Latest Post

Dar es Salaam, Tanzania- Bank of Africa Tanzania yawapa mbinu mpya wafanyabishara wa kati na waodogo jinsi ya kupanua wigo wa biashara , matumizi , elimu ya fedha , uwekezaji wa kimkakati ili kusaidia ukuaji wa biashara zao nchini.

‎Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika mafunzo hayo, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo , Bw Hamza Cherkaoui alisema kwamba sekta ya SME ina mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa Tanzania , utoaji wa ajira na kuboresha maisha ya watu wenye kipato cha kati na kidogo.

Bank of Africa Tanzania , Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Biashara) , Bw Hamza Cherkaoui akizungumza kwenye mafunzo ya siku moja ya masuala ya usimamizi wa fedha na biashara katika muendelezo wa utaoaji wa mafunzo kwa wafanyabiashara nchini ‘SME Clinics’ yaliyowakutanisha wafanyabiashara zaidi 100 jijini Dar es Salaam 

‎“Takribani wafanyabiashara na wajasiriamali 100 wamehudhuria mafunzo haya ya elimu ya fedha na kupata mbinu za kuweza kuvuka changamoto na vikwazo vyao vya kibiashara kwa kupata mafunzo kutoka kwa wataalamu wa fedha waliobobea,” 

‎Aliongeza kwenye mafunzo hayo wanapata fursa na nafasi ya kukutana na kupanua wigo wa mtandao wa ushirikiano wa kibiashara na kutafuta masoko mapya ya bidhaa zao kwa kupata fursa za majukwaa mapya ya biashara.

‎“tuna matawi sehemu mbalimbali za Africa , kuanzia Kigali, kampala , Lubumbashi na sehemu zingine na ni muhimu ukienda kufanya biashara huko mnaweza kutembelea matawi yetu na kuongeza wigo wa ushirikiano wafanyabiashara wa nchini hizo na kufungua fursa zingine za biashara Afrika Mashariki,” alisema Bw Cherkaoui 

‎Alisema kwamba Bank of Africa itaendelea kutoa mafunzo na ushirikiano na wafanyabiashara na wajasiriamali hapa nchini ili kuhakikisha kwamba wanakua pamoja katika kuboresha na kukuza uchumi wa nchini na mtu mmoja mmoja kwa kufanya biashara kwa ufanisi.

‎Kwa upande wake , Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa kati na Wadogo (SME) , Bi Beatrice Richard alisema kwamba wafanyabiashara waliopata mafunzo hayo wanatoka kwenye sekta tofauti kama vile usafirishaji , kilimo, vyakula , vifaa vya umeme, ujenzi na sekta ya fedha katika Mkoa wa Dar es Salaam,

Bank of Africa Tanzania,  Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa kati na Wadogo (SME) , Bi Beatrice Richard akizungumza na wafanyabiashara wa kati na wadogo kutoka sekta mbalimbali (hawapo pichani) kwenye mafunzo ya siku moja ya mafunzo ya elimu ya fedha , biashara na masoko yaliyofanyika jijini Dar es Salaam

‎“Umuhimu wa kuendesha mafunzo haya ya fedha na biashara kwa wafanyabiashara wa kati na wadogo ni kuwasaidia kupanua uelewa wao uhusu maswala ya fedha , kodi na na jisni ya kupata masoko mapya ili kukuza mapato yao,” alisema Bi Beatrice 


‎Alifafanua kwamba katika kauli mbiu ya “kukua Pamoja” ni juhudi za benki katika kuhakikisha kwamba uelewa biashara kwa wafanyabiashara unaongezeka , jinsi ya kuweka akiba na mbinu za kuja na bidhaa mpya sokoni.

‎Naye mfanyabiashara ambaye alihudhuria mafunzo hayo , Ndugu Kahlan Mazrui alisema kwamba mafunzo ni muhimu wa wafanyabiashara kwa sababu inaongeza uelewa wa matumizi ya fedha na maswala ya kodi na jinsi ya kuzungumza na wateja ili kukuza biashara zao.

‎“Mimi ni Mkurugenzi wa Sokoni Microfinanc kupitia benki hii nimeweza kuwa na matawi 28 ya biashara ya ukopeshaji fedha kwa wajasiriamali wadogo wadogo na wajane hapa nchini ni hatua kubwa sana nimeipiga,” alisema 

‎Pamoja na mambo mengine mafunzo haya yalikuwa ni fursa adhimu kwa wafanyabiashara kupata nafasi ya kujifunza namna bora ya kuzungumza na wateja na uanzishwaji wa bidhaa na uelewa mahitaji ya soko husika, Aliongeza Mazrui 

‎Meneja wa Tawi Jipya la Lumumba la Bank of Africa Tanzania, Bi Gloria Victor alisema kwamba ni muhimu kwa wafanyabiashara kupata mafunzo ya fedha , mikopo na aina ya uwekezaji ambao unafaa.

‎Alisema kwamba Bank of Africa Tanzania wamefungua tawi jipya la Lumumba ili wajasiriamali na wafanyabiashara kupata huduma za kifedha na mikopo kwa karibu zaidi.

‎Bank of Africa Tanzania wamejikita katika kuhakikisha wanawapatia wajasiriamali wadogo na wa kati maarifa, nyenzo na masuluhisho ya kifedha wanayohitaji ili kustawi. 

 Baadhi ya wafanyabiahsara waliohudhuria mafunzo hayo ya “SME Clinics’ wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wataalamu wa fedha kutoka Bank of Africa Tanzania , jijini Dar es Salaam.

‎Kupitia programu kama SME Clinic, wanajenga ushirikiano endelevu na wa kudumu na wateja wao Kwa kauli mbiu ya , “Kuwezesha Ukuaji Pamoja” , wanadhihirisha dira yao ya kuwa mshirika wa kifedha anayeaminika anayekua sambamba na wateja wake  na sekta ya biashara  za Tanzania.

‎Warsha n mafunzo kama hayo hufanyika kila mwaka na  ikisisitiza dhamira yake ya utoaji wa elimu ya masuala ya kifedha inayo lenga kuwawezesha wajasiriamali na kusaidia ukuaji wa biashara zao nchini kote.

‎SME Clinic ni sehemu ya Programu ya Elimu ya Fedha ya Bank of Africa Tanzania , iliyoanzishwa mwaka 2021 kufuatia Kanuni za Ulinzi wa Watumiaji wa Huduma za Fedha za mwaka 2019. Kifungu cha 19 cha kanuni hizo kinahitaji kila mtoa huduma za kifedha kuandaa programu za elimu ya fedha kwa wateja wake. 

‎Tangu ilipoanzanishwa programy hii, Bank of Africa Tanzania  imefanikiwa kuendesha warsha hizi (SME Clinics) mikoa ya  Dar es Salaam , Mwanza na Kahama na tayari imeweza kuwafikia zaidi ya wateja 800. 

‎Kwa kauli mbiu ya mwaka huu  “ukuaji wa Pamoja”  SME Clinic inaendelea kutimiza malengo makuu ya benki yakiwemo, Kuunga mkono agenda ya Bank of Africa Tanzania  ya maendeleo endelevu hasa ahadi  yake namba 5, Kuhamasisha maendeleo ya watu kila maeneno na katika kutimiza Kanuni za Ulinzi wa Watumiaji wa Huduma za Fedha ya mwaka 2019.

‎Mafunzo hayo yanalenga kuboresha ujuzi katika usimamizi wa biashara kwa wateja, Kuimarisha uhusiano kati ya Bank of Africa Tanzania  na wateja wake, na Kuhimiza matumizi ya mifumo na teknolojia za kidijitali ili kuongeza ufanisi wa biashara.

‎Kuhusu Bank of Africa (T) Limited

‎BANK OF AFRICA – TANZANIA ni benki ya kibiashara binafsi inayofanya shughuli zake nchini Tanzania kwa kuhudumia wateja wakubwa, wateja wadogo na wa kati pamoja na wateja wa rejareja. Ilianza rasmi nchini Tanzania mwezi Juni 2007 baada ya kununua Eurafrican Bank ambayo ilikuwa inafanya kazi tangu Septemba 1995. BANK OF AFRICA – TANZANIA ni sehemu ya BANK OF AFRICA GROUP ambayo ilianzishwa mwaka 1982 nchini Mali.

‎BANK OF AFRICA GROUP ni kundi la kibenki la kimataifa barani Afrika, likifanya kazi katika nchi 18 za Afrika ikiwemo Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Kati, na pia ina ofisi Paris, Uhispania, London (Uingereza) na China. Tangu mwaka 2010, BANK OF AFRICA imekuwa kampuni tanzu inayomilikiwa kwa kiwango kikubwa na BMCE Bank, benki ya tatu kwa ukubwa nchini Morocco, yenye uwepo katika nchi 31 na mabara manne.

‎Kwa sasa, BANK OF AFRICA – TANZANIA ina matawi 17 ikiwemo 8 jijini Dar es Salaam na 9 katika mikoa mingine kama Arusha, Mwanza, Zanzibar na miji mingine mikuu.

Bank of Africa Tanzania , Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Biashara), Bw Hamza Cherkaoui akimkabidhi cheti mmoja ya wafanyabiashara aliyeshiriki mafunzo hayo ya masuala ya fedha yaliyoandaliwa na benki hiyo.

Bank of Africa Tanzania , Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Biashara0 Bw Hamza Cherkaoui akibadilishana mawazo na wafanyabiashara waliohudhuria mafunzo hayo ya masuala ya fedha , uelewa kodi na jinsi ya kupanua masoko ya bidhaa zao ,yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

‎Mwisho

Quality Assurance in Higher Education Conference: Integrating Artificial Intelligence for Institutional Excellence

26th –27th  March 2026 @ The Capital Empire, Sandton, Johannesburg.

 

Dear Colleague,

We are pleased to invite you to the Quality Assurance in Higher Education Conference: Integrating Artificial Intelligence for Institutional Excellence, a high-impact international forum designed to address one of the most critical transformations facing higher education today.

Under the theme "Harnessing AI to Transform Quality Assurance and Drive Global Competitiveness in Higher Education," this conference responds to the growing need for smarter, data-driven, and future-ready quality assurance (QA) systems. As higher education institutions navigate globalisation, digitalisation, and increasing accountability demands, traditional QA approaches are no longer sufficient on their own. Artificial Intelligence (AI) now offers powerful tools to enhance transparency, efficiency, and institutional performance.

This conference brings together senior university leaders, QA professionals, policymakers, ICT specialists, and EdTech innovators to explore how AI can be practically and ethically integrated into QA frameworks. Through keynote addresses, hands-on workshops, panel discussions, and a dedicated technology exhibition, participants will gain real-world insights into AI-driven performance monitoring, accreditation support, curriculum enhancement, and strategic decision-making.

Key highlights of the conference include:

·       Practical demonstrations of AI tools for QA and institutional performance monitoring

·       Regional and global case studies on successful AI integration

·       Expert discussions on policy, ethics, governance, and data protection

·       Strategic guidance on funding and investment models for AI-driven QA systems

·       Opportunities to build regional and international collaboration networks

Participants will leave with actionable strategies, an AI-integrated QA roadmap, and access to a post-conference implementation guide to support institutional transformation.

We believe your participation will add significant value to the dialogue while equipping you with the knowledge and networks needed to lead quality assurance innovation in your institution and beyond.

We would be honoured to have you join us and contribute to shaping the future of higher education. For registration or inquiries, please contact us at+27 (0)11 568 8240 / Email: admin@cskba.co.za.

Regards,

 

Asanda

CSK Business Architects

447 vale avenue

Randburg, Ferndale

South Africa

Call: +27 (0) 11 568 8240

Email:admin@cskba.co.za

Website. www.cskba.co.za

 Mgodi wa North Mara viongozi wake kwa asilimia 100 ni Watanzania

Dodoma:Waziri wa madini,Mh.Antony Mavunde amesema mgodi wa North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara ambao unaendeshwa na kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals umekuwa kinara katika kwa utekelezaji wa sheria na kanuni ya Maudhui ya Ndani (Local Content) ikiwemo upande wa ajira ambapo asilimia 100 ya viongozi wanaoendesha mgodi ni Watanzania.Mbali na viongozi wa mgodi huo pia Meneja wa Barrick nchini (Country Manager)  ni Mtanzania.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mkakati wa Serikali wa kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo mzima wa sekta ya madini alisema  kwenye miradi ya madini, amesema kumeshuhudiwa ongezeko la ajira kwa watanzania kutoka ajira 6,668 kati ya ajira 7,003 sawa na asilimia 95 kwa mwaka 2018 hadi kufikia ajira 18,853 kati ya ajira 19,356 sawa na asilimia 97 kufikia Desemba 2024.

Alisema katika nafasi zinazohitaji kupata uzoefu kutokana na kukua kwa teknolojia duniani, kumekuwa na utaratibu wa kisheria wa urithishwaji wa Watanzania kwa nafasi zinazoshikiliwa na Wataalamu wa Kigeni na kutoa mfano wa kampuni ya Barrick kupitia mgodi wake wa North Mara ambapo nafasi zote za juu za uongozi wanaoendesha shughuli kwa weredi mkubwa zinashikiliwa na Watanzania kwa asilimia 100.

Kupitia mkutano huo Waziri Mavunde pia alitangaza rasmi orodha ya Huduma na Bidhaa 20 zinazopaswa kutolewa Migodini kupitia kampuni zinazomilikiwa na watanzania kwa asilimia 100 ikilenga kuongeza wigo wa ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo mzimawa sekta ya madini baada ya kufanywa marekebisho ya Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania kwenye Sekta ya Madini za Mwaka 2018.

‘’Kwa awamu ya kwanza tarehe 14 Novemba, 2025 Tume ya Madini ilitangaza orodha ya bidhaa na huduma zinazotakiwa kutolewa na kampuni zinazomilikiwa na kampuni za kitanzania kwa asilimia 100, ambapo kwa mara ya kwanza Tume ya Madini itatatangaza kupitia Kanuni 13A,’’ amesema Waziri Mavunde.

Akizungumzia manunuzi ya huduma na bidhaa kwa kampuni za kitanzania amesema yameongezeka kutoka kiasi cha Shilingi trilioni 1.85 kati ya manunuzi ya huduma na bidhaa za jumla ya kiasi cha Shilingi trilioni 3.01 sawa na asilimia 62 kwa mwaka 2018 hadi kufikia Shilingi trilioni 4.41 ambayo ni sawa na asilimia 88 ya kiasi cha Shilingi trilioni 5.00 ya manunuzi yote yaliyofanyika mwaka 2024.

Pia alisema Serikali inaendelea kufungua wigo kwa ushiriki wa watanzania katika sekta ya madini na kuongeza manufaa ya rasilimali madini kwa kutenga eneo maalum la uwekezaji la ulipokuwa Mgodi wa uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu la Barrick Buzwagi lenye ukubwa wa ekari 1331, kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kuzalisha bidhaa za migodini na kusema tayari viwanda sita vimekwisha jengwa huku wamiliki wa viwanda 15 wakionesha nia ya kujenga viwanda katika eneo hilo.

Waziri Mavunde ameitaka sekta binafsi nchini Tanzania kuchangamkia fursa ya usambazaji wa bidhaa na utoaji wa huduma migodini ili kuhakikisha fedha kiasi kikubwa inabaki nchini Tanzania na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.

Amewasisitiza wawekezaji wote kuzingatia Sheria za madini na utekelezaji wa Kanuni za Ushirikishwaji Watanzania kwenye sekta ya madini sambambamba na kuwataka watanzania kuchangamkia fursa zilizopo katika miradi ya madini ili kukabiliana na changamoto za ajira kwa manufaa ya mtu mmoja mmoja na manufaa ya taifa.

Waziri wa Madini , Anthony Mavunde akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) juu ya ushirikishwaji wa watanzania kwenye sekta ya madini nchini.

 Zahanati mpya yazinduliwa katika kijiji cha Mangucha..

Na Mwandishi Wetu, Tarime 

Katika hafla ya kukabidhiwa zahanati ya wananchi wa mangucha moja ya kijiji kilichopo Jirani na mgodi wa dhahabu wa North Mara Wilayani , Tarime walionekana kkuwa na nyuso za furaha na matumaini ya kuondokana na changamoto ya kutembelea mwendo mrefu kufuata huduma za afya.

Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ilikabidhiwa zahanati ya Kijiji ambayo imejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 164 zilizotokana na fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) zilizotolewa na Mgodi wa Barrick North Mara unaoendeshwa na kampuni Barrick kwa ubia na serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals.

Ufanikisha wa mradi huu ni moja ya utekelezaji wa mkakati endelevu wa kampuni ya Barrick unaojumuisha ushirikiano na wadau na vipaumbele ambavyo vimelenga kufanikisha kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii zinazoishi kwenye maeneo yaliyopo Jirani na migodi yake sambamba na kufanikisha utekelezaji wa Malengo Endelevu ya Dunia (SDGs).

Akiongea wakati  wa hafla ya makabidhiano ya zahanati hiyo Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime,Albinus Kirina,alisema kukamilika kwa ujenzi wa zahanati ya Mangucha kutawaondolea wakazi 4,460 wa kijiji hicho adha waliyokuwa nayo ya kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta huduma za afya nje ya kijiji hicho.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime (DAS) Saul Mwaisenye, alisema ujenzi wa zahanati hiyo umezingatia viwango vya ubora na thamani ya fedha iliyotumika (value for money).”Nimeridhika na ujenzi wa zahanati hii ndio maana nimekata utepe  na kuruhusu Mgodi na Halmashauri kutiliana saini za makabidhiano haya”alisema Mwaisenye akiyemwakilisha Mkuu wa wilaya ya Tarime,Meja Edward Gowele kama Mgeni Rasmi.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime (DAS) Saul Mwaisenye (wa pili kutoka kushoto) akikata utepe katika hafla ya uzinduzi wa zanati ya Mangucha iliyojengwa na mgodi wa Barrick North Mara,wengine pichani wa kwanza ksuhoto ni Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Barrick North Mara , Francis Uhadi na wa tatu kulia ni Mbunge wa Tarime Vijijini , Mwita Waitara na viongozi wengine wa wilaya ya Tarime na Mgodi katika hafla ya makabidhiano ilifanyika mwanzoni mwa wiki kijijini Mangucha.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, Mwita Waitara, aliitaka idara ya afya kutumia baadhi ya vyumba vya zahanati hiyo kwa ajili ya huduma za wanawake wanaojifungua wakati ujenzi wa majengo ya mama na mtoto na miundombinu ya kichoma taka yakisubiriwa.“Haitakuwa na maana kama akina mama hawatapata huduma za kujifungulia hapa,” alisema Mbunge Waitara.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Matera Newland Chacha, naye aliushukuru Mgodi wa Barrick North Mara na kuahidi kuendelea kuupatia ushirikiano katika utekelezaji wa miradi mingine ya CSR ndani ya halmashauri hiyo.

Naye Diwani wa Kata ya Nyanungu, Tiboche Richard, aliishukuru Barrick North Mara kwa kuwezesha ujenzi wa zahanati hiyo ambayo imesogeza huduma za afya jirani na wananchi wa Mangucha.“Tunawashukuru sana watu wa Mgodi wa Barrick North Mara na tutaendelea kuwa mabalozi wazuri wa mgodi,” alisema Diwani Tiboche.

Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Barrick North Mara, Francis Uhadi (kushoto) akiongoza ujumbe wa viongozi wa Serikali wilaya  ya Tarime kutembelea maeneo ya zahanati ya Mangucha iliyojengwa na Fedha za CSR zilizotolewa na mgodi huo wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika mwanzoni mwa wiki.

Awali, Meneja Mahusiano wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara, Francis Uhadi, alisema afya ni moja ya sekta ambazo wanazipa kipaumbele kwenye utekelezaji wa miradi inayogharimiwa na fedha za mpango wao wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR).

"Sekta ya afya ni ya pili kwa ukubwa wa uwekezaji wa CSR, ikiwa na asilimia 20 ya fedha zote tulizowekeza hadi sasa. Tangu mwaka 2020 hadi sasa, mgodi umewekeza shilingi bilioni 5.4 katika ujenzi wa zahanati, vituo vya afya, nyumba za watumishi na vifaa tiba.

"Kwa mwaka 2025, tunatekeleza miradi 21 ya afya yenye thamani ya shilingi bilioni 2.4. Miradi mingi ipo kwenye hatua za mwisho, ikiwemo huu wa Zahanati ya Mangucha uliokamilika kwa asilimia 100, na mingine itaendelea kukabidhiwa kwa halmashauri kadiri inavyokamilika.

“Makabidhiano ya zahanati hii ni ushahidi wa mafanikio tunayoyapata kupitia utekelezaji wa miradi ya CSR kwa ushirikiano wa karibu kati ya Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime pamoja na wananchi kwa ujumla,” alisema Uhadi.

Akizungumza kwa niaba ya wana-Mangucha, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Kemahi Irumbe Mgesi,alitoa shukrani kwa kujengewa zahanati hiyo na aliahidi kushirikiana na wananchi kulinda miundombinu yake kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.

Ripoti ya utekelezaji Mkakati Endelevu ya mwaka 2024 ya kampuni ya Barrick Mining Corporation iliyotolewa karibuni imebainisha mafanikio muhimu yaliyopatikana katika uendeshaji wa shughuli zake katika mataifa mbalimbali duniani.

Mafanikio muhimu endelevu yaliyopatikana yaliyobainishwa katika ripoti hiyo ni kampuni kuwekeza katika matumizi ya vyanzo vya nishati mbadala,Uwezeshaji biashara katika maeneo yake ya kazi,miradi ya jamii na Serikali, na kuunda ushirikiano na jamii zinazoishi Jirani na maeneo yake ya kazi kwa kutekeleza miradi ya kujenga shule,vituo vya afya,upatikanaji wa maji safi ya kunywa na miundombinu mingine muhimu-pamoja na uwekezaji katika kuwezesha upatikanaji wa walimu bora,wauguzi na vifaa vinavyohitajika kuboresha upatikanaji wa huduma hizo.

Mwisho

Na Damas Makangale  - Dodoma 

Taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa Afrika - Tanzania (Misa - Tan), imetoa mafunzo ya uandishi wa habari za amani (Peace Journalism)  kwa wanahabari zaidi ya 100 kutoka mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani ili kuboresha uelewa wao kuhusu kuripoti nyakati za migogoro.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Denis Lazaro Londo, akizungumza wakati akifungua mafunzo kuhusu Uandishi wa Habari wa Amani (Peace Journalism) yaliyoandaliwa na MISA Tanzania

Mafunzo hayo ya siku moja yamekuja baada ya vurugu za uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, na kuonekana ombwe ya uandishi wa habari za amani ambayo inalenga kupunguza mikwarazo ya makundi ndani ya jamii na kuleta utengamano.

Waandishi hao walikutana jijini Dodoma hivi karibuni ili kuwajengea uwezo waandishi wa habari namna ya kuripoti taarifa za vurugu , machafuko na migogoro kwa kuzingatia maadili , desturi na miiko ya uandishi wa habari.

Mafunzo hayo pia yalilenga kuwajengea uwezo waandishi kuelewa dhana ya Uandishi wa Habari za amani, aina ya uandishi unaojikita katika kuimarisha utulivu, kuzuia uchochezi, kupunguza upotoshaji, na kuandika habari zinazojikita kwenye utatuzi badala ya uchochezi.

Akifungua mafunzo hayo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani. Denis Lazaro Londo, alisema waandishi wana jukumu la kulinda umoja wa kitaifa kupitia matumizi ya lugha inayojenga, utoaji wa taarifa sahihi, na kuepuka taarifa zinazoweza kuchochea migogoro, haswa nyakati za migogoro na machafuko.

Aliongeza waandishi wa habari ni daraja muhimu linalounganisha Serikali na wananchi, hivyo lazima watekeleze wajibu wao kwa uadilifu bila kuyumbishwa na mtu yeyote mwenye nia ya kuichafua tasnia hiyo.

"Tuna imani kwamba mafunzo haya yataleta tija kupitia kwenu wanahabari mliohudhuria, serikali inawahakikishia kuwa mtaendelea kuwa salama na vifaa vyenu wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yenu." Alifafanua Londo 

Amewataka wanahabari kutambua kwamba uandishi wa habari ni muhimu lakini uandishi wa habari za amani ni muhimu zaidi, zinazojikita kutunza maslahi  na tunu ya Taifa na wananchi wake.

Aliongeza kwamba wizara ya mambo ya ndani iko tayari kushirikiana na wanahabari katika kulinda misingi ya utawala bora na demokrasia ili kupanua wigo wa ushirikiano kwa maslahi ya Taifa.

Alisema kwamba serikali inaendelea kuhakikisha wananchi wanapata haki ya kupata taarifa na kwamba falsafa ya 4R inalenga kulinda wanahabari na kutetea uhuru wa kujieleza akitolea mfano wa vyombo vya habari vilivyofungiwa kufunguliwa.

"Nafarijika kuwa Misa Tanzania mmekuwa mdau mwaminifu kwa serikali katika nyakati nzuri na hata ngumu. Huu ndio uzalendo tunaoutaka  kutanguliza maslahi ya Taifa mbele bila kuathiri uhuru wa kitaaluma." Aliongeza 

"Wizara ya mambo ya ndani inaendelea kushirikiana nanyi katika mambo yote yanayohusu usalama wa wanahabari, ulinzi wa amani na mafunzo kwa wanahabari katika kuhakikisha kwamba, tunalinda uhuru wa habari, wanahabari wanalindwa, tunatetea uhuru wa kujieleza lakini pia haki ya wananchi wetu kupata taarifa."

"Tukio la Oktoba 29,2025 ni funzo kwetu sote, sisi serikali, nyinyi wanahabari na jamii nzima kwa ujumla. Ni kweli wanahabari mnalo jukumu la kulinda amani haki utulivu na umoja wa kitaifa na tunawashukiru sana kwa kuendelea kuhamasisha amani."

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwenyekiti wa MISA Tanzania, Edwin Soko, alsiema vyombo vya habari nchini Tanzania havitakubali kuchonganishwa na wananchi bali vitaendelea kusimamia maadili, uzalendo na weledi katika kuripoti.

Pamoja na mambo mengine alisema kwamba waandishi wa habari ni daraja muhimu linalounganisha Serikali na wananchi, hivyo lazima watekeleze wajibu wao kwa uadilifu bila kuyumbishwa na mtu yeyote mwenye nia ya kuichafua tasnia hiyo.

“Vyombo vya habari ni nguzo kubwa ya usalama wa Taifa,” alisema Soko. “Hatutaruhusu mtu yeyote kutikisa au kuathiri misingi yetu ya uzalendo. Waandishi wa Tanzania ni wazalendo, si wasaliti”,aliongeza Soko.

Akigusia tukio la Oktoba 29, Soko alifafanua kwamba sekta ya habari iliguswa moja kwa moja, kwani baadhi ya waandishi waliumia, walipoteza wenzao na wengine kupoteza vifaa vya kazi.

Ametoa wito kwa Wizara ya Mambo ya Ndani kuendelea kulinda amani ya nchi pamoja na kuhakikisha waandishi wanakuwa salama wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku.

Aliongeza  kuwa MISA Tanzania itaendelea kutoa mafunzo ya Uandishi wa Habari wa Amani ili kujenga uwezo wa wanahabari kuandika habari zinazohamasisha amani, kushusha joto la mgogoro, kupunguza taarifa za uchochezi na kuchochea  umoja na mshikamano wa kitaifa

Mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam Alex Sichona aliwasihi wanahabari kufanya uandishi wa habari unaochochea amani, kupunguza mifarakano miongoni mwa jamii na inayopunguza maumivu kwenye jamii baada ya kutokea migogoro.

“popote panapotokea mgogoro basi ni lazima mawasiliano ndio chanzo kikuu cha huo mgogoro husika lazima jamii ijue mawasiliano ni nyenzo muhimu katika kufikia maridhiano na maelewani na utengamano wa jamii husika” alisisitiza Dk Sichona.

Alisema ni vyema wanahabari wakazingatia maadili ya uandishi hususani kwenye vyombo vya habari vya mtandaoni ambavyo wengi wao wamekuwa wakiwahi kutoa taarifa (Breaking News) bila kujiridhisha ama kwa kutumia vichwa vya habari vinavyozua taharuki ili kuvutia wasomaji na wafuatiliaji wa mitandao ya kijamii.

"Uandishi wa habari wa mtandaoni na mitandao ya kijamii isitumike kukuza migogoro kwa ingawa changamoto ni kubwa katika kushughulika na uandishi wa kiraia (citizen journalism) na hii ni kutokana na ukauji wa teknolojia na mawasiliano ambayo kila mtu anaweza kufanya au kusambaza taarifa kupitia simu yake ya kiganjani,” aliongeza 

Alifafanua kwamba uandishi wa habari kiraia au (Citizen Journalism) unakuwa kwa kasi na ndio mara nyingi huweka na kupata taarifa kwa haraka (Breaking News) bila kujiridhisha kutoka vyanzo vya uhakika vya utoaji wa taarifa na kuzingatia miiko na kanuni za uandishi wa habari.

Kwa upande Mhadhiri , Dkt  Dotto Bulendu alisema kwamba ni muhimu kujua tabia za vijana maana ndio Kundi kubwa kwenye jamii na linakabiliana na wimbi kubwa la mwamko wa kihalaiki kutokana na msukumo wa mitandao ya kijamii duniani.

Aliongeza kwamba kuna tatizo la upotoshaji wa taarifa mkubwa (information disorder) ambayo inaanza kwenye mitandao ya kijamii hadi kwenye vyombo vya habari rasmi vya ndani na nje ya nchii.

“kwa mfano vyombo vya habari vya nje vinaripoti kwamba Rais wa Tanzania , Dkt Samia Suluhu Hassan aliapishwa kwenye kambi ya Jeshi wakati ilikuwa ni kwenye viwanja vya mashujaa hii ni upotoshaji mkubwa na mpaka sasa hakuna aliyerekibisha hiyo,” alisema 

Alifafanua ni muhimu kwa kila mwandishi wa habari anatakiwa kuzingatia madhara na faida ya taarifa kabla ya kuitoa, kuangalia manufaa yake kwa jamii anayoitumika.

DODOMA: Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limewataka wadau wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi nchini (TVET) kutumia viwango vipya vya ubora pamoja na miongozo iliyoboreshwa ili kuzalisha wahitimu wenye ujuzi, umahiri na uwezo wa kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya uchumi na jamii.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) Dkt.Mwajuma Lingwanda.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa NACTVET, Bernadetta Ndunguru, ameyasema hayo wakati wa warsha ya utoaji taarifa kuhusu viwango vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) pamoja na miongozo mbalimbali kwa wadau wa tasnia hiyo, iliyofanyika leo Novemba 18, 2025 mkoani Dodoma.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa NACTVET, Dk. Mwajuma Lingwanda, amesema Baraza litaendelea kuandaa, kupitia na kuboresha miongozo kadri inavyohitajika ili kuhakikisha kunakuwepo mazingira bora ya kujenga rasilimali watu yenye ujuzi stahiki kulingana na malengo ya serikali na matarajio ya soko la ajira.

Aidha, amesema wamedhamiria kuendelea kufanya warsha kama hizo mara kwa mara kadiri itakavyowezekana, kwa lengo la kukutana, kufahamiana, kujadili na kushirikiana kuhusu malengo ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi.

Warsha hiyo imeshirikisha wadau kutoka Vyuo vya Ufundi (TET), Vyuo vya Ufundi Stadi, Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, Shule za Sekondari Mkondo Amal, pamoja na wawakilishi na viongozi mbalimbali kutoka wizara mbalimbali ikiwemo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.







By Correspondent

Sudanese Ambassador to Tanzania, Dr Mohamed Abdalla Abdelhameed, has accused the international community for dilly-dallying in taking legal action against the Rapid Support Militia (RSF) despite their decisive attacks on diplomatic missions, the UN and aid organisations.

Ambassador of Sudan in Tanzania, Dr Mohamed Abdalla Abdelhameed

Speaking in an exclusive interview with this correspondent in his office in Dar es Salaam earlier this week, Dr Abdelhameed said the ongoing war in Sudan was a war waged by the RSF, a group that rebelled against the state with local, regional, political and logistical support.

“It began with an attempt to seize power by force of arms and the rebellion quickly evolved into a full-scale war against the Sudanese state and people,” he emphasised.

He went on to say that the RSF were engaged in a proxy war, acting on behalf of foreign powers pursuing their own interests against the government and people of Sudan.

Explained that the RSF deserved to be designated as a terrorist organisation for its grave crimes, supported by regional financiers and foreign mercenaries that helped them to destroy the Sudanese soil.

“Here we express regret that Tanzania was among the earliest victims, when the RSF looted a Tanzanian Embassy vehicle near the International University of Africa on the first day of the war,” he lamented.

He underscored that the militia continued defying international law, the Jeddah Declaration, and UN Security Council resolution, including the arms embargo on Darfur and a resolution on Al-Fashir.

“Since mid-2024, the Rapid Support Forces (RSF) imposed a suffocating siege on the city of El Fasher, the capital of North Darfur State, blocking the entry of food, medicine, and humanitarian aid to hundreds of thousands of trapped civilians,” 

“As battles intensified and roads were cut off, living conditions deteriorated sharply—pushing the population to the brink of famine—while international organizations were unable to reach the city safely,” he said.

After eighteen months of continuous siege, RSF militia stormed El Fasher in late October 2025, opening a new and tragic chapter in the humanitarian disaster that has long plagued the Darfur region.

This development was not merely a military victory in a local battle, but a catastrophic turning point in the balance of the Sudanese conflict—one that unleashed scenes of horror and atrocities reminiscent of the darkest episodes of modern humanitarian crises, perpetrated by the RSF militia. He lamented 

As RSF militia entered El Fasher, reports quickly emerged of mass executions and widespread looting targeting civilians along ethnic and tribal lines—some of which were recorded by the militia’s own cameras.

Ambassador Dr Abdelhameed went on to say  eyewitnesses described horrific scenes: bodies lying in the streets, hospitals reduced to rubble, and entire neighborhoods burned to the ground.

Humanitarian agencies that had been operating in the city confirmed that more than 2,000 civilians were killed within the first 48 hours of the RSF’s takeover.

He explained further that thousands more fled on foot toward remote areas seeking safety, while the United Nations and the international community have so far been unable to verify the full extent of the catastrophe due to continuing insecurity and systematic violence by RSF fighters.

Credible human-rights reports indicate that the events in El Fasher were not random acts of revenge, but a planned, ethnically-motivated campaign aimed at specific communities based on their identity and tribal affiliation.

“Weeks before the city’s fall, UN High Commissioner for Human Rights Volker Türk warned of “the imminent risk of mass atrocities” in El Fasher—warnings that went largely unheeded by the international community,” he mentioned.

He noted that according to multiple international media and intelligence reports—including Le Monde (November 2025) and The Washington Post (September 2025)—the United Arab Emirates provided logistical and military support to the RSF through supply lines running across neighbouring countries. These investigations also revealed that Emirati territory was used as a hub for the purchase and export of Sudanese gold, believed to be financing RSF operations.

Private companies based in the UAE allegedly facilitated the transport of military equipment via cargo aircraft to areas near Darfur and Chad. These claims are supported by satellite imagery, field testimonies, and documentation from UN expert panels.

What happened in El Fasher cannot be dismissed as an isolated episode in Sudan’s civil war; it constitutes a crime against humanity under international law.

Observers and rights advocates are calling for the establishment of an independent international investigation under UN supervision to identify and prosecute those responsible—regardless of rank or affiliation.

The continuing silence of the international community in the face of recurring massacres in Sudan is no longer acceptable. Failing to act is tantamount to complicity with the perpetrators.)

Dr Abdelhameed assured that the government of Sudan remained open to any initiative aimed at ending the war, “provided that no state or organisation supports and participates in the war through supplying weapons, facilitating their transfer, offering political and any other form of support to the rebels.”

He noted that the SAF is one of the oldest state institutions in Sudan, operates professionally, free of partisan allegiance, and is committed to democratic transition. He added that it was ready to hand over power to any consensus-based elected civilian government.

Among other things, the Ambassador said the government struggled to find solutions as seen in the Jeddah Declaration in May 2023, which facilitated border openings and airports to alleviate the sufferings of citizens and facilitated the delivery of humanitarian aid, reaffirming the government’s commitment to international law to protect civilians.

“Under the leadership of LTG Abdel Fattah Al- Burhan, the SAF have sought from the very beginning to avert the outbreak of war, from the early weeks of the conflict, they have worked to bring it to an end through Jeddah Platform and continue to maintain their position in favour of ending hostilities,” he said.

Despite the ongoing war, Tanzania and Sudan also have good cooperation and coordination in security and counter-terrorism and they promise opportunities for cooperation, taking advantage of Tanzania’s potential for teaching Kiswahili language.

Ends.

By Damas Makangale

The Republic of Sudan seeks to benefit more from Tanzania’s mining sector (especially gold), tourism, the development of natural reserves and electric railways after the reopening of bilateral ties.

Speaking in an exclusive interview with this newspaper in Dar es Salaam recently, the Ambassador of Sudan to Tanzania, Dr Mohamed Abdalla Abdelhameed, said the two countries would complete the signing of a memorandum of cooperation as soon as possible.

Ambassador of Sudan in Tanzania, Dr Mohamed Abdalla Abdelhameed

“There is a need for high level visits between the two countries. The time has also come to complete the steps of establishing a political consultation committee,” he said.

He noted that historical relations that bound together Sudan and Tanzania could be traced to the leadership of the Founding Father of the Nation, President Julius Nyerere, and the most telling evidence was that the Sudanese Embassy in Dar es Salaam was one of the very first embassies to be opened in Dar es Salaam in March 1962, just three months after Tanganyika got its independence.

“Sudanese people proudly recall the historic visit of President Julius Nyerere to Sudan in November 1974 during which a grand reception held for him in Abu Deleig, East of Khartoum, remains one of the largest gatherings in Sudan’s history.”

Dr Abdelhameed reaffirmed Sudan’s commitment and readiness to fully cooperate in elevating bilateral relations to the highest level across political, economic and cultural domains as Tanzania pursued a reformist policy of opening up to the regional and international community with great emphasis on economic diplomacy.

“While upholding the principles of African unity espoused by Mwalimu Nyerere, Tanzania demonstrates readiness to share its successful experiences with African states. This approach resonates with Sudan’s own vision towards Africa, anchored in a comprehensive perspective on cooperation at bilateral, regional, continental and international levels,” he emphasised.

He noted that there were plans and programnes to develop and promote investment and increase trade exchange between the two nations without forgetting the unprecedented development that Tanzania had made in its two major projects. He said Julius Nyerere Hydropower Project and the Standard Gauge Railway (SGR) made Tanzania increase the capacity of hydropower generation and boast of high-speed electric railways in Africa.

Dr Abdelhameed noted, among other things, that it was a clear sign that the two nations had opened a new chapter of cooperation after the recent re-opening of Tanzania’s Embassy in Khartoum after a period of closure that lasted more than 30 years.

Among other things, the Ambassador said the areas of cooperation between two countries were promising after the cessation of the work of the Joint Economic Committee that had negatively affected trade exchange between the two countries.

“Tanzania, especially, lost one of its largest markets of tea and coffee trade after the withdrawal from COMESA in 2000, as about 80 per cent of Sudanese tea imports came from Tanzania until the end of the 1990s.”

He said as soon as he arrived in Tanzania, he held several meetings with the Tea Board of Tanzania (TBT) to discuss ways to facilitate the export of Tanzanian tea to Sudan,” he explained.

He emphasised that Tanzania and Sudan also had good cooperation and coordination in relation to counter-terrorism and there were promising opportunities for cooperation, taking into account of Tanzania’s potential in teaching Kiswahili language.

 

Ends

The Embassy of the Kingdom of the Netherlands in Dar es Salaam on Wednesday hosted a one-day seminar on Dutch-Tanzania poultry knowledge exchange, aimed at improving efficiency and productivity within the country’s poultry sector.

In her opening remarks, the Ambassador of the Netherlands to Tanzania, H.E. Marjo Crompvoets, stated that the seminar was intended to connect Dutch poultry firms with their Tanzanian counterparts in an effort to advance the local industry.

“The longstanding relationship between Tanzania and the Netherlands spans over four decades, with strong cooperation in trade and agribusiness,” she said. Ambassador Crompvoets noted that the Netherlands, renowned for its innovation and sustainability in poultry farming, is keen to strengthen its partnership with Tanzania through shared expertise and practical collaboration.

“As the new Ambassador since July 2025, it is my pleasure to welcome you to this Tanzania-Dutch Poultry Knowledge Exchange Seminar,” she said. “The Netherlands' success in the poultry sector is a result of close cooperation between businesses, academic institutions and government—something we believe can benefit Tanzania as well.”

The seminar, she said, is tailored for medium and large-scale poultry farmers, offering them access to Dutch insights in areas such as feed management, poultry health, digital technologies, and processing.
Counsellor at the Netherlands Embassy, Mr Bart Pauwels, described the event as a valuable opportunity for Tanzanian farmers to learn directly from Dutch poultry companies, particularly on technical practices and innovative farming methods.

“We’ve brought in Dutch companies to share their experience and work with Tanzanian stakeholders to help transform the sector into a more efficient and profitable one,” said Mr Pauwels.
He pointed out that Tanzania holds considerable potential in poultry farming, but faces gaps in knowledge, technology, and practical experience. The seminar, he said, serves as a platform for mutual learning and growth.

“The idea is for every Tanzanian stakeholder to view poultry as a viable and promising industry, one that can contribute significantly to the national economy,” he said.Secretary General of the Tanzania Feed Manufacturers Association (TAFMA), Mr Sufian Zuberi Kyarua, commended the initiative, saying it offers an opportunity for local feed producers and farmers to enhance their knowledge and embrace sustainable farming techniques.

“This seminar opens the door for the poultry sector to scale up to the next level,” he said. “By learning from the Dutch experience, we can improve livelihoods and build a stronger, more sustainable industry.”Mr Kyarua added that the seminar would be followed by a poultry exhibition, providing a platform for farmers and stakeholders to further engage, learn about the sector’s potential, and explore solutions to existing challenges.

Zahor Abdallah Zahor, a poultry farmer from Lindi, said the seminar encourages local farmers to transition from traditional to commercial poultry farming.“It’s about changing the mindset,” he said. “Farmers need to see poultry as a business, and that requires the right knowledge, technology, and support.”

He acknowledged that while access to finance remains a challenge, there are still opportunities for growth through adoption of modern practices and collaboration with international partners such as those from the Netherlands.

The seminar follows a recent collaboration between the Netherlands Embassy and the Ministry of Livestock and Fisheries, which launched a poultry curriculum assessment project aimed at strengthening skills and improving productivity in the poultry industry across Tanzania.
Ends


 Netherland Ambassador to Tanzania , Honourable Excellence, Marjo Crompvoets (second left) listens tentatively to the presentations during one day seminar of poultry exchange knowledge , (second right) is the agricultural counselor of the Netherland Embassy in Dar , Bart Pauwels  and first right is Theo Mutabingwa , Agricultural Advisor at the Netherland  Embassy in Dar.

A cross sections of farmers and poultry stakeholders from Dutch companies and Tanzanians attending a one day seminar on poultry knowledge exchange in Dar es Salaam on Wednesday.


.




Mteja wa Bank of Africa-Tanzania (BOA),Bw.Dolvin Salvatory Olomi, kutoka Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro,amebahatika  kuibuka mshindi wa jumla wa shilingi milioni 5 kupitia kampeni iliyomalizika iitwayo “Miamala ni Fursa.”

Meneja wa Tawi la Bank of Africa Tanzania tawi la  Moshi, Bi. Mpoki Mwanjala akikabidhi hundi ya mfano ya shilingi milioni 5 kwa Bw. Dolvin Olomi, mshindi wa kampeni ya Miamala ni Fursa, baada ya kutangazwa mshindi wa kampeni hiyo katika hafla iliyofanyika katika tawi la Benki hiyo.

Kampeni hiyo, iliyoanza Juni hadi Septemba 2025, iliwezesha zaidi ya washindi 60 nchi nzima kujinyakulia  zawadi, huku wateja wakipata zawadi za kila wiki za Shilingi 50,000 kwa kutumia huduma za kidigitali zinazotolewa na Benki. Kampeni ilifikia kilele kwa droo kubwa ya mwisho, ambayo ilitoa zawadi kubwa  ya Shilingi 5 milioni kwa mtumiaji bora wa huduma ya kidijitali—aliyetangazwa rasmi kuwa mshindi mkuu kupitia droo ya bahati nasibu hiyo.

"Kushinda Shilingi milioni 5  kwa kutumia  huduma ya benki kwa njia ya simu kumebadilisha maisha yangu," alisema Bw Olomi, ambaye alitoa shukurani zake za dhati kwa Bank of Africa-Tanzania,  kwa kukuza ushirikishwaji wa kifedha kupitia kampeni za kibunifu na zenye kuleta manufaa kwa wateja wake.

Kampeni ya “Miamala ni Fursa” ilizinduliwa Juni 4, 2025, na ilianzishwa ili kuhimiza utumiaji wa huduma za benki kidijitali kwa kufanya miamala ya kila siku, ikijumuisha uhamishaji wa fedha kutoka benki  kwa matumizi mbalimbali, kufanya malipo ya ankra,kununua   muda wa maongezi au umeme. Kampeni hii ni sehemu ya dhamira pana ya benki ya kuunga mkono  ajenda ya Serikali ya Tanzania ya  matumizi ya huduma za kidijitali na kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma za fedha kwa wote.

Ofisa Mkuu wa Huduma za Kidijitali wa Bank Of Africa-Tanzania ,Lameck Mushi alisema: "Mafanikio ya kampeni ni ishara tosha kwamba Watanzania wako tayari kutumia huduma za kibenki za kidijitali ambazo ni rahisi, zinaweza kufikiwa na ni zenye manufaa. Kupunguza ada ya uhamisho kutoka benki kwa matumizi mbalimbali kwa zaidi ya asilimia 50% na kufanikisha kuongeza matumizi ya huduma za kifedha kwa njia ya simu kufanya miamala, na msisimko wa kushinda zawadi uliongeza zaidi."

Bw Mushi aliongeza: "Iwe unaishi maeneo ya mjini au vijijini, matumizi ya huduma za Kibenki kwa njia ya simu yalimpatia kila mmoja fursa ya   kushinda. Kampeni hii ni uthibitisho kwamba huduma ya benki ya kidijitali inaweza kuwa ya kila mtu."

Benki pia ilihamasisha  wafanyakazi wake  katika matawi mbalimbali nchini  kuelimisha wateja, watumiaji wapya, na kutoa msaada wa kiufundi muda wote wa kampeni.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano , Nandi Mwiyombella alisema kampeni ya "Miamala ni Fursa” ilikuwa zaidi ya kujitangaza. “Tumewawezesha wateja si tu kwa zawadi za pesa taslimu, lakini pia kuwahakikishia pia wateja wetu kuwa huduma zetu za kidijitali ni zenye uhakika na wanaweza kuzitumia bila wasi”.

 Bank of Africa Tanzania inawashukuru washiriki wote na inampongeza mshindi   wa jumla wa zawadi kutoka Moshi, pamoja na washindi wengine wa kila wiki waliozawadiwa  kwa matumizi ya huduma za kidigitali zinazotolewa na benki.

Wakati benki inao mkakati wa kuleta kampeni za kunufaisha wateja siku za mbele,itaendeleza  dhamira yake kuongeza ujumuishaji wananchi katika sekta rasmi za kifedha na kuwezesha wananchi kunufaika na mapinduzi ya teknolojia na ya kidigitali.

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.