April 2, 202508:24:44 PM

 Na Damas Makangale,

Kitengo cha Kompyuta cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (University of Dar es Salaam Computing Centre – UCC) kimeandaa warsha maalum ya siku tatu kuanzia tarehe 20 Machi 2025 hadi 24 Machi 2025, itakayolenga kujadili na kuwajengea uwezo wataalamu wake wa mifumo (Software Developers na Training Instructors) katika masuala ya usalama wa mtandao (Cyber Security).

 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa warsha hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa UCC, Bi. Leticia Ndongole, alibainisha kuwa lengo kuu ni kuwawezesha watendaji wa UCC kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazotokana na kasi ya maendeleo ya teknolojia duniani.

 

"Katika ulimwengu wa sasa, teknolojia inabadilika kwa kasi kubwa. Tunaona maendeleo ya akili bandia (AI), sarafu za kidijitali kama Bitcoin, na mifumo mingine ya kisasa. Hata hivyo, pamoja na maendeleo haya, tumeona pia ongezeko la uhalifu wa mtandaoni, changamoto inayotukumba si Tanzania pekee bali dunia nzima. Kupitia warsha hii, tunalenga kuwajengea uwezo wataalamu wetu ili waweze kulinda mifumo na data za taasisi na wateja wetu kwa ufanisi zaidi," alisema Bi. Ndongole.

 

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa UCC, Bi Leticia Ndongole, alielezea kwa ufupi maudhui makuu ya warsha hiyo wakati wa ufunguzi rasmi uliofanyika katika ukumbi wa Maktaba Mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

UCC, ikiwa ni moja ya taasisi kinara wa TEHAMA nchini Tanzania, imeendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta hii kwa kutengeneza mifumo mbalimbali ya kidigitali inayotumika serikalini, katika sekta binafsi, na hata kimataifa. Mbali na hilo, UCC pia inahusika katika kutoa mafunzo, ushauri wa kitaalamu, na usimamizi wa mifumo ya TEHAMA kwa wadau mbalimbali.

 

Warsha hii inatarajiwa kuwawezesha washiriki kupata ujuzi wa kina kuhusu mbinu za kisasa za kulinda mifumo dhidi ya mashambulizi ya mtandaoni, matumizi salama ya teknolojia, na namna ya kukabiliana na uhalifu wa mtandao.


Warsha hii inaendeshwa na Bwana Yusuph Kileo ambaye mtaalamu wa usalama wa mtandao, mtoa mafunzo, na mshauri wa masuala ya usalama wa kidijitali. Amejipatia umaarufu katika Afrika Mashariki na kimataifa kutokana na mchango wake katika kuelimisha jamii kuhusu usalama wa mtandao.

Muwezeshaji mkuu na mbobezi aliyebobea katika masuala ya usalama wa mtandao (Cyber Security), Bwana Yusuph Kileo, akiendelea kutoa ujuzi wake.


Wataalamu wa UCC wakifuatilia mafunzo kwa makini na umakini mkubwa.











Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

Post a Comment

    Author Name

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Powered by Blogger.