KOCHA wa zamani wa Bayern Munich Felix Magath amedai kuwa meneja mpya wa Mabingwa wa Bavarian almaarufu kama Bayern Munich, Josep " Pep" Gardiola amejitakia mwenyewe matatizo kwa kumsaini  kiungo kinda Thiago Alcantara kuichezea Bayern Munich msimu huu mpya.
 
Alcantara, Kiungo wa Spain mwenye Miaka 22, aliihama Barcelona Mwezi uliopita na kuhamia Bayern Munich kwa Dau la Euro Milioni 20 na kuungana na Kocha Mhispania mwenzake aliekuwa Barcelona, Pep Guardiola, ambae pia ndie alimwinua Alcantara kutoka Timu B hadi Kikosi cha Kwanza cha Barca.

Lakini Felix Magath, aliekuwa kocha wa Bayern Munich kati ya wwaka 2004 na 2007, amesema uamuzi wa Guardiola kumchukua Alcantara utamletea matatizo na atajutia.

Magath ametamka: “naona ni tatizo kwa kocha Mhispania kumsaini Mhispania mwenzake. Pep atapata matatizo na Thiago. Ama wachezaji wenzake watakasirika kwa kuwa anachezeshwa mara kwa mara au watu watahoji uhamisho wake wa dau kubwa ikiwa hachezi! Kocha Josep Gurdiola almaarufu kama Pep angeweza kuepuka hili,"

Mbali ya utata huo, Felix Magath, ambae Msimu uliopita alikuwa Kocha wa Klabu ya Bundesliga Wolfsburg, pia anaamini Pep Guardiola hatashinda ile vita ya kupiku mafanikio ya Msimu uliopita ya Kocha Jupp Heynckes ambae aliiwezesha Bayern Munich kuweka Historia ya kuwa Klabu ya kwanza ya Germany kutwaa ‘Trebo’ yaani, Ubingwa wa Germany, Ubingwa wa Ulaya na kubeba German Cup.

Magath amedai: “Pep ana tatizo kubwa la kurithi Timu ambayo ilishinda kila kitu Msimu uliopita. Hivyo hawezi kuwafanya wawe bora zaidi ya hapo!”
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.