi za fedha kwa kufanya miamala ya kulipa bili au kutuma fedha unaonyesha kuwa vitendo vidogo, lakini vya mara kwa mara vina mchango mkubwa. Zaidi ya hapo, tumeongeza unafuu kwa wateja wetu kwa kupunguza ada za miamala ya Bank-to-Wallet kwa zaidi ya asilimia 50."


Kila wiki, wateja watano watakaokamilisha miamala mitatu ya Bank-to-Wallet (B2W) na muamala mmoja wa ziada (malipo ya bili, ununuzi wa muda wa maongezi au umeme) kupitia B-Mobile watakuwa na nafasi ya kushinda.

Mwisho wa kampeni hii, ambayo itaendelea hadi Septemba 2025, mshindi mkuu atajinyakulia zawadi ya pesa taslimu Sh5 milioni.

Afisa Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa RejaReja Asupya Nalingigwa, alisisitiza: “Lengo letu ni kufanya huduma za kibenki ziweze kufikiwa kwa urahisi, ziwe na manufaa na ziwaguse wateja wetu kwa ukaribu zaidi. Iwe uko mjini au kijijini, mradi una B-Mobile, unaweza kushiriki na kushinda.”

Ili kuhakikisha ushirikishwaji wa wote, Bank of Africa-Tanzania imehamasisha timu zake za matawi kote nchini kusaidia kuwaunganisha wateja wapya na kutoa mafunzo ya kutumia huduma hizo za kidigitali. Timu maalumu ya msaada wa kiufundi pia ipo tayari kusaidia kutatua changamoto zozote za upatikanaji na kuhakikisha uzoefu mzuri kwa watumiaji wote.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano Nandi Mwiyombella, aliongeza: “Kampeni hii si kuhusu zawadi pekee, bali ni kuhusu kuwapa nguvu wananchi. Kwa kuhamasisha matumizi ya huduma za kidigitali kwa njia shirikishi na rahisi, tunawasaidia Watanzania wengi zaidi kushiriki katika mfumo rasmi wa kifedha.”

Kwa zawadi zaidi za fedha na washindi wapya kutangazwa kila wiki, Bank of Africa -Tanzania inawaalika wateja wake wote kufanya miamala, kushinda, na kufurahia huduma za kibenki kwa urahisi kupitia simu zao.

 

 Kuhusu BOA Bank (T) Limited

BOA-Tanzania ni benki ya biashara binafsi inayotoa huduma kwa wateja wa kampuni kubwa, wateja wa kati (SME) na wateja wa rejareja nchini Tanzania. Ilianza shughuli zake Juni 2007 baada ya kununua Eurafrican Bank iliyokuwa ikifanya kazi nchini tangu Septemba 1995.

Benki hii ni sehemu ya kundi la Benki ya Afrika, ambalo lilianza shughuli zake mwaka 1982 nchini Mali.

Kundi hili linafanya kazi katika nchi 19 za Afrika, ikiwa ni pamoja na Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Kati, pamoja na ofisi za uwakilishi Paris (Ufaransa), Hispania, London (Uingereza) na China. Tangu mwaka 2010, Benki ya Afrika imekuwa chini ya umiliki mkubwa wa BMCE Bank, benki ya tatu kwa ukubwa nchini Morocco, inayotoa huduma katika nchi 31 na mabara 4.

Kwa sasa, BOA-Tanzania ina matawi 17 ya rejareja, yakiwemo 8 Dar es Salaam na 9 katika mikoa ya Arusha, Mwanza, Zanzibar na miji mingine mikubwa.


Mawasiliano ya Vyombo vya Habari:

Tovuti: www.boatanzania.com

Beatrice E. Mirigo – Maendeleo ya Bidhaa & Mawasiliano

Barua Pepe: beatrice.mirigo@boatanzania.co.tz

 

Simu: +255 699 000 260

 

 Mwisho………..

Na Mwandishi Wetu

Ikiwa imebaki miezi michache tu kufanya uchaguzi mkuu, serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetekeleza miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali za uchumi na kuboresha huduma za kijamii nchini. Katika yote haya, imekuwa nyota inayong’aa si tu kwa Afrika Mashariki, bali pia kwa Bara la Afrika kwa jumla.

Utekelezaji wa miradi ya maendeleo na uboreshaji wa huduma za kijamii umefanyika kwa kuongozwa na sera, sheria, kanuni, taratibu na utekelezaji wa mikakati mbalimbali kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo endelevu.

 Dkt Samia Suluhu Hassan alianzisha ajenda ya ‘4R’ kama nguzo muhimu ya maendeleo inayolenga maridhiano, ustahimilivu, mabadiliko na kujenga upya mustakabali wa kitaifa kisiasa. Lengo ni kuboresha mahusiano kitaifa, kikanda na kimataifa, na kuhakikisha tunajenga taswira mpya ya Tanzania, huku tukiendelea kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika sekta mbalimbali za uchumi.

 Alipolihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 22, 2021, Dkt Samia Suluhu Hassan aliahidi kuimarisha demokrasia, haki za binadamu, kuboresha huduma za kijamii na miundombinu ya maji, kuboresha usafiri wa umma na usafirishaji wa mizigo, kuimarisha mazingira ya uwekezaji na mahusiano ya kitaifa, kikanda na kimataifa, na kuendeleza mazuri ya awamu zilizopita, ikiwa ni pamoja na kuleta mambo mapya, yanayoendana na wakati tuliomo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya madaktari na wauuguzi nchini.

Ukuaji wa Uchumi:

Serikali yoyote duniani katika ukusaji wa mapato ili kuimarisha uchumi wa ndani inategemea usimamiaji madhubuti wa sera, programu na mikakati mbalimbali kwa kuhakikisha mapato yanazidi kukua siku hadi siku. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/21, serikali ilikusanya kiasi cha Shilingi trilioni 20.59 na katika mwaka wa fedha 2023/24, ilikusanya kiasi cha Shilingi trillioni 28.83, ambazo ni mapato ya ndani. Pamoja na mambo mengine, katika ukusanyaji wa mapato, Shilingi trilioni 120.16 zilikusanywa kutoka vyanzo vya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wizara, wakala wa serikali na serikali za mitaa.

 Elimu:

Katika kuhakikisha Ilani ya CCM inatekelezwa kikamilifu, serikali ya awamu ya sita iliamua kuondoa ada, na ilianza kusambaza vitabu, na kujenga madarasa, na pamoja na mambo mengine kufanya mapitio ya Sera ya Elimu, mafunzo ya ufundi na mitaala ili kuhakikisha wahitimu wanapata maarifa na ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipata maelezo jinsi miundombinu ya maji safi na salama inavyojengwa ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana kwa Watanzania wote. Pamoja naye ni Waziri wa Maji Juma Aweso.

Katika sekta ya elimu, ambapo mapitio ya Sera ya Elimu ya mwaka 2014 (Toleo la 2023) yanalenga kuhakikisha wahitimu wanakuwa na maarifa, ujuzi, na maadili ili waweze kupenya katika soko la ajira.

Serikali iliamua kujenga shule 26 za wasichana za masomo ya sayansi kila mkoa, na shule 7 za wavulana kila kata nchi nzima, shule za msingi na sekondari 191,708 zilijengwa hadi mwaka 2020, na shule 254, 393 zimejengwa nchi nzima hadi mwaka 2025.

Pamoja na mambo mengine, shule za msingi mpya zilizojengwa mwaka 2025 ni 17, 986 na hadi mwaka 2020 zilizokuwepo shule 16,406. Idadi ya shule zote hizi ni matokeo chanya ya Ilani ya CCM.Vile vile serikali iliongeza vyuo vya ufundi stadi kutoka vyuo 662 mwaka 2020 hadi vyuo 860 mwaka 2024 kuendeleza ujuzi wa Watanzania katika sekta ya ufundi.

 Afya:

Msingi wa maendeleo ni pamoja na kuboresha afya ya umma. Serikali chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan iliwekeza katika sekta ya afya kwa kuongeza vituo vya afya kutoka 8,783 mwaka 2020 hadi vituo vya afya 12, 846, na kuboresha miundombinu ya majengo, kununua vifaa tiba, kuboresha huduma za kibingwa na kusomesha madaktari na wahudumu wengine katika sekta ya afya.

“Miaka minne iliyopita idadi ya vifo vya akina mama wanaojifungua ilikuwa 556 kati ya 100,000, lakini kutokana na uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya, idadi ya vifo ilipungua hadi kufikia 104. Lengo la dunia ni vifo 70. Nina hakika tutafika huko na kuondoa kabisa vifo vya akina mama wakati wa kujifungua,” alisema Dkt Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa hospitali mpya mojawapo nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, akimjulia hali mgonjwa katika moja ya hospitali za rufaa nchini. Rais Samia Suluhu Hassan ndiye mfariji mkuu wa Watanzania


Maji:

Miaka michache iliyopita akina mama walikuwa wakiamka alfajiri na kutembea umbali mrefu kutafuta maji, ambayo pia walikuwa hawana uhakika kama wangeweza kuyapata. Hadi kufikia mwaka huu, serikali ya awamu ya sita imetekeleza miradi ya usambazaji wa maji 2,331 katika miji na vijiji. Miongoni mwa miradi hiyo, ni ile ya Same, Mwanga na Korogwe ambapo wananchi wapatao 456,930 wamenufaika na miradi ya maji safi na salama.

Kilimo

Kwa miaka mingi kumekuwa na kauli mbiu mbalimbali za uhamasishaji wa kilimo tangu serikali ya awamu ya kwanza kama vile siasa ni kilimo, kilimo cha kufa na kupona, na kilimo kwanza (ambayo ilikuwa kauli mbiu ya serikali ya awamu ya nne). Kilimo ni uti wa mgongo, na kauli mbiu hii inathibitisha utekelezaji wa sera ya kilimo kwa serikali ya awamu ya sita kwa kuongeza bajeti yake kutoka Shilingi bilioni 294 mwaka 2021/22 hadi Shilingi trilioni 1.24 mwaka 2024/25, na kuifanya sekta ya kilimo kuchangia asilimia 26.2 kwa pato la taifa

Miaka ya nyuma Tanzania ilitofautisha mazao ya chakula, na ya biashara, lakini kwa sasa mazao karibu yote ni ya biashara, na mahitaji ni makubwa kwenye soko la nje, hata nyama kutoka Tanzania ambayo ni fursa muhimu kwa wakulima na wafugaji, lakini pamoja na mambo mengine, uzalishaji wa mazao ya chakula umeongezeka kutoka tani milioni 17.1 mwaka 2021 hadi tani million 22.8 mwaka 2024, huku serikali ikitoa ruzuku ya Shilingi billioni 300 katika kuimarisha sekta ya kilimo, ambayo huajiri takribani asilimia 65 ya nguvu kazi.

 Mifugo na Uvuvi

Serikali ya awamu ya sita imbadilisha mfumo wa kizamani na kuweka mfumo wa kisasa kuhakikisha ajira za Watanzania zinaendelea kuongezeka na usalama wa chakula una kuwa wa uhakika kwa kuongeza uzalishaji wa chakula cha mifugo kutoka tani millioni 1.38 mwaka 2020 hadi tani millioni 2.6 mwaka 2025, na kuongeza maeneo ya malisho ya mifugo kutoka hekta millioni 2.78 hadi hekta millioni 3.48. Ongezeko hili limepunguza migogoro ya wakulima na wafugaji, huku mauzo ya nyama nje ya nchi yakiongezeka pia kutoka tani 1,774 zenye thamani ya Dola za Kimarekani (USD) millioni 4.2 mwaka 2020 hadi tani 9,863.41 zenye thamani ya Dola za Kimarekani (USD) millioni 44 mwaka 2025.

 

Madini:

Sekta ya madini kwa muda mrefu ilionekana kama urithi wenye laana, lakini kwa sasa sekta hii muhimu kwa maendeleo ya taifa imeboreshwa kupitia mabadiliko ya Sheria ya Madini ya mwaka 2019, na mwaka 2022 mchango wake katika pato la taifa umeongezeka kutoka asilimia 6.8 mwaka 2020 hadi asilimia 10.1 mwaka 2025. Masoko ya madini yameongezeka kutoka 41 mwaka 2021 hadi kufikia 43 mwaka 2025 na vituo vya madini vimeongezeka kutoka 61 hadi kufikia vituo 109. Uboreshaji katika sekta ya madini umesogeza huduma kwa wananchi, na kuongeza uwazi katika sekta hii muhimu kwa maendeleo ya taifa.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, akizindua Mradi wa maji Butimba Mwanza.

Katika kuhakikisha mchango wa sekta hii unaendelea kukua kwa kasi, serikali ya awamu ya sita iliamua kununua mitambo 15 ya uchongoraji kwa wachimbaji wadogo wadogo na kuisambaza sehemu mbalimbali ili kuongeza upatikanaji wa taarifa za kijiolojia na kupanua uwazi wa sekta ya madini.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Amali-Mwamapalala katika kukamilisha ujenzi wa shule kama moja ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika sekta ya elimu nchini.

Pamoja na mambo mengine, baada ya kilio hicho cha muda mrefu na baadaye kwa kuwa na Sera ya Madini ya mwaka 2009 ya kuwawezesha Watanzania wazawa kushiriki katika sekta ya uchimbaji wa madini, kupata kazi za ukandarasi, zabuni na kutoa huduma mbalimbali kupitia Kanuni ya Maudhui ya Ndani (Local Content) Watanzania wamekuwa wakipata ajira ndani ya migodi na nafasi za menejimenti kushikwa na wazawa.

 Kwa sasa serikali iko mbioni kujenga kituo cha kisasa cha maabara kwa ajili ya upimaji wa madini katika ukanda wa Afrika Mashariki kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) ambayo ipo jijini Dodoma. Katika kipindi cha miaka minne ya awamu ya sita, chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan, serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Maudhui ya Ndani (Local Content) kwa kutoa fursa kwa wazawa katika sekta ya madini kwa upatikanaji wa kazi migodini na marekebisho ya Uwajibikaji wa Jamii (CSR).

 Viwanda

Katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na uchumi wa kijani kupitia viwanda, na kupunguza tatizo la ajira nchini kuanzia mwaka 2020 hadi 2025 jumla ya viwanda 47,063 vilianzishwa. Kati ya hivyo, viwanda vikubwa ni 428, vya kati ni 1,393, vidogo ni 11,847 na vidogo sana ni 33,395, na pamoja na mambo mengine, kuendeleza kiwanda cha ngozi (Kilimanjaro Leather International Company Limited) kinachomilikiwa na Mfuko wa Hifadhi kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa asilimia 86, na Jeshi la Magereza kwa asilimia 14 kwa uwekezaji wa Shilingi billioni 152.96. Kwa hakika sekta ya viwanda ni injini kwa maendeleo ya taifa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, akitizama ng’ombe kwenye moja ya programu za BBT za kunenepesha mifugo hapa nchini ili kukuza mahitaji ya mauzo ya nyama nje ya nchi na kuongeza kipato kwa wakulima na serikali kwa ujumla.

Makala haya hayawezi kutosha kueleza utekelezaji wa Ilani ya CCM, ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ameisimamia kikamilifu ili kulinda na kuendeleza maliasili na utalii, uchukuzi, miundombinu, ardhi, nishati, mawasiliano na sekta zingine mtambuka kwa masilahi mapana ya nchini yetu.

Mwisho….


MJI WA SERIKALI, DODOMA –

Serikali ya Tanzania imepongezwa kwa mafanikio yake katika kuimarisha mifumo ya tahadhari na ufuatiliaji wa majanga kupitia Kituo cha Dharura cha Taifa (Situation Room) kilichopo Mtumba, Dodoma.

Pongezi hizo zimetolewa na wataalamu kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso waliopo nchini kwa mafunzo ya siku tatu ya kubadilishana uzoefu, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Menejimenti ya Maafa, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amesema kituo hicho kimeongeza uwezo wa taifa kutoa tahadhari mapema kwa wananchi na kuratibu mashirika mbalimbali kukabili majanga.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Kituo hicho, Bi. Jane Kikunya, amesema wageni hao wameonesha nia ya kuiga mfumo huo katika nchi zao kutokana na mafanikio waliyojionea.

Aidha, wageni hao wameeleza kufurahishwa na jinsi taarifa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kuwasilishwa kwa wananchi kwa haraka na kwa usahihi.










 NAMWANDISHI MAALUM

Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. James Kilabuko amehimiza ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na majanga ya kibinadamu yanayochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa, kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kuimarisha vituo vya ufuatiliaji wa majanga na tahadhari ya mapema (Situation Room).

Akizungumza leo wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalum ya kubadilishana uzoefu, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na UNDRR na Kituo cha Sayansi cha Afrika Magharibi kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (WASCAL), Dkt. Kilabuko alisema mafunzo hayo ni sehemu ya kuimarisha uwezo wa kanda katika kukabili matukio ya majanga. Mafunzo hayo yalihusisha ujumbe kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso.

Dkt. Kilabuko alieleza kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa majanga, kupitia vituo vyenye uwezo wa kukusanya taarifa mbalimbali, zikiwemo za hali ya hewa, maji, kijamii na kiuchumi, jambo linalosaidia kukabili majanga kama vile ukame na mafuriko.

 “Tunauzoefu mkubwa wa kiutendaji ambao unasaidia kuhakikisha vituo vyetu vinafanya kazi kwa ufanisi kwa kuratibu taasisi mbalimbali kukabiliana na majanga,” alisema Dkt. Kilabuko.






Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.