WADAU wa vita dhidi ya UKIMWI wilaya ya Ikungi,wametakiwa kutobweteka na kitendo cha kupungua kwa maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI,na badala yake waongeze juhudi zaidi ili ifikapo mwaka 2015,maambukizi ya virusi vya UKIMWI,unyanyapaa na vifo vinavyosababishwa na UKIMWI,vifikie asilimia sifuri.

Changamoto hiyo imetolewa juzi na afisa ustawi wa jamii sekretarieti ya mkoa wa Singida,Zuhura Kyara,wakati akifungua mkutano wa wadau wa UKIMWI wilaya mpya ya Ikungi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wananchi mjini hapa.

Alisema maambukizi mapya ya VVU katika halmashauri ya wilaya ya Singida na Ikungi,takwimu zinaonyesha kuwa yamepungua kutoka asilimia nne hadi mbili hadi mwaka huu.

Kyara alisema hayo ni mafanikio mazuri lakini hata hivyo,juhudi zaidi zinapaswa kuongezwa ili kufikia mwaka 2015,pasiwepo kabisa na maambukizi mapya,unyanyapaa na vifo vitokanavyo na UKIMWI kama dunia ilivyoazimia.

"Dira na maono yetu kama wadau,ni kuhakikisha tunaweka misingi imara yenye mwelekeo wa kutimiza azma hii.Hivyo tutumie fursa hii ya mkutano huu kufanya majadiliano juu ya mikakati ya kukabili changamoto  mbalimbali za VVU/UKIMWI",alifafanua Karya.

Afisa huyo alitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni kupunguza maambukizi yanayosababishwa na ngono hasa kwa vijana wanaofanya ngono kama sehemu ya kujipatia kipato.

Karya alitaja changamoto zingine kuwa ni kupunguza vifo vyote vinavyosababishwa na ugonjwa wa kifua kikuu na kuhakikisha upatikanaji wa dawa za kufubaza VVU kwa watu wote wanaoishi na VVU na kupatiwa matibabu yote wanayostahili kupewa.
MWISHO. 
Labels:

Post a Comment

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.