BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imesema kuwa inautambua mchango wa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo wadogo katika kukuza uchumi wa taifa na hivyo itaendelea kuwa karibu nao na kuwapa mafunzo ya mara kwa mara.



Akizungumza na gazeti hili jana kuhusu kongamano la siku mbili la Wajasiriamali Vijana lililofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Meneja Ukuzaji wa Biashara Huduma za Kibenki kwa Wateja Wakubwa na Kati, Jonathan Bitababaje alisema wajasiriamali wengi waliofanikiwa ni wale walioanzia ngazi za chini. Business devv man sme banking dept


“Kumbukumbu na nyaraka za kibenki zinaonyesha kuwa wale walioanza kwa mikopo midogo na kuendelea kufanya biashara na NBC ndio wamekuja kufanikiwa sana na ndio maana benki hii itaendelea kuwapa mafunzo na ushauri unaofaa wajasiriamali vijana,” alisema.


Alisema kupitia makongamano, wajasiriamali hupata nafasi ya kufahamu ni biashara gani inatakiwa kwa wakati, bidhaa gani inatakiwa na hata washindani wake ni akina nani.


Akizungumza wakati wa semina hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Don Bosco kwa niaba ya Waziri wa Vijana, Habari, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mkandala, Naibu Mkurugenzi wa Vijana wizarani hapo, James Kijugusi aliwashauri wajasiriamali hao kuwa na tabia ya kuziwekea bima biashara zao.


“Biashara lazima ziwe na kinga. Kwa sasa  sema uchumi wan chi na hata wa dunia hauwezi kukua iwapo wajasiriamali wakijitoa katika biashara hasa katika enzi hizi zaunaTes Tfanyabiasharsiku ya kwanza biashara wajasiriamali .


Alisema kuwa kwa sasa Serikali ipo katika mazungumzo na mashirika ya hifadhi za jamii na bima kwa ajili ya kuweka utaratibu wa kuwasaidia wajasiriamali iwapo watapatwa na majanga ya aina hiyo.

NBC Bank  Business Development SME Banking Department, Jonathan
Bitababaje speaking during a Youth Entrepreneurship Summit 2012
organised by an NGO known as Young Entrepreneurship Support initiative
YESi under sponsorship of NBC Bank in Dar es Salaam.  Looking on is
YESi Executive Chairman, Dennis Maira.
Kongamano hio liliwajumuisha washiriki 250 kutoka kada mbalimbali za wajasiriamali vijana wa jijini Dar es Salaam.
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.