Msichana mwenye umri wa miaka 22 mkaazi wa Mjini Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba amefanyiwa kitendo cha kinyama cha kubakwa na kisha kutelekezwa na dereva wa gari lilikokuwa limempa msaada na kupitishwa sehemu ambayo alikusudia kwenda .

Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa kumi za jioni katika eneo la Weni Wete ambapo msichana huyo (jina linahifadhiwa) kubakwa na kutelekezwa kutokana na dereva wa gari hiyo kumkimbia baada kutekeleza kitendo hicho .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Shekhan Mohammed Shekhan amesema tayari jeshi hilo linamshikilia kijana Mohammed Kaithar Ali (45) Mkaazi wa Wete ambaye anatuhumiwa kuhusika na kitendo hicho .

Amesema kuwa mtuhumiwa huyo ametekeleza kitendo hicho baada ya kutakiwa kumpa msaada (lift) kwenye gari lake na alipofika maeneo ya Weni kijana huyo alifunga vioo vya gari lake na kisha kumtia machepe mdomoni ili sauti yake isitoke .

Kamanda Shekhan amefahamisha kwamba msichana aliyefanyiwa kitendo hicho amepata maumivu sehemu zake za siri pamoja na kupata michubuko shingoni ambayo imetokana na harakati za kutaka kujinasua ili asifanyiwe kitendo hicho .

‘Kwa kweli mtuhumiwa anadaiwa kutekeleza kitendo hicho tayari yupo mikononi mwa jeshi la Polisi ,na msichana aliyebakwa yuko chini ya uangalizi wa daktari licha ya kwamba alitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani .

Aidha Kamanda Shekhan amewataka wananchi kuwa makini na madereva ambao sio waaminifu na kujiepusha kuomba msaada kwa madareva wasiowafahamu ili kuepusha kutokea kwa matenda ambayo yanaweza kuepukika.

Akizungumzia operesheni ya kamata kamata inayofanywa na jeshi hilo kwa madareva , Kamanda Shekhan amefahamisha kwamba zaidi ya magari 50 yamakamatwa na baada ya kufanyiwa uchunguzi magari 23 yamabainika kuwa hayafai kutembea barabarani .

Amesema kuwa madareva wa magari hayo wamefikishwa mahakamani ambapo wametozwa faini ya kati ya shilingi elfu 80 na lakai tatu kutokana na makosa yaliyobainika kwenye magari yao .

Amesema kuwa operesheni hiyo itakuwa ni endelevu na ina lengo la kuhakikisha kwamba madereva , abiria pamoja na wamiliki wa magari hizo wanatii sharia za usalama wa barabarani bila ya kushurutishwa.

Na Masanja Mabula –Pemba
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.