BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imeeleza kwamba hakuna hata senti moja kutoka kwenye akaunti ya wateja wao ambayo imepotea baada ya kutokea tatizo la kiufundi katika mifumo ya kibenki kupitia mitandao ya simu za mkononi (Mobile Banking System) hali hiyo ilijitokeza siku ya Jumatano wiki hii.
 
Kaimuy mkuu wa Kitengo cha Biashara na Mawasiliano wa Benki ya NBC, Bi Rukia Mtingwa akisisitiza jambo wakti wa utoaji wahabari hizo
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Afisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki hiyo, Jimmy Myalize alisema kuwa matatizo ya kiufundi ambayo yalitokea siku ya Jumatano ni baada ya kugundua mifumo ya kibenki kwa njia ya mtandao wa simu za mkononi kushidwa kufanya kazi.

Alisema kutokana na tatizo wateja hawakuweza kusoma amana zao au akiba zao kwenye simu zao za mknononi au ilikuwa inaonyesha sifuri na ilisababisha usumbufu kwa wateja wote wa benki hiyo nchi nzima.

"Mafundi wetu na wataalamu wa mitandao katika benki wanafanya kazi ili kuhakikisha kwamba wateja wa  benki hiyo nchini kote wanaweza kupata taarifa za amana zao na kuendelea kufanya shughuli zao za kifedha kupitia simu zao za mkononi," Alisema.
 
Kaimu Afisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki hiyo, Jimmy Myalize akiongea na Waandishi wa habari jana kuhusu na hitilafu hiyo kushoto kwake ni kaimu mkuu wa kitendo cha Biashara na mawasiliano wa benki hiyo Bi Rukia Mtingwa.
Aliongeza kuwa NBC ni benki ya muda mrefu hapa nchini tangu mwaka 1967 na wataendelea kutoa huduma  nafuu na salama za kifedha nchini kote na katika jitihada kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa Watanzania.

"Tatizo lilianza asubuhi na mafundi wetu walichukua hatua ya haraka kwa kutambua na kutatua mara moja, walilazimika kukata huduma za kibenki kwa njia ya simu ili kuruhusu mafundi wetu kufanya kazi kwa urahisi ili kutatua kikamilifu tatizo hilo la kiufundi, alisema kaimu Mkuu wa Masoko na Mahusiano , Rukia Mtingwa.

"Katika tatizo hilo wateja wangependa kuthibitisha amana au akiba zao, wanaweza kufanya hivyo kwa kutembelea tawi lolote la NBC au ATM.

"Tungependa kuomba radhi kwa usumbufu wowote uliosababishwa na mafundi wetu wanaendelea kufanya kazi kwa karibu ili kuhakikisha kwamba huduma ya kibenki kupitia simu za mkononi zinarudi haraka iwezekanavyo," aliongeza Rukia.

Kwa upande mwingine, Benki hiyo imekanusha madai ya hivi karibuni kupitia Mitandao ya habari (social media) kwamba benki hiyo imekuwa mwathirika wa wizi wa kupitia mashine zake za ATM na kuomba wateja kuondoa fedha zao.

Benki hiyo ilisema kwamba taarifa hizo si za kweli na inapenda kuwajulisha wateja wao na wananchi kwa ujumla kuwa habari hizo si za kweli kwamba kuna wizi wa mitandao kupitia mashine zake za ATM nchini.

Uongozi wa benki hiyo ilisema matatizo makubwa ya wizi kupitia mashine za ATM kushughulikiwa kwa pamoja na Taasisi ya Benki Tanzania (TBA).





Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.