Benki ya Barclays Tanzania imezindua mpango wa kuboresha huduma zinazotolewa na benki hiyo kwa kuweka dhamana katika huduma zake kwa wateja. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha Mipango na Bidhaa na Kaimu Mkurugenzi wa wateja binafsi, Musa Kitoi alisema kuwa katika mpango huo wa dhamana katika huduma, benki inaahidi kutoa huduma zake kwa muda na kipimo kinachokubalika. 

“Siku zote tunahakikisha mteja anapoingia katika benki yetu anapata huduma bora kama anavyotegemea na kwa kupitia dhamana hii ya huduma tunatoa ahadi kuwa huduma zetu zitakuwa bora maradufu.

“Kwa kuanzia, mteja yeyote atakayeomba kadi ya ATM, atapatiwa katika muda usiozidi dakika ishirini na vile vile kwa wanaohitaji vitabu vya hundi watapatiwa ndani ya siku tano, viwango hivi ni vya juu sana katika soko letu. 

“Lakini pia, pale tutakapogundua kuwa mteja hakupata huduma kama tulivyomuahidi tutahakikisha tunamlipa fidia ndani ya masaa 24,” alielezea Bw Kitoi.

Alisema kwamba Barclays inajizatiti kutoa huduma tofauti za kibenki kwa wateja wake ambazo zinatumia teknolojia ya hali ya juu na pia huduma za viwango vya juu kupitia wafanyakazi wake.
Kitoi alifafanua kwamba benki hiyo imepiga hatua kubwa kuboresha njia mbali mbali za utoaji wa huduma kwa kuzindua mipango ya kupunguza foleni katika matawi yake na kuondoa utumiaji wa fomu za kibenki ambazo zinachelewesha utolewaji huduma haraka.

 “Nia yetu ni kuwa benki inayotoa huduma haraka zinazostahili kwa wateja wetu na tutaendelea kuleta mabadiliko mbalimbali yenye nia ya kuboresha huduma, ziwe za kisasa ili kutimiza azma yetu ya kufanya huduma za benki kuwa rahisi kupatikana na kwa haraka na hivyo kuwapa wateja wetu muda zaidi wa kushughulikia biashara zao,”  alielezea zaidi Bw Kitoi.

Kwa upande wake, Meneja wa Miradi na Mikakati ya Kibenki wa Benki hiyo, Jane Mbwilo alisema kwamba hivi karibuni Barclays ilizindua huduma ya benki bila kutumia makaratasi ambayo inaruhusu wateja kuweza kutoa na kuweka fedha kwa kutumia tu kadi zao na hivyo kupunguza muda mwingi unaotumika kujaza fomu mbali mbali za kuombea huduma. 

Aliongeza kwamba benki hiyo imewekeza katika technolojia mbali mbali ili kutoa huduma za kisasa na kwa bei nafuu.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.