Ripoti ya Kamati ya Mifugo,Utalii, Uwezeshaji na Habari imeitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuipitia upya mikataba ya Ujenzi wa Miundombinu na Uendeshaji wa mitambo ya Digital kati ya Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo na Kampuni ya AGAPE. 

Akiwasilisha Muhtasari wa Ripoti ya Kamati hiyo katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mlinde Mbarouk Juma amesema kumekuwa na malalamiko mengi na shutuma mbali mbali kutoka kwa makundi tofauti ya jamii  kuhusiana na mradi huo  hivyo Kamati haikuridhishwa na utendaji wa Kampuni hiyo.

 Amesema kuwa Wawekezaji wa AGAPE wameshindwa kufanya kazi na kuitia hasara serikali kwa kutumia wataalamu na rasilimali za serikali na hatimae kushindwa kukidhi mahitaji wa wananchi.

Aidha Kamati imesikitishwa sana na mikataba ya usimamizi na uendeshaji  kati ya Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo na wawekeza wa AGAPE  kwamba haufahamiki vizuri katika utendaji wake.

“Kamati imegundua kwamba Shirika la Utangazaji Zanzibar halikushirikishwa kikamilifu katika maamuzi wala mapato yanaypatikana katika mradi huo wa Digital”, alifahamisha Mwenyekiti huyo.

Kamati hiyo pia imesikitishwa na matumizi mabaya ya Jengo la zamani la ZBC ambalo limebadilishwa na kufanywa kuwa nyumba ya starehe kinyume na matumizi yake ambalo hukodishwa na kufanyiwa shughuli mbali mbali za kijamii zikwemo harusi na siku ya kuzaliwa (birth day)na kupoteza haiba yake. 

Hata hivyo Kamati hiyo imeshitushwa na taarifa za uvamizi uanoendelea katika shamba la Mifugo Pangeni katika Mkoa wa Kaskazini Unguja na kusema kuwa vitendo hivyo vimeshamiri katika maeneo mbali mbali ambavyo huleta hasara kwa serikali.
Akichangia Ripoti ya Kamati hito Mwakilishi wa Jimbo la Rahaleo Nassor Salim Ali (Jazira) ameomba serikali kuwapatia maposho yao kwa wakati waandishi wa Habari wanaohudhuria katika kikao cha Baraza la Wawakilishi .

Mwakilishi huyo  amefahamisha kuwa waandishi wa habari wamekuwa  hawapatiwi posho zao kwa wakati kitendo  ambacho kinawavuja moyo na kufanya hivyo ni kutowafanyia haki na  mshahara wao pia  mdogo sana ukilinganisha na kazi wanazozifanya
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.