Kauli aliyoitoa Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholaus Musonye, dhidi ya kocha wa Yanga, Marcio Maximo, inanadimiza soka katika ukanda huo kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Shrikisho la mpira Afrka Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholaus Musonye

Musonye akizungumza na Mwananchi (Gazeti dada la Mwanaspoti), alisema Maximo aache woga wa kuhofia kufungwa kwa kupeleka kikosi cha pili kwenye mashindano ya kombe la kagame linaloanza leo jijini Kigali, Rwanda.

Musonye amemhukumu Maximo kwa kumwita mwoga bila ya kuzingatia programu ambayo kocha huyo amejipangia katika timu yake ya Yanga. Kauli aliyoitoa Musonye, pia imekuwa ikitolewa na baadhi ya wadau wa soka hapa nchini ambao nao mara kwa mara wanasema kocha huyo ni mwoga wa kufungwa.

Sitaki kuamini kama Maximo anaogopa kufungwa kwa kuwa atashiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara na atakutakana na upinzani, hivyo kama kufungwa atafungwa tu.
Naamini kocha huyo anajipanga na kuamini kile anachokifanya kwa ajili ya timu yake na kazi aliyopewa.

Watanzania wanaosema Maximo ni muoga watakuwa bado hawajaelewa falsafa ya kocha huyo kwani hata alipokuwa akiifundisha Taifa Starz, aliamnini katika kujenga timu kwa kuwatumia wachezaji vijana.

Maximo anajua anachokifanya katika kuandaa timu yenye ushindani tofauti na kauli ya Musonye.

Tatizo la watu wa Afrika Mashariki na Musonye akiwamo, tumekariri majina ya wachezaji wa soka tofauti na mipango ya kocha kama Maximo.

Tunapenda njia za mkato, ndiyo maana Tanzania na Kenya zimetolewa na  Msumbiji na Lesotho katika harakati za kuwania kufuzu makundi kuelekea fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika Morocco mwakani.

Musonye alitaka Yanga ishiriki Kagame kama Tanzania na Kenya zilivyoshiriki mbio za kwenda Morocco dhidi ya Msumbiji na Lesotho, kwa kuwa hazikuwa na maandalizi ya kutosha,

Maximo hajakaa na kikosi chake chote na kuna wachezaji mpaka leo hii anaziona picha zao magazetini tu. Wachezaji aliokaa nao ni hao aliowachagua kwenda Rwanda.

Lakini mtu kama Musonye ambaye naamini hajui lolote kuhusu ukocha pamoja na kuwepo kwenye soka kwa muda mrefu, anaendelea na kukariri majina ya akina Mrisho Ngasa!

Katimu Mkuu huyo wa Cecafa hajiulizi kwa nini nchi za Malawi, Zambia, Lesotho na Zimbabwe zinapiga hatua katika soka?

Kwa nini Musonye anaendeleza siasa zilizozifanya nchi hizo kuanzisha shirikisho lao la Cosafa ambalo linaonekana kuwa na nguvu kuliko Cecafa?

Ikumbukwe kwamba wakati tukiwa pamoja, nchi zetu za Afrika Mashariki zilikuwa zikipata upinzani wa kweli kutoka kwao, Tanzania haikuwa na uwezo wa kuifunga Zambia!
Baada ya nchi hizo kujitoa na kuunda Cosafa, bado kina Musonye wanaendelea kupiga siasa zilizotufikisha hapa.

Musonye hawataki wachezaji vijana, eti hawawezi kufanya biashara anadhani kina Ngasa watacheza soka mpaka lini?

Naamini biashara ingeweza kuanguka kama timu mwenyeji angeingiza kikosi cha pili lakini kwa Yanga siioni madhara zaidi faida ya kuzalisha vipaji vinavyopotea.

Katika hili siiuoni uoga wa Maximo, kocha hawezi kuwabeba wachezaji kama mizigo kwenye mashindano.

Tanzania tunahitaji vipaji vipya, Maximo alikuwa na mkakati wa kuvizalisha kwa ajili ya Yanga, Taifa Stars na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Binafsi nitamhukumu Maximo kwa uwezo wake wa kufundisha uwanjani siyo wa kwa tuhuma za woga.

Makala hii imeandikwa na Mohamed Kuyunga kupitia Meseji Senti ya gazeti la Mwanaspoti kuyungajunior@gmail.com
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.