Watu wasiopungua 48 wameuawa huko Tana River Kenya na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya kutokea mapigano ya kikabila.
Taarifa zaidi zinasema, mapigano hayo yaliyotokea kusini mashariki mwa Kenya yamezihusisha jamii za Pomoko na Orma. Polisi ya eneo yalipotokea mapigano imetangaza kuwa, mapigano hayo yalianza baada ya wanachama wa jamii ya Pomoko kuwashambulia wenzao wa jamii ya Orma. Kamishna Msaidizi wa Polisi Angelus Karuru ambaye anaongoza kikosi cha usalama katika eneo yalipozuka mapigano amesema kwamba,  juhudi za kiusalama zinafanyika ili kumaliza mapigano hayo. Taarifa zaidi zinasema, ngombe wasiopungua 60 pia wameteketezwa katika mapigano hayo. Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya limetangaza kuwa, watu waliouawa katika mapigano hayo ni kati ya 30 na 50. Aidha watu 30 kati ya waliouawa ni wanawake na watoto wadogo. Baadhi ya watu wametoweka na hawajulikani waliko.
Source: kwetubongo
Newer Post
This is the last post.

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.