Majengo pacha yenye ghorofa 35 ya PSPF Towers yaliyopo mtaa wa Sokoine jijini Dar es Salaam yemezinduliwa Septemba 16, 2015 na Rais Jakaya Kikwete.

Imeelezwa kuwa PSPF Towers ni moja ya majengo machache marefu barani Afrika na ndiyo jengo refu zaidi lililokamilika Afrika Mashariki na Kati, likiwa na urefu wa meta 147.
Ujenzi wa jengo hilo ulichukua miaka minne (2011 hadi 2015) na limegharimu shilingi bilioni 139.20 za Kitanzania. Lina maeneo ya ofisi na nyumba za makazi 88, sehemu ya mgahawa, mabenki, bwawa la kuogelea, sehemu za kufanyia mazoezi, maegesho ya magari na kadhalika.
Majengo mengine marefu Afrika ni Carlton Centre (meta 223) lililopo Afrika Kusini, Hassan II Mosque (meta 210) lililopo Moroko, Ponte City (meta 173) lililopo Afrika Kusini, Necon House (meta 160) lililopo Nigeria, Marble Tower (meta 152), Pear dawn (meta 152), Met Life Centre (meta 150) na 88 on field (meta 147) yote ya Afrika ya kusini.

Kudumu kwa rekodi ya urefu ya PSPF Towers lenye minara miwili na ukubwa wa meta za mraba 73,000, kutategemea kukamilika kwa majengo mengine yanayochipua kwa kasi barani Afrika.






Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa pensheni wa PSPF Bw. Adam Mayingu alipowasili kuzindua majengo pacha ya ghorofa 35 ya PSPF TOWERS mtaa wa Sokoine jijini Dar es salaam leo Septemba 16, 2015


Mrisho Mpoto na Mjomba Band wakitumbuiza kwenye sherehe za majengo pacha ya ghorofa 35 ya PSPF TOWERS mtaa wa Sokoine jijini Dar es salaam leo Septemba 16, 2015


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bw. William Erio na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dr. Ramadhani Dau alipowasili kuzindua majengo pacha ya ghorofa 35 ya PSPF TOWERS mtaa wa Sokoine jijini Dar es salaam leo Septemba 16, 2015


Majengo pacha ya ghorofa 35 ya PSPF TOWERS mtaa wa Sokoine jijini Dar es Salaam yaliyozindulia leo Septemba 16, 2015


Rais Jakaya Mrisho Kikwete hutubia kabla ya kuzindua rasmi majengo pacha ya ghorofa 35 ya PSPF TOWERS mtaa wa Sokoine jijini Dar es salaam leo Septemba 16, 2015


Rais Kikwete na msanii Mrisho Mpoto baada ya kuzindua majengo pacha ya PSPF


Rais Kikwete akikagua sehemu ya majengo hayo


Rais Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi na wakuu wa mifuko ya pensheni


Rais Kikwete akiwa na Bodi ya PSPF


Makandarasi wazalendo waliojenga majengo pacha ya PSPF Towers


Watumishi wa PSPF


Rais Kikwete akifunua pazia kuzindua rasmi majengo pacha ya PSPF TOWERS


Rais Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi majengo pacha ya PSPF TOWERS


Rais Kikwete akipokea zawadi ya picha ya PSPF Towers na Bw. George Yambesi

Source by www.wavuti.com









































Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.